Mbunge wa Sikonge, CCM, Said Nkumba ametangaza kukihama hicho na kujiunga na Chadema, kwa madai CCM ‘haina mapenzi na watu’.
Nkumba anakuwa mbunge wa sita kutoka CCM kutimkia upinzani katika kipindi kisichopungua mwezi mmoja.
Wabunge
waliokihama chama hicho ni Edward Lowassa (Monduli), Goodluck Ole
Medeye (Arumeru Magharibi), Makongoro Mahanga (Segerea), James Lembeli
(Kahama) na mbunge wa viti maalum, Esther Bulaya.
Lowassa
ametimkia Chadema na ndiye aliyepewa jukumu la kupeperusha bendera ya
chama hicho kwa mwavuli wa Ukawa, kugombea urais katika uchaguzi wa
Oktoba 25, mwaka huu.
Akizungumza na Mwananchi kwa simu
jana kutoka Tabora, Nkumba alisema: “Sikushawishiwa, nimejiondoa CCM
kwa uamuzi wangu na nimefanya hivi kwa kuwa sikuwa nasikilizwa kwa kile
nilichokisema.
“Niliipenda CCM kwa dhati kabisa, lakini
sikuona sababu ya kuendelea kubakia CCM, sisikilizwi, chama hakina
mapenzi na watu, ndiyo maana tunaondoka.”
Nkumba
aliyekuwa kinara wa kuipinga Ukawa ambao baada ya kutoka bungeni kwenye
Bunge la Katiba, alisimama kidete na kuanzisha “Tanzania Kwanza, Mbili
yatosha” alisema amejiunga na upinzani ili kujenga chama cha Chadema.
“Mimi
najiamini, ninakubalika ndani ya chama, sasa nimekuja huku, nataka
kuendelea mazuri ya Chadema, ninaona huku kunanifaa,” alisema Nkumba.
Akizungumzia kuwa wanaokwenda upinzani ni makapi, Nkumba alisema kuwa hata makapi bado yanakuwa na faida.
“Unajua
kuwa wakati mwingine makapi ya asali labda ukamua sawasawa, lakini kwa
hapa, sisi bado tuna asali, si makapi yasiyokuwa na kitu.”
Kuhusu
hatma ya CCM na kuondokewa watu mbalimbali na kujiunga upinzani, Mbunge
huyo alisema kuwa wakuu wa chama hicho, lazima washtuke na wasipokuwa
makini, huu utakuwa mwisho wa CCM.
“Hivi wewe hushtuki,
wanaona kabisa chama kikubwa lakini watu wanaondoka, wanaona kabisa
mwelekeo haupo, halafu wanaendelea na yao, ni wazi kuwa wataanguka,”
alisema.
No comments:
Post a Comment