Thursday 28 February 2013

Photo show ends on Monday, the day Kenyans go for the General Election




Head of Public Service Francis Kimemia (left) and Presidential Press Service boss Isaiya Kabira tour the photo exhibition, The Kibaki Years, which Mr Kimemia officially opened at KICC on February 4. It ends on March 4. Photo/FILE NATION MEDIA GROUP
The story of President Kibaki and his political journey has been told for the whole month on the walls of an expansive room.

The room at the Kenyatta International Conference Centre in Nairobi, has a collection of his memorable pictures on display.

Kenyans who’ve been at the photo collection have left glowing messages for their President, and many more were streaming in to view the photo collection, with just four days left to the election date.

The photo exhibition too will close on March 4 — next Monday — when Kenyans go to the ballot to pick Mr Kibaki’s successor.

There are those like Charles Kinyua who viewed the exhibition as “a great idea”, and others like Philip Masese who viewed it as a “remarkable exhibition” according to comments left in the visitors’ book at the KICC.

There’s a video with his clips at different functions, like the one where he’s telling all parents to take their children to primary school, and another clip where he’s warning all those businessmen who dodge taxes that tax evasion will not be tolerated.

There are sections at the exhibition showing Kibaki as a family man, his life in Parliament, his contribution to the economy, his days with Kenyatta, and then there’s the First Lady Lucy Kibaki.

There is one where the President is all smiles between Olympic athletics champions David Rudisha and Ezekiel Kemboi. Interestingly, the one that he took with Jamaica’s athlete Usain Bolt is not there.

There’s also a picture of President Kibaki with former US president Bill Clinton and two pictures showing Mr Kibaki with the current US President Barack Obama, when he visited Kenya as a senator, and one taken at the White House with Michelle Obama, after Mr Obama was elected for his first term. There is also a photo of the President with great African icon Nelson Mandela.

A section shows how Mr Kibaki was instrumental in ensuring regional stability, and he is right there with Dr John Garang, the then leader of the Sudan People’s Liberation Army, which was fighting for secession. Dr Garang died in 2005, but the Comprehensive Peace Agreement brokered by Kenya ensured that in the end, the South became independent in 2011.

And just for the record, Mr Kibaki met former Libyan leader Muammar Gaddafi, and was also given a replica shirt of the Brazilian football team, with number 10 at the back.

If the exhibition was meant to show President Kibaki as the man who rebuilt Kenya — the roads, the schools, the hospitals and the sports — it achieved exactly that.

“A great journey enviable by anyone. Great job!” Daniel Ng’etich noted in his comments on the visitors’ book.

Ms Michelle Muthoni wrote in past tense: “He was a great and inspirational leader. Fantastic job!”

Others like Edward Wafula saw all the pictures and simply wrote: “Enjoy your retirement”. Lyne Kayugira added: “History made to be remembered”.

“This is a wonderful journey. Great achievements. I am very proud of you,” noted Njeri Kiragu.

There’s also another picture of President Kibaki pushing a wheelbarrow full of wet concrete when he launched a road construction in Lilongwe, Malawi.

The only thing that might make one sad is that some of the pictures have no captions, and still others with captions, do not have dates or places where they were taken.
Then there’s the promise that more pictures can be viewed and downloaded on the website (http://www.kibakipresidency.go.ke) but when the Nation visited the website, using multiple browsers, there was no photo gallery or even information. It is still a skeleton.

Trained curators, who spoke to the Nation, off-the-record complained that the photos are not chronologically arranged, but they hope that if President Kibaki sets up a gallery in future the pictures will have to be arranged in a way that tell a story to people who do not know the history of Kenya.

The hope is that the photo gallery and the video might all be uploaded on the website for those Kenyans who would want to know their President a bit more, but did not get the chance to visit the KICC for the exhibition.

“This is a great step. It keeps us in touch with the outgoing President. God bless him and (Jomo) Kenyatta,” noted Linah Kimani.

Ann Ayodi added: “Old man, may the almighty God bless you for the rest of your life”.

Harambee Cash from the poor must have hurt Kibaki

There are two pictures at the exhibition that might inform why President Kibaki banned harambees (public fundraisings involving government officers) when he got into office.

Of course the official version was that the President wanted to keep public servants away from temptation of extorting people or stealing public resources, to get money for harambees..

But those two pictures show President Kibaki receiving donations from poor people, back in the days when he was Finance minister.

“A one-shilling donation may not be very much, but when it is all you’ve got, it means a great deal,” reads a caption of a photo showing Mr Kibaki in a suit getting the one shilling from a shy boy in small short, and an ill-fitting shirt in Isiolo. The money was for Merti Primary School and Sh21,000 was raised in 1972.

Another undated photo shows a mother lifting her four-year-old daughter so that the daughter hands over a Sh20-donation for building Kwale Primary School. Mr Kibaki then Vice President .

No wonder he quickly agreed with Mr Muriuki Karue, a former ol Kalou MP, when he proposed the Constituency Development Fund.

When a cheaper diploma pays more than a costly degree

Results. The A-Level results show that 76, 151 obtained at least two principal passes, which ideally qualifies them to enlist for post-secondary education.
Kampala.

Three years ago, Samuel Imbadi eyed an under-graduate course in Electrical Engineering. Kyambogo University was his choice institution.

An Advanced-Level subject combination of Physics, Economic and Mathematics (PEM) theoretically placed him in good stead to achieve his dream.
When results of the 2010 Uganda Advanced Certificate of Education (UACE) were released in early 2011, Mr Imbadi garnered 8 points, significantly lower than what is required for admission for a Bachelor of Electrical Engineering degree course. He was dejected.
His colleague and alumni of Old Kampala SS opted to repeat, enlist as private students on other university course(s) or drop out altogether – and many of last year’s A-Level students, whose resulted were released yesterday, face similar choices.

Uganda’s largely theoretical education focused on literacy, numeracy and the learning has encouraged recitation and memorisation, but not practical skills crucial for innovations, production and wealth creation. Yet the country has chosen sciences over humanities, which President Museveni preaches as the right medicine to transform Uganda.
But what does his government do to realise this vision?
The A-Level results show some 76, 151 obtained at least two principal passes, which ideally qualifies them to enlist for post-secondary education.

Government sponsors only some 4, 000 students at the five public universities; Makerere, Kyambogo, Mbarara, Gulu and Busitema. Others with handsome financing will enroll and pay for – perhaps buy – degree courses at these public and the other 27 private universities.
However, several thousand will miss out either because they lack money for tuition or have significantly lower scores than the threshold admission requirement.
So what are the alternatives, or should they even be second-rate options?

“Successful candidates”, Education Minister Jessica Alupo said while releasing the results on Tuesday; will get university slots.
She added: “I must (however) encourage A-Level leavers to seriously consider enrolling for technical, vocational and other courses at diploma level that lead to employment opportunities at the middle-level in the economy in both formal and non-formal sectors.”
Experts criticise such casual – almost derogatory - manner in which bureaucrats rate technical and vocational training as an anathema.

According to Fagil Mandy, an education consultant who chairs the country’s examinations body, “people managing education don’t understand and articulate the critical role vocational and technical skills play in a nation’s transformation”.
This skewed view is premised on the “deceptive” notion that tertiary institutions are for ‘failed students’, who in turn pity instead of asserting themselves, the former commissioner in the Ministry of Education said.

Self-pity is what Imbadi felt before he found himself offering a diploma in Automobile Maintenance and Repair at Nakawa Vocational Training Institute, a few kilometres from Kyambogo University where he originally intended to enroll.
“At first I didn’t like [the idea of joining a technical institute],” he said a matter-of-factly, before an exposure to vehicle handling at a garage during his vacation changed things.

Now he relishes the sight of vehicles he has helped fix wheeze out of the Nakawa workshop – a fulfillment that only a hand-on involvement can bring. “You get the real feel of doing something, not just the theory,” he said. Besides, there is money to make for upkeep and Imbadi, 22, just started his 2nd year at the institute.
More, university students doing the related courses come for practicals at Nakawa Vocational Training centre where Imbadi says he has on occasions shown them “how to do mechanical and electrical things”.

“People should stop looking at Business, Technical, Vocational education and training as a last resort,” said Paul Amoru, spokesman of the statutory entity that examines these courses. “We are looking for the best brains, not failures.”

A person who learns automobile servicing like Imbadi will become a mechanic, another one smart in wood work can own or be employed at a workshop making fine furniture and diploma-level masonry training produces a fine builder – all job creators of sorts.

And there are at least 10 public institutions offering diplomas in diverse fields such as cooperatives and business administration, boat building and marine mechanics, fisheries management and technologies, cartography, physical planning, land management and valuation, surveying, meteorology as well as wild life and allied natural resources management.

So, why are these courses that give practical skills often shunned by students and parents?
The problem, Mr Mandy says, is negative perception. To surmount it, he proposes that institutions (see list in table) should be well managed, financed and the theme of apprenticeship and vocational training articulated and popularised by all education stakeholders.
That tosses the ball back to government’s court. Primary and secondary schools offering practical subjects such as metal or wood works and technical drawing are an exception, rather than the rule, and persuading uninitiated students after A-Level becomes an albatross.

Mr Amoru says Parliament’s enactment of the Business, Technical and Vocational Education and Training (BTVET) Act, establishing Uganda Business and Technical Examinations Board (UBTEB), means the country is on course to streamline and exercise control in technical education. That would entail deeper reforms in the education sector.

Home Business Business Barclays Bank Tanzania worst performer in EA





Barclays Bank’s Adan Mohamed. Analysts cite the bank’s ‘Hello Money’ service as one way of reducing costs instead of laying off workers. le="text-align: left;" trbidi="on">

Barclays Bank’s subsidiary in Tanzania is the lender’s worst performer among its East African units, a new Citi Group research report shows, citing spiralling costs and falling net earnings.

Data from the research released last week shows earnings from the Tanzanian unit have declined at an annual compounded rate of 43 per cent over the past six years.

During that period, the Kenyan unit has recorded a growth of 11.6 per cent while Uganda’s earnings have surged by 5.5 per cent.

The Tanzania unit’s cost to income ratio — a financial measure that shows a company’s costs in relation to its income — stood at 94 per cent, higher than that of the subsidiaries in Kenya and Uganda, a factor that Citi says has eroded the lender’s value.

Kenya’s cost to income ratio is at 52.5 per cent (above the industry average of 50 per cent) while Uganda’s is at 72 per cent. Ordinarily, this ratio gives investors a clear view of how efficiently a firm is being run — the lower it is, the more profitable the bank will be.

“What makes the high cost to income ratio even more unacceptable, in our view, is that Barclays Tanzania earns 44 per cent of its revenue in the form of non-interest revenues (NIR), which is markedly higher than for most of Barclays’ operations in Africa. We believe Barclays Tanzania needs to cut costs and/or increase lending margins otherwise it has no value,” said the analysts.

NIR is basically income earned from sources other than what banks charge customers for loans — such as deposit and transaction fees and monthly account service charges.

Barclays Bank’s operations in the region have struggled to contain expenses, with the Kenyan subsidiary announcing on February 13 it will cut 200 jobs this year as it tries to bring down costs.

For the Kenyan operation, costs jumped by their largest margin in five years for the 12 months ending December 2012. Operating costs jumped five per cent from Ksh13.8 billion ($157 million) to Ksh14.2 billion ($165 million).

Barclays Bank of Kenya posted a 7.7 per cent increase in profits after tax, riding on higher returns from government securities, which pushed net profits to Ksh8.74 billion ($97.6 million) for the full year 2012 compared with Ksh8.11 billion ($94.3 million) a year earlier.

Laying off workers

Last year, Barclays Tanzania closed down 10 branches, and laid off 100 employees in an attempt to bring down costs.

Analysts at Old Mutual see the “laying off workers approach” as unsustainable in the long run. “They can lay off this year, but what about say next year?” asked Erick Munyowki, a research analyst at Old Mutual, adding that investing in technology would be a more suitable way of bringing down costs.

“For example, on average, a bank incurs Ksh7 ($0.08) for every mobile-based transaction compared with Ksh100 ($1.16) for over the counter transactions. Agency transactions cost less than Ksh30 ($0.34),” said Mr Munyowki.

Uganda to spend $377,000 on MPs’ iPads



/-56xvqRDGh6Q/US8ncYSDwDI/AAAAAAAAATw/nxl_IbRhJco/s1600/ipads.jpg" imageanchor="1" >
The Ugandan Parliament is to spend about $377,000 on iPad tablet computers for MPs.

Parliamentary officials say apart from bringing MPs up to speed with evolution in technology, they hope to save money in the long run by cutting on printing and other stationery expenses.

“They (iPads) would be Parliament property but when someone uses one for five years you don’t expect it to be in shape for use by another legislator for another five years,” commissioner Elijah Okupa told the Daily Monitor.

“They will indirectly become their personal property because of depreciation,” he added.

Figures from Parliament show that the government spent at least $12.1 million over the last two financial years on computer supplies, printing, stationery, photocopying, binding, postage, courier and other communication costs.

They hope to save money by moving to paper-less operations in the House. For instance, any document from the Finance ministry has to be photocopied into almost 400 copies for each MP and other Parliament officials. These will now be e-mailed to the MPs instead. “It is a necessary tool of work, and we need them as MPs so that we avoid the amount of paper work which is always put in our pigeon holes,” Busiro East MP Medard Segona (DP) told the Daily Monitor.

Many MPs are not familiar with the gadgets, sources said, and the firm that will be contracted to supply them is expected to receive a training contract as well. “We can mitigate these costs and the only way is to use iPads now which are cheaper by the way if only members are trained on how to use them.

PSI: Tumezuia mimba milioni 1.2 zisizotarajiwa



Mtung’e alisema kifurushi hicho kitakuwa na vifaa vyote vitakavyohitajika kwa mjamzito kujifungua salama ambavyo alivitaja baadhi kuwa ni jozi mbili za glovu, nyuzi mbili, pamba, shuka kwa ajili ya matumizi ya mara moja, kitambaa cha joto cha mtoto, dawa ya kusafishia mikono, vidonge vitatu vya kuzuia mama kutokwa na damu nyingi.


SHIRIKA lisilo la kiserikali la PSI limesema kwamba limefanikiwa kuzuia mimba zisizotarajiwa 1.2 milioni mwaka uliopita.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam juzi, Mkurugenzi wa Afya ya Uzazi wa shirika hilo, Dk Nguke Mwakatundu alisema hiyo ilitokana na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa kwa mkakati wake wa kutoa huduma za uzazi wa mpango nchini.

“Tumefanikiwa kutokana na kutoa huduma za uzazi zaidi ya matumizi ya kondomu. Ukiangalia tangu shirika lilipoanzishwa miaka 20 iliyopita, matumizi ya kondomu yalikuwa yakitumika zaidi. Lakini sasa njia hiyo imepita na nyingine kama lupu, vipandikizi, vidonge na sindano ambazo matumizi yake yameongezeka maradufu,” alisema.

Alisema katika mwaka wa jana, njia za muda mrefu za uzazi wa mpango zilitolewa kwa watu 102,772 ikilinganishwa na watu 48,518 mwaka uliotangulia ikiwa ni ongezeko la asilimia 92.
Alisema mafanikio hayo yametokana na mkakati wa shirika hilo kupanua wigo wake wa kusambaza huduma za afya katika maeneo ya mbali...

“Tumeongeza utoaji wa huduma katika sekta ya umma kwa asilimia 145. Kitu kikubwa tulichofanya ni kuongeza timu ya watoa huduma katika maeneo hayo kutoka tano hadi 10 na kila timu ina wauguzi wawili.”

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa PSI Tanzania, Romanus Mtung’e alisema katika kuhakikisha kwamba utoaji huo wa huduma unakuwa salama, shirika lake linaandaa Kifurushi Salama kwa ajili ya Kujifungua (Clean Delivery Pack), kitakachoanza kusambazwa Aprili mwaka huu.

Mtung’e alisema kifurushi hicho kitakuwa na vifaa vyote vitakavyohitajika kwa mjamzito kujifungua salama ambavyo alivitaja baadhi kuwa ni jozi mbili za glovu, nyuzi mbili, pamba, shuka kwa ajili ya matumizi ya mara moja, kitambaa cha joto cha mtoto, dawa ya kusafishia mikono, vidonge vitatu vya kuzuia mama kutokwa na damu nyingi.

Alisema lengo la shirika lake siyo kupunguza idadi ya watu kama ambavyo imekuwa ikitafsiriwa na wengi, bali kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ili watu wapate watoto kwa mpangilio utakaowawezesha kuwatunza na kuwahudumia vyema na wao kupata fursa ya kushiriki katika masuala ya kiuchumi.

Ole Sendeka ahojiwa na timu ya Mangula





MBUNGE wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na vigogo kadhaa wa CCM Wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Manyara, wamehojiwa na maofisa wa CCM, kuhusiana na malalamiko ya ukiukwaji wa taratibu katika uchaguzi wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa ya chama hicho (Nec) wa wilaya hiyo.


Hatua hiyo ni utekelezaji wa mikakati ya Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), Phillip Mangula, ambaye aliahidi kushughulikia malalamiko yote ya chaguzi zilizopita na kuyatolea uamuzi. Mangula ndiye Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Maadili ya CCM.


Kuhojiwa kwa Sendeka na viongozi wengine wa Simanjiro, kumekuja siku chache baada ya kuhojiwa kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk Mary Nagu ambaye pia ushindi wake wa Nec Wilaya ya Hanang, ulilalamikiwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye akisema kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu na kanuni za uchaguzi wakati wa kinyang’anyiro hicho.


Katika uchaguzi wa Simanjiro, Sendeka alishinda kwa kupata kura 471 dhidi ya Diwani wa CCM Kata ya Mirerani, Justin Nyari ambaye alipata kura 126.


Maofisa hao kutoka Makao Makuu ya CCM, wakiongozwa na Mwanasheria wa CCM, Glorius Luoga waliwahoji Sendeka na Katibu wa CCM Wilaya ya Simanjiro, Jamillah Mujungu, Nyari na viongozi wengine wa chama hicho.


Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho kilichofanyika wikiendi iliyopita, zimebainisha kuwa Nyari na makada kadhaa wa CCM, wanalalamikia ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi huo, ikiwamo kufanyika kwa kampeni kinyume cha taratibu kama kutawaliwa na ukabila, pia baadhi ya wapigakura kutokuwa halali.


Hata hivyo, Luoga ambaye pia ni Mjumbe wa Nec anayetoka Songea Vijijini, alipotakiwa kuelezea hatma ya malalamiko hayo, hakutaka kufafanua kwa maelezo kuwa yupo Zanzibar.
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Manyara, Ndekubali Ndeng’aso alikiri kufika kwa maofisa wa makao makuu ya chama hicho mkoani hapo na kuhojiana na walalamikaji na walilalamikiwa.


“Nadhani hizi ni taratibu za kawaida tu ndani ya chama, kuna ambao wamelalamika sasa chama kimeona ni busara kuwafuata na kujua malalamiko yao,” alisema Ndeng’aso.
Sendeka na Nyari hawakupatikana jana kuelezea kilichojiri katika mahojiano hayo kwani simu zao za mkononi ziliita bila ya kupokewa.


Hata hivyo, Mujungu licha ya kukiri kuhojiwa alisema wenye mamlaka ya kuzungumza ni maofisa hao wa makao makuu... “Hili jambo lipo ngazi za juu nadhani wao ndiyo wana majibu ya maswali yenu.”

Papa wawili katika mgongano wa kimadaraka




YAMETIMIA. Safari ya miaka saba ya Baba Mtakatifu Benedict XVI inakamilika leo pale atakapong’atuka rasmi katika uongozi wa Kanisa Katoliki, ifikapo saa 2:00 usiku kwa saa za Italia (saa 4:00 usiku kwa saa za Tanzania).


Kwa siku mbili, Papa amekuwa na shughuli nyingi katika makao yake, Gandolfo Castel, Vatican akijiandaa kimwili kuondoka, akiweka sawa nyaraka zake binafsi na zile za kanisa ambazo zitawekwa katika kumbukumbu.


Kwa upande mwingine Vatican, nchi ambayo ipo ndani ya Jiji la Rome iliyozungukwa na ukuta, ikiwa na ukubwa wa hekta 44 na wakazi 832 pekee, imekuwa katika hekaheka nyingi.
Jana, waumini zaidi ya 50,000 na wengine wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani wakiwamo makardinali, maaskofu, mapadri na walei walialikwa kwa shughuli rasmi ya kumuaga kiongozi huyo.


Tofauti na kanuni yake, leo Benedict hatavaa viatu vyekundu kama ilivyozoeleka na badala yake amechagua viatu rahisi vya ngozi vilivyobuniwa Mexico. Alipewa viatu hivyo ikiwa ni zawadi wakati wa ziara nchini humo 2012.


Tangu alipotangaza uamuzi wake wa kung’atuka Februari 11, mwaka huu, utata umegubika nafasi yake katika maisha mapya ndani ya Vatican, akiitwa Papa Mstaafu.


Waumini, wataalamu na hata viongozi mbalimbali wa Kikatoliki wameanza kuhoji ni jinsi gani viongozi wawili (Papa) wataishi, huku wote wakivaa mavazi meupe wakiitwa Papa, wakiishi umbali mdogo kati yao, wakiwa na wasaidizi wengi wanaowahudumia.

Vatican
Nje ya Gandolfo Castel, ulinzi umeimarishwa na vibali vya kuingia Vatican vimesitishwa.
Juzi, Vatican ilitangaza kwamba Papa Benedict XVI atajulikana kama ‘Emeritus Pope’, yaani Papa Mstaafu mwenye cheo cha heshima, akiendelea kuitwa, ‘mtakatifu’ na ambaye ataendelea kuvaa nguo nyeupe.


Mavazi na hata jina lake jipya ni masuala ambayo yamezua uvumi mwingi, huku suala la mrithi wake mpya pia likiwa gumzo, kwani tukio kama hilo lilitokea miaka 600 iliyopita.
Ni uamuzi uliolishtua kanisa hilo lenye waumini 1.2 bilioni duniani na wengi wanasema awali, haikushauriwa Papa kustaafu kwani kwa kufanya hivyo kunaacha mizozo na minong’ono ya kuwania madaraka.


Hata hivyo, uongozi wa Vatican umesisitiza kuwa uamuzi huo wa Papa Benedict XVI ni wa kipekee na hakuna mzozo ambao utatokea baina yake na mrithi wake ambaye mchakato wa kumpata unatarajiwa kuanza ndani ya wiki mbili zijazo.


“Kulingana na mabadiliko katika kanisa letu, kuna Papa mmoja. Ni dhahiri kwamba katika hali ya sasa hakutakuwa na tatizo,” anasema Mhariri wa Gazeti la L’Oservatore Romano linalomilikiwa na Vatican, Giovanni Maria Vian.

Hofu iliyopo
Hata hivyo, wakosoaji wa mambo hawakubaliani na hoja hiyo na baadhi ya makardinali walioko Vatican kwa usiri mwingi, wanazungumzia suala hilo wakieleza kwamba litazua tatizo kubwa kwa Papa ajaye, hasa ikiwa mtangulizi wake, Benedict akiwa bado hai.


Mtaalamu wa tauhidi (theolojia), raia wa Uswisi, Hans Kueng ambaye amekuwa mtu wa karibu wa Papa Benedict XVI, ingawa kwa sasa ni mkosoaji wake amesema:
“Kwa sasa, Benedict XVI akiwa bado hai, kuna hatari ya kuwa na Papa kivuli, mwenye mamlaka kamili ambaye kwa chinichini anaweza kumshinikiza mrithi wake kufikia uamuzi.”
Hans Kueng alisema hayo alipozungumza na Gazeti la Der Spiegel la Ujerumani.


Msemaji wa Vatican, Padri Federico Lombardi alisema Papa Benedict XVI kwa upande wake aliamua aitwe Papa Mstaafu au ‘kiongozi mstaafu wa Roma.’ Anasema haelewi ni kwa nini ameamua kuacha jina lake la sasa la Askofu wa Rome.


Kwa wiki mbili zilizopita, maofisa mbalimbali wa Vatican wamekuwa wakifikiri kwamba Papa angeanza kuvaa mavazi meusi na kutumia jina la Askofu Mstaafu wa Rome ili kuepuka mkanganyiko na mrithi wake.
Mwingine ambaye amekuwa akizusha mkanganyiko ni Katibu wa Papa, Askofu Mkuu, George Gaenswein ambaye ataendelea kuwatumikia Papa wote wawili, yaani Benedict XVI kwenye Monasteri ndani ya Vatican na kazi yake ya kawaida ya kuwa kiranja katika nyumba ya Papa mpya.


Kwa upande wake, Papa Benedict XVI anasema anastaafu na sasa ataishi maisha ya sala na tafakuri ya kina, mbali na majukumu mengine ya kidunia.
Hata hivyo, bado atakuwapo kwenye nchi ndogo ya Vatican, mahali ambako makazi yake yatakuwa jirani na mnara wa kurushia matangazo wa Kituo cha Redio cha Vatican, akiliangalia vizuri Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.


Kwa upande wake, Kueng anasema ni kosa kwa Askofu Gaenswein kuwatumikia Papa wawili kwa wakati mmoja na pia Benedict XVI kubakia jirani na mahali hapo.
“Hakuna padri ambaye anapenda mtangulizi wake kuishi karibu naye na kufuatilia anayoyafanya.


Hata kama Askofu wa Rome, haipendezi kutenda kazi huku mtangulizi wako akiona na kufuatilia.”
Mbali na mitazamo hiyo, wengine wamedhani kuwa uamuzi wa Papa Benedict XVI unalenga kudumisha utamaduni wa watangulizi wake.


“Ninashangazwa kuona Papa Benedict XVI akiendelea kuitwa mbarikiwa na kuvaa nguo nyeupe,” anasema Padri James Martin, Mtawa wa Jesuit pia mwandishi na mhariri, lakini baadaye anajirudi na kusema:
“Lakini sioni ajabu, mbona marais wastaafu wa Marekani, bado wanaitwa Rais? ni alama ya heshima kwake.”


Katika mkanganyiko huo, wapo wanaoamini kwamba yanayotokea yanatokana na nguvu ya roho mtakatifu, huku wengine wakipiga upatu kwamba ni zamu ya Afrika kutoa Papa na wanatajwa Makardinali Peter Turkson wa Ghana na Francis Arinze wa Nigeria.

Mtanzania apewa uwaziri Rwanda

Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na

RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.


Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.


Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na Menejimenti ya Maafa) na Oda Gasinzigwa (Ofisi ya Waziri Mkuu- Familia na Jinsia).


Akizungumza kwa simu na mwandishi wetu jana, mdogo wa Profesa Rwakabamba, Timothy Rwamushaija anayeishi Dar es Salaam, alisema ndugu yake alizaliwa katika Kijiji cha Bushagara, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.


Alisema Profesa Rwakabamba alikuwa Mtanzania aliyeamua kuchukua uraia wa Rwanda na wote baba yao ni Mzee Titus Rwamushaija... “Huyu ni kaka yangu wa tumbo moja na kwa kweli tumefurahi sana kwa mafanikio yake sisi kama wanafamilia.”


Naibu Makamu Mkuu - Taaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Profesa Makenya Maboko alisema Profesa Rwakabamba alifanya kazi katika chuo hicho na aliondoka akiwa Mkuu wa Kitivo cha Uhandisi.


“Aliondoka wakati Kagame alipoingia madarakani na alikwenda kuongoza Taasisi ya Teknolojia ya Kigali (KIST) kabla ya kwenda katika Chuo Kikuu cha Kigali,” alisema Profesa Maboko.


Msomi huyo alikwenda Rwanda mwaka 1997, baada ya kuombwa na Rais Kagame ambaye alikwenda UDSM kuwaomba baadhi ya wahadhiri kwenda Kigali kufungua chuo kikuu katika taifa lake baada ya kumalizika vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1994.


Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa kwanza wa KIST na kukifanya kuwa miongoni mwa vyuo bora barani Afrika kwa masuala ya teknolojia jambo lililomfurahisha Rais Kagame.


Baada ya mafanikio hayo, Rais Kagame alimteua kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda, Butare ambako pia alijizolea sifa baada ya kusimamia vyema ujenzi wa mabweni kwa wingi na kiongozi huyo alimtunukia uraia wa nchi hiyo kama zawadi.


Hata hivyo, Profesa Rwakabamba atakuwa amelazimika kuukana uraia wa Tanzania kwa kuwa katiba ya nchi hairuhusu uraia wa nchi mbili.
Profesa Rwakabamba alipata elimu ya msingi huko Muleba na akajiunga na Shule ya Sekondari ya Ihungo.


Baada ya hapo, alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds, Uingereza na kupata Shahada ya Uhandisi mwaka 1971 na 1975 alipata Shahada ya Uzamivu katika fani hiyohiyo.


Wednesday 27 February 2013

Pinda: Hatukukosea kuunda tume *Asema lengo ni kubaini kiini cha tatizo


WAZIRI Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, amesema tume iliyoiunda ili kuchunguza matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa Februari 18 mwaka huu, itaanza kazi siku mbili au tatu zijazo.


Bw. Pinda aliyasema hayo Dar es salaam jana wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua ni lini
tume hiyo itaanza kazi na kuongeza kuwa, pamoja na watu
kuipinga, Serikali haikukosea kuiunda ili ifanye uchunguzi
wa kina kubaini kiini cha tatizo.

“Yanayosemwa ni mengi...wapo wanaosema tatizo linajulikana, jambo ambalo si kweli hivyo lazima tume ichunguze ili kujua mkweli na muongo,” alisema Bw. Pinda.

Aliongeza kuwa, tume hiyo pia itachunguza maeneo mengine
yenye utata mkubwa ili kuona jambo hilo halitokei tena.

Hivi karibuni, Bw. Pinda aliunda tume itakayochunguza sababu
ya matokeo mabaya kwa wanafunzi wengi waliofanya mtihani
wa kidato cha nne mwaka 2012.

Asilimia 60 ya wanafunzi waliofanya mtihani huo walipata sifuri ambapo tume hiyo itajumuisha Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi, Chama cha Walimu nchini (CWT), Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii na Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari nchin

Waziri Muhongo akataa chakula hotelini aenda kwa mamalishe



Nipelekeni mahali nitakapopata chakula cha Kitanzania, ili tuwe sawa na Watanzania wenye hali ya chini kwani hizi fedha tunazokwenda kula huko ni jasho lao.”

Arusha
WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekataa chakula Hoteli ya Mount Meru na kwenda kula chakula cha Mamalishe.
Tukio hilo lililowashangaza watu 13 waliokuwa katika msafara wake lilitokea hivi karibu wakati

Profesa Muhongo alipokwenda Arusha kwenye mkutano wa wataalamu wa umeme wa nchi 11 za Afrika Mashariki, Kati na Kaskazini.

Waziri Muhongo aliandaliwa chakula hotelini hapo, lakini aliwashangaza wenyeji wake ambao ni Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na uongozi wa wizara yake.

Baada ya kufika katika mgahawa wa Pizza Point uliopo katikati ya mji wa Arusha, Waziri Muhongo aliagiza ugali na samaki kwa bei ya Sh7,000.

Tukio la waziri huyo kukataa kula chakula cha usiku katika hoteli hiyo ya kifahari, iliwashangaza hata wafanyakazi wa mgahawa huo baada ya kupata taarifa hiyo.
Ingawa haikufahamika mara moja sababu za waziri huyo kukataa kula katika hoteli hiyo kutokana na kuchukua uamuzi ghafla, lakini taarifa za ndani zinadai hakutaka kutumia fedha za walipa kodi kwa matumizi binafsi.

“Waziri aliandaliwa chakula katika Hoteli ya Mount Meru Arusha na mpaka tunatoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia), ilijulikana tunakwenda kwenye hoteli hiyo lakini chakushangaza alipofika karibu na geti la kuingia hapo, akabadili uamuzi na kuamuru apelekwe mahali atakapopata chakula cha Kitanzania, huku akisema haoni sababu ya kula vyakula vya bei mbaya wakati kuna Watanzania hawana umeme,” alisema ofisa mmoja wa wizara hiyo ambaye hakutaka kutajwa na kumkariri Waziri Muhongo:

“Nipelekeni mahali nitakapopata chakula cha Kitanzania, ili tuwe sawa na Watanzania wenye hali ya chini kwani hizi fedha tunazokwenda kula huko ni jasho lao.”

Hata hivyo, Profesa Muhongo anadaiwa kuruhusu maofisa waliokuwa kwenye msafara wake ambao wangependa kula Mount Meru kuwashusha, ili akitoka kwa mamalishe awapitie kwa sababu kila mtu ana uamuzi wake.

Msafara wa waziri huyo ulikuwa na watu 13 akiwamo Msaidizi wake na Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud ambao wote walilazimika kula chakula katika banda la Pizza Point.

Mmiliki wa mgahawa huo, Grace Lyatuu alisema hakutarajia ujio wa waziri huyo na msafara wake, lakini baada ya kutambua kuwa ni Profesa Muhongo akamshukuru Mungu kwa kumfikisha hapo.

“Kwakweli ilikuwa ni usiku mgumu kwangu, kwani msafara ulikuwa mkubwa na wagafla, sikuwa na uhakika wa kupata vyakula vya kuwatosha lakini baada ya chakula kupatikana nikamshukuru Mungu kwani ilikuwa ni usiku na tulikuwa na maandalizi ya kufunga mgahawa,” alisema Lyatuu.

Profesa Muhongo alitumia Sh100,000 kwa chakula cha watu 13 na vinywaji na kuokoa zaidi ya Sh344,500.

Vigogo 10 wahusishwa mabilioni ya Uswisi


ZITTO ASISITIZA NYARAKA ZIPO, DK HOSEAH NDIYE ANAYEZIZUIA

VIGOGO 10 wametajwa kuhusika katika kashfa ya kuficha Sh303.7 bilioni katika benki mbalimbali nchini Uswisi.
Katika orodha hiyo inadaiwa kuwa yupo kiongozi mmoja mwandamizi mstaafu, maofisa watatu wastaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), mawaziri wastaafu ambao baadhi yao bado ni wabunge na aliyewahi kuwa kiongozi mwandamizi wa Benki Kuu Tanzania (BoT).
Majina hayo ambayo mwandishi wetu amefanikiwa kuyaona, yamo katika orodha ya mchunguzi mmoja wa kimataifa wa masuala ya ufisadi (jina tunalo).
Juzi, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alimshukia Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah akimtuhumu kuandika barua Uswisi akisema Tanzania haina masilahi na mabilioni ya fedha yaliyofichwa katika benki zilizopo nchini humo. Hata hivyo, Dk Hoseah alikanusha madai hayo akisema hajawahi kufanya hivyo.
Akizungumza jana Zitto alisisitiza kauli yake akisema: “Sijawahi kumsema Dk Hoseah kwa lolote, kwa nini leo nimsingizie? Yeye mwenyewe anajua ushirikiano niliompa wakati wabunge wanapinga yeye asichunguze malipo ya posho mara mbili kwa wabunge.”
“Nilisimama kidete kusema Takukuru wapo sahihi na mimi nilikwenda mwenyewe kwao kuhojiwa na kuagiza wajumbe wa kamati yangu (Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma), waende kuhojiwa. Spika aliyestaafu (Samuel Sitta) akaizima kashfa ya wabunge kupokea posho mara mbilimbili. Mwulizeni amesahau? Sasa leo nimzushie ili iwe nini?.”
Alisema orodha ya Watanzania wenye fedha huko Uswisi, ipo na ameiona na nyaraka zinaweza kutolewa kwa taasisi za Serikali tu.
“Dk Hoseah kazuia nyaraka hizo. Akitaka nimwonyeshe mtu anayeweza kutoa nyaraka hizo, nipo tayari isipokuwa aahidi kuiweka wazi,” alisema Zitto.
Alisema katika orodha ambayo Waziri wa Fedha wa Ufaransa anayo, kuna Watanzania lakini akaituhumu Serikali akisema haitaki kufuata njia halali za kupata orodha hiyo kwa kuwa viongozi wengi na wafanyabiashara wakubwa wana akaunti katika benki za Uswisi.
Juni 26, mwaka huu gazeti hili lilichapisha habari kuhusu utoroshwaji wa fedha hizo na kueleza kuwa Polisi wa Kimataifa (Interpol) nchini kwa kushirikiana na Takukuru inachunguza suala hilo.
Kiasi hicho cha fedha kimedaiwa kuingizwa katika akaunti za Watanzania na kampuni moja ya uchimbaji mafuta na kampuni kadhaa za uchimbaji madini ambazo zinafanya kazi Tanzania.
Chanzo hicho kiliongeza kwamba kiasi hicho cha fedha kipo katika akaunti sita tofauti zinazomilikiwa na Watanzania wakiwamo wanasiasa wakubwa.
Hata hivyo, chanzo hicho kilieleza kuwa tangu akaunti hizo zifunguliwe, wamiliki wake halali hawajawahi kuingiza hata shilingi.
“Uchunguzi wetu unaonyesha kuwa fedha hizo zipo katika akaunti sita tofauti ambazo zinamilikiwa na wanasiasa wakubwa nchini na wenzetu wa Uswisi wameeleza fedha hizo zimeingizwa na kampuni kadhaa ambazo zinahusika na mafuta pamoja na madini hapa nchini,” kilidokeza chanzo hicho.
Kugundulika kwa kiasi hicho cha fedha katika benki za Uswisi ni kutokana na ripoti ya Benki ya Taifa ya Uswisi (SNB) iliyotolewa mwaka huu.

Urais 2015: Utafiti wa Synovate wapondwa,wadau wadai una ajenda ya siri: Huko tuseme ni kuiogopa Cadema??




BAADHI ya wasomi nchini wameuponda utafiti uliofanywa na Shirika la Synovate huku miongoni mwao wakienda mbali zaidi kwa kusema: “Ulikuwa na ajenda ya siri.”


Utafiti huo pia umepondwa na wanasiasa akiwamo Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ambaye amesema haziamini tafiti zinazotolewa na Syonovate akidai hazina ukweli wowote.


Licha ya matokeo ya utafiti huo wa Desemba mwaka jana kuonyesha kushuka kwa asilimia 25 kwa umaarufu wa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa pamoja na chama chake, lakini unaweka wazi kwamba kiongozi huyu angechaguliwa kuwa Rais kama uchaguzi huo ungefanyika sasa.


Dk Slaa anaongoza kwa asilimia 17, akifuatiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.


Katika maoni yao, baadhi ya wasomi kutoka taasisi mbalimbali za elimu ya juu nchini walieleza wasiwasi wao kuhusu usahihi wa matokeo hayo na kuhoji mbinu zilizotumika wakisema inawezekana hazikuwa sahihi.
Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Alexander Makulilo ameuponda akisema haukufuata misingi ya sayansi ya siasa.


Dk Makulilo alisema alifanya utafiti kwa kampuni zinazofanya tafiti kama hizo kati ya mwaka 2010 hadi 2011 na kugundua udhaifu mkubwa katika kampuni hizo.


“Kwanza wanakosea, kwa mfano wanaposema kuwa utafiti huu ni mwendelezo wa ule uliofanyika Desemba 5 hadi 18, 2011. Ukichunguza utakuta data hizo hazipo. Zilizopo ni za Mei 2 hadi 19, 2011.”


“Kwa kawaida uelewa wa wananchi wa vijijini ni mdogo ukilinganisha na mijini kwa sababu mijini kuna vyombo vya habari. Kwa mfano, ukiangalia swali la nani anafaa kuwa Rais, mwaka 2011 walisema Dk Wilbrod Slaa alikuwa na asilimia 42, lakini sasa ana asilimia 17.


Vijijini wengi bado wanaikubali CCM kutokana na uelewa mdogo, iweje Dk Slaa ambaye chama chake hakina wafuasi wengi vijijini ashinde?” alihoji.


“Utafiti wa Synovate una dosari kubwa kisayansi, hauonyeshi tarehe wala wapi umefanyika. Waliohojiwa wameonyeshwa umri wao, lakini hawaelezwi maoni yao kulingana na umri, jinsia, wanatoka vijijini na mijini. Nilipofanya utafiti wangu niliwafuata wakakimbia…” alisema Dk Makulilo.


Mhadhiri mwingine wa UDSM, Profesa Gaudence Mpangala alisema nyakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu, tafiti nyingi hufanyika zikiwa na malengo ya kubeba watu au chama fulani.


Hata hivyo, alisema kilichofanywa na Synovate ni utafiti hivyo kwa kuwa yeye hajafanya utafiti ni vigumu kuupinga moja kwa moja... “Ila kwa mtizamo wa kawaida unatia shaka.”

Alisema kitendo cha utafiti huo kuonyesha kuwa CCM inakubalika zaidi kuliko Chadema kwa sababu kwa siku za karibuni chama hicho kimekuwa kikizungumzia zaidi mambo ya kitaifa, pia kunampa shaka.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (Sua), Dk Clavery Tungaraza alisema tafiti zinazofanywa na Synovate ni mara nyingi matokeo yake huwa hayaakisi uhalisia wa maisha.


Dk Tungaraza alisema utafiti wa Sayansi ya Jamii ndiyo wenye kuaminika zaidi kutokana na kutobadilikabadilika tofauti na tafiti za Synovate ambazo hutegemea mtu aliyehojiwa yuko katika hali gani kwa wakati huo.


Msomi huyo alieleza kushangazwa na tafiti za taasisi hiyo ambazo alidai kuwa mara nyingi hufanywa wakati nchi inapojiandaa kuingia kwenye uchaguzi akisema ingekuwa ni uungwana kama zingekuwa zinafanywa kila mwaka ili kujiridhisha na uhalali wa matokeo yake.


Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (Saut), Baraka Nafari alisema ana shaka na utafiti huo na kudai kwamba inawezekana umefanywa kwa lengo la kumsafisha mtu fulani.


Alisema kwa kawaida matokeo ya utafiti uliofuata kanuni na taratibu zote, unatakiwa mwingine akiufanya mara 100, apate majibu kama yale ya utafiti wa awali mara 95.


“Hiyo inaitwa confidence level, (namna ya kujiaminisha, kuwa na imani na majibu). Kwa mfano, wanasema Watanzania hawaoni kuwa rushwa ni tatizo, wakati ukweli kwetu sisi rushwa ni janga, kuna shirika moja la kimataifa lilitaja nchi zenye rushwa Tanzania ikawa kwenye nafasi za juu sana,” alisema.


Kutokana na hali hiyo, alisema utafiti huo unaonekana kama chumba maalumu cha kuwasafisha baadhi ya watu na vyama vyao badala ya kusimamia kwenye ukweli... “Nautilia shaka kama uliandikwa kwa kuzingatia vigezo na siyo kwa lengo mahususi.”


Mhadhiri wa Chuo cha Mipango Dodoma, Dk Mark Msaki alisema kinachomtatiza ni kutoainishwa njia zilizotumika katika kufanya utafiti huo.


“Sikatai wala kukubali utafiti huu, lakini kwa kuwa ni jukumu la taasisi hizo kufanya tafiti nchini, zitekeleze hayo kwa kuzingatia haki kwa Watanzania wote na si vinginevyo,” alisema.


Dk Msaki pia alisema haridhishwi na taasisi za kisayansi kujikita katika kutafiti nani ana nafasi gani katika kupata urais wa Tanzania, huku nchi ikikabiliwa na changamoto nyingi zinazogusa moja kwa moja maendeleo ya jamii.


Alisema anaamini kuwa kitendo cha taasisi hizo kuibuka na tafiti zinazohusu urais, huku Uchaguzi Mkuu ukiwa bado takriban miaka miwili, ni ishara taasisi hizo kuhusika moja kwa moja katika kugeuza siasa ya Tanzania mchezo wa mpira wa miguu.

Wanasiasa wang’aka
Profesa Lipumba alisema: “Kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, Synovate walitoa utafiti ulioonyesha kwamba asilimia 94 ya Watanzania wako tayari kupiga kura lakini baadaye Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) ilitoa takwimu zake zilizoonyesha kuwa waliopiga kura walikuwa asilimia 42 tu.”


“Inawezekana hata hao waliotoa utafiti huo wakawa wanamtengenezea mtu fulani njia tu kwa mtindo wa kumpigia debe, binafsi siwaamini hasa baada ya makosa yale ya mwaka 2010.”
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika alisema matokeo ya utafiti huo yanaacha maswali kwani hakuna maelezo yaliyotolewa kuhusu methodolojia na sampuli iliyotumika.
Alisema matokeo ya utafiti huo yanakinzana na ripoti nyingine za mwaka wa 2012 hasa ule wa Economic Intelligence Unit ambao unaonyesha kuwa Chadema kinazidi kupanda.


Katibu Mkuu wa NCCR Mageuzi, Sam Ruhuza alisema kati ya vinara tisa wa urais waliotajwa, hakuna hata mmoja anayeweza kuwa Rais wa Tanzania na kuongeza kuwa ushahidi wa hilo ni huko kupanda na kushuka kwa umaarufu wao kisiasa.


“Huko kushuka na kupanda, ni ishara kuwa hakuna Rais kati ya hao, haiwezekani mtu anayependwa na kuungwa mkono aporomoke kutoka asilimia 42 mpaka 17 na huu ni mwaka mmoja tu. Ikipita miaka miwili si wengine watabaki na asilimia moja au sifuri?”



RAILA ODINGA AMBWAGA UHURU KINYATTA KURA ZA MAONI

tr" style="text-align: left;" trbidi="on">

Matokeo ya utafiti wa Consumer Insight yanaonyesha kuwa Odinga hivi sasa anaungwa mkono na asilimia 46.8 ya wapigakura dhidi ya mwenzake, Kenyatta aliyepata asilimia 42.9. Mashabiki wa Mudavadi wamepungua kutoka asilimia 5.4 hadi 4.2.

WAGOMBEA urais wanaochuana vikali Kenya, Raila Odinga wa Muungano wa Cord na Uhuru Kenyatta wa Jubilee, wameendelea kukabana koo ikiwa ni siku tano kabla ya Uchaguzi Mkuu Jumatatu ijayo.

Tafiti tatu tofauti zilizodhaminiwa na Nation Media Group (NMG), ambazo matokeo yake yametoka jana, zimeonyesha kuwa wagombea hao wanatofautiana kwa asilimia zisizozidi 1.5, hali inayoonyesha kuwa lolote linaweza kutokea siku ya uchaguzi. Hata hivyo, Odinga ana nafasi zaidi katika uchaguzi wa marudio.

Matokeo yote hayo yamebainisha kuwa hakutakuwa na mshindi wa moja kwa moja, kwa kuwa wote hawatafikisha nusu ya kura zinazohitajika, huku utafiti ukibainisha kuwa katika mzunguko wa pili utakaofanyika ndani ya wiki tatu tangu kufanyika kwa uchaguzi wa awali, Odinga ana nafasi kubwa ya kushinda.

Matokeo ya Pollster Infotrack
Utafiti wa Kampuni ya Pollster Infotrack, unaonyesha kuwa kama uchaguzi ungefanyika leo, Odinga angeongoza kwa asilimia 46, Kenyatta angefuatia akiwa na asilimia 44.6, huku mgombea wa Amani, Musalia Mudavadi akiwafuata kwa mbali baada ya kupata asilimia 4.3.

Kwa mujibu wa matokeo hayo ya kura za mwisho za maoni, wote wawili, Odinga na Kenyatta wameongeza kura kwa asilimia moja kila mmoja, ikilinganishwa na matokeo ya wiki iliyopita.
Kwa mujibu wa sheria za Kenya, si ruhusa kufanya wala kuchapisha kura za maoni siku tano kabla ya uchaguzi.

Kulingana na matokeo ya Infotrack Poll, Odinga anatazamiwa kushinda matokeo ya mzunguko wa pili kwa asilimia 49.2 huku mwenzake akiwa na asilimia 47.2.

Utafiti huo unaonyesha kuwa nusu ya wapiga kura wa Mudavadi watahamia kwa Odinga wakati Kenyatta atapata wale waliowapigia kura wagombea wengine, Martha Karua wa Narc, James Ole Kiyiapi (Restore and Build Kenya) na Peter Kenneth (Kenya National Social Congress).
Kwa upande wa makundi ya wagombea, Cord inaongoza kwa kuungwa mkono ikiwa na asilimia 45.8 ikifuatiwa na Jubilee (45.6%) na Amani ya Mudavadi ikiwa na asilimia 4.4.

Utafiti wa Consumer Insight
Matokeo ya utafiti wa Consumer Insight yanaonyesha kuwa Odinga hivi sasa anaungwa mkono na asilimia 46.8 ya wapigakura dhidi ya mwenzake, Kenyatta aliyepata asilimia 42.9. Mashabiki wa Mudavadi wamepungua kutoka asilimia 5.4 hadi 4.2.

Kampuni ya Consumer Insight imebaini kuwa iwapo uchaguzi utakwenda hadi marudio, Odinga atatangazwa mshindi kwa kufikisha asilimia 50.6 dhidi ya Kenyatta mwenye asilimia 46.3.
Utafiti huo wa Consumer Insight unaonyesha kuwa umaarufu wa Cord uko asilimia 47.8 wakati ule wa Jubilee ni asilimia 44.1.

Utafiti wa Strategic Pollster
Utafiti wa Strategic Pollster unaonyesha kuwa Odinga ataibuka mshindi kwa kupata asilimia 45.7 dhidi ya Kenyetta mwenye 43.8. Mudavadi bado ni wa tatu akiwa na asilimia 5.7.

Katika uchaguzi wa marudio, Strategic Pollster inasema Odinga ataibuka kidedea kwa asilimia 51.7 huku mwenzake Kenyetta akisimama kwenye asilimia 45.7.
Tafiti hizi zimetumia sampuli ya watu 2,600 wanaowakilisha wananchi 14,337,399 waliojiandikisha kupiga kura.

Wagombea urais walichuana vikali kwa mara ya pili juzi katika mdahalo, ambao ulikuwa fursa ya mwisho kupimwa na wapiga kura kabla ya uchaguzi utakaofanyika Jumatatu ijayo.
Kivuitu afariki dunia
Wakati huohuo, aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kenya (ECK), Jaji Samuel Kivuitu amefariki dunia, siku tano kabla ya Uchaguzi Mkuu.

Kivuitu (74) alifariki dunia saa nne usiku wa kuamkia jana katika Hospitali ya MP Shah ya Nairobi alikokuwa amepelekwa kutokana na mshtuko wa moyo.

Kivuitu anakumbukwa na mambo mawili makubwa na Watanzania. Matukio ya Uchaguzi Mkuu wa Kenya mwaka 2007 na pia kusoma Tanzania.

Alizua balaa Kenya baada ya kumtangaza katika mazingira ya kutatanisha Mwai Kibaki kama mshindi wa urais mwaka 2007 na kuzua vurugu za kikabila kutokana na mpinzani wake n Raila Odinga kuamini alipokonywa ushindi.

Alikuwa mmoja wa wanafunzi wa kwanza kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1961 na kumaliza mwaka 1965, akiwa katika Kitivo cha Sheria.

Familia ya marehemu Kivuitu imesema mazishi yatasubiri hadi Uchaguzi Mkuu umalizike Machi 4, mwaka huu

TCRA yafungia vituo viwili vya redio nchini

Felix
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano(TRCA)Walter Bugoya akitoa tamko la kuzifungia Redio Imani na Redio Kwa Neema kwa kipindi cha miezi 6 kutokana kutangaza matangazo yanayodaiwa kuwa ya kichochezi jijini Dar es Salaam jana.Kushoto ni Mkurungenzi wa Idara ya Habrio Maelezo Arthur Mwambene na Kaimu Mkurugenzi wav Utangazaji wa (TRCA)Andrew Kisaka.Picha na Fidellis
KAMATI ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa adhabu ya kuvifungia muda wa miezi sita vituo viwili vya redio za dini, Imani na Kwa Neema kwa kile kilichoelezwa ni kuendesha vipindi vya uchochezi.

Vilevile kamati hiyo imetoa adhabu ya faini ya Sh5 milioni kwa Kituo cha redio cha Clouds FM baada ya kubainika pia kukiuka taratibu za utangazaji kwa kurusha hewani kipindi kilichotafsiriwa kuwa ni cha uchochezi.


Kamati hiyo ya maudhui ilitangaza adhabu hizo jana jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari ikisisitiza kuwa lengo lao ni kuhakikisha kuwa vyombo vya habari vinazingatia maadili.


Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya TCRA,Walter Bugoya alisema TCRA imefikia hatua hiyo baada ya kuyafanyia uchunguzi wa kina malalamiko yaliyotolewa na wasikilizaji wa vituo hivyo vya redio.


Bugoya alisema redio hiyo ilitangazia wasikilizaji wake wasishiriki kwenye mkakati huo wa Sensa ya Taifa kwa kile walichodai kulingana na imani ya Kiislamu, wasingejua hatima ya mkakati huo.


Kuhusu Redio Kwa Neema inayorusha matangazo yake kutokea Geita, Bugoya alisema ilieneza uchochezi dhidi ya mtafaruku wa kidini uliozuka mkoani humo juu ya upande gani una haki ya kuchinja wanyama kwa ajili ya kitoweo.


Akizungumzia Kituo cha redio cha Clouds, Buyoga alisema kamati imeitaka kulipa fidia ya Sh5 milioni baada ya kubainika kuwa nacho kilienda kinyume cha maadili ya utangazaji kupitia kipindi chake cha Power Break Fast, cha Jicho la Ng’ombe walitoa kauli za uchochezi.

Tuesday 26 February 2013

HILI SUALA LA UDINI LITATUFIKISHA WAPI NDUGU WATANZANIA?


HAKI YA KUCHINJA Waislamu, Wakristo wapigana mapanga *Mchungaji auawa kinyama, saba wajeruhiwa *Kisa ng'ombe, mbuzi waliochinjwa na Mkristo

SAKALA la nani mwenye haki ya kuchinja kati ya Wakristo na Waislamu, jana lilichukua sura mpya katika Kijiji cha Buselesele, Wilaya ya Chato, mkoani Geita baada ya kutokea vurugu kubwa
na kusababisha mauaji ya Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste,
Mathayo Kachila (48) na watu wengine saba kujeruhiwa.

Vurugu hizo zilitokea jana kijijini hapo kuanzia saa tatu asubuhi katika Soko Kuu la Buselesele, baada ya mtu mmoja ambaye inadaiwa ni Mkristo, kuchinja ngombe mmoja, mbuzi wawili.

Inadaiwa kuwa, Mchungaji Kachila alishambuliwa na kundi la Waislamu jirani na msikiti wakati akiwasindikiza wageni wake
baada ya vurugu hizo kupamba moto.

Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Paul Kasagabo, alithibitisha taarifa za kifo hicho na kuongeza kuwa, watu wengine saba walijeruhiwa vibaya kutokana na vurugu hizo.

“Chanzo cha vurugu ni mwananchi mmoja ambaye inadaiwa ni Mkristo aliyefahamika kwa jina moja la Obadia, kuchinja ngo'mbe mmoja, mbuzi wawili na nyama hizo kuuzwa katika bucha ambayo nje ilifungwa kitambaa chenye ujumbe unaosema 'Yesu tena bucha', ambayo anaimiliki hivyo hali hiyo iliwachukiza Waislamu.

“Katika vurugu hizi, bucha ya mtu anayelalamikiwa ilivunjwa pamoja na dula lililokuwa likitoa huduma ya M-Pesa na mwili
wa Mchungaji Kachila umehifadhiwa katika Hospitali ya
Wilaya ya Geita,” alisema.

Kamanda Kasagabo aliongeza kuwa, hadi sasa hakuna mtu ambaye amekamatwa kutokana na vurugu hizo ila jeshi hilo linaendelea kuwasaka wahusika ili waweze kufikishwa mahakamani.

Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dkt. Ernest Nkwabi, alithibitisha kupokelewa kwa mwili wa Mchungaji huyo hospitalini hapo na majeruhi saba.

“Tumepokea mwili mmoja wa marehemu na majeruhi saba ambao kati yao, wawili wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza kwa matibabu zaidi kutokana na hali zao kuwa mbaya.

“Mwili wa marehemu una majeraha ya kukatwa na panga mara nne kichwani, mkono wa kushoto na kiganga chake chote kukatwa katwa hivyo kusababisha avuje damu nyingi,” alisema.

Aliwataja majeruhi waliopelekwa Hospitali ya Bugando kuwa ni Ramadhan Paschal (36), aliyejeruhiwa vibaya katika fuvu la kichwa upande wa mbele na Said Ntamopagafe (47) ambaye amejeruhiwa mguu wa kulia kwa kukatwa mapanga.

Alisema majeruhi wawili Vicent Raymond (18) na Yassin Rajab (56), bado wamelazwa hospitalini hapo wakiendelea na matibabu
na wengine wawili walitibiwa na kuruhusiwa.

Mkuu wa Wilaya ya Chato, Rodrick Mpogolo, alisema vurugu hizo zimedhibitiwa kijijini hapo na hali ya utulivu kurudi kama kawaida ambapo wananchi wanaendelea na shughuli zao bila hofu yoyote.
Share on linkedin Share on facebook Share on twitter Share on email More Sharing Services 0

CHADEMA wambana JK tatizo la udini


MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA), ambaye pia ni Mbunge wa Mpanda Mjini, Bw. Said Arfi, ameitaka Serikali iwaeleze Watanzania kwanini inafumbia mambo tatizo la udini linaloendelea nchini.


Bw. Arfi aliyasema hayo mjini Dodoma jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Mwanga Bar, Kata ya
Uhuru na kusisitiza kuwa, tatizo hilo linaweza kuiweka nchi
mahali pabaya kwa siku za usoni.

Alisema Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali yake, bado haijachukua hatua zozote ili kuepusha machafuko yanayoweza
kutokea na kusababisha amani iliyopo kuwa historia.

“Awali Chama cha Wananchi CUF kilionekana cha Waislamu hivyo Wakristo wakakiogopa na kukimbia udini...hivi sasa CCM inadai CHADEMA ni chama cha Wakristo.

“Kutokana na propaganda hizi, tayari yameanza kutokea machafuko ambayo Wakristo na Waislamu wanapigana mapanga, tunamtaka Rais Kikwete alieleze Taifa kwanini chama chake kinasimamia
zaidi masuala ya udini,” alisema Bw. Arfi.


Aliongeza kuwa, baada ya mbinu za CCM kudai CHADEMA ni chama cha kikabila, sasa wameibuka na mbinu mpya wakidai
chama chao cha Wakristo jambo ambalio si kweli.

Alisema hivi sasa, CCM inatumia mamilioni ya fedha za wananchi katika mambo yasiyo na tija kwa jamii na Taifa badaya ya fedha hizo kuelekezwa katika sekta ya elimu ili kuongeza ufaulu wa
wanafunzi kwa lengo la kuongeza wataalamu.

“Tafiti mbalimbali zilizowahi kufanyika katika sekta ya elimu, zinasema uwekezaji mdogo katika sekta hii imechangia watoto wengi kuanza kidato cha kwanza wakiwa hawajui kusoma
wala kuandika lakini hakuna hatua zilizochukuliwa,” alisema.

Awali Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo wa chama hicho Taifa, Bw. Benson Kigaila, aliwataka viongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kujiuzulu kutokana na matokeo mabaya ya wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka 2012.

Ole wenu mnaoona dini ni bora kuliko Mungu!

CHRISTIANS and Muslims in Tanzania can be partners in building a society shaped by the values taught by God: tolerance, justice, peace and concern for the poorest and the weakest.” Hiyo ni kauli ya kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani wakati huo, Baba Mtakatifu Yohane Paulo II aliyoitoa kwa Watanzania alipozuru nchini Septemba mwaka 1990.

Kwa tafsiri isiyo rasmi, ujumbe huu ulitaka kumaanisha kwamba, “Wakristu na Waislamu wa Tanzania wanaweza kuwa wadau katika kujenga jamii yenye maadili ya Kimungu; uvumilivu, haki, amani na kuwajali maskini na wanyonge.”

Nimelazimika kuanza na nukuu hii ili kuwaonyesha tu wafuasi wa kweli wa dini hizi jinsi walivyo na jukumu kubwa katika kuunda jamii yenye uvumilivu na mshikamano wa dhati ambao ndio msingi wa namna Mungu anavyotaka tuishi.

Kwa ufahamu mdogo nilionao kuhusu Uislamu (ninaweza kusahihishwa katika hili), ni kwamba jina tu lenyewe linamaanisha unyenyekevu na zaidi sana Uislamu ni dini ya amani na ukiwasikiliza baadhi ya wanazuoni wa Kiislamu wanasema Waislamu pia wamefundishwa namna ya kuishi na watu wasio wa dini yao kwa amani.

Na kwa kweli ziko baadhi ya hadithi zinashuhudia kuwa hata Mtume Mohamad (S.A.W) alipata msaada kwa namna moja ama nyingine kutoka kwa Wakristo na watu wengine wasio Waislamu, wakati anahamia Madina toka Makka.

Lakini pia katika Ukristu, upo msingi mmoja mkubwa wa imani yao, wanatakiwa wawapende jirani zao kama nafsi zao na zaidi sana wanatakiwa wawapende hata adui zao kwa sababu upendo ndiyo amri yao kuu.

Yako masimulizi katika Injili kwamba Bwana Yesu aliwaambia wale wote wanaomfuata na kuamini katika yeye kuwa wanaweza kuwa na uwezo hata wa kuhamisha milima, lakini kama wanatindikiwa na upendo ni kazi bure, utaona ni jinsi gani upendo ulivyo sehemu muhimu ya imani hii.

Bahati mbaya tuliyonayo katika jamii yetu kwa sasa, tumeanza kutumia dini hizi badala ya kuwa daraja la kutuunganisha, kutumia tofauti zetu kama njia ya kutuweka pamoja zaidi, sasa tunatumia tofauti za dini zetu kama sababu ya kuwa maadui na kujenga matabaka hasimu katika jamii yetu.

Kipo kitu kimoja ambacho viongozi na wafuasi wa imani hizi wanatakiwa watambue kuwa ni mpango wa Mungu wanayesema wanamwabudu, kutuumba tukiwa tunatofautiana.

Jinsi ambavyo tunatofautiana sura zetu na mawazo yetu ndivyo ambavyo tunatakiwa tutarajie tutatofautiana katika mitazamo ya mambo mbalimbali ikiwemo ya imani. Hili Mungu wanayemwabudu analijua na ndiyo maana kuna mbingu na jehanamu.

Sasa kama Mungu mwenye kuwaumba Binadamu hawa pamoja na uwezo wake wote usio na mipaka, lakini amewaacha binadamu hawa hawa waamue kuishi maisha watakayo kwa utashi wao binadamu mwingine ni nani mpaka atake watu wote waamini kama anavyoamini yeye?

Wataalamu wa elimu ya genetic wanatuambia kuwa ili kuwe na mtu ambaye anafanana na wewe kwa kila kitu, yaani sura, mawazo unayowaza wewe na yeye awaze hivyo na muwe na mtazamo unaofanana kwa kila kitu, ni lazima mzaliwe watoto laki tatu katika familia ya baba mmoja na mama mmoja, mtoto wa laki tatu na moja ndiye atakuwa anafanana kwa kila kitu na yule mzaliwa wa kwanza wa familia hiyo.

Hapa tunaweza kuona ni jinsi gani haiwezekani kutaka kufananisha mitazamo, kwa kuwa ni Mungu pekee na mwenye uwezo wa kila jambo chini na juu ya jua aliyeamua kutuwekea tofauti hizi na sisi hatuna namna wala uwezo wa kufanya vinginevyo, tunachoweza kufanya ni kutaka kuziishi tofauti hizo kwa manufaa yetu na kuifanya Tanzania iwe sehemu nzuri ya kuishi kila mmoja wetu apendavyo bila kuingilia uhuru wa mtu.

Kwa hakika ni uendawazimu na ujinga wa kiimani kutaka au hata kuthubutu tu kuwaza mikakati na mbinu za kuwafanya watu wote wawe Wakristu au Waislamu, hilo halitawezekana kwa sababu ni Mungu aliyedhamiria kutufaya tutofautiane namna hii, hizi tofauti zetu hatukuchagua wenyewe, tumejikuta kwa njia mbalimbali tuna mitazamo hiyo inayokinzana ambayo siyo lazima itufanye tupigane.

Dini hizi ni kama zinataka kuharibu taifa hili kama tu ambavyo dini zimeharibu mataifa mengine mengi yaliyotukuka kwa kuwa na amani na mshikamano na nguvu za kiuchumi.

Madai yanayoendelea sasa ya nani ana haki ya kuchinja kuliko mwingine, yanaweza kuwa ya msingi kulingana na imani za watu na hapa sitaki kuingia katika mtego wa kupuuza imani ya mtu, lakini hivi waumini hawa wamejiuliza ni kwa kiasi gani maisha ya mtu yana thamani kuliko hiyo nyama wanayogombania kuchinja?

Haiwezekani kwamba, Waislamu na Wakristu ambao hawazidi asilimia 50 ya Watanzania wote wanataka ndiyo wawe madereva wa nchi hii, wapo pia Watanzania wenye haki zao ambao wana haki ya kuishi kwa amani na hapa ndiyo wajibu wa Serikali unapoingia.

Katika hiki, Serikali haiwezi kukwepa wajibu wake katika damu za Watanzania zilizomwagika. Kwa sababu ni kweli kwamba, Serikali imetajwa legelege mno katika kusimamia mambo ya msingi ya taifa, hatimaye tumejikuta tunaliingiza taifa katika hali ambayo kama tukipuuzia kuchukua hatua za makusudi kulimaliza hili, tutaingia katika zama ambazo tunaweza tusitoke huko.

Tumeshindwa kuvumiliana kwa sababu ya vibaraka na uzembe wa Serikali kutotambua wajibu wake, ama imeamua kuupuuza kwa makusudi na sijui ni kwa maslahi ya nani.

Ole wetu tusipochukua hatua mujarabu kwa wakati na wananchi na wafuasi wa dini hizi wanaoshabikia mambo kama vile Yanga na Simba, wasifikiri hii ni ngoma ya kitoto.

Nchi hii ikilipuka wote tutakuwemo bila kujali nani anamwabudu nani kwa imani gani.

Yale tuliyozoea kuyaona kwenye mchakato wa Katiba, watu wanagombania kila mtu awe na mamlaka juu ya Katiba dhidi ya wenzao, hili nao lilikuwa Salamu ya jinsi gani tumefika hapa, kila jambo siku hizi tunahitaji kuliangalia kwa jicho la dini kwa manufaa ya dini zetu, hili halitatufikisha siyo tu tuendako kama taifa, bali hata wanaomwamini hawatafika kwa Mungu wao kwa mtindo huu.

Hili hata kwenye haki za kikatiba pia, hatuwezi kuwa waumini safi wa dini zetu kama tunapoandika Katiba kila mtu anataka imtambue yeye zaidi kuliko wengine, wako watoto wa mitaani, hawa wanatakiwa Waislamu na Wakristu wanaokwenda kutoa maoni kwenye Tume ya kuratibu maoni ya Katiba wawatetee.

Wako watoto wadogo wanaodhulumiwa haki, hawa hawawezi kusema kwenye Katiba, wakuwasemea ni sisi Waislamu na Wakristu tunaomjua Mungu kwa sababu Mungu kawaweka hawa katikati yetu ili aone sisi aliotujalia zaidi kuliko wao, tunatumia vipi neema hizo kwa manufaa ya wenzetu wasiojiweza.

Tuzifanye dini zetu ziwe sehemu ya kutupatanisha kwa msingi wa uvumilivu kwa sababu Mungu mwenyewe mwenye dini hizi tunazotumia kumwabudu ni mvumilivu kuliko tunavyoweza kufikiri.

Jaribu kujiuliza wewe unayetaka dini yako tu ndiyo iwe bora kuliko ya wengine, unadai huwezi kuvumilia wenye imani tofauti na wewe, hebu fikiria Mungu angekuwa siyo mvumilivu hata kwa nukta moja.

Wewe kiongozi wa dini unayehamasisha watu wa imani yako wawachukie na wasifungamane na wengine, jiulize kwa siku moja unawaza na kufanya mangapi ambayo Mungu angeamua kukushughulikia hapo hapo ungeweza kudumu kwa muda gani?

Mungu anavyotupenda tumezungukwa na mifano mingi sana ya jinsi dini na tofauti zozote za kijamii zimesababisha machafuko katika nchi za wenzetu, lakini sijui kwanini hatutaki kujifunza.

Migogoro inayozaa vita za kidini au za kikabila huwa inaanza namna hii kwa kukosa uvumilivu miongoni mwa wanajamii, tujue kwamba hata mbuyu ulipoanza kuchipua ardhini ulikuwa mdogo na dhaifu kama mchicha, lakini baada ya muda ukawa ulivyo.

Chokochoko za kidini tunaweza kuziona ndogo na zinafanywa na wapuuzi, hivyo haziwezi kutuletea madhara na mitafaruku katika jamii.

Tutakuwa tunajidanganya, tusipokuwa macho na kuchukua hatua sasa mambo yakishashika kasi sina hakika tutakimbilia wapi, lakini walau nina hakika na jambo moja kwamba, machafuko yakianza hakuna atakayebaki salama, si Muislamu au Mkristo.

Ole wao wanaoziona dini ni bora kuliko Mungu.

Katiba mpya ifute mfumo wa ‘Westminister’ - Kujenga Umoja na Utambulisho wa Kitaifa


WAKATI tunajadili utungaji wa Katiba mpya ya Tanzania, ni vizuri tukatafakari kwanza misingi itakayotuongoza katika kuandaa maudhui ya Katiba hiyo. Katika waraka huu napenda kutoa mawazo machache kuhusiana na suala hilo. Napendekeza misingi ifuatayo:

Kujenga umoja na utambulisho wa kitaifa, Kupanua uhuru na haki za msingi za raia, kupanua demokrasia, kuweka mfumo wa uwazi wa utawala na uongozi na kudhibiti ufisadi, kuimarisha uchumi na uzalishaji, kujenga umoja na ushirikiano wa kikanda na hatimaye umajumui wa Afrika nzima.

Kabla sijajadili misingi hiyo, nizungumzie kidogo suala la mchakato wa kuandaa Katiba. Katiba ni chombo chenye mamlaka juu ya kila mtu na kila chombo katika jamii.

Katiba lazima itawale mamlaka zote kuanzia kwa Rais hadi kwa balozi wa nyumba kumi na kuishia kwa mtu binafsi. Katiba sharti itawale asasi zote kuanzia Bunge hadi mahakama, polisi, asasi za kiraia na kidini, n.k.

Ndiyo maana haifai kwa Katiba kuamuliwa na vyama vya siasa ambavyo ni vikundi vyenye maslahi maalumu ndani ya Katiba hiyo.
Kujenga Umoja na Utambulisho wa Kitaifa
Katiba yoyote ile ya nchi huwa na jukumu la kujenga utaifa na utambulisho wa Taifa linalohusika na hivyo kuchunga na kulinda usalama na uzalendo wa Taifa hilo. Ndiyo maana Katiba za mataifa mengi hutaja mipaka ya nchi, Bendera ya Taifa, Wimbo wa Taifa, Lugha ya/za Taifa na lugha nyingine rasmi kama zipo.

Katiba za baadhi ya nchi hutaja hata hati za maandishi za lugha yao na vipengele muhimu vya utamaduni wa Taifa, kama vile dini, mila na kadhalika. Katiba ya sasa ya Tanzania inataja baadhi ya mambo haya lakini si yote. Kwa mfano haitaji Lugha ya Taifa!

Kujenga utambulisho na utaifa ni pamoja na kujenga umoja wa kitaifa kuweka misingi imara ya umoja inayokubalika kwa wananchi wote wa makundi na matabaka yote, kujenga uzalendo, mapenzi ya nchi na moyo wa kuwa tayari kuitetea na kuifia nchi ikibidi.

Ni wazi kwamba, suala la kuruhusu uraia wa nchi mbili au zaidi ambalo linapigiwa debe sana hivi sasa na baadhi ya watu, inabidi litazamwe kwa kuzingatia msingi huu wa uzalendo na maslahi ya Taifa: Mathalan, itakuwaje iwapo raia wa Marekani (au nchi nyingine), ambaye pia ni raia wa Tanzania, atatumwa na Rais wake wa Marekani na kupewa nyenzo zote kuja kututawala na kutekeleza matakwa ya nchi yake (ya Marekani) hapa kwetu? Utamzuiaje?

Hatusemi kwamba kiongozi asiyekuwa na uraia wa nchi ya kigeni hawezi kutumiwa na nchi hiyo kutekeleza maslahi yake katika nchi anayoiongoza. Tunawafahamu viongozi vibaraka wengi waliotumiwa hivyo. Tunachosema hapa ni kwamba, tusiwarahisishie maadui zetu mchakato wa kupata vibaraka miongoni mwetu.

Suala la utamaduni sharti lipewe uzito kikatiba, maana bila utamaduni hakuna Taifa na njia ya uhakika ya kumdhibiti na kumtawala mtu ni kumteka kitamaduni na kiakili.

Hapa suala la lugha sharti lipewe uzito unaostahiki; Lugha ya Taifa, Kiswahili ipewe nafasi muhimu kikatiba na lugha za kijamii na za kigeni tunazozihitaji zisisahaulike. Katiba itaje wazi kwamba Kiswahili ndiyo lugha ya Taifa na lugha rasmi ya kwanza na Kiingereza ni lugha rasmi ya pili.

Katiba ielekeze kwamba itatungwa sheria mahsusi itakayofafanua nafasi, dhima na matumizi ya lugha ya Taifa na lugha nyinginezo katika jamii.
Kupanua Uhuru na Haki za Raia
Katiba inapaswa kulinda uhuru na haki za raia ambazo ni pamoja na haki za kuishi, kuheshimiwa kama binadamu, kufanya kazi na kupata malipo ya haki kwa kazi hiyo, kupewa pensheni ya uzeeni, kujumuika, kusafiri, kuishi popote, kuabudu au kutokuabudu.

Haki za lugha na utamaduni pia zinahusika hapa. Na haki hizo lazima ziwe ni kwa raia wote bila kujali jinsi, kabila, rangi, dini, cheo, umri au nasaba.

Katiba ya sasa inatoa haki hizo kwa kiasi fulani. Katiba ijayo ingefaa isisitize na kufafanua zaidi haki hizi za msingi.
Kumtaja Mungu katika Katiba
Hapa tunaweza kueleza kuwa pendekezo la Jaji Mstaafu Barnabas Samatta, katika kongamano moja kuwa Katiba mpya itaje Mwenyezi Mungu halikubaliki kwa sababu linakwenda kinyume na uhuru wa kuabudu tunaouzungumzia.

Kwa kuwa Katiba tayari inatoa uhuru wa kuabudu, hakuna sababu ya kuufunga uhuru huo kwa kuuhusisha na imani fulani maalumu, zile zinazozingatia dhana ya Mungu. Ni vyema Katiba iendelee kutofungamana na imani ya dini yoyote.
Kupanua Demokrasia
Katika ulimwengu wa sasa na ujao, utawala wa kidemokrasia hauepukiki. Hivyo tunahitaji Katiba inayotambua haki na haja hiyo ya kujenga na kuimarisha demokrasia. Demokrasia tunayozungumzia hapa ni demokrasia pana inayojumuisha wananchi wote wa makundi yote. Hatuzungumzii demokrasia ya vyama vya siasa tu.

Katiba yetu ya sasa kwa kiasi kikubwa inajikita katika demokrasia ya vyama badala ya demokrasia ya Umma. Labda hili linahitaji ufafanuzi zaidi.

Miaka kadha iliyopita makundi mbalimbali ya wanasiasa, yalianza kufanya kampeni ya kutaka majimbo ya uchaguzi yaongezwe ili kuimarisha uwakilishi na demokrasia.

Tulishuhudia madiwani wa halmashauri mbalimbali, wakipitisha maazimio ya kuongeza majimbo ya udiwani na ubunge. Baadhi ya wabunge na vyama vyao vilevile walipendekeza majimbo mapya yaanzishwe.

Kampeni hiyo ilifanikiwa kwa kiasi fulani na majimbo mapya kadha yaliundwa, japo ilitolewa tahadhari kuwa jengo la sasa la Bunge mjini Dodoma halina nafasi ya kuongeza wabunge wengi. Msingi wa kampeni hii ni dhana potofu kuwa demokrasia maana yake ni kuwa na wawakilishi wengi wa vyama katika Bunge na mabaraza ya madiwani.

Mtazamo huu wa kimajimbo kuhusu uwakilishi unadaiwa kutokana na mfumo wa Westminister, yaani mfumo wa Bunge la Uingereza. Hii ni kweli kwa kiasi fulani tu.

Waingereza wana utaratibu wa uwakilishi wenye historia ya karne nyingi za mapambano ya kitabaka na kikatiba kati ya mamwinyi, mabwanyenye, watwana na wafanyakazi na kati ya ufalme wa England na falme za Wales, Scotland na Ireland, ambazo kwa pamoja zinaunda Ufalme wa Muungano wa Uingereza (UK).

Baada ya miaka mingi ya kupambana na kumwaga damu na baadhi ya viongozi na wafalme kukatwa vichwa, hatimaye Waingereza walikubaliana kuwa na Bunge lenye chemba au mabaraza mawili ili kuzingatia maslahi ya pande zote.

Mabaraza hayo ni lile la Mamwinyi (House of Lords) na lile la Makabwela (House of Commons). Wajumbe wa Baraza la Mamwinyi hawachaguliwi na wananchi na hujumuisha mamwinyi wenye kumiliki ardhi kubwa na viongozi wakuu wa Kanisa la Uingereza. Wajumbe wa Baraza la Makabwela huchaguliwa majimboni.

Mapambano ya kudai demokrasia nchini Uingereza, vilevile yaliibua vyama vikuu viwili, Conservative (chenye kuwakilisha maslahi ya mamwinyi na mabwanyenye) na kile cha Labour (ambacho awali kiliwakilisha maslahi ya matabaka ya wazalishaji wafanyakazi na vibarua.

Siku za karibuni, kimezuka chama kingine kikuu cha tatu, Liberal Democrats, ambacho kimetokana na muungano wa vyama vidogo viwili vya Liberal Party na Social Democratic Party, hicho ni chama cha kiliberali cha mrengo wa kati.

Vipo vyama vingine vidogo vidogo, lakini havina athari kubwa kiutawala. La muhimu kufahamu kuhusu mfumo huu wa Uingereza ni kwamba, vyama vyote vinavyoshika utawala huendeleza takriban sera zilezile za uchumi, utaifa na mambo ya nje na hakuna hata kimoja kwa sasa kinachowakilisha maslahi ya mnyonge.

Jingine la kukumbuka ni kwamba mfalme au malkia wa Uingereza, ni nguzo mojawapo ya Bunge la Uingereza kama alivyo Rais hapa kwetu.

Hivyo, madai ya kwamba Tanzania inafuata mfumo wa Westminister yana walakini maana hayasemi ukweli wote. Hata hivyo, kuna jambo moja la Westminister ambalo Tanzania na nchi nyingi za Jumuiya ya Madola zinaling’ang’ania, nalo ni uwakilishi na utawala kupitia katika vyama.

Huu ni utaratibu ulioletwa kwetu na nchi za Magharibi nasi tukaupokea na kuukubali bila kuusaili. Lakini je, utaratibu huu unahakikisha kuwapo kwa mfumo bora wa uwakilishi wa makundi yote ya wananchi?

Mugyabuso Mulokozi ni Profesa Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Viongozi wapunguze anasa kunusuru maisha ya mama na mtoto

NI Jumatano nyingine tena, tunakutana katika safu yetu ya Jicho la Mtanzania. Jumatano ya leo safu hii itajikita katika suala la afya ya mama na mtoto kwa kuijadili hospitali yetu ya taifa Muhimbili.

Sote tunafahamu kuwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ndiyo hospitali mama katika nchi yetu. Ni hospitali ambayo magonjwa sugu hutibiwa, ina wataalamu waliobobea katika fani mbali mbali za afya pamoja na uwepo wa vifaa vya kisasa.

Binafsi, pamoja na kuwa mkazi wa Jiji la Dar es Salaam kwa muda mrefu, sijawahi kupata nafasi ya kufika katika Hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu bali kusindikiza wagonjwa au kwenda kuona. Mara ya kwanza kufika hospitalini hapo nilimsindikiza rafiki yangu wa karibu aliyekuwa akiuguliwa na mtoto wake mchanga.

Mwanaye huyo, alizaliwa katika hospitali hiyo akiwa hajatimiza umri wa kuzaliwa (pre mature), kutokana na matatizo ya uvimbe tumboni mwa mama yake. Wakati mama wa mtoto anaruhusiwa kurudi nymbani aliambiwa na daktari wake kuwa ataendelea kuhudhuria kliniki chini ya uangalizi wa daktari bingwa wa watoto hapo Muhimbili mpaka daktari wake atakaporidhishwa na maendeleo ya mtoto ndipo atapewa ruhusu ya kuhudhuria kliniki nyingine.

Siku nilifika Muhimbili nikiwa na rafiki yangu, mwanaye alikuwa ameugua ghafla na hivyo kulazimika kuwahishwa hospitalini Muhimbili.

Tukiwa kitengo cha huduma za dharura, mama na mtoto walipokelewa na kuingizwa ndani kwa ajili ya kuonwa na daktari. Tulimsubiri mapokezi kwa takribani saa nne ndiyo akatoka huku akitueleza kuwa mtoto ameandikiwa kulazwa. Ilibidi tena tusubiri kwa karibu saa moja ili gari la kuwapeleka wodini kufika.

Tulipofika wodini tulikutana na daktari wa zamu ambaye naye alichukua maelezo kabla ya mama kuonyeshwa wodi. Baadaye alimwita muuguzi na kumwambia amtafutie kitanda lakini muuguzi baada ya kuzunguka huko na kule alirejea na kueleza hakukuwa na kitanda isipokuwa anaweza kutoa msaada wa kumtafutia kitanda ambacho itabidi atumie na mgonjwa mwingine.

Kitanda kilipopatikana tulimpeleka mtoto na mama yake wodini. Kitanda ambacho alitakiwa kukitumia kilikuwa tayari kina mtoto wa umri kama miaka miwili akiwa amelala na mama yake.

Muuguzi alimwamsha mama aliyekuwa amelala na kumwambia kuwa itabidi atumie kitanda hicho pamoja na mwenziye.

Wakati huo, nilikuwa nikijaribu kuangalia uwezekano wa kitanda kile ambacho ni kidogo kutumiwa na watu wanne. Kimsingi uwezekano ulikuwa mdogo kwani hata huyo mama tuliyemkuta akitumia na mwanaye walikuwa wamelala kwa kujibana.

Mama tuliyemkuta aliamka kwa upendo na kushauri mke wa rafiki yangu amlaze mtoto na wao wakae macho mpaka asubuhi kwa sababu isingewezekana kulala wote kitandani hapo kutokana na udogo wa kitanda.

Moyoni nilisikitishwa na hali ile. Rafiki yangu aliniomba ushauri wa kumuhamisha mgonjwa wetu pale kutokana na mazingira tuliyoyaona na baada ya kujadiliana tulikwenda kumwomba daktari atupe ruhusa na kurudi siku inayofuata asubuhi, jambo ambalo alilikubali baada ya kutazama hali ya mtoto na pia kuangalia mazingira ya pale wodini.

Nilijiuliza maswali mengi, lakini kubwa lilikuwa iwapo Serikali yetu ina dhamira ya dhati ya kupunguza vifo vya akina mama na watoto. Jibu lililonijia haraka ni kwamba pamoja na tatizo la ufinyu wa bajeti ambalo nchi yetu inakabiliana nalo, bado Serikali haijaweza kuonyesha nia ya dhati ya kutokomeza vifo hivi ambavyo vinaweza kuepukika.

Katika mkutano wa wakuu wa nchi za Kiafrika uliofanyika Kampala nchini Uganda mwaka 2010, viongozi wa Afrika walikubali kuongeza uwekezaji kwenye sekta ya afya kwa kupanua wigo wa afya ya mama na mtoto. Raisi Jakaya Kikwete, alitamka kuwa kupunguza vifo vya akina mama na wototo ni kipaumbele namba moja kwa Tanzania.

Lakini takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa vifo vya watoto wachanga bado viko juu. Jumla ya watoto 32 hufa kwa kila watoto 1000 wanaozaliwa wakiwa hai ikiwa na maana kuwa vifo vya watoto wachanga 44,000 hutokea kila mwaka sawa sawa na asilimia 47 ya vifo vyote vya watoto wachanga.

Kimsingi, maisha ya watoto hasa chini ya mwaka mmoja hutegemea sana maisha ya mama zao au kwa lugha nyingine ni kuwa kama mtoto wa chini ya mwaka mmoja atafiwa na mama yake, uwezekano wa yeye kuishi unakuwa ni mdogo na ndiyo maana afya ya mama ina uhusiano wa karibu na ya motto.

Niliwaza mambo mengi kutokana na ile hali niliyoiona pale Muhimbili. Kwanza niliwaza kuwalaza watoto wawili wagonjwa ambao umri wao unapishana sana. Mmoja ana miaka miwili mwingine kwa wakati huo alikuwa hajafikisha hata umri ambao kwa kawaida mtoto anatakiwa kuzaliwa japokuwa tayari alikuwa ameshazaliwa akiwa na karibu mwezi mmoja.

Kwa mujibu wa maelekezo ya daktari wake, mtoto huyo alitakiwa kupata uangalizi wa karibu sana na kuwekwa kwenye mazingira safi na salama bila ya kushikwa au kuonwa na watu tofauti na wazazi wake ambao walishapewa masharti ya kumtunza kwani mwili wake ulikuwa bado ni dhaifu, hivyo ni rahisi kwake kupata magonjwa, lakini siku hiyo alilazwa na mgonjwa mwingine.

Kwa upande mwingine sote tunafahamu kuwa, malaria ni ugonjwa namba moja unaosababisha vifo vya maelfu ya Watanzania kila mwaka. Kina mama wale ambao walikuwa wameamua kukesha wakiwaangalia watoto kutokana na kukosa vitanda vya kulalia, walikuwa kwenye hatari ya kupata malaria kutokana na mbu jambo ambalo siyo tu ni hatari kwa afya zao bali hata kwa afya za watoto wao ambao wanawategemea.

Tukitazama kwa pamoja hii ya Hospitali ya Taifa ikiwa katika hali hiyo, nyingine hali ikoje? Waliopata nafasi ya kutembelea Hospitali za Amana, Mwananyamala na Temeke wanaweza kuwa mashahidi wazuri wa hali mbaya za hospitali hizo.

Haina shaka kwamba, kama viongozi wetu na familia zao wangekuwa wanatibiwa katika hospiali zetu hizi, pengine wangeona umuhimu wa kuboresha hali ya utoaji huduma kwa hospitali hizi.

Mameya wa Jiji na viongozi wengine wa manispaa zetu wanatembelea magari ya gharama aina ya Toyota VX V8. Haya ni magari ya kifahari na yenye gharama kubwa. Fedha hizi zinaweza kujenga wodi kubwa kwa ajili ya akina mama wajawazito pamoja na kuwawekea vitanda na vifaa vingine muhimu.

Hakuna sababu kwa viongozi wetu kutumia magari ya gharama kubwa kama haya kama taifa limekusudia kupunguza vifo vya akina mama na watoto.

Viongozi wetu wakiamua akina mama na watoto wasife kwa kukosa huduma na vifaa tiba inawezekana iwapo watakubali kuachana na anasa walizozikumbatia sasa.

Mulugo: Michango ya CWT hulinda maslahi ya walimu

SERIKALI imesema fedha ambazo walimu huchangia katika Chama cha Walimu Tanzania (CWT), hulinda na kutetea maslahi ya walimu wawapo kazini. Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, aliliambia Bunge jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Kiembesamaki, Waride Bakari Jabu.

“Kwa mujibu wa Sheria namba sita ya mwaka 2004 ya CWT inabainisha wazi kuwa, makato ambayo walimu hukatwa ni kwa ajili ya kulinda na kueteta maslahi wawapo kazini, lakini sheria hiyo haijaelezea mafao ya walimu mara wanapostaafu ama kufariki,” alisema Mulugo.

Aidha, alitoa wito kwa wabunge kuhakikisha wanatoa mapendekezo ya kuwapo kwa mabadiliko ya sheria hiyo na hatimaye walimu hao mara wanapostaafu ama kufariki waweze kupata mafao yao.

Katika swali lake la nyongeza, alitaka kujua walimu wananufaikia vipi pindi wanapostaafu ama kufariki kutokana na wao kuchangia kiasi cha Sh bilioni 2.2 ikiwamo makato ya NSSF kwa kila mwezi.

Alihoji fedha hizo ambazo walimu wanachangia kama zimekuwa zikikaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).

Akijibu swali hilo, Mulugo, alisema CWT hawakaguliwi na CAG bali hukaguliwa na mamlaka ambaye humchagua wao na wala fedha hizo hazikaguliwi na CAG na baada ya ukaguzi wa mtaalamu huyo ripoti zote za fedha zilizokaguliwa hupelekwa kwa Msajili wa Vyama.

Naye, Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Rita Kabati, alitaka maelezo ya Serikali kuhusiana na kuwapo kwa malalamiko toka kwa walimu kutokana na kukatwa asilimia mbili na Hazina wanapoajiriwa.

Akijibu swali hilo, alikiri kuwapo kwa suala hilo na kudai lipo katika Sheria ya CWT ya mwaka 2004 na fedha hizo hukatwa kutokana na chama hicho kufikisha wanachama zaidi ya asilimia 50.

Vyombo vya habari vyashutumiwa kesi ya Lulu


ARAZA la Habari Tanzania (MCT), limevishutumu vyombo vya habari kwa kuandika habari zenye mwelekeo wa kumhukumu msanii Elizabeth Michael, maarufu kama Lulu, kwamba amemuua msanii mwenzake, Steven Kanumba.

Akisoma tamko la Kamati ya Maadili ya MCT Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jaji mstaafu Thomas Mihayo, alisema wamesikitishwa na ukiukwaji mkubwa wa maadili uliojitokeza kwa baadhi ya vyombo vya habari katika kuripoti kuhusu kifo cha msanii, marehemu Kanumba.

Alisema hatua hiyo ni ukiukwaji mkubwa uliovuka mipaka wa maadili ya uandishi wa habari.

Alisema vyombo hivyo vimemhukumu msichana Lulu kuwa amemuua msanii huyo bila kuzingatia kwamba kufanya hivyo ni kosa.

Alisema ukiukwaji huo umejitokeza baada ya msichana huyo kufikishwa mahakamani ambapo baadhi ya magazeti yanayoheshimika katika jamii yaliandika vichwa vya habari vinavyomhukumu moja kwa moja Lulu kama ni muuaji.

“Kwa mujibu wa sheria na maadili ya uandishi wa habari, mtu yeyote anayekamatwa kwa tuhuma yoyote ile ni mtuhumiwa hadi atiwe hatiani na mahakama.

“Kanuni hii ya siku nyingi katika fani ya uandishi wa habari inafahamika kwa waandishi na wahariri wote kujiepusha na habari au vichwa vya habari vinavyohukumu ambavyo vinaonekana kushawishi au kushinikiza uamuzi wa mahakama,” alisema Jaji Mihayo.

Aidha, alionya kesi ya msanii huyo si rahisi kama wengi wanavyofikiri na vyombo vya habari vifanye kazi yake kwa mujibu wa taaluma na viache kuongozwa na taarifa za pembeni, zikiwamo za katika mitandao.

Naye, Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga, aliwataka waandishi wa habari kuchunguza undani wa kifo cha marehemu Kanumba kwa sababu kinaingilia masuala ya unyanyasaji wa kijinsia.

“Nawakumbusha waandishi wenzangu, tuzame zaidi kulitazama suala hili, tukio limetokea kwa utatanishi, habari ya kifo cha Kanumba inaingilia masuala ya kijinsia, maana jamii inalishwa sumu kwamba kuna mmoja ambaye ni malaya na mwingine sivyo, hii si sawa,” alisema Kajubi.

Serikali yafanya kufuru

*Yapandisha mishahara ya vigogo ghafla Waziri Kombani adai imefuata taratibu,Wengine waongezewa Sh milioni moja
SERIKALI imefanya marekebisho ya mishahara kwa watumishi wake kwa mwaka wa fedha 2012/2013. Sambamba na hilo, mishahara ya viongozi wa Serikali kwa mwaka huo wa fedha, nayo imefanyiwa marekebisho.

Marekebisho hayo ni kwa mujibu wa waraka wenye kumbukumbu namba S/AC 205/ 399/ 01/ 44, kutoka Ofisi ya Rais Ikulu (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), uliotolewa Julai 25, mwaka huu.

Waraka huo, umesambazwa kwa wakuu wote wa idara za Serikali, wakurugenzi wa majiji, manispaa, miji na wakurugenzi wa halmashauri zote za wilaya nchini.

Waraka huo, uliosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu (Utumishi), Hab Mkwizu, umehusisha pia marekebisho ya ngazi za mishahara kwa viongozi hao wa Serikali.

Kwa mujibu wa waraka huo, ngazi za mishahara zilizokuwa zinaanzia TGS I hadi TGS Q, zimebadilishwa na sasa zitasomeka LSS (E) 1 hadi LSS (E) 9.

Watumishi na viongozi wa Serikali walionufaika na marekebisho hayo, ni pamoja na makatibu wakuu wa wizara, manaibu wao pamoja na wakurugenzi wa idara zote za Serikali. Marekebisho hayo yameanza kutekelezwa Julai, 2012.

Hata hivyo, marekebisho hayo yamelalamikiwa na baadhi ya watumishi wa Serikali, wakidai kuwa hayana uwiyano unaoeleweka kati ya mishahara ya wamtumishi wa Serikali.

Marekebisho hayo yanaoneshwa katika kiambatanisho namba 1 cha waraka huo, ambapo watumishi na viongozi hao wameongezewa mshahara usiopungua 400,000.

Mfano mshahara wa mtumishi wa ngazi TGS P, umepanda kutoka Sh 3, 216, 000 hadi Sh 4, 500, 000 katika ngazi mpya ya LSS (E) 9, ongezeko ambalo ni zaidi ya Sh milioni moja.

Mmoja wa wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambaye hakutaka jina lake litajwe, alikosoa marekebisho hayo na kusema kuwa, hayana uwiyano mzuri kati ya mshahara wa mtumishi na mtumishi mwingine.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi), Celina Kombani, amekiri kuwapo kwa marekebisho hayo ya mishahara kwa watumishi na viongozi wa Serikali.

Akizungumza na MTANZANIA kwa njia ya simu, Kombani alisema, marekebisho hayo ni ya kawaida na kwamba yanawagusa watumishi wote wa Serikali bila kubagua.

“Serikali ikifanya marekebisho ya mishahara, inafanya hivyo kwa watumishi wake wote. Hatuchagui nani aongezewe nani asiongezewe ni wote,” alisema.

Alisema vigezo vilivyotumika katika marekebisho hayo, ni pamoja na aina ya kazi, uzoefu na muda aliotumia mtumishi kukaa kazini.

“Unauliza kwanini watumishi wengine wamepewa nyongeza kubwa na wengine kidogo, ndugu yangu sifa zinatofautiana, mtumishi anayeanza kazi leo, hawezi kulipwa mshahara na mtumishi aliyepo kazini kwa miaka 20,” alisema.

Alipoulizwa ni sababu zipi zilizoifanya Serikali kurekebisha ngazi ya mshahara kutoka TGS na sasa kutumia ngazi mpya ya LSS, Waziri Kombani alisema. “Hayo ni masuala ya kitaalamu zaidi.”

Kombani alikiri kima cha chini cha mshahara ni kidogo na kueleza kuwa, Serikali ipo katika majadiliano.

“Kima cha chini kilipanda kutoka Sh 130, 000 hadi Sh 170, 000. Tunajua kima hiki hakitoshi lakini tupo katika majadiliano,” alisema.

Chadema waonyesha picha za video alivyouawa Mwangosi



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeonyesha picha za mnato na video zinazoonyesha jinsi Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Television cha Channel Ten, Daudi Mwangosi, alivyouawa.

Picha hizo zilionyeshwa jana jijini Dar es Salaam, wakati wa kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho kilichohudhuriwa pia na waandishi wa habari. Kikao hicho cha Kamati Kuu kilikuwa ni cha dharura na kilifunguliwa na kuongozwa na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe.


Wakati picha hizo zikionyeshwa wazi wazi, viongozi wa CHADEMA na waandishi wa habari, walishindwa kujizuia kwani baadhi yao walijikuta wakiangua vilio wakionyesha kusikitishwa na jinsi Mwangosi alivyouawa.

Katika tukio hilo, Mbowe ni kati ya waliolia na ilifika wakati akanyanyuka kutoka meza kuu na kwenda nje ya ukumbi, ili asiendelee kushuhudia Mwangosi alivyouawa.

Wakati picha hizo zikionyeshwa kwa zaidi ya masaa mawili, askari polisi walioshiriki kumuua Mwangosi walionekana wazi wazi na pia Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, alionekana pia eneo la tukio akishuhudia Mwangosi akiuawa.

Kwa mujibu wa picha hizo, mwandishi wa habari aliyeanza kukamatwa na askari polisi na kupata kipigo ni Godfrey Mushi wa Gazeti la Nipashe.

Picha hizo za video zilionyesha kuwa, baada ya Mushi kukamatwa, Mwangosi alikwenda kumuokoa mwenzake huyo na alipofika eneo la tukio, askari hao walianza kumpiga na hatimaye kumuua mbele ya Kamanda Kamuhanda.

Picha hizo zinaonyesha kuwa, kabla Mwangosi hajauawa, polisi mmoja alipitisha bunduki yake miguuni kwa polisi mwenzake kisha Mwangosi akauawa.

Baada ya tukio hilo, picha hizo zinaonyesha kuwa, baadhi ya askari polisi waliokuwa wakimpa kipigo Marehemu Mwangosi, walikimbia na kuacha mwili wa marehemu ukiwa vipande vipande.

Kwa mujibu wa picha hizo, polisi hao walipokuwa pembeni, wenyewe kwa wenyewe walianza kulaumiana huku baadhi yao wakimlaumu muuaji na kusema umefanya nini hicho?.

Baada ya hapo, mmoja wa polisi hao alisikika akisema twende tukamchukue mwenzetu na walipofika mahali alipokuwa mwenzao ambaye alikuwa amejeruhiwa kwa bomu lililomuua Mwangosi, gari ya Kamanda Kamuhanda ilisogea karibu na kumpakia askari polisi aliyejeruhiwa.

Picha hizo za video ambazo zinaonekana zilirekodiwa kwa umakini wa hali ya juu, zinaonyesha baada ya mauaji hayo, askari walishikwa na butwaa huku baadhi yao wakionekana kushika pua.

Wakati hayo yakiendelea baadhi ya askari ambao ni wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), walionekana katika mkanda huo wa video, wakifungua kofia zao zilizokuwa zimefunika uso na macho yao, ili waone vizuri maiti ya Mwangosi iliyokuwa vipande vipande.

Wakati wakivua kofia hizo, baadhi yao walikuwa wakinawa nyuso zao kutokana na moshi uliokuwa umesambaa eneo la tukio wakati walipokuwa wakiwatawanya wafuasi wa CHADEMA.

Pia picha hizo, zilionyesha askari polisi mmoja akiwa amevaa kiraia, huku shingoni akiwa na skafu ya CHADEMA lakini baada ya vurugu kuanza, askari huyo alionekana akiivua skafu hiyo na kuiweka mfukoni.

Alipoivua na kuiweka katika mfuko wa nyuma wa kaptula aliyokuwa amevaa, mwenzake mmoja akampa kofia ya kujikinga na moshi kisha askari huyo akachomoa bastola kwa ajili ya mapambano.

Pamoja na picha hizo kuwaonyesha askari polisi walivyotekeleza tukio hilo, Kamanda wa Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) wa CHADEMA, Benson Kigaila, alionekana pia akijibizana na ofisa mmoja wa Jeshi la Polisi, Mkoa wa Iringa kuhusu wafuasi wa CHADEMA kuwepo katika Kijiji cha Nyololo kilichopo Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa.

Vile vile, picha hizo za video, awali zilionyesha marehemu Mwangosi alivyokuwa akimuuliza Kamanda Kamuhanda kuhusu sheria ya kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na maswali hayo yalionyesha jinsi kamanda huyo wa polisi alivyokuwa amechukizwa nayo.

Kutokana na picha hizo, Mbowe alisema huo ni ushahidi wa kutosha kuonyesha jinsi Jeshi la Polisi lilivyokuwa limedhamiria kuua.

Kwa mujibu wa Mbowe, CHADEMA itatoa tamko zito leo kuonyesha ni hatua gani zitachukuliwa baada ya kifo cha Mwangosi.

Serikali yamwaga ajira kwa walimu

SERIKALI imetangaza kumwaga ajira mpya za walimu 28,746 katika shule za msingi na sekondari, kuanzia mwezi huu. Hatua hiyo, itapunguza nusu ya ukosefu wa walimu katika shule za Serikali.

Mpaka sasa, Tanzania ina upungufu wa walimu 57,177 katika shule za Serikali, tatizo ambalo Serikali inasema italimaliza katika miaka michache ijayo, kutokana na idadi kubwa ya walimu wanaofundishwa katika vyuo mbalimbali kuhitimu masomo.

Rais Jakaya Kikwete, alitoa kauli hiyo mjini Igunga juzi, ambapo alisema kati ya walimu watakaoajiriwa na kusambazwa, 14,600 watakuwa wa shule za msingi, walimu 14,060 watakuwa wa shule za sekondari na 80 watakuwa walimu wa vyuo vya ualimu.

Akihutubia maelfu ya wananchi wa mjini Igunga kwenye Uwanja wa Barafu, Rais Kikwete alisema mikoa yenye uhaba mkubwa zaidi wa walimu, ndiyo itapewa kipaumbele katika mgawo huo wa walimu.

Mkoa wa Tabora ni moja ya mikoa yenye uhaba mkubwa wa walimu, ikiwa na ukosefu wa walimu 2, 055 na Wilaya ya Igunga pekee inahitaji walimu 285.

Hii itakuwa mara ya pili, Serikali kuajiri na kusambaza idadi kubwa ya walimu wa shule za msingi na sekondari katika jitihada za kumaliza tatizo hilo.

Mwaka juzi, Serikali iliajiri na kusambaza walimu 24,621 ambao kati yao 11,379, walikuwa wa shule za msingi, walimu 13,246, walikuwa wa shule za sekondari na walimu 42 walikuwa ni wa vyuo vya elimu.

Wakati shule za Serikali, zinaendelea kukabiliwa na upungufu wa walimu, shule binafsi zina ziada ya walimu, shule za msingi zikiwa na ziada ya walimu 2, 857 na zile za sekondari zikiwa na ziada ya walimu 459, hali inajionyesha katika matokeo mazuri ya mitihani kwa wanafunzi wa shule hizo.

Rais Kikwete aliwaambia wananchi kuwa Serikali, inakabiliana ipasavyo na matatizo mengine yanayoikabili sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maabara, ukosefu wa nyumba za kutosha za walimu na ukosefu wa vitabu vya wanafunzi.

Pia alizungumzia suala la huduma ya maji, akisema Serikali imeonyesha jitihada za kukabiliana na ukosefu wa maji katika maeneo mbalimbali ya Tanzania.

Kwa upande wa Igunga, Rais Kikwete alisema kufuatia kuzinduliwa kwa mradi wa Maji wa Bulenya, mji wa Igunga na vijiji vitatu vinavyozunguka mji huo sasa vinapata maji kwa asilimia 70.
CWT YAJIBU
Akizungumzia ajira mpya za walimu, Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania, Ezekiel Oluochi, alisema Serikali imefanya jambo la maana, lakini imechelewa kuchukua hatua haraka.

“Naipongeza Serikali, lakini kimsingi natofautina na Serikali katika hili, imechelewa sana kutoa ajira kwani takwimu zinaonyesha kuna upungufu wa walimu 150,000 kwa shule za msingi na 50,000 shule za sekondari.

“Mpaka sasa walimu waliopo ni 234,054, tunahitaji walimu 200,000, kwa maana hiyo walimu waliopo hivi sasa ni asilimia 90,” alisema Oluochi.

Aliitaja mikoa ambayo, inakabiliwa na uhaba wa walimu, kuwa ni Shinyanga, Singida na Arusha katika wilaya za Ngorongoro, Longido na Monduli.

Aliitaja mikoa mingine na wilaya zake kwenye mabano kuwa ni Dodoma (Kondoa), Kagera (Muleba), Mwanza (Ukerewe, Misungwi), Tabora (Uyui, Sikonge na Urambo), Lindi (Kilwa, Nachingwe, Liwale, Ruangwa, Lindi Mjini na Lindi Vijijini).

Alisema mikoa ya Mtwara na Lindi, ina hali mbaya zaidi kuliko mingine Tanzania.

“Sababu kubwa ya mikoa hii kuwa na hali mbaya, inatokana na mazingira magumu wanayokutanayo walimu wapya wanaopangiwa huko.

“Asilimia 12 ya walimu wapya wanaoajiriwa, wanaacha kazi hasa wa shule za msingi na walimu wenye shahada ambao wengi wao wanapelekwa vijijini na kujikuta hawatimizi ndoto zao,” alisema Oluochi.

Alisema kama kweli Serikali imedhamiria kumaliza tatizo hilo, basi kuanzia sasa ihakikishe walimu wapya wote wanalipwa stahiki zao, ikiwa ni pamoja na nauli, posho ya siku saba na fedha za kusafirishia mizigo ya tani moja na nusu, kama sheria inavyotaka.

Monday 25 February 2013

MAUAJI YA PADRI Z'BAR Pengo atoa tamko zito

SIKU moja baada ya Padri Evaristus Mushi wa Kanisa Katoliki la Minara miwili Zanzibar, kuuawa kwa kupigwa risasi tatu kichwani na watu wasiofahamika, Askofu Mkuu wa kanisa hilo Jimbo Kuu
la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo,
ametoa tamko zito kwa Serikali.


Padri Mushi aliuawa juzi asubuhi wakati akishuka katika gari lake
ili kwenda kuongoza ibaada katika Kanisa la Betras ambapo tayari Jeshi la Polisi nchini, limeanza uchunguzi wa kina ili kuhakikisha wahusika wa tukio hilo, wanakamatwa kwa gharama yoyote.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana,
Kardinali Pengo alivitupia lawama vyombo vya ulinzi na usalama
kwa kushindwa kuzuia mifarakano kati ya dini moja na nyingene.

Alisema vyombo hivyo vimeshindwa kusoma alma za nyakati kwani baada ya tukio la kupigwa risasi Padri Ambrose Mkenda wa kanisa hilo Parokia ya Mpendaye, Desemba 24,2012, wafuasi wa Jumuiya ya Uamsho Zanzibar walisambaza vipeperushi vilivyokuwa na ujumbe uliokusudia kufanya jambo kubwa la uhalifu.

“Vipeperushi hivi vilikuwa na ujumbe unaosema, mapambano yataendelea hivyo vyombo vya ulinzi na usalama vilipaswa
kufanya uchunguzi wa kina ili kuzuia ualifu uliopangwa
kufanywa na wafuasi hao.

Aliongeza kuwa, tukio la kuuawa Padri Mushi halikutokea kwa dharura bali vyombo hivyo vilikuwa vinafahamu mkakati wa
jumuiya hiyo lakini bado vilishindwa kuchukua hatua.

“Padri Mushi hakuuawa akiwa baa wala sehemu nyingine tofauti na eneo lake la kazi bali mauaji yamemkuta akiwa kanisani ambako alikwenda kutekeleza jukumu lake la kikzai,” alisema.

Alisema mauaji hayo ni pigo kubwa kwa Taifa ambapo usaalama
wa imani moja ukikosekana kutokana na imani ya dini nyingine
ni tatizo na haijulikani nini kitatokea siku za mbeleni.

Alivitaka vyombo hivyo kuwa makini, kusoma alama za nyakati
ili kuzuia machafuko yanayoendelea yasitokee tena na kuwakata
waumini wa kanisa hilo, kutolipiza kisasi badala yake watulie, kuomba amani na kumuombea Padri Mushi.

Aliwataka Mapadri wengine wa kanisa hilo kuchukua tahadhari
ili kujiepusha na vitendo vya uhalifu dhidi yao na kusisitiza kuwa, umefika wakati wa viongozi wa nchi kulinusuru Taifa lisigawanyike kwa misingi ya imani za dini.

Kardinali Pengo, alisema Februari 24 mwaka huu, kanisa hilo litafanya ibada kubwa Zanzibar na Dar es Salaam kwa ajili ya kumuombea Padri Mushi.

Aliongeza kuwa, vipeperushi vilivyomfikia ambavyo alidai vimesambazwa na wafuasi wa jumuiya hiyo vina ujumbe
unaosema; “Kwa nguvu hizo, tumeweza kuyachoma makanisa
yao na kumtuliza kibaraka wa Kiislamu Soroga, alhamdulillah
hata nje hatoki (laanatullah).

“Lakini nguvu za ushindi mkubwa tulioupata ni huu wa kuwatuliza Makatoriki katika mkesha wao wanaoujua wenyewe (laanatullah), kumkosa Ambrose wa Kanisa la Mpendae, haijawa mwisho wa mapambano, tutahakikisha kila kiongozi wa Makanisa hapa
Zanzibar, hapati nafasi tena ya kuendeleza ujumbe wao”

“Wapenzi Waislamu, viongozi wetu (waliopo mahabusu), wanaendelea vizuri, ipo siku watatoka ishallah kwa nguvu za
allah, jambo kubwa la faraja viongozi wetu waliomo ndani ya Serikali na nje ya nchi, wametuhakikishia huu ndio mwisho wa kusherehekea sherehe za Mapinduzi (laanatullah)”

“Vijana wetu waliokuwa masomoni Somari, wametuhakikishia
kabla ya kusherehekea siku ya kuzaliwa Mtume Mohamed (s.a.w), kutatokeza sherehe nyingine yoyote,” ulisema ujumbe huo.

Katika ujumbe huo, Soroga ambaye ametajwa na wafuasi hao ni Katibu wa Mufti wa Zanzibar na jina lake kamili ni Shekhe Fadhil Soroga ambaye alimwagiwa tindikali na kukimbizwa Dar es Salaam ili kupata matibabu zaidi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kardinali Pengo alisema, kutokana na vyombo hivyo kukosa umakini, ndiyo maana vipeperushi vyenye ujumbe mzito kama
huo, vilisambazwa hadi kumfikia yeye ambaye ni kiongozi wa
ngazi ya juu katika kanisa hilo jambo ambalo kama hatua za
haraka hazitachukuliwa, kutatokea madhara makubwa.

Dkt. Shein ashtushwa

Kutokana na mauaji hayo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein, amepokea msiba
huo kwa mshtuko mkubwa, kutoa pole kwa waumini, ndugu,
jamaa, marafiki na wananchi wote wa Zanzibar.

Akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Dkt. Shein, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Bw. Mohamed Aboud Mohamed, alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga upya kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama na vyengine kutoka nchi za nje ili kuongeza nguvu ya kuwasaka wauaji.

“Zipo kasoro katika Jeshi la Polisi lakini limekuwa likifanya kazi nzuri, nawaomba wananchi mtoe ushirikiano ambao utafanikisha kukamatwa wahalifu wanaofanya matukio mbalimbali.

Alisema kutokana na jiografia ya Zanzibar, kuna maeneo
ambayo watu wanaweza kupitisha silaha lakini Jeshi la Polisi
kwa kushirikiana na Vikosi vya SMZ, litaziba mianya yote.

Bw. Mohamed, alikanusha taarifa zilizopo mitaani kuwa silaha nyingi zipo mikononi mwa wasiostahili kuwa nazo na kuwataka kuondoa hofu waliyonayo kwani hizo ni njama za watu wachache wanaotaka kuiingiza nchi katika machafuko ya kidini.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete na Dkt. Shein hawapendi kusikia vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani vikitokea nchini, kutokana na sababu hizo wameomba
msaada kwa nchi nyengine kuja kufanya uchunguzi wa
kuwabaini wahusika wanaofanya vitendo hivi,” alisema.

Maalim Seif alaani

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amelaani mauaji ya Padri Mushi na kusema kitendo hicho kimevuruga sifa njema ya Zanzibar kuwa kisiwa cha amani.

Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), aliyasema hayo Kisiwani Pemba wakati akifungua semina
ya madiwani wa chama hicho.

Alisema mauaji hayo hayakubaliki kwani Wazanzibari wamekuwa wakiishi kwa kuvumiliana hivyo ni wajibu wao kuendeleza sifa hiyo kwa kuendeleza upendo dhidi yao na kuwapa matumaini wageni wanaokuja kuitembelea Zanzibar kwa shughuli mbalimbali.

Marekani walaani mauaji

Katika hatua nyingine, Serikali ya Marekani imelaani vikali tukio
la mauaji ya Padri Mushi na kutoa salamu za pole kwa ndugu,
jamaa na marafiki wa familia ya marehemu.

Balozi wa Marekani nchini, Bw. Alfonso Lenhardt, aliyasema hayo katika taarifa yake aliyoituma kwa vyombo vya habari na kusisitiza kuwa, nchi yake ipo tayari kushirikiana na Watanzania ili kukomesha matukio ya aina hiyo.

Alisema vurugu za kidini hazipaswi kupewa nafasi Tanzania nchi ambayo inasifika kwa amani na utulivu, umoja na mshikamano
wa Watanzania wote.

“Watanzania mnapaswa kupuuzia vurugu hizi ambazo zinachochewa na watu wachache wenye dhamira ya kusambaratisha amani, utulivu, usalama na taswira ya muonekano bora wa ardhi yenu,” alisema.

Jumuiya ya Maimamu

Nayo Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) imedai kupokea taarifa za mauaji hayo kwa masikitiko makubwa na kulaani kitendo hicho ambacho wamekihusisha na uharamia ili kuitia doa Zanzibar.

Taarifa waliyoitoa kwa vyombo vya habari jana na Katibu wa jumuiya hiyo, Shekhe Juma Muhiddin, imesema Zanzibar ni
kisiwa cha amani na ukarimu tokea enzi na enzi.

Alisema kutokana na mauaji hayo, jumuiya hiyo inawataka Wanzanzibari wote pamoja na dini zote, kuwa watulivu katika
kipindi hiki kigumu, kutunza amani iliyopo na mshikamano
chini ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa.