Saturday 30 March 2013

Odinga akwaa kisiki tena



Nairobi.Mahakama ya Juu ya Kenya imemthibitisha Uhuru Kenyetta kuwa Rais halali mteule wa nchi hiyo pamoja na mgombea mwenza wake, William Ruto.


Mahakama hiyo iliwathibitisha Kenyatta na Ruto jana katika uamuzi wa kesi ya kupinga matokeo uliowapa ushindi katika uchaguzi mkuu uliofanyika Machi 4, 2013, iliyofunguliwa na mpinzani wao mkuu katika kinyang’anyiro hicho, Waziri Mkuu, Raila Odinga.


Odinga katika kesi hiyo aliituhumu Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya nchi hiyo kuwa ilihujumu matokeo ya uchaguzi ili kumpa ushindi, Kenyatta.Hata hivyo, katika uamuzi wake jana Mahakama hiyo ilisema kwamba Kenyatta na Ruto walichaguliwa kihalali katika uchaguzi huo mkuu.

Maaskofu waijia juu Serikali



Dodoma. Wakristo wamesema Serikali ya Rais Jakaya Kikwete imeshindwa kuwasaidia ili waishi kwa amani na utulivu katika nchi yao.


Kauli hiyo ilitolewa jana na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu, wakati akisoma tamko la Maaskofu wa madhehebu ya Kikristo Tanzania katika ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika katika Kanisa lililopo eneo la Jamatini.

Katika tamko hilo alilolisoma kwa niaba ya Maaskofu wote, Kinyunyu alisema kuwa umefika wakati ambao Wakristo wamechoka na vitendo wanavyofanyiwa na baadhi ya waumini wa dini zingine.


“Tatizo ni kuwa Serikali inashindwa kuchukua hatua mapema, makanisa yanachomwa, migogoro inazidi, lakini hakuna hatua zozote ambazo Serikali inachukua katika kunusuru hali hiyo, tumechoka,” alisema.


“ Serikali imeshindwa kuchukua hatua kwa muda mwafaka kwa kila jambo ambalo linatokea kwa Wakristo na hata inapoonyesha kuwa imechukua hatua haionyeshi sana kujali juu ya yale wanayofanyiwa Wakristo. Askofu huyo alisema kuwa matokeo yanayotokea Zanzibar mathalan, Wakristo wanaoishi huko yamewasababishia hofu hivyo wengi kuanza kuvikimbia visiwa hivyo na kukimbilia Tanzania Bara.


Kwa mujibu wa Askofu Kinyunyu, suala la uchomaji wa makanisa hadi sasa limeshindwa kupatiwa ufumbuzi na kila kukicha bado makanisa yanaendelea kuchomwa moto akahoji Serikali kukaa kimya maana yake nini.

Aidha, tamko hilo limeitaka Serikali kuweka utaratibu mzuri na ufafanuzi wa kina kuhusu uchinjaji wa nyama ambao umekuwa ni tatizo kubwa hapa nchini. “Hapa litolewe tamko kila mtu kwa imani yake achinje mwenyewe siyo kuanza kulaumiana au kumpa haki mmoja akachinja na mwingine akaachwa. Tunaomba sana ufafanuzi wa kina juu ya suala hilo ili kuondoa mgogoro baina yetu na wenzetu.”
wamekuwa wakifanyiwa, lakini akasisitiza kuwa wanatakiwa kupigana kwa maombi na ndiyo silaha kubwa ya ushindi.


Katika hatua nyingine, wakati Wakristo wakiwa na hofu ya kusherehekea Sikukuu ya Pasaka watu wasiofahamika wamevamia makanisa matatu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi ya Kaskazini na kuvunja ofisi za wachungaji na wainjilisti.

Serikali yatwishwa zigo migogoro ya kidini nchini


“Baada ya kufa kwa Azimio la Arusha nchi ilipoteza itikadi imara ya kitaifa, kukosekana kwa itikadi hii ndiyo kumesababisha nchi kuongozwa bila kuwa na mfumo unaoeleweka. Mambo hayo ndiyo yanayosababisha migogoro…,” alisema Profesa Mpangala.

lakini walifumbiwa macho na kutochukuliwa hatua yoyote, sasa tabia hiyo imeota mizizi.
Juzi maaskofu hao walitoa tamko hilo katika ibada ya Ijumaa Kuu mjini Dodoma, kusema umefika wakati ambao Wakristo wamechoka na vitendo wanavyofanyiwa na baadhi ya waumini wa dini zingine.


“Tatizo ni kuwa Serikali inashindwa kuchukua hatua mapema, makanisa yanachomwa moto visiwani Zanzibar, migogoro inazidi, lakini hakuna hatua zozote ambazo Serikali inachukua katika kunusuru hali hiyo, tumechoka,” ilisema taarifa ya maaskofu.


Wakati maaskofu hao wakieleza hayo, jana Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum aliliambia Mwananchi Jumapili kwamba Serikali inatakiwa kuwakutanisha masheikh na maaskofu ili kumaliza tofauti zilizopo.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Helen-Kijo Bisimba alisema Serikali ilitakiwa kuchukua hatua miaka mingi iliyopita kwa kuwa mgogoro huu haukuanza leo.


“Migogoro ya kidini ilianza siku nyingi lakini Serikali ilikuwa kimya, wapo watu waliokamatwa kwa tuhuma za kukashifu dini za wenzao lakini hawajachukuliwa hatua yoyote,” alisema Bisimba.


Akizungumzia hali hiyo Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Profesa Gaudence Mpangala alisema migogoro hiyo ilianza kuchipua miaka michache baada ya kufa kwa Azimio la Arusha.


“Baada ya kufa kwa Azimio la Arusha nchi ilipoteza itikadi imara ya kitaifa, kukosekana kwa itikadi hii ndiyo kumesababisha nchi kuongozwa bila kuwa na mfumo unaoeleweka. Mambo hayo ndiyo yanayosababisha migogoro…,” alisema Profesa Mpangala.

Alisema jambo jingine ni kufa kwa Siasa za Ujamaa na Kujitegemea, ongezeko la umaskini na watu kukosa ajira, hivyo kuwa wepesi kushawishika kujiingiza katika migogoro ya kidini.

“Nadhani umefikia wakati wa Serikali kufuata sheria ili kumaliza hali hii, ikiwa ni pamoja na kukutana na pande zenye migogoro,” alisema Mpangala.

Mhadhiri mwingine wa Chuo hicho, Dk Kitila Mkumbo alisema Serikali inatakiwa kufanya mambo mawili ili kumaliza tatizo hilo. Jambo la kwanza ni kuzikutanisha pande zote mbili huku yenyewe ikiwa katikati na kutoegemea upande wowote.


Katika maelezo yake, Sheikh Mussa alisema, “Serikali ndiyo mlinzi wa amani hivyo inatakiwa kuhakikisha inawakutanisha watu wa pande zinazosigana kiitikadi, lakini Watanzania pia tunatakiwa kutambua thamani ya amani yetu hivyo tunatakiwa kuisaidia Serikali katika jambo hili.”

Katika tamko la maaskofu hao lililosomwa na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu alisema, “Serikali imeshindwa kuchukua hatua kwa muda mwafaka, pindi inapotokea migogoro au dini moja kutishiwa amani.”

“Matokeo yanayotokea Zanzibar mathalan, Wakristo wanaoishi huko yamewasababishia hofu, hivyo wengi kuanza kuvikimbia visiwa hivyo na kukimbiliaTanzania Bara.”

Kwa mujibu wa Askofu Kinyunyu, suala la uchomaji wa makanisa hadi sasa limeshindwa kupatiwa ufumbuzi na kila kukicha bado makanisa yanaendelea kuchomwa moto akahoji Serikali kukaa kimya maana yake nini?

Ni simanzi, taharuki zatawala D’Salaam


Zoezi la kutafuta miili iliyokwama katika vifusi inaendelea, zaidi ya maiti 22 zapatikana.
Dar es Salaam. Idadi ya watu waliokufa kutokana na kufukiwa na kifusi cha jengo la ghorofa 16 lililoporomoka juzi asubuhi jijini Dar es Salaam, imefikia 22.


Habari zilizopatikana kutoka eneo la uokoaji na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova zinaeleza kuwa miili iliyopatikana imepelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.


Jengo hilo lililokuwa likijengwa mkabala na Msikiti wa Shia Ithnasheri ulioko Barabara ya Indira Gandhi na Kampuni ya Lucky Construction Limited liliporomoka saa 2.30 asubuhi wakati mafundi na vibarua wakiendelea na ujenzi huku chini watoto wakicheza mpira na mama lishe wakiendelea na biashara zao kama kawaida.

Rais Kikwete
Rais Jakaya Kikwete ambaye jana pia alifika katika eneo la tukio, kama ilivyokuwa juzi, alipata taarifa fupi ya maendeleo ya uokoaji kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, Said Meck Sadik na Kamanda Kova.


Baada ya kupewa taarifa hiyo, Rais Kikwete alimwagiza Kamanda Kova kuhakikisha wahusika wanakamatwa akiwamo Mkadiriaji Majengo (Quantity surveyor), mchora ramani za majengo (Architecturer), Mhandisi Mshauri (Consultant) na Mhandisi wa Jiji la Dar es Salaam. Juzi baada ya kutembelea eneo la tukio, Rais Kikwete aliagiza wahusika wote wa ujenzi huo wachukuliwe hatua kali.


Habari zilizopatikana jana zilidai kuwa Diwani wa Kata ya Goba, Wilaya Kinondoni, Ibrahim Kisoka ambaye ndiye mmiliki wa kampuni ya ujenzi, na Mhandisi Mshauri kwa pamoja wamejisalimisha Kituo Kikuu cha Polisi na hadi saa 8:00 jana mchana walikuwa wakihojiwa.


Awali Kamanda Kova aliwaambia waandishi wa habari kuwa amemtaka mmiliki wa Kampuni ya Lucky Construction Limited ambaye ni Diwani wa Kata ya Goba, Kisoka na wahusika wengine kujisamilisha kituo cha polisi, kabla hawajaamua kutumia nguvu kumtafuta.

Pinda atembelea eneo la tukio
Waziri Mkuu Mizengo Pinda alifika eneo hilo saa 3:41 asubuhi, kujionea hali ilivyo, lakini hakutoa tamko lolote. “Sina la kusema,” alisema Waziri Mkuu alipoulizwa na waandishi wa habari kutoa kauli ya serikali kuhusiana na tukio hilo.


Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi aliyefuatana na Pinda, alisikika akimwagiza Kamanda Kova kuhakikisha mchora ramani wa jengo hilo naye anatiwa nguvuni kwa kuwa jengo hilo lilikuwa la ghorofa 10, lakini likajengwa hadi 16. Mtu mwingine ambaye anatafutwa na jeshi la polisi kukamatwa ni Mhandisi Mshauri.


Lukuvi alimwagiza Kova kuwa watu waliokuwa karibu na jengo jingine la ghorofa 15 lililojengwa na mkandarasi huyo, kuhama mara moja na ubomoaji ufanyike bila kuleta madhara.

Mwenyekiti wa CUF
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba alitumia fursa hiyo kuitaka Serikali kuwabana makandarasi wasio na sifa kwani wanahatarisha maisha ya watu.
“Huu ni uzembe, wahandisi wa jiji walikuwa wapi? Wasimamizi na washauri walikuwa wapi hadi jengo linafikia ghorofa 16?” Alihoji Profesa Lipumba.


Profesa Lipumba aliitaka Bodi ya Makandarasi (CRB) kufuta leseni ya kampuni hiyo, kwani imeonyesha kuwa haiwezi kusimamia ujenzi na hivyo kusababisha vifo.

Huzuni, vilio na simanzi
Vilio na huzuni viliendelea kutanda jana katika eneo hilo ambapo waokoaji walikuwa wakijitahidi kufukua vifusi na kuzingirwa na watu waliokuwa wakisubiri ndugu zao waliofukiwa na kifusi kutolewa.


Watu wengi tangu asubuhi walikuwa wamesimama karibu na eneo hilo huku wengi nyuso zao zikiwa zimegubikwa na simanzi na wengine wakilia. Mama mmoja aliyekuwa akilia mapema asubuhi katika Mtaa wa Mshihiri, alisema mwanawe ni fundi na jana hakurudi, lakini pamoja na kilio, alisema bado haamini kama mwanawe amepoteza maisha.


Mwingine aliyekuwa ameshikiliwa na wenzake, alisikika akisema miongoni mwa waliopotea ni mume wake aliyemuaga asubuhi kuwa anakwenda kibaruani lakini hadi usiku wa manane hakurudi hivyo ilibidi afike eneo hilo.


Mama mwingine wa jamii ya Kihindu aliyekuwa akilia, alizirai kabla ya kuzinduka baada ya kupatiwa huduma ya kwanza. Mama huyo alisema mtoto wake ni miongoni mwa waliokwama kwenye kifusi hicho.

Barabara zafungwa
Mbali ya watu hao barabara zote zinazoingia katika eneo hilo zimefungwa.
Barabara hizo ni Mshihiri na Morogoro, Hazrat Abbas, Mali -Asia, Mali-Zanaki, Mtaa wa Zanaki, India na Indira Ghandhi.

Wachina walishangaa ‘zege’
Wachina wa Kampuni za ujenzi za China zilizopo nchini, Beijing Construction Engineering Group, BCEG iliyojenga Uwanja wa Taifa, na ile ya China Civil Engineering Construction Company (CCECC) inayojipanga kwa ujenzi wa Daraja la Kigamboni, ni miongoni mwa waliofika kusaidia uokoaji.

0
inShare


Mmoja wa Wachina hao alichukua kipande cha zege kilichotoka kwenye jengo hilo, na kukisaga kwa kutumia mkono, kikapukutika.


“Hii mchanga mingi..., hakuna zege kama hii,” alisema Mchina huyo kutoka Kampuni ya CCECC ambaye hata hivyo alikataa kutaja jina lake.
Wachina hao walitoa kijiko ambacho ndicho kilichosaidia kwa kiasi kikubwa katika uokoaji huo.

Huduma za kijamii
Mashirika mbalimbali ya hisani, yalikuwa na kazi ya kuleta vyakula, maji na vitu vingine kwa waokoaji ili kazi iendelee bila kusimama.


Malori ya Kampuni ya Strabag yanayotumika kwa ujenzi wa Barabara ya Morogoro kwa mabasi yaendayo kasi, yalishiriki kikamilifu saa 24 kuzoa kifusi hicho kilichokuwa kimejaa nondo za kila saizi.


Vikosi vya uokoaji pamoja na manesi wa Hospitali ya Mwananyamala, Hospitali ya Ibrahim Hajj na Chama cha Msalaba mwekundu, wameweka kambi wakiwa na dawa, dripu, na vitu mbalimbali vya huduma ya kwanza.

Matukio mengine
Hii ni mara ya pili kwa mwaka huu jengo kuanguka, kwani Februari jengo la ghorofa nne lilianguka maeneo ya Kijitonyama Mpakani jijini Dar es Salaam na kusababisha kifo cha mtoto wa miaka 9.


Licha ya ujenzi wa jengo hilo kusimamishwa miaka 10 iliyopita, familia ya marehemu iliendelea kuishi katika jengo hilo.


Juni 21, 2008 jengo la ghorofa 10 lilikuwa likiendelea kujengwa na Kampuni ya NK Decorators katika Mtaa wa Mtendeni Kisutu jijini Dar es Salaam liliporomoka na kuua mtu mmoja.


Mwaka 2006 jengo la ghorofa lilianguka eneo la Chang’ombe Village Inn na kuua mtu mmoja, baada ya tukio hilo aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, Edward Lowassa aliunda tume kuchunguza tukio hilo ambayo ilibaini kuwa zaidi ya maghorofa 100 jijini Dar es Salaam yalikuwa yamejengwa kinyume na taratibu za ujenzi.

Saturday 23 March 2013

Wanyamapori 15,000 wauawa nchini



Moshi. Zaidi ya wanyamapori 15,220 wameuawa na majangili katika hifadhi mbalimbali zilizopo chini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) katika kipindi cha miaka minne iliyopita wakiwamo tembo 419.


Kutokana na ukubwa wa tatizo hilo, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka alipendekeza kuundwa kwa kamati teule ya Bunge kuchunguza kuimarika kwa mtandao wa ujangili nchini.

“Ni mtandao wa kimafia ambao hata baadhi ya watendaji serikalini wanaujua, lakini wanauogopa sasa. Katika mazingira haya ni vyema Bunge likachunguza ni kina nani hawa ambao wanaogopwa,” alisema.


Kwa mujibu wa Mhifadhi Mkuu wa Tanapa, Mtango Mtahico, baadhi ya wanyama waliouawa kwa ajili ya kitoweo walikaushwa na kusafirishwa nje ya nchi zikiwamo nchi za Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Sudan.


Mtahico alisema katika wanyamapori hao 15,220 waliouawa na majangili kati ya mwaka 2009 na 2012, kwa ajili ya kitoweo wamo nyumbu, mbogo, nyamera, pofu, pundamilia, swala na wanyama wengine.


Mhifadhi huyo alitoa taarifa hiyo juzi katika kikao cha wadau wa uhifadhi Kanda ya Kaskazini kilichohudhuriwa na wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wabunge na wakurugenzi wa halmashauri.


“Ujangili huu wa wanyama ambao unaongezeka nchini unachochewa na mahitaji ya kitoweo na pia mahitaji ya kibiashara kama ya pembe za ndovu na faru duniani”alisema Mhifadhi Mkuu huyo.

Mtahico alisema katika miaka ya hivi karibuni, mitandao ya ujangili imekuwa ikijiimarisha na kutumia silaha za kivita, sumu na nyaya ambazo mpaka sasa hazijulikani zinatoka maeneo gani ya nchi.“Utafiti unaendelea kujua hizi nyaya zinatoka wapi maana zinakamatwa nyingi, lakini hazipungui na hizi hazichagui zikishategeshwa zinaweza kuua hata nyumbu 100 kwa mara moja,” alisema Mtahico.


Akizungumza katika mkutano huo wa siku mbili, mbunge wa Karatu, Israel Natse alilalamikia unyama unaofanywa na askari wa Tanapa wanaodhibidi ujangili akitaka wabadili mtazamo wa utendaji kazi.


“Rangers (askari) ni wanyama mno, vitendo wanavyofanya utadhani ni vitendo vile vilivyokuwa vikifanywa na Makaburu,” alisema Natse akilalamikia pia fidia ndogo kwa watu wanauawa na wanyama.


Kauli hiyo iliungwa mkono pia na mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari ambaye alisema kuna udhalilishaji mkubwa wanaofanyiwa wananchi wanaokutwa wakiwa ndani ya hifadhi hizo.

Xi Jinping kusaini mkataba ujenzi wa Bandari Bagamoyo



Dar es Salaam. Rais wa China, Xi Jinping anatarajiwa kuwasili nchini kesho kwa ziara ya siku moja, ambapo pamoja na mambo mengine atasaini mikataba 17, kati ya nchi hiyo na Tanzania, ukiwamo wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo mkoani Pwani.


Ujenzi huo utakaofanywa na Kampuni ya Merchants Holding ya China, utakwenda sambamba na ujenzi wa barabara inayounganisha bandari hiyo na Reli ya Kati na Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara).


Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisema ujio wa rais huyo aliyechaguliwa wiki mbili zilizopita, utakuwa wa manufaa makubwa kwa Tanzania.


“Mbali na mkataba huo pia tutasaini mikataba wa kidiplomasia. Vilevile, China imefungua soko la Watanzania kuuza tumbaku nchini humo na mkataba wa kuliendeleza Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC),” alisema Membe.


Waziri huyo alisema kiongozi huyo wa China pia atafungua jengo la kisasa la mikutano la Mwalimu Nyerere.


“Kwa kuwa anakuja Afrika kwa mara ya kwanza huku Tanzania ikiwa nchi ya kwanza, Jinping pia atatoa hotuba yake juu ya msimamo wa China kwa Tanzania na Afrika kwa jumla,” alisena Membe.

Waziri Sitta awaanika wabunge wa Afrika Mashariki kuhusu posho




Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amewajibu wabunge wa Afrika Mashariki akisema wengi hawahudhurii vikao vya kupewa mwongozo kuhusu bunge hilo kwa kuwa “wanataka kulipwa posho”.

Kauli hiyo ya Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, imekuja siku moja tangu wabunge hao waichongee wizara hiyo kwa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, kwamba imeshindwa kuwapa mwongozo pale wanapokwenda kwenye vikao vya Bunge la Afrika Mashariki.

Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo jana, Sitta alisema wabunge hao wamekuwa vinara wa kuomba posho kila wanapotakiwa kuhudhuria kwenye mikutano ya wizara yake.

Katika maelezo yake Sitta alimeshutumu Katibu wa Wabunge hao, Shyrose Bhanji kuwa ndiye anayeongoza kwa kutoa udhuru mara kadhaa, hivyo kutoudhuria vikao vinavyoitishwa na wizara hiyo.

“ Wizara imejiwekea utaratibu mzuri wa kukutana na wabunge hao, lakini nafikiri katibu wao ndiye anayeongoza kwa kutohudhuria,” alisema Sitta na kuongeza:

“Nadhani amekuwa na shughuli nyingi sana, tuna utaratibu wa kukutana kila baada ya miezi mitatu, lakini ndiye aliyeongoza pia kutoa malalamiko hayo yasiyo na ukweli.”

Waziri Sitta katika majibu yake alifafanua kwamba wizara hiyo bado haijapewa majukumu rasmi ya kutoa mwongozo kwa wabunge hao.

Mbali na Sitta, naibu wake, Abdullah Juma Saddallah naye alieleza tabia za wabunge hao huku akisisitiza kuwa posho kwao ndiyo jambo la umuhimu zaidi.

Saddallah alisema malalamiko hayo ni ya ajabu na yamewashtua kwa sababu hayana ukweli, lakini wamekuwa wakijikuta kwenye mtihani kwani kuna baadhi ya wabunge hao wakiitwa kuudhuria vikao utambulia kuuliza posho.

“Wizara haina fungu la kuwahudumia wabunge hao, hili limekiwishajadiliwa katika vikao vya kamati vilivyopita na ilikubalika kuwa ofisi ya bunge itaangalia uwezekano wa kuwapatia ofisi na vitendea kazi vingine,” alisema Saddallah.

Alisema pia kabla ya kuteuliwa wabunge hao wizara hiyo kwa kushirikiana na ofisi ya Bunge ilifanya uchambuzi na kuandaa mwongozo utakaowezesha ushirikiano na uwajibikaji baina ya Bunge la Tanzania na wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

“Mwongozo huu umewezesha kuundwa kwa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambayo awali ilitarajiwa kuwa Kamati ya Bunge ya Afrika Mashariki inayotoa nafasi ya kutoa taarifa za utekelezaji na kupata mwongozo,” alisema Naibu Waziri huyo.

Aliongeza kuwa “Wizara kwa kushirikiana na Bunge iliandaa semina kwa wabunge hawa mara baada ya kuteuliwa kwao ili kuwajengea uelewa wao kuhusu jumuiya kabla hawajaanza kazi zao, semina hii ilifanyika Mei 2012,” alisema.

Naibu Waziri huyo alisema katika semina waliyopewa wabunge hao mbala na kutolewa kwa mada mbalimbali kuhusu mfumo wa utendaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki pia wabunge

walipewa vitabu ambavyo vinaonyesha ni taratibu, misingi na hatua za Mtangamano.

Naibu Waziri huyo alibainisha zaidi kuwa wabunge hao wa EALA wamekuwa wakishirikishwa katika shughuli mbalimbali za wizara, akitoa mfano kuwa mwenyekiti wao hualikwa katika uwasilishaji wa hotuba ya Bajeti na uzinduzi wa shuhghuli mbalimbali za wizara hiyo.

Katika madai yake juzi Bhanji alidai kuwa wanashindwa kujadili maslahi ya wananchi katika Bunge la Afrika Mashariki kutokana na kutengwa na wizara, huku mwenzake Abdalah Mwinyi akisema kuwa, mpaka sasa serikali haina sera ya mtangamano ambao utawaweka pamoja wabunge wa Tanzania.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mussa Zungu alisema kamati imeridhika na maelezo yaliyotolewa na wizara hiyo, ikiwa ni pamoja na hatua ambazo imezichukua katika kuhakikisha sera inakuwepo.

Thursday 14 March 2013

SIRKAKA BLOG: Papa mpya apatikana, achagua jina la Francis

SIRKAKA BLOG: Papa mpya apatikana, achagua jina la Francis

Tume ya Mizengo Pinda yaanza kuhoji wanafunzi, walimu


Dar es Salaam. Tume ya Kuchunguza Matokeo ya Kidato cha Nne mwaka 2012, imeanza kazi kwa kuwahoji walimu, wanafunzi na wajumbe wa bodi za shule kuhusu sababu za matokeo mabaya.

Mwenyekiti wa tume hiyo Profesa Sifuni Mchome, alisema jana kwamba shughuli hiyo imeanza katika Kanda ya Dar es Salaam ambapo wajumbe watatembelea shule 12.


“Tumeamua kuzungumza na wanafunzi waliopo shuleni na wale waliofanya mtihani huo watakaopatikana ili kujua ni nini kilichofanya wakapata alama hizo, pia itakuwa njia rahisi ya kupata watu wengi ikiwa ni pamoja na bodi za shule,” alisema Profesa Mchome:
“Kazi kwa Dar es Salaam ilianza Jumatatu na itaisha Ijumaa, kuna shule ambazo zimeainishwa. Tukifika kwenye hizo shule na kama zipo shule zingine jirani tutawaita waje kutoa maoni yao.” alisema.


Profesa Mchome alisema kuwa, ili kufanikisha shughuli hiyo wameteua kanda tano ikiwamo ya Dar es Salaam, Kusini, Mashariki, Kati na Kanda ya Magharibi ambayo itahusisha Mikoa ya Geita na Simiyu.


Profesa Mchome alieleza kuwa, ili kupata maoni ya wananchi wengi wamefungua tovuti inayoitwa www.tumek4.go.tz ili wengine watoe maoni huko.


Alisema kuwa, kanda hizo zimetengwa kwa kuzingatia hadidu za rejea zilizotolewa na Waziri Mkuu, ambapo wamechangua shule zilizofanya vibaya, zilizokuwa na ufaulu wa kati na zilizofanya vizuri ambazo ni zile za Serikali na zisizo za Serikali.


Alisema kuwa, tayari wameshazungumza na maofisa elimu pamoja na Muungano wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (Tahosa).


Alisema kuwa, baada ya kutembelea shule hizo Dar es Salaam, juma lijalo timu hiyo itaenda katika kanda nyingine ambapo zitatembelewa shule 13.


Alisema kuwa, leo ratiba ya shughuli ya tume hiyo itawekwa katika tovuti yao.Profesa mchimo aliwataka wananchi watoe zaidi maoni yao kupitia tovuti hiyo, pamoja na vyombo vya habari ili waweze kukamilisha shughuli hiyo kwa kupata maoni ya watu wengi.


Papa mpya apatikana, achagua jina la Francis


Kardinali Jorge Bergoglio wa Argentina amechaguliwa kuongoza Kanisa Katoliki Duniani, akiwa ni wa kwanza kutoka barani Amerika na wa kwanza kutoka nje ya Ulaya kwa zaidi ya miaka 1,000.

Baada ya kuchaguliwa na makardinali wenzake 115, Kardinali Jorge Bergoglio (76) alichagua kufahamika kwa jina la Francis I.

Maelfu ya mahujaji, watalii na waumini wa Kanisa Katoliki waliokuwa wamejazana katika Viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Petro, Vatican kushuhudia moshi mweupe uliofuka saa 4:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki kuashiria kuchaguliwa kwake, waliripuka kwa shangwe, nderemo na vifijo.

Muda mfupi baada ya moshi huo kutoka, kardinali mmoja alisimama katika ‘varanda’ ya Kanisa la Mtakatifu Petro na kutangaza “Habemus Papum” (tumepata papa mpya).
Papa Francis I alikuwa miongoni mwa waliokuwa wanawania nafasi hiyo na papa anayeondoka, Benedict XVI mwaka 2005, ambapo aliripotiwa kuibuka wa pili.

Kabla ya kuchaguliwa kwake, Papa Francis I ambaye kwa wadhifa wake pia anakwenda kuwa Askofu wa Roma, alikuwa Askofu Mkuu wa Jimbo la Buenos Aires, Argentine na kwa muda wote wa utumishi wa utumishi alikuwa huko huko nyumbani.

Anakuwa Papa wa 266 kuwahi kuongoza kanisa hilo lenye waumini zaidi ya bilioni 1.2 duniani.
Baada ya kutangazwa kwake, Papa Francis I alijitokeza kuzungumza kwa mara ya kwanza kama Askofu wa Roma.

Akiwa amechaguliwa katika awamu ya tano ya upigaji kura, inaelezwa kuwa alikuwa miongoni mwa mapapa waliochaguliwa kwa haraka baada ya muda mrefu, akiwa sawa na Benedict XVI (2005) na Pius XII aliyechaguliwa mwaka 1939.

Mshindi alitakiwa kupata kuta 77 au robo tatu ya makardinali 115 walioshiriki uchaguzi huo.
Papa Francis I anachukua nafasi iliyoachwa na Papa Benedict XVI aliyejiuzulu Februari 28, mwaka huu, ikiwa ni miaka 600 tangu Papa wa mwisho kujiuzulu.

Yeye ni nani
Papa Francis I, ni Papa wa kwanza kutoka Shirika la Jesuit ambaye ametumia muda wake mwingi wa utumishi nyumbani Argentina.

Anafahamika kwa utumishi uliotukuka kwa uangalizi wa kanisa na mapadri, mambo ambayo yanatajwa kuwa sifa kubwa ya kuchaguliwa kuwa Papa.

Papa huyo amedumu katika maisha ya kufundisha na kuongoza mapadri. Amefanya kazi Amerika ya Kusini ambako kuna Wakatoliki wengi. Kardinali Bergoglio anatambulika kwa kutamadunisha Kanisa la Argentina, lililokuwa miongoni mwa makanisa ya kihafidhina huko Amerika Kusini.

Amechagua jina la Papa Francis I, chini ya uangalizi wa Mtakatifu Francis wa Assisi.
Alizaliwa Buenos Aires katika familia ya mfanyakazi wa reli. Alipata upadrisho mwaka 1969.
Aprili 15, 2005, mwanasheria wa haki za binadamu alimfungulia mashtaka ya jinai kwa kushirikiana na maofisa wa jeshi kuwateka mapadri wawili wa Jesuit mwaka 1976, akiwa kiongozi wao aliwafukuza katika utumishi kutokana na migogoro katika jumuiya hiyo.
Msemaji wake alikanusha vikali tuhuma hizo na hakuna uthibitisho uliotolewa kumhusisha na madai hayo.

Kauli yake ya kwanza
Baada ya kutangazwa kuwa Papa wa 266, Kardinali Jorge Bergoglio (76) aliwataka waumini wa Kanisa Katoliki duniani kumwombea.

Papa huyo aliyechagua jina la Francis I, alisema: “Kama mnavyofahamu, kazi ya mkutano wa uchaguzi ilikuwa ni kuchagua Askofu wa Roma,” Francis I aliueleza umati uliokuwa unashangilia katika Viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Petro, huku akiwapungia mikono.

“Ni mimi hapa. Ninadhani makardinali wenzangu wamenichagua mimi kutoka mbali...Niko hapa. Ninapenda kuwashukuru kwa kunipokea.”

Akiwa kardinali alipambana na Serikali ya Argentina chini ya Rais Cristina Fernandez de Kirchner kuhusu msimamo wake dhidi ya ndoa za mashoga na utoaji bure wa huduma za uzazi wa mpango, ambazo zimekuwa zikipingwa na Kanisa Katoliki duniani kote.

Wednesday 13 March 2013

Waislamu waonya kauli za uchochezi




Dar es Salaam. Wakati Kiongozi wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila akitiwa mbaroni kwa tuhuma za uchochezi wa kidini, viongozi wa Jumuiya ya Kiislamu Tanzania wametoa tamko na kusema kuwa baadhi ya kauli za viongozi wa Serikali na viongozi wa dini zina mwelekeo wa kukuza mfarakano wa kidini kuliko kuleta maelewano.

Wiki iliyopita Mchungaji Mtikila alikamatwa mkoani Rukwa akituhumiwa kuwahamasisha Wakristo wawavamie Waislamu.

Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema Mchungaji Mtikila alichochea uhasama kwa kuwaeleza viongozi wa Kikristo kuwa, wamekuwa wakionewa na Waislamu kutokana na matukio yanayoendelea kutokea hapa nchi.

Katika tamko lao, viongozi wa Kiislamu walisema kuwa mara nyingi kauli za viongozi wa dini na Serikali hazina nia njema bali zimekuwa za kibaguzi au za kiupendeleo.

“ Imekuwa ni kawaida kila anaposhambuliwa au kuuawa Padri baadhi ya viongozi wa Serikali, na wale wa Kikristo, vyombo vya habari, baadhi ya asasi na taasisi za kiraia wamekuwa wakiwanyooshea vidole na kuelekeza lawama zao kwa jamii ya Waislamu,” lilisema tamko hilo.

Katika tamko hilo Jumuiya ya Waislamu ilieleza kuwa Waislamu wamekuwa wakinyooshewa vidole kutokana na matukio hayo pasipo kuwa na ushahidi.

Iliongeza kuwa wamekuwa wakishutumiwa kuhusika katika matukio kabla hata ya uchunguzi wa vyombo vya usalama na polisi kufanyika.

Tamko hilo lilisema kuwa serikali kupitia waziri wa mambo ya ndani ilitoa kauli kuwa mauaji ya padri huyo ni matokeo ya kazi za ugaidi.

Tamko hilo lilisisitiza kuwa linaungana na wapenda amani wote kulaani mauaji, manyanyaso na udhalilishaji wa aina yoyote unaowalenga viongozi wa dini.

Jumuiya hiyo imewataka viongozi wa dini na Serikali kuhakikisha wanahimiza amani na mshikamano badala ya kuwa vyanzo vya kuchochea vurugu.

Wamesema hawatafumbia macho tabia ya kuendelea kunyoshewa vidole Waislamu kila linapotokea tukio la uvunjifu wa amani nchini na wamewataka Watazania wote kwa umoja wao kusimamia ushirikiano na kuiimba amani ili kulinusuru taifa na aina yoyote ya vurugu.

Benki Kuu yaingilia kati wizi wa ATM



Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika sekta ya benki nchini.


Kutokana na wizi huo kukithiri katika baadhi ya benki, wafanyabiashara na wananchi wameanza kujipanga kuondoa fedha zao katika akaunti.


Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndullu alizungumza kwa njia ya simu mwishoni mwa wiki kwamba wameziagiza benki kuweka kifaa cha umeme (electronic chip) kwenye kadi zao za ATM ambazo si rahisi kughushi.


“Wizi kama huo unatokea wakati mtu anaweka namba za siri kwenye ATM kwani kuna watu huweka kamera ambazo husoma na namba hizo kufanikiwa kuzipata kisha kufanya wizi ,” alisema Profesa Ndullu.


Alisema kuwa kutokana na wizi kukithiri wamezitaka benki zote kuweka mifuniko katika eneo la namba za siri ili wezi wanaoweka kamera ili kuzinasa wakati mtu anatoa fedha washindwe kufanya hivyo.


Profesa Ndullu alisema wanafuatilia mfumo wa utendaji wa benki ili kuondokana na tatizo hilo ambalo hivi sasa limeibua mijadala na hofu kubwa miongoni mwa wananchi.


Benki kubwa nchini zimekumbwa na mtikisiko wa wizi wa fedha kwa kadi za ATM, ambao umeongezeka kwa kasi kiasi cha kufanya wananchi wengi kuhifadhi fedha zao kwenye mitandao ya makampuni mbalimbali ya simu za mikononi ambayo hata hivyo ripoti zimekuwa zikieleza kuwa nako usalama wake si wa kiwango cha juu.


Baadhi ya benki ambazo zimekumbwa na matukio hayo zimekuwa zikisita kutoa taarifa kueleza sababu za kushindwa kuzuia wizi huo na badala yake zimekaa kimya kuhofia kupoteza wateja.


Kukua kwa teknolojia za kifedha ambako kumerahisisha ufanisi wa matumizi na utunzaji wa fedha, sasa kunaonekana kugeuka na kuwa balaa kutokana na kuibuka kwa wizi mkubwa mahala zinakohifadhiwa kwenye akaunti za wateja kwa kutumia njia ya mtandao.


Taarifa za wizi huo zilianza kurindima mwezi Machi, 2010, ambako kiasi cha mabilioni ziliibwa kupitia katika mashine za ATM huku kati ya kiasi hicho jumla ya Sh360 milioni zikihusisha benki moja nchini.


Hata hivyo, mwaka huo watu wanne walikamatwa baada ya kuripotiwa wizi huo mkubwa. Sambamba na kukamatwa kwa watu hao, pia alikamatwa mfanyabiashara mmoja aliyekuwa akifanya jaribio la kuiba kimafia Sh221 milioni kutoka benki ya NBC.


Wimbi la wizi huo limeibuka tena katika kipindi cha Oktoba 2012 hadi Februari 2013 na inakadiriwa kuwa jumla ya kiasi cha Sh700 milioni kimeibwa katika benki mbalimbali kwa nyakati tofauti.
Hivi karibuni, Polisi mkoani Mwanza kwa kusaidiana na maofisa wa Benki ya NMB, iliwatia mbaroni watu watatu ambao walidaiwa kuiba kiasi cha Sh700 milioni kwa nyakati tofauti.


Watuhumiwa hao walinaswa baada ya kuwekewa mtego na maofisa wa benki pamoja na polisi usiku wa Februari 10, mwaka huu. Mtuhumiwa mmoja alinaswa akichukua fedha katika mashine ya ATM ya NMB kwenye Tawi la PPF Plaza.


Baada ya kunaswa kwa mtuhumiwa huyo, alisaidia kuwaelekeza polisi walipo wenzake, ambao walikutwa katika hoteli moja jijini Mwanza wakiwa wamejipumzisha.

Muargentina awa Baba Mtakatifu wa kwanza kutoka Amerika ya Kusini,aitwa Francis I




Ni Baba Mtakatifu wa kwanza kutoka Amerika ya Kusini. Kwenye hotuba yake ya kwanza amwombea Benedict, aomba Kanisa "litembee pamoja katika imani"
Jesuit Cardinal Jorge Bergoglio wa Buenos Aires amechaguliwa kuongoza Wakatoliki billioni moja kama Papa Francis I.

Ni Baba Mtakatifu wa kwanza kutoka Amerika ya Kusini. Kwenye hotuba yake ya kwanza amwombea Benedict, aomba Kanisa "litembee pamoja katika imani".

Ametoa baraka yake ya kwanza ya umma saa nne unusu EAT. Awaomba waumini wamwombee.Wachambuzi wasema Francis ni Papa "mnyenyekevu."

Dk Slaa amkumbuka Sitta


Mvutano uliopo hivi sasa kati ya Chadema na Bunge ulianza Februari 4 katika kikao cha Bunge mjini Dodoma baada ya wabunge wa Chadema kupinga msimamo wa kiti cha Spika wakieleza unapendelea

Boniface Meena na Mussa Juma, Mwananchi
Kutokana na mvutano ambao umekuwapo mara kwa mara kati ya Chadema na Spika wa Bunge, Anne Makinda, chama hicho kimemkumbuka aliyekuwa Spika wa Bunge la 10, Samuel Sitta kikieleza kuwa alikuwa hapindishi sheria na kanuni za Bunge na ndiyo maana lilikuwa limetulia.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kuhusu wabunge wa chama hicho kutakiwa kuhojiwa na Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema Spika Makinda amekuwa akipindisha kanuni na ndiyo maana kumekuwa hakuna utulivu bungeni.


“Spika Sitta aliyekuwepo kabla ya Makinda alikuwa hapindishi sheria na alikuwa anajirekebisha pale anapokosea na tulikuwa tukishauriana kwamba asijihusishe na mambo ya vyama,” alisema Dk Slaa.


Alisema Sitta, ambaye hivi sasa ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki alikuwa hafuati mambo ya vyama kwa kuwa alitakiwa kuwa ni mtu ambaye hapendelei upande wowote. Sitta, ambaye alikuwa Spika kuanzia mwaka 2005-2010, alikuwa anajinadi kwa kuendesha Bunge kwa spidi na viwango.


“Makinda aachane na ushabiki wa CCM kwani anajua kabisa kanuni ya nane inamtaka Spika asifungamane na upande wowote hivyo aache kufanya hivyo,” alisema Dk Slaa.


Alisema ni muhimu Spika akawaeleza kimaandishi amepata wapi mamlaka ya kuruhusu kamati iendelee wakati zote zilivunjika rasmi katika Bunge lililopita.
“Spika kama hajui kanuni aende shule kujifunza kuliko kututia aibu, wanasheria, wabunge wamsaidie ili aweze kuelewa.”


Dk Slaa alisema katika mabunge ya kidemokrasia, kupongeza ni jambo halali na kuzomea pia ni jambo halali hivyo kitendo cha wabunge wao kuzomea ni sawa kwa kuwa ni njia yao ya kufikisha ujumbe. Akizungumzia suala la wabunge wake kuhojiwa na kamati hiyo ya Bunge, alisema hawatakwenda kuhojiwa na kamati hiyo na kama Bunge litaamua kuwafukuza lifanye hivyo ili wananchi waelewe.


“Hawawezi kwenda kuhojiwa na kamati ambayo haipo kisheria, nilipokuwepo bungeni nilishiriki kuandaa kanuni hizi za Bunge, Spika hana mamlaka anayojipa ya kuongeza muda wa kamati, hivyo aache kulidhoofisha Bunge na badala yake alisaidie,” alisema Dk Slaa.


Akizungumzia suala hilo, Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alisema anashangazwa na Naibu Spika, Job Ndugai kusema kuwa kuna kamati ambazo huwa zinaendelea wakati nyingine zinapokuwa zimemaliza muda wake.


Lema aitisha maandamano
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, ametangaza kuandaa maandamano makubwa yatakayoshirikisha wanawake na watoto katika Jiji la Arusha ili kushinikiza Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Arusha (AUWSA) kuwasambazia maji.


Akizungumza jana, Lema alisema ameamua kuandaa maandamano hayo ya kudai maji kwani kwa zaidi ya miezi sita sasa asilimia 70 ya wakazi wa Jiji la Arusha hawapati maji safi.


“Nimewaandikia barua AUWSA wiki mbili sasa nikiwataka wanipe mipango yao ya muda mfupi na mrefu ya kuondoa tatizo la maji Arusha, kwani mimi kama mbunge ninaweza kushirikiana nao kupunguza tatizo hili, lakini hawajajibu sasa tutawashinikiza kwa nguvu wa umma,” alisema Lema.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa AUWSA, Mhandisi Ruth Koya hakupatikana kuelezea kama amepokea barua hiyo baada ya kutopatikana ofisini, pia simu yake ya mkononi ilikuwa haipatikani.

Monday 11 March 2013

Ushindi wa Kenyatta wachambuliwa


USHINDI wa Uhuru Kenyatta katika kinyang’anyiro cha kihistoria cha Uchaguzi Mkuu wa Kenya, umeonesha kuwa siasa za ukabila nchini humo, bado zina nguvu.

Uhuru juzi alitangazwa kuwa Rais wa nne wa Kenya, baada ya kujipatia asilimia 50.07 ya kura zote zilizopigwa, dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga, aliyepata asilimia 43.28 ya kura hizo.

Kwa mujibu wa Katiba mpya ya Kenya, mgombea wa urais, ni lazima afikishe zaidi ya asilimia 50 ya kura, masharti ambayo Uhuru aliyatimiza japo kwa asilimia 0.07.

Akizungumza jana na gazeti hili, Mhadhiri wa Siasa na Utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana, alisema siasa za ukabila ni saratani ambayo bado inaendeleao kuitafuna Kenya na kuwa jambo hilo si zuri kwa mustakabali wa nchi hiyo.

Alisema ukabila ni vigumu kuumaliza nchini humo, na imejionesha katika uchaguzi uliomalizika, jinsi wapigakura walivyokwenda kupiga kura zao kwa kumfuata mtu na si sera na itikadi za vyama.

Kauli hiyo pia imeungwa mkono na mhadhiri mwingine wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Audax Kweyamba, aliyesema kuwa Kenya bado inasumbuliwa na donda la ukabila.

“Nimefuatilia sana uchaguzi wa Kenya, hata ushindi unaonesha kabisa siasa za ukabila ni tatizo jambo ambalo si zuri kwa mustakabali wa nchi hiyo,” alisema.

Ushauri Bana alisema katika kutekeleza kauli yake ya kuunda Kenya moja, ni vema Uhuru aje Tanzania kujifunza msingi ya kujenga taifa kama alivyofanya Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere.

“Uhuru kama anataka kujenga nchi yenye umoja, aje kujifunza namna ya kujenga taifa, lakini hili hawezi kumaliza peke yake, isipokuwa kwa kusaidiwa na kambi ya Odinga na Wakenya kwa ujumla.

“Kinyume chake Wakikuyu (kabila la Uhuru) na Wakalenjini (kabila la Mgombea Mwenza, William Ruto), wataendelea kuongoza kwa sababu ndio wengi na wanajitokeza kupiga kura,” alisema Dk Bana. Kweyamba yeye alishauri Uhuru ateue viongozi au mawaziri, kulingana na uwezo wao na kuzingatia sura ya utaifa ili kuondoa picha ya ukabila iliyojengeka. Asilimia 0.07?

Akizungumzia ushindi mwembamba wa Uhuru, Dk Bana alisema haijalishi, ilimradi Katiba ya Kenya iliyopitishwa na wananchi wenyewe, inaruhusu mshindi kutangazwa akiwa amefikia zaidi ya asilimia 50 ya kura.

Hata hivyo, alisema ni vema nchi za Afrika ikiwemo Tanzania inayojiandaa kupata Katiba mpya, ziangalie suala hilo katika katiba zao.

Alipendekeza Katiba ziagize uundwaji wa Serikali ya Umoja ya Kitaifa, endapo kunakuwa na kuzidiana kwa kura chache, ili kuondoa manung’uniko kwa walioshindwa.

“Katika hali ya kawaida, ukishindwa kwa tofauti ndogo huamini matokeo, lakini hili linaweza kumalizwa kwa kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, kinyume chake kiongozi aliyeshinda, atatawala kwa nguvu ya dola kutokana na sehemu kubwa kumpinga,” alisema.

Naye Kweyamba alisema jambo la msingi ni hiyo asilimia 0.07 iliyompa Uhuru ushindi, iwe imetokana na Tume kuendesha uchaguzi huru na wa haki na imepatikana kihalali.

Wapigakura Kweyamba alisema Kenya imevunja rekodi ya idadi kubwa ya wapiga kura kujitokeza kutumia haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi, kwa kile kinachoonekana ni kuwa na matumaini mapya baada ya vurugu zilizotokea mwaka 2007.

“Tuombe Mungu, mambo yote yaishe salama na Kenya iwe salama, kwani endapo kutatokea machafuko, kuna hatari ya kushusha morali ya wananchi, ambao wamejitoa kutumia haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi,” alisema Kweyamba.

Alisema, Watanzania wanatakiwa kujifunza namna ya kutumia haki ya kuchagua vongozi, na kuachana na tabia ya kuona kuwa hawana haja ya kushiriki kwenye uchaguzi.

Alisema asilimia 42.8 zilizofikiwa mwaka 2010 haikuwa idadi nzuri. Naye Dk Bana alisema hiyo ni hatua nzuri, ambayo inaonekana imechangiwa na vyama siasa vya Kenya kutoa hamasa kwa wananchi na jinsi Serikali ilivyofanya kazi ya kutoa elimu ya uchaguzi kwa wananchi wake.

Mauaji ya albino yaichafua Tanzania


Mpango wa Afrika wa Kutathmini Utawala Bora (APRM), umebaini kwamba rushwa na ukiukaji wa haki za binadamu ni tatizo kubwa nchini linalohitaji kufanyiwa kazi ili kuimarisha utawala bora.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim alisema jana jijini Dar es Salaam kwamba, licha ya Tanzania kuonyesha mafanikio katika utawala bora, bado maeneo hayo yanahitaji nguvu za ziada.

Mahadhi alisema hayo wakati wa kuadhimisha Siku ya APRM ikiwa ni miaka 10 tangu ilipoanzishwa.

“Ripoti ya APRM iliwasilishwa na Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa wakuu wa nchi za Kiafrika na kusifiwa sana,” alisema.

Alisema kuna mambo machache yalijitokeza na yanayoharibu jina la Tanzania na watu wake.
Alisema kukithiri kwa rushwa ni sehemu ambayo ilitia doa katika ripoti hiyo na kwamba inahitaji kufanyiwa kazi.

“Tunahitaji kuimarisha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Tume ya Maadili ya Viongozi ili kuondokana na kasoro hizo,” alisema Mahadhi.
Aidha alisema eneo la haki za binadamu nalo lilitia doa katika ripoti hiyo hasa mauaji ya walemavu wa ngozi (albino).

Uchaguzi Mkuu Kenya: Ghasia zaanza Kisumu





Nairobi: Polisi wa kutuliza ghasia juzi walilazimika kutumia mabomu ya machozi Mjini Kisumu kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakipinga kutangazwa kwa matokeo ya urais ambayo mgombea wao, Raila Odinga alianguka.

Vurugu hizo ziliibuka, baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais yaliyompa ushindi Uhuru Kenyatta.

Maelfu ya vijana wamekuwa wakirandaranda kwenye maeneo kadhaa ya Kisumu wakichoma majengo na kufunga barabara, huku wakiimba: “Bila Raila, hakuna amani.”

Vurugu hizo zilizoanza juzi jioni zimesababisha maduka kufungwa huku makundi ya vijana wenye hasira wakiendelea kurandaranda mitaani wakipambana na polisi ambao walifanya jitihada za kuwatuliza na kurejesha amani.

Ilielezwa kwamba, muda mfupi tu baada ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kumtangaza Kenyatta kuwa mshindi, zaidi ya vijana 100 waliibuka na kuanza kuwarushia mawe polisi na muda mfupi baadaye idadi ya vijana hao iliongezeka na kusambaa katika maeneo karibu yote ya Kisumu.

Odinga ambaye alikuwa mgombea wa Muungano wa Cord, amewataka wafuasi wake kuwa watulivu kwa kuwa anahitaji kufuata mkondo wa sheria kupinga matokeo hayo.
Matokeo hayo yaliyotangazwa juzi, yalimpa ushindi Kenyatta aliyesimama kwa tiketi ya Muungano wa Jubilee, wa asilimia 50.07 dhidi ya asilimia 43 alizopata Raila.

Raila atinga mahakamani
Muungano wa Cord, leo utawasilisha vielelezo mahakamani kupinga ushindi wa Kenyatta.
Mwanasheria Mkuu wa zamani wa Kenya, Amos Wako ametajwa kuwa miongoni mwa wajumbe wa jopo la wanasheria watakaopinga ushindi wa Kenyatta.

Jopo hilo la wanasheria linaongozwa na mwanasheria mkongwe, George Oraro na baadhi ya mawaziri wakiwamo; Mutula Kilonzo, James Orengo na Ababu Namwamba ambao ni washauri wakuu wa jopo.

Oraro alimtetea aliyekuwa Waziri wa Viwanda, Henry Kosgei wakati alipokabiliwa na kesi kwenye Mahakama ya Kimataifa ya ICC, The Hague.
Wengine wanaounda timu hiyo ni Gitobu Imanyara, Pheroze Nowrojee, Chacha Odera, Ambrose Rachier na Paul Mwangi.

Cord imepanga kufungua kesi ikitaka Mahakama itengue hatua ya kutangazwa kwa Kenyatta kuwa Rais wa Kenya kwa kuwa taratibu za ukusanyaji matokeo zilikiukwa.
Tangu juzi, jopo hilo la wanasheria lilikuwa na vikao mfululizo kuandaa ushahidi wa kesi hiyo ikiwamo kukusanya vielelezo watakavyosimamia katika kesi hiyo kwa mujibu wa Kifungu namba 163 cha Katiba ya Kenya.

Mfuasi wa Uhuru afariki
Shamrashamra za kushangilia ushindi wa Kenyatta ziliingia doa kwenye Mji wa Nyeri baada ya lori lililobeba mashabiki wa mgombea huyo kutumbukia kwenye korongo na kuua mtu mmoja. Katika ajali hiyo watu 30 walijeruhiwa lakini wakiwa katika hali mbaya.

Mwili wa mtu aliyefariki ulipelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Nyeri wakati wengine waliojeruhiwa wamelazwa kwenye hospitali hiyo.
Lori hilo lilikuwa likienda maeneo ya Giakanja kwa ajili ya kukusanya mashabiki wengine na kuanza safari ya kuzunguka mitaa ya mji huo kushangilia ushindi. Kamanda wa Polisi Nyeri, Kirunya Limbitu alithibitisha ajali hiyo na kusema lori hilo lilikuwa kwenye mwendokasi na kupoteza mwelekeo kabla ya kutumbukia kwenye korongo na kupinduka.

Kibaki set to hand over mantle of power to his godson Uhuru


Is it a twist of fate or Shakespeare’s predetermined destiny that President Kibaki will be handing over power to Mr Uhuru Kenyatta?

No one would have imagined it 51 years ago. Not even Uhuru’s mother, Mama Ngina, nor even his father, Mzee Jomo Kenyatta, would have had such inkling.

That time, Mr Kibaki, a staunch Catholic like Mama Ngina, was to be Mr Kenyatta’s godfather following the birth of Uhuru on October 26, 1961.

Executive officer

The outgoing Head of State has had his life tied by fate to the incoming President from the latter’s birth, on the eve of Uhuru (independence), when young Kibaki was the executive officer of Kanu, the party that was to usher in freedom in the country two years later.

Mr Njenga Karume, in his book From Charcoal to Gold, says he and Mr Kibaki went to visit Mama Ngina in the company of Mzee Kenyatta at home in Gatundu following the birth of a baby boy.

Mr Karume says it was Mr Kibaki who suggested to Mzee that the new-born be named Uhuru since independence was only a few months away.

Other accounts from those close to the family indicate that Mr Joseph Murumbi, the man who was to become Kenya’s second vice-president and a close friend of Mzee Kenyatta, also suggested the name.

Still, Mr Kibaki, who is expected to hand over power to Mr Kenyatta on March 26, has had to fight political wars with his godson.

Such was the bitter fight during the 2002 presidential elections pitting Mr Kibaki in Narc against Mr Kenyatta as the Kanu candidate to succeed President Moi.

Mr Kibaki was to trounce his godson, garnering 62 per cent of all the votes cast in the election.

Though political foes, Mr Kibaki still had a soft spot for Uhuru, even as they had gone different ways in politics.

This was the case after the 2005 referendum when Mr Kenyatta teamed up with Mr Raila Odinga in the Orange team that successfully campaigned to defeat the draft Constitution. Mr Kenyatta later aligned himself to his godfather ahead of the 2007 poll.

Mr Kibaki went on to appoint Mr Kenyatta as Deputy Prime Minister after a negotiated coalition government against all expectations. Many thought he would appoint former Gichugu MP Martha Karua, who was instrumental in the negotiations on the Kibaki side after violence broke out following the disputed presidential elections of 2007.

Safari kuelekea uchaguzi wa Papa yaanza kesho Vatican


Afrika na Amerika Kusini, zikilinganishwa na mabara ya Ulaya na Marekani, zinaelezwa kuwa zina idadi kubwa ya waumini wapya , makanisa yake yanajaa, idadi ya mapadri inaongezeka, tofauti na Ulaya na Marekani inakopungua

VATICAN CITY, Vatican
MCHAKATO rasmi wa kumpata kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani atakayemrithi Papa Benedict XVI aliyejiuzulu Februari 28, unaanza kesho. Katika mchakato huo, makardinali 115 wataingia kwenye Kanisa la Sistine kwa kazi hiyo ngumu ya kupiga kura.

Kura hiyo ya siri inatarajiwa kurudiwa mara kadhaa hadi apatikane mtu anayekubalika.
Tayari kanuni za uchaguzi huo zimeshaandaliwa zikiwamo za namna ya kupiga kura kwa usiri na wasimamizi wa kura.

Makardinali hao kutoka mataifa mbalimbali duniani, wamekuwapo Vatican ambako kila walipowasili walikula kiapo cha kutunza siri wakati wote wa kikao hicho muhimu.
Viongozi hao wa kidini, wataongozwa zaidi na sala na maombi kwa roho mtakatifu.

Kama ilivyokuwa katika miaka ya nyuma, kampeni haziruhusiwi katika mchakato huu mzima.

Kukosekana kwa kampeni, hata hivyo, hakuzuii watu kutoa mawazo yao kuhusu nani angefaa kuchaguliwa.

Wengine wanaipa nafasi kubwa Italia, yaliko makao makuu ya kanisa hilo, Vatican, ingawa pia kuna wale wanaofikiri kuwa sasa ni zamu ya Afrika na Amerika Kusini kutoa kiongozi wa juu wa kanisa hilo lenye waumini bilioni 1.2.

Pia, wengine wanadhani kuwa Ulaya, ambayo ina makardinali wengi zaidi, bado inastahili kutoa kiongozi huyo kama ilivyokuwa kwa Poland na Ujerumani katika miaka ya hivi karibuni.

Kwanini Afrika?
Sababu ya msingi inayotajwa kuipendelea Afrika kwa sasa ni, ongezeko la waumini wapya ambako takwimu zinaonyesha kuwa nchi kama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Tanzania, Uganda zimo katika orodha ya 20 bora duniani kwa waumini wengi wa Kikatoliki.

Afrika na Amerika Kusini, zikilinganishwa na mabara ya Ulaya na Marekani, zinaelezwa kuwa zina idadi kubwa ya waumini wapya , makanisa yake yanajaa, idadi ya mapadri inaongezeka, tofauti na Ulaya na Marekani inakopungua .

Makardinali wawili, Francis Arinze mwenye umri wa miaka 80, raia wa Nigeria na mwenzake, Peter Turkson (64) kutoka Ghana, wamekuwa wakitajwa kuwa miongoni mwa wale wanaofaa kwa kazi hiyo.

Wakati wote wa mchakato huo, makardinali hao 115 hawatakuwa na mawasiliano yoyote na ulimwengu wa nje hadi apatikane papa mpya ndani ya wiki mbili.

Kwa pamoja, wataishi katika hosteli ya kisasa iliyomo ndani ya eneo hilo, umbali mdogo kutoka katika Kanisa la Sistine, ambalo milango na madirisha yake yamezibwa kuzuia watu kuchungulia ndani yake.
Hosteli hiyo ya kisasa inayojitegemea, imeandaliwa mahsusi kwa kazi hiyo, ikiwa na huduma zote za msingi. Ina madaktari, mapadri ambao watawahudumia makardinali hao wakihitajika.

Kila kardinali ataishi katika chumba chake kidogo chenye kitanda, meza ndogo na kabati la nguo, akisali zaidi na wakati huo akifanya tafakuri ya kina kati yake na Mungu ni nani hasa kati yao aliyeteuliwa kuliongoza kanisa hilo.
Inaelezwa kuwa wakati wote wa mchakato, makardinali hao hawazungumzi, bali kusali na kufanya tafakuri na kukutana wakati wa chakula.

Ni nchi gani zinawakilishwa?
Zipo nchi kadhaa ambazo zina uwakilishi katika uchaguzi huo.
Hizi ni pamoja na: Italia (28), Marekani (11), Ujerumani (6), Hispania, India, Brazil (5) kila moja, Ufaransa, Poland (4) kila moja Mexico, Canada (3) kila moja
Ureno, Nigeria, Argentina ( 2) kila moja

Australia, Austria, Ubelgiji, Bolivia, Bosnia Herzegovina, Chile, China, DR Congo, Colombia, Croatia, Cuba,Czech , Dominica, Ecuador, Misri, Ghana, Guinea,Honduras, Hungary, Ireland, Kenya,Lebanon, Lithuania, Uholanzi, Peru, Ufilipino, Senegal, Slovenia, Afrika Kusini, Sri Lanka, Sudan, Uswisi, Tanzania, Venezuela, Vietnam (1) kila moja.

Sunday 10 March 2013

Ni kuonewa Ni stahili Katiba mbovu Siri za Zitto nje


SIRI kubwa kuhusu mwenendo wa Zitto Kabwe (Mb) ndani ya chama chake zimeanikwa mitaani na zinaweza kumzamisha kisiasa,.

Siku nne baada ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Willibrod Slaa kusema wamenasa taarifa za mawasiliano ya Zitto, baadhi ya taarifa zimepatikana jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Zitto ananukuliwa akiapa kusaidia wagombea uongozi katika vyama vingine; na katika moja ya taarifa ananukuliwa akisema atasaidia David Kafulila kupata ubunge “hata kabla ya akina John Mnyika…”

Mnyika ni Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa CHADEMA na Kafulila alikuwa Afisa Habari ambaye baada ya kuondolewa wadhifa huo amekimbilia NCCR-Mageuzi. Mnyika anatarajia kugombea ubunge jimbo la Ubungo.

Naye Zitto amenukuliwa na gazeti la Mwananchi la Jumatatu akilalamika kuwa ameingiliwa katika mawasiliano yake ya baruapepe (e-mail); jambo ambalo Mkurugenzi wa Upelelezi, Robert Manumba, amedakia haraka na kusema Zitto akiwapelekea malalamiko watashughulikia.

Kwa mujibu wa mpangilio wa taarifa husika, lazima aliyezitoa amepata ufunguo wa baruapepe (password) wa ama Zitto au mwandishi wa habari wa Mwananchi, Denis Msacky.

Karibu mawasiliano yote ni kati ya Zitto na Msacky juu ya “ushujaa” wa Zitto na jinsi anavyopendwa nje ya chama huku “akichukiwa” na viongozi wake wakuu.

Katika moja ya mawasiliano, inaonyeshwa kuwa Msacky alimwandikia Zitto akieleza, “Leo hii Mrema (Augustine Lyatonga) anasema anakuheshimu wewe, lakini si Mbowe; hivyo hivyo, Lipumba (Profesa Ibrahim) na James Mbatia wanasema wewe una visheni.”

Katika mawasiliano hayo ya Jumanne, 1 Desemba 2009, saa 6.45 adhuhuri, Msacky anaonyeshwa kumwambia Zitto pia kuwa, “CCM nao…wanakusifu kwamba pamoja na kwamba unawaliza sana, lakini ni kiongozi shupavu.”

“Leo hii siasa za CHADEMA zingekuwa zinatisha kama ungekuwa mwenyekiti wa CHADEMA, vijana nchi nzima wangejiunga na chama, uko nao karibu, unaongea nao, una elimu nzuri, unajua mambo, unasoma sana,” imeeleza sehemu ya mawasiliano kutoka kwa Msacky kwenda kwa Zitto.

Kinacholeta wasiwasi ndani ya CHADEMA kinaweza kuwa lugha inayotumiwa katika mawasiliano hayo. Kwa mfano, katika waraka huohuo, Msacky ananukuliwa akiandika:

“Wanataka kukumaliza, nami sitakubali mtu ammalize rafiki yangu nikiangalia…wanasema Mbowe hata Mbatia akikaa vema anaweza kumpita kama siasa za kufukuza zitaendelea. Muhimu, usisikilize watu, tulia, urudi tupange tufanye nini? Lakini ukweli ni kwamba sasa wanakuogopa…Mwenyekiti Mtarajiwa…”

Mawasiliano yanaonyesha kuwa Zitto hakufurahishwa sana na taarifa za Mwananchi kuwa amemsaidia Kafulila magari matatu kwenda Kigoma kufanya kampeni chini ya NCCR-Mageuzi, lakini Msacky anaonyesha kumfariji.

“Kaka, mimi nimeiona story, haina matatizo zaidi ya kuwafanya akina Mbowe kusitisha mpango mbaya dhidi yako maana wanaanza kuogopa. Hata Mrema Lyatonga amesema kwamba Zitto huwa unamsaidia akiwa na shida. This shows that ur a leader katika opposition, wewe ni mtu wa maridhiano, unakuza upinzani Kigoma,” anaeleza.

Anasema, “Leo nasikia akina Mnyika wanahaha sana, waambie familia yako wasiingie katika mtego wa kuanza kuhojiwa na akina Kubenea (Saed wa MwanaHALISI), watawachanganya. Wewe usiongee kitu chochote, wabaki wanahaha, lakini for sure you are safe, na hizo kampeni za Mnyika kukuchafua huku akitaja majina ya Kafulila, ataziacha.”

Akionyesha juhudi za kushawishi, kuliwaza au kufarakanisha, Msacky anaandika, “Katika hili Zitto, mimi niko na wewe, huna kosa ambalo umefanya, na wala usihofu maana wewe utakuwa nguzo ya upinzani Tanzania…Wanakupa majina ya ajabu, wanakuita Mr Dowans, wanatumia akina Halima Mdee kukuchafua katika magazeti…”

Awali Zitto alikuwa amemwandikia Msacky akisema, “Stori niliyoiona kwenye mwananchi itaniletea matatizo sana.” Hiyo ilikuwa Jumatatu 30 Novemba 2009, saa 5.21 asubuhi. Baruapepe hiyo ilikuwa na kichwa kisemacho: “Muhimu na haraka.”

Aidha, katika mawasiliano mengine, Zitto anaendelea kuonyesha kutofurahishwa na taarifa juu ya magari matatu kwa safari ya Kafulila.

Naye anaandika kwa Msacky, “tatizo la stori ni wingi wa magari, itaonekana mimi nina magari mengi na ni fisadi unajua? Hilo ndio tatizo.”

Saini ya Zitto inatofautiana katika baadhi ya baruapepe. Pengine anaandika “zitto” na kwingine anaandika “Zi.”

Moja ya mawasiliano ambayo yanazua mashaka yanaonyesha Zitto akikiri kuwa na mawasiliano na waasi nchini Kongo akiandika, “take it from me (niamini), nina contacts nyingi sana Congo na hao rebels (waasi) huwa wananiomba sana ushauri na kutaka kuwaunganisha.”

Katika moja ya mawasiliano, Msacky anamwonya Zitto kutotumia baruapepe ya “CHADEMA kwa mawasiliano ya siri” na kutaka amwambie mama yake Shida Salum akatae kuongea na waandishi wa habari. “…nasikia Mbowe anataka mama awe akiongea na waandishi, usikubali,” alieleza.

Zitto alipoulizwa kuhusu taarifa ya Mwananchi kuwa anatembea na barua mfukoni ya kujiuzulu uanachama CHADEMA, alisema “Sina la kusema.”

Alipong’ang’anizwa kwamba imekuwaje hawezi kuzungumzia suala hilo ambalo ni muhimu kwa mustakabali wake wa kisiasa kwa chama chake, Zitto alisema, “Ni kwa sababu sitaki kuingia katika malumbano na katibu mkuu wangu (Dk. Willibrod Slaa) kwani malumbano hayo hayataijenga CHADEMA.”

Alipotakiwa kueleza juu ya baruapepe ambazo zinadaiwa kuwa mawasiliano kati yake na Msacky, haraka alijibu, “Sina la kusema.”

Alipoelezwa umuhimu wa yeye kueleza msimamo wake juu ya baruapepe hizo, Zitto alijibu, “Chochote nitakachosema sasa hivi, kitawachanganya Watanzania.

“Sitaki malumbano. Hakuna sababu ya kuwachanganya Watanzania. Hiyo haina maana yoyote,” alisema Zitto kwa sauti ya ukali. Zitto alikuwa akiongea kutoka Ujerumani kwa simu Na. +4915222493231.

MwanaHALISI ilimtafuta Msacky. Baada ya kuita kwa muda mrefu bila kupokelewa, hatimaye aliandika ujumbe “Kaka, niko katika kikao. Tuma ujumbe.”

Msacky aliulizwa, “Kaka, tumesikia kwamba umetajwa katika sakata la Zitto na chama chake na kwamba wewe ndiye mtibuaji. Je, ni kweli?” Hakujibu ujumbe na alipopigiwa simu ilikuwa inaita hadi kukatika.

Gazeti lilipowasiliana na Mnyika na kumueleza kwamba amekuwa akitajwa katika ujumbe wa Zitto na Msacky, alikiri kupokea ujumbe huo wa baruapepe uliotoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa ni “Mtanzania mwema.”

Alisema alipoona ujumbe mmoja unahusu Zitto kushauri Msacky kutochapisha habari za mkutano wake na waandishi wa habari, ndipo aliamua kupeleka ujumbe huo kwa Zitto.

“Nilimuuliza kuna hiki kitu nimetumiwa. Je, haya ni maandishi yako au kuna mtu ameingilia emaili yako na kujiandikia haya? Hadi leo hii, bado sijapata jibu,” alisema Mnyika kwa sauti ya masikitiko. Alisema yeye hana cha kusema na kuongeza, “labda umuulize Zitto.”

Alipoulizwa anachukuliaje suala hilo, Mnyika alisema, “Ukiniuliza mimi kwa upande wangu, nilitegemea mambo hayo yangemalizwa katika vikao vya chama na si kwa vyombo vya habari. Lakini kwa hatua ya hivi sasa, nadhani Zitto bado anayo fursa ya kulieleza hili.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe alipoulizwa juu ya madai ya kuwapo njama za kuhujumu chama chake zinazofanywa na Msacky kwa kumtumia Zitto, haraka alijibu, “tuna utaratibu wetu wa kushungulikia mambo ndani ya CHADEMA.”

Alisema, “Sina la kusema. CHADEMA ina utaratibu wake wa kushughulikia mambo yake.”

Kwa kadri mawasiliano ya Zitto na Msacky yanavyoonyesha na iwapo yatathibitishwa kuwa kweli, jambo ambalo linaanza kuthibitishwa na Zitto kwa kulalamika kuingiliwa kwenye faragha, basi uhusiano wake katika chama utakuwa umepata nyufa.

Wachunguzi wa siasa za upinzani nchini wanasema kwa hali hii, uwezekano wa Zitto kubaki ndani ya chama chake ni mdogo. “Ama atajiondoa mwenyewe au hatimaye atafukuzwa,” ameeleza mkufunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Hata hivyo, Zitto amenukuliwa na Mwananchi akisema, “Sitaki kugombana na mtu mimi. Wala msiniweke kwenye kifungo cha siasa. Ni bora niishi huru kuliko katika mateso ya siasa za kipumbavu kabisa. Nitafanya maamuzi ambayo hayajawahi kufikiriwa.”

Wiki iliyopita Kafulila aliwaambia waandishi wa habari kwamba Zitto atafanya maamuzi makubwa ambayo hawakutegemea.



Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu ambao ni mkusanyiko wa asasi zaidi ya 70 za kiraia zinazotetea haki za binadamu (THRD-Coalition) , kwa kushirikiana na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC),vimeelezea kulaani vikali shambulio la kinyama alilofanyiwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda.

Uchunguzi tulioufanya bado haujatujapatia habari za undani zaidi na uhakika wa tukio hilo, lakini kwa taarifa za awali kwa asilimia kubwa linahusiana na kazi yake ya utetezi wa haki za binadamu kupitia taaluma yake ya uandishi wa habari.

"Tunasema hivyo kwa sababu vitisho dhidi ya wanahabari na watetezi wengine wa haki za binadamu,vinataka kuzoeleka sasa hapa nchini jambo ambalo halikuwapo katika miaka ya nyuma.

"Takribani ndani ya miezi 10 sasa, zaidi ya watetezi wa haki za binadamu 10 wakiwamo waandishi wa habari wameshajeruhiwa, wamepata vitisho au kuuawa."

Ilisema taarifa hiyo iliyosainiwa na Onesmo Olengurumwa, Mratibu wa Mtandao huo kuwa matukio hayo yanaashiria lengo la kutaka kuzima sauti za watetezi wa wanyonge kwa visingizio mbalimbali na wakati mwingine matukio haya yakipewa sura tofauti ikiwamo uhalifu wa kawaida, visa vya kudhulumiana na visasi vya kimapenzi.

"Hatupendi kuingilia wala kukwamisha utendaji kazi wa jeshi hilo, lakini pia hatupendi wanahabari na watetezi wengine wafanye kazi yao katika mazingira ya woga. Tunaamini kwamba zipo njia muafaka zaidi za kushughulikia masuala yanayohusu taaluma ya habari," ilisema taarifa hiyo.

Mtandao huo umewataka watu wote wanaotumika au wanaoendeleza wimbi la mashambulizi kwa wanahabari na watetezi wote wa haki za binadamu kwa ujumla, waache kufanya hivyo kwani wataliingiza nchi katika machafuko makubwa pamoja na kuisihi Polisi na Serikali kubeba jukumu lao la kuhakikisha usalama wa watetezi wa haki za binadamu, na raia wote.
Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu ambao ni mkusanyiko wa asasi zaidi ya 70 za kiraia zinazotetea haki za binadamu (THRD-Coalition) , kwa kushirikiana na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC),vimeelezea kulaani vikali shambulio la kinyama alilofanyiwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda.

Uchunguzi tulioufanya bado haujatujapatia habari za undani zaidi na uhakika wa tukio hilo, lakini kwa taarifa za awali kwa asilimia kubwa linahusiana na kazi yake ya utetezi wa haki za binadamu kupitia taaluma yake ya uandishi wa habari.

"Tunasema hivyo kwa sababu vitisho dhidi ya wanahabari na watetezi wengine wa haki za binadamu,vinataka kuzoeleka sasa hapa nchini jambo ambalo halikuwapo katika miaka ya nyuma.

"Takribani ndani ya miezi 10 sasa, zaidi ya watetezi wa haki za binadamu 10 wakiwamo waandishi wa habari wameshajeruhiwa, wamepata vitisho au kuuawa."

Ilisema taarifa hiyo iliyosainiwa na Onesmo Olengurumwa, Mratibu wa Mtandao huo kuwa matukio hayo yanaashiria lengo la kutaka kuzima sauti za watetezi wa wanyonge kwa visingizio mbalimbali na wakati mwingine matukio haya yakipewa sura tofauti ikiwamo uhalifu wa kawaida, visa vya kudhulumiana na visasi vya kimapenzi.

"Hatupendi kuingilia wala kukwamisha utendaji kazi wa jeshi hilo, lakini pia hatupendi wanahabari na watetezi wengine wafanye kazi yao katika mazingira ya woga. Tunaamini kwamba zipo njia muafaka zaidi za kushughulikia masuala yanayohusu taaluma ya habari," ilisema taarifa hiyo.

Mtandao huo umewataka watu wote wanaotumika au wanaoendeleza wimbi la mashambulizi kwa wanahabari na watetezi wote wa haki za binadamu kwa ujumla, waache kufanya hivyo kwani wataliingiza nchi katika machafuko makubwa pamoja na kuisihi Polisi na Serikali kubeba jukumu lao la kuhakikisha usalama wa watetezi wa haki za binadamu, na raia wote.

Besigye beats security to attend Kategaya’s burial



Presidential security appeared anxious in Itojo, Ntungamo District, yesterday when Dr Kizza Besigye made a surprise appearance, joining thousands of mourners at the burial of First Deputy Prime Minister Eriya Kategaya.

Amidst a heavy downpour, the arrival of the former leader of the Forum for Democratic Change coincided with the landing of a military helicopter carrying President Museveni.

Dignitaries from government institutions like, judiciary, military and parliament attended the somber occasion that saw Mr Museveni describe his former bosom buddy as a “well-formed gentleman who kept no grudges.

“We disagreed twice but reconciled. In 1973, we disagreed on the setbacks we encountered when we attacked Mbarara. We parted ways; he went to Lusaka (Zambia) and I to Arusha. We later reconciled and worked together,” Mr Museveni said.

Making mention of the 2001-2003 events that split the once bosom-buddies, Mr Museveni said;“If you go left and I go right, that does not stop us from working together in the future,” giving the example of the third deputy premier Moses Ali.

“I salute him for being a fully reformed person in terms of character and ideology. There should be no need for us as men to endlessly be at loggerheads,” he added.

Kategaya fell out with the President and joined the opposition when he opposed the lifting of presidential term limits from the Constitution by the Seventh Parliament at the reported instigation of the country’s leader. He was sacked from Cabinet and Mr Museveni, who had then come to his second and last constitutionally-accepted a five-year term and went on to run for office again in 2006.

Ms Joan Kategaya, first wife to the deceased, asked government to construct a fully-equipped hospital in Kategays’s memory.

“We were only looking for a hydro-therapy machine to save his life. That is why we had to go to Nairobi,” Ms Kategaya said.

Mr Museveni proposed the construction of a technical school in Ntungamo to be named after Kategaya.

Besigye arrives
At approximately 1.30pm, Dr Besigye walked into the main square at the Itojo home just as Mr Museveni’s chopper appeared over the Kategaya homestead.

Catching mourners by surprise, Dr Besigye’s arrival was announced by the master of ceremonies, State Minister for Labour Mwesigwa Rukutana, prompting a rapturous welcome from the crowd.
Current FDC president, Maj. Gen. Mugisha Muntu left his chair to welcome Dr Besigye who sat next to him.

Since Tuesday, Dr Besigye has repeatedly been arrested almost the moment he steps out of his Kasangati residence. Police has accused him of attempting to restart the walk-to-work activities that nearly paralysed operations in Kampala city for close to a year.

FDC western youth leader Francis Mwijukye said it was imperative for Besigye to bury his former comrade-in-arms, who was one of the founders of the FDC.

In Kampala, security around Dr Besigye’s residence appeared unaware that he had slipped past them.
They (security personnel) sleep hungry, on water and biscuits and are expected to guard and follow a person they do not know what his day’s plans are. Their superiors take all the operations money. Besides, we have the capacity to be anywhere at any time,” Mr Mwijukye said.

Security sources have told this newspaper Mr Museveni’s security detail was unsure how the public would react in the presence of the two politicians in the same place, who are former friends, but now arch rivals.

Uhuru Kenyatta's victory speech


My fellow Kenyans, thank you.

Thank you for all your patience and your support along the way

Asanteni Sana.

I thank God for sustaining us and for bringing us this far.

I thank all those who have remained vigilant in prayer for our nation during this time.

I want to thank the people of the republic of Kenya who have shown patience over the last few days as we all awaited the outcome of this election.

I thank the thousands of officials who worked with the IEBC to make this, the most free and most fair general election in our nation's history.

Despite the challenges that you faced, you managed to keep the trust of Kenyans and to do your job professionally.

While we look forward to a day when electoral results are relayed in real-time to curb anxiety, we acknowledge that every process can be refined and I pledge to give you my support as you seek more efficient ways to conduct future elections.

I would also like to acknowledge and thank the police and all security agencies for their diligence and commitment to ensuring security.

I would especially like to acknowledge the police officers who lost their lives on the eve of the elections. They made the ultimate sacrifice, laying down their lives,in the name of democracy.

To their families, I offer my sincere condolences for your loss and I assure you that I, and the people of Kenya are standing with you in prayer.

The incidents that took the lives of our officers are a reminder that security remains one of the biggest challenges in our nation. It is unacceptable to see such violent and unnecessary loss of life. As we move forward, I pledge to meet all threats to our national security with the full force of Kenya's resources and with utmost urgency.

To the Kenyan media - you have shown remarkable responsibility as this country’s fourth estate. You have shown sensitivity in the dissemination of news and impartiality in your treatment of the results. You have no doubt helped to keep the country calm.

We are grateful for this, and we will continue to consider you our true partners as we embark on our journey.
To the presidential candidates – I salute you all.

You have contributed to ensuring a robust democratic process.

I in particular want to single out my brother, Raila Odinga, for his spirited campaign.

I know that all the candidates have made tremendous personal sacrifices for the progress of our country and today, I welcome them to join us in moving our nation forward.

My fellow Kenyans today, we celebrate the triumph of democracy; the triumph of peace; the triumph of nationhood.

Despite the misgivings of many in the world- we demonstrated a level of political maturity that surpassed expectations.

We dutifully turned out; we voted in peace; we upheld order and respect for the rule of law and we maintained the fabric of our society.

That is the real victory today. A victory for our nation. A victory that demonstrates to all that Kenya has finally come of age. That this, indeed, is Kenya’s moment.

I am honored and humbled that in a free and fair election- you, the people of Kenya, have placed your trust in me- to lead our nation as your next President.

I am here because of you.

I am here because of the unyielding support of millions of Kenyans, from all walks of life, from every corner of our nation, who sacrificed their time, energy and resources to make this campaign a success.

Thousands of you volunteered through Team Uhuru. Hundreds of you mobilized through grassroots organizations. Hundreds of you campaigned through your university associations and millions of Kenyans across the nation engaged us through our various online platforms.

Throughout this process you, the people, have remained unwavering in your belief not only in me - but in the possibility of a stronger, more prosperous Kenya.

A Kenya that has room for all our hopes and aspirations.

Last but not least, I am here because of my family:
My wife, Margaret; our children and all the members of my family.

However, this is has never been about me, this has been about you- about the people of Kenya. You have put your faith not in one man , but in a team.

In our Deputy President – Elect: Hon William Ruto. A man with a proven trackrecord, who has demonstrated to all of us, his ability to both speak and act with un-matched zeal and energy.

You put your trust in my sister, Charity Ngilu and my brother, Najib Balala both of whom have remained committed to serving the people and putting our nation first.

You put your trust inTNA, URP and the wider Jubilee family.

And because you gave us this trust, I am proud to say that the majority of women who were elected to parliament come from the Jubilee Coalition – a fact that demonstrates this teams commitment to supporting women and to supporting the full implementation of all the provisions within our constitution.

I want to say to all the Jubilee aspirants- those who won, and especially, those who did not – you have done your parties, and this coalition- proud.Your dedication, to the ideals that the Jubilee Coalition represents has been an inspiration to me. We came together as a team, and we will continue to work together as a team- for the good of all the people of Kenya.

However , today is about more than one Coalition or Party.

It is about all Kenyans: those of you who voted Jubilee and those who did not.

My fellow Kenyans, My pledge to you is that as your President, I will work on behalf of all citizens regardless of political affiliation.

I will honor the will of Kenyans and ensure that my Government protects their rights and acts without fear or favor; in the interests of our nation.

To all those who won various seats –regardless of what party or coalition you may belong to - let us remember that we are , first and foremost, Kenyans, and that the people have bestowed upon us the responsibility to work for them.

I extend a hand of friendship and cooperation to you so that together, we can truly serve the Kenyan people.

In the nearly 5 decades since independence, we have made great strides as a nation.

Kenya has experienced huge success but there have also been enduring problems.
In the last 10 years, under the Presidency of Mwai Kibaki we have begun to overcome many of our national challenges.

We are indebted to his leadership and grateful for the services he has rendered to our country.

As I assume office, my task, and the task before us all is to secure the gains we have made while focusing on solving the challenges that remain.

My fellow Kenyans, the elections are now over.

Today, in itself, is not an end ; it is a beginning and there is much work to be done.

That work begins with all of us taking personal responsibility for the future of our country- the inheritance of our children.

For those who are celebrating let us be modest in victory. To those who voted for any of my opponents - let us keep in mind the broader victory of Kenya, and continue to uphold peace. Let us remember that while, in a democracy, some contestants must, inevitably, lose - the citizens of a country never do. In this election, every vote mattered and from this moment, every voice that contributes to the national dialogue- will be heard.

Fellow Kenyans, our duty now is to return to our lives. To return to our jobs, our businesses; our farms – and continue making the daily decisions that will transform Kenya.

I promise to do my part, but I need every Kenyan to play their part as well.

To our brothers and sisters in the region and in Africa as a whole we appreciate your support and encouragement before, during and after the elections. This is the true spirit of Africa. We look forward to playing our rightful role in the region and in the continent. The African star is shining brightly and the destiny of Africa is in our hands.

To the nations of the world I give you my assurances that I and my team understand that Kenya is part of the community of nations and while as leaders we are, first and foremost, servants of the Kenyan people, we recognize and accept our international obligations and we will continue to co-operate with all nations and international institutions– in line with those obligations.

However we also expect that the international community will respect our sovereignty and the democratic will of the people of Kenya.

Indeed it is the desire of the people of Kenya to be a nation that is at peace with itself, at peace with her neighbors, at peace with our continent and at peace with the world at large.

We will pursue this ideal - upholding the values enshrined in our constitution and continuing in the spirit embodied in the words of our national anthem

Oh God of all creation
Bless this our land and nation

Justice be our shield and defender

May we dwell in unity, peace and liberty.

Plenty be found within our borders.

Thank you,

God bless you And God bless the Republic of Kenya.

Haki za Binadamu nao watoa tamko



Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu ambao ni mkusanyiko wa asasi zaidi ya 70 za kiraia zinazotetea haki za binadamu (THRD-Coalition) , kwa kushirikiana na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC),vimeelezea kulaani vikali shambulio la kinyama alilofanyiwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda.

Uchunguzi tulioufanya bado haujatujapatia habari za undani zaidi na uhakika wa tukio hilo, lakini kwa taarifa za awali kwa asilimia kubwa linahusiana na kazi yake ya utetezi wa haki za binadamu kupitia taaluma yake ya uandishi wa habari.

"Tunasema hivyo kwa sababu vitisho dhidi ya wanahabari na watetezi wengine wa haki za binadamu,vinataka kuzoeleka sasa hapa nchini jambo ambalo halikuwapo katika miaka ya nyuma.

"Takribani ndani ya miezi 10 sasa, zaidi ya watetezi wa haki za binadamu 10 wakiwamo waandishi wa habari wameshajeruhiwa, wamepata vitisho au kuuawa."

Ilisema taarifa hiyo iliyosainiwa na Onesmo Olengurumwa, Mratibu wa Mtandao huo kuwa matukio hayo yanaashiria lengo la kutaka kuzima sauti za watetezi wa wanyonge kwa visingizio mbalimbali na wakati mwingine matukio haya yakipewa sura tofauti ikiwamo uhalifu wa kawaida, visa vya kudhulumiana na visasi vya kimapenzi.

"Hatupendi kuingilia wala kukwamisha utendaji kazi wa jeshi hilo, lakini pia hatupendi wanahabari na watetezi wengine wafanye kazi yao katika mazingira ya woga. Tunaamini kwamba zipo njia muafaka zaidi za kushughulikia masuala yanayohusu taaluma ya habari," ilisema taarifa hiyo.

Mtandao huo umewataka watu wote wanaotumika au wanaoendeleza wimbi la mashambulizi kwa wanahabari na watetezi wote wa haki za binadamu kwa ujumla, waache kufanya hivyo kwani wataliingiza nchi katika machafuko makubwa pamoja na kuisihi Polisi na Serikali kubeba jukumu lao la kuhakikisha usalama wa watetezi wa haki za binadamu, na raia wote.

Je hii ni njia ya kuwapa watanzania ajira, kama mtakuwa mnawalimbikizia wabunge madaraka?



abunge watatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mmoja wa Baraza la wawakilishi Zanzibar wameteuliwa kuwa wajumbe wa Bodi ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

Wabunge hao ni Faith Mtambo na Mary Chatanda (wote viti maalumu (CCM), Mbunge wa Nzega (CCM), Dk Hamis Kigwangala na Ali Mzee Ali ambaye ni mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Katika orodha hiyo ya wajumbe wapya, pia yumo Wilson Masilingi ambaye alikuwa Mbunge wa Muleba Kusini mpaka mwaka 2010, ambapo alishindwa katika kura za maoni ndani ya chama chake na mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Profesa Anna Tibaijuka ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inaeleza kuwa , Rais Jakaya Kikwete amemteua kwa kipindi cha pili, Balozi Christopher Liundi kuwa mwenyekiti wa Bodi hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu na kwamba uteuzi huo umeanza rasmi Machi 6,mwaka huu.

Liundi aliteuliwa kushika nafasi hiyo mwaka 2010, huku wajumbe wake wakati huo wakiwa ni Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu, Rose Lugembe, Shabani Mnubi, Nuru Milao, Joseph Chilambo, Wilfred Nyachia, Makumba Kimweri, Dk Aggrey Mlimuka na Issa Suleiman.

Wajumbe wengine wa bodi hiyo mpya ni Aggrey Mlimuka, Dash-Hood Mndeme, Dk Ali Mndali na Balozi mstaafu Abdi Mshangama. Kwa nini wana siasa wapewe nafasi za uongozi? Kwa nini sisi watanzania tusifike sehemu tuone kwamba kuwa mwanasiasa siyo kwamba unaweza kufanya kila kitu?
Je ni kujenga ajira kweli huku kama wale watu wenye madaraka tayari wataendelea kulimbikiziwa madaraka?Wale vijana amabao wanamemaliza vyuo vyetu je wao wataenda kufanya kazi wapi au hadi wajiunge na CCM?

Kibanda angolewa jicho nchini Afrika ya Kusini



Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (Tef), Absalom Kibanda ambaye amelazwa Hospitali ya Millpark, Johannesburg nchini Afrika Kusini kutokana na kupata majeraha makubwa baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana, ameng’olewa jicho.


Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tef, Neville Meena inaeleza jana aliingizwa kwenye chumba cha upasuaji katika hospitali hiyo, kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji na kurekebishwa sura.


“Nachukua fursa hii kuwapa maendeleo ya tiba ya Mwenyekiti wa Tef Absalom Kibanda, ambaye amelazwa Hospitali ya Millpark, Johannesburg nchini Afrika Kusini, leo ameingizwa theater (chumba cha upasuaji) ili kuanza kufanyiwa upasuaji na kurekebishwa sura, baada ya kupungua kwa uvimbe katika majeraha aliyokuwa nayo sehemu mbalimbali za mwili wake, hususan kichwani na usoni,” alisema Meena katika taarifa yake hiyo.

Meena alifafanua kuwa upasuaji huo unazingatia matokeo ya uchunguzi uliofanywa kwa zaidi ya saa 48 na jopo la madaktari, ambao walibaini kwamba mbali na madhara ya awali, Kibanda pia aliumizwa taya lake la kushoto.

“Kuhusu jicho lake la kushoto ambalo pia lilijeruhiwa, madaktari walisema wangetoa uamuzi kuhusu aina ya upasuaji ambao wangeufanya baada ya kubaini hali halisi, wakati watakapokuwa wakirekebisha sura yake ambayo iliharibiwa kwa majeraha,” alisema.

Alisema Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd ambao ni wachapishaji wa magazeti ya Rai,

Mtanzania, Dimba na Bingwa, bado ana maumivu makali kutokana na majeraha aliyopata, kwani hata wakati akipelekwa kwenye upasuaji huo uliotarajiwa kuchukua saa zaidi ya nne, alikuwa akilalamika kwa maumivu zaidi kwenye kidonda kilichopo kwenye mguu wake wa kushoto.


“Tutaendelea kufahamishana kila hatua ya tiba ya mwenyekiti wetu, na tunaomba tuendelee kumwombea ili apone haraka,” alisema Meena.

Juzi jopo la madaktari wanaomtibu katika hospitali hiyo walibaini madhara zaidi aliyoyapata Kibanda, kutokana na unyama aliofanyiwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia Jumatano wiki hii.

Madhara hayo ni pamoja na kukatika kwa mshipa unaounganisha pua na mdomo, kulegea kwa meno sita, awali ilibainika kuwa ametobolewa jicho lake la kushoto, kung’olewa meno mawili, kunyofolewa kucha, kukatwa mara tatu kwenye kichwa chake.


Katika hatua nyingine, Rais Jakaya Kikwete jana alimtembelea Kibanda hospitalini alikolazwa akiongozana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.


Meena alisema Rais Kikwete amesema Serikali itajitahidi kuwasaka waliohusika na tukio la utesaji wa Kibanda, ili wafikishwe mahakamani kwa mujibu wa sheria.

Rais Kikwete na Kinana wapo Afrika Kusini kwa ziara ya kikazi, ambapo waliamua kutumia fursa hiyo kwenda kumtembelea mhariri huyo.

Hadi Kibanda anasafirishwa kwenda Afrika Kusini Alhamisi wiki hii kwa matibabu zaidi, viongozi wa Serikali waliofika kumjulia hali ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi pamoja na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, wahariri na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari nchini.

Balozi India ahoji uadilifu viongozi nchini


“Sielewi vizuri sababu za Tanzania kutowashtaki mahakamani viongozi wanaokataa kutaja mali, labda ndivyo mnavyotaka, lakini nchini kwetu mali za viongozi ziko wazi, tena iko tovuti maalumu ambayo viongozi huandikwa mali zao, sisemi sheria zenu mbaya, bali ni maamuzi yenu Watanzania kuangalia,” alisema Shaw katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hii jana ofisini kwake.


Wakati Watanzania wakiilalamikia Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuwa ni mzigo kwa taifa kwa vile haina meno ya kuwashughulikia wanaokataa kutaja mali, Balozi wa India nchini, Debnath Shaw anasema kwao usipotaja mali unashtakiwa.

“Sielewi vizuri sababu za Tanzania kutowashtaki mahakamani viongozi wanaokataa kutaja mali, labda ndivyo mnavyotaka, lakini nchini kwetu mali za viongozi ziko wazi, tena iko tovuti maalumu ambayo viongozi huandikwa mali zao, sisemi sheria zenu mbaya, bali ni maamuzi yenu Watanzania kuangalia,” alisema Shaw katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hii jana ofisini kwake.

Hapa nchini iko sheria inayowataka viongozi kutangaza mali zao, hata hivyo, hakuna rekodi yoyoye inayoonyesha kama kuna kiongozi yeyote nchini aliyewahi kufikishwa mahakamani kwa kukataa kwake kutaja mali alizonazo.

Hali kadhalika mali zinazotangazwa haziko wazi kwa wananchi, hata mtu anapokwenda ofisi za tume ya maadili ili kujua kiongozi gani anamiliki nini, hatakiwi kudurufu alichokiona wala kutangaza, hivyo kuondoa maana au umuhimu wa chombo hicho.

India yakataa kuikopesha tena Tanzania

Balozi huyo pia alizungumzia taarifa za India kukataa kuikopesha tena matrekta Tanzania akisema “Hatujakaa kutoa mkopo kwa sababu nyingine zozote, bali mkopo una taratibu zake”.

Hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete alilitaka Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (Suma JKT), kulipa deni.Serikali za India na Tanzania ziliingia mkataba wa mkopo wa Sh40 bilioni kwa ajili ya ununuzi wa matrekta ambayo yalikabidhiwa kwa Suma JKT, hata hivyo kumekuwa na kashfa za baadhi ya vigogo kunufaika isivyo halali na matrekta hayo, tofauti na ilivyolengwa kwamba yangekopeshwa zaidi wananchi wa kawaida wanaojihusisha na kilimo.

Mkopo huo uliosainiwa mwaka 2010 utadumu kwa miaka mitano huku Tanzania kupitia Suma JKT, ikitakiwa kulipa Sh42 bilioni ikiwemo riba.

Hadi sasa Suma JKT imekusanya Sh16 bilioni ambazo ni kiasi kidogo ikilinganishwa na ukubwa wa deni, jambo ambalo Kikwete alikiri lingeweza kuifanya isikidhi vigezo vya kukopeshwa tena.

Hivi karibuni Tanzania iliomba tena mkopo, lakini India ilikataa. Balozi alipoulizwa kama kutolipwa madeni kwa ufasaha ni sababu ya kutokopeshwa tena alijibu kwa kifupi “Nafikiri madeni yanapolipwa, tutapata nguvu za kukopesha zaidi”.

Alipoulizwa kuhusu Serikali kuwa na deni kubwa, hivyo kuwekewa vikwazo vya kupewa mikopo, Waziri wa Fedha, William Mgimwa alisema kuwa jambo hilo analifahamu na kutaka atafutwe leo mchana ili aweze kulitolea ufafanuzi.

Mgimwa ambaye ni mbunge wa Kalenga alisema, “Kwa sasa niko jimboni, ila kuhusu hili suala la Suma JKT naomba unitafute kesho (leo) mchana tutazungumza na kukupa ufafanuzi zaidi.”

Uhuru Kinyatta atafuata nyayo za baba yake?




Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta amewashukuru wananchi pamoja na Mwenyezi Mungu kwa kumwezesha kushinda nafasi hiyo huku akiahidi kuijenga upya Kenya.

Uhuru amesema ataweka kipaumbele kwenye kutunza rasilimali za nchi na kuhakikisha zinawanufaisha wananchi wote, pia kuwawezesha wanawake na vijana.
Katika hotuba yake aliyotoa muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi jana, Kenyatta alisema anawashukuru wagombea alioshirikiana nao katika mchakato wote wa uchaguzi na kuwakaribisha kuungana.


“Nawashukuru wagombea wenzangu wote kwa kujitolea kwa moyo kushiriki katika kinyang’anyiro hiki kwa kuwa jambo hilo limezidi kuonyesha demokrasia iliyopo nchini,” alisema.


Aliongeza kuwa anaahidi kushirikiana vyema na wagombea hao akiwamo Raila Odinga kwa ajili ya kuijenga upya nchi yao, akiwakaribisha na kuwataka waondoe kinyongo kutokana na ushindi alioupata.


“Tulianza zoezi zima kama timu na nitashirikiana nanyi kama timu, ikiwamo kuhakikisha tunafuata yale yote yaliyopo kwenye katiba hususan kuhakikisha kila mwananchi anapata haki yake anayostahili.”


Kiongozi huyo pia aliwashukuru watu mbalimbali waliofanikisha uchaguzi huo kwenda vyema ikiwamo vyombo vya habari katika nchi hiyo ambavyo vilikwenda sambamba katika kuripoti matukio yote ya uchaguzi, pamoja na vyombo vya usalama vilivyosimamia chaguzi hizo.


“Usalama bado ni tatizo katika nchi yetu, lakini ningependa kuvishukuru vyombo husika kwa kufanikisha tunavyozidi kuendelea suala hilo litakuwa vizuri,” alisema.

Uhuru alieleza hayo baada ya Tume Huru ya Mipaka na Uchaguzi (IEBC) kumtangaza kuwa mshindi katika uchaguzi uliofanyika Machi 4 akiwa amegombea kwa tiketi ya muungano wa Jubilee.

Uhuru aliibuka mshindi katika uchaguzi huo kwa kupata zaidi ya asilimia 50 ya kura zilizohitajika ili kupata ushindi kulingana na mahitaji ya Katiba Mpya ya nchi.

Matokeo yaliyotolewa na IEBC yanaonyesha kuwa Uhuru alipata kura 6,173,433 ambazo ni asilimia 50.07 huku mpinzani wake Raila Odinga akipata 5,340,546 ambazo ni asilimia 43.28.

Kwa ushindi huo, Uhuru amepata idadi kubwa ya kura inayohitajika na Katiba Mpya ambayo ni zaidi ya asilimia 50+1 na kuzuia uwezekano wa kurudiwa kwa uchaguzi.

Uhuru pamoja na mgombea mwenza wake, William Ruto wamepata ushindi huo huku wakiwa wanakabiliwa na mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.

Ushindi huo umepingwa na mpinzani mkuu wa Uhuru, mgombea urais kupitia muungano wa Cord, Raila Odinga ambaye amesema ‘kamwe hawatayatambua’ na kuahidi kuyapinga mahakamani.

Akizungumza muda mfupi baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Odinga alisema anajiandaa kwenda mahakamani kupinga matokeo ya urais yaliyompa ushindi Uhuru.

Odinga, aliwaambia waandishi wa habari kuwa matokeo yaliyotolewa na tume hiyo yalikuwa yamehujumiwa hasa baada ya kutokea hitilafu katika mitambo ya elektroniki iliyokuwa inatumiwa katika shughuli hiyo.

“IEBC imerudia makosa yaleyale ya uchaguzi mkuu wa 2007, kwa kuwa tuna mahakama tunayoiamini tunaomba watu wetu watulie hadi mahakama itakapotoa uamuzi. Wenzetu pia wajiepushe na aina yoyote ya ghasia,” alisema.

Alisema kwamba hana tatizo la kushindwa iwapo ameshindwa kihalali, lakini kwa matokeo haya ana jukumu kubwa la kupinga mahakamani ili kulinda mahitaji na heshima ya wapiga kura.

Aidha, alisema kugoma kwa mitambo hiyo kulichanganya mambo katika shughuli ya kuhesabu kura.

Alisema kuwa baada ya kutokea hitilafu, kura alizokuwa amepata katika maeneo bunge ambayo ni ngome zake, ziliongezwa kwenye hesabu ya kura za muungano pinzani wa Jubilee.

Siku moja kabla ya kutangaza matokeo hayo, IEBC ilikiri kuwa matatizo yaliyosababishwa na mtambo wake wa kupeperusha matangazo ni pamoja na kuongeza mara nane kura zilizoharibika.

Baadhi ya wananchi walieleza kuwa na wasiwasi kuhusu idadi kubwa ya kura zilizoonekana kuharibika, kwani zilikuwa kura zaidi ya 300,000 ambapo kwa sasa zimepungua mpaka kufika idadi ya kura 80,000, baada ya kuhakiki kura hizo kwa mara ya pili.

Pingamizi lao lilikataliwa

Mapema wiki hii, wakati shughuli ya kuhesabu kura za urais ilikuwa inafanyika, wanaharakati walifungua kesi mahakamani kutaka uchaguzi usimamishwe kutokana na hitilafu mbalimbali zilizotokea , lakini mahakama kuu ilitupilia mbali kesi yao ikisema kuwa haina uwezo wa kufanya uamuzi katika kesi hiyo, na kuwa ni mahakama ya juu zaidi pekee inayoweza kusikiliza kesi hiyo.

Matokeo hayo na mivutano yote iliyopo kwa sasa vinatokea baada ya siku tano tangu Wakenya kupiga kura kuchagua rais, magavana, maseneta, wabunge, wawakilishi wanawake na wawakilishi wodi.

Tume ya uchaguzi ilichukua zaidi ya saa tano kukagua hesabu ya kura hizo kabla ya kutangaza matokeo hayo jana mchana.

Kwa mujibu wa maagizo yaliyopo katika Katiba Mpya ya nchi hiyo, mshindi wa uchaguzi anatakiwa kutangazwa iwapo tu ametimiza masharti ya kikatiba ya kutangazwa kuwa rais wa nne wa Kenya.

Pamoja na ushindi wa kura kwa zaidi ya asilimia 50 lazima awe ameshinda asilimia 25 katika nusu ya kaunti zote 47 nchini Kenya.