Tuesday, 26 February 2013

Serikali yafanya kufuru

*Yapandisha mishahara ya vigogo ghafla Waziri Kombani adai imefuata taratibu,Wengine waongezewa Sh milioni moja
SERIKALI imefanya marekebisho ya mishahara kwa watumishi wake kwa mwaka wa fedha 2012/2013. Sambamba na hilo, mishahara ya viongozi wa Serikali kwa mwaka huo wa fedha, nayo imefanyiwa marekebisho.

Marekebisho hayo ni kwa mujibu wa waraka wenye kumbukumbu namba S/AC 205/ 399/ 01/ 44, kutoka Ofisi ya Rais Ikulu (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), uliotolewa Julai 25, mwaka huu.

Waraka huo, umesambazwa kwa wakuu wote wa idara za Serikali, wakurugenzi wa majiji, manispaa, miji na wakurugenzi wa halmashauri zote za wilaya nchini.

Waraka huo, uliosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu (Utumishi), Hab Mkwizu, umehusisha pia marekebisho ya ngazi za mishahara kwa viongozi hao wa Serikali.

Kwa mujibu wa waraka huo, ngazi za mishahara zilizokuwa zinaanzia TGS I hadi TGS Q, zimebadilishwa na sasa zitasomeka LSS (E) 1 hadi LSS (E) 9.

Watumishi na viongozi wa Serikali walionufaika na marekebisho hayo, ni pamoja na makatibu wakuu wa wizara, manaibu wao pamoja na wakurugenzi wa idara zote za Serikali. Marekebisho hayo yameanza kutekelezwa Julai, 2012.

Hata hivyo, marekebisho hayo yamelalamikiwa na baadhi ya watumishi wa Serikali, wakidai kuwa hayana uwiyano unaoeleweka kati ya mishahara ya wamtumishi wa Serikali.

Marekebisho hayo yanaoneshwa katika kiambatanisho namba 1 cha waraka huo, ambapo watumishi na viongozi hao wameongezewa mshahara usiopungua 400,000.

Mfano mshahara wa mtumishi wa ngazi TGS P, umepanda kutoka Sh 3, 216, 000 hadi Sh 4, 500, 000 katika ngazi mpya ya LSS (E) 9, ongezeko ambalo ni zaidi ya Sh milioni moja.

Mmoja wa wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambaye hakutaka jina lake litajwe, alikosoa marekebisho hayo na kusema kuwa, hayana uwiyano mzuri kati ya mshahara wa mtumishi na mtumishi mwingine.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi), Celina Kombani, amekiri kuwapo kwa marekebisho hayo ya mishahara kwa watumishi na viongozi wa Serikali.

Akizungumza na MTANZANIA kwa njia ya simu, Kombani alisema, marekebisho hayo ni ya kawaida na kwamba yanawagusa watumishi wote wa Serikali bila kubagua.

“Serikali ikifanya marekebisho ya mishahara, inafanya hivyo kwa watumishi wake wote. Hatuchagui nani aongezewe nani asiongezewe ni wote,” alisema.

Alisema vigezo vilivyotumika katika marekebisho hayo, ni pamoja na aina ya kazi, uzoefu na muda aliotumia mtumishi kukaa kazini.

“Unauliza kwanini watumishi wengine wamepewa nyongeza kubwa na wengine kidogo, ndugu yangu sifa zinatofautiana, mtumishi anayeanza kazi leo, hawezi kulipwa mshahara na mtumishi aliyepo kazini kwa miaka 20,” alisema.

Alipoulizwa ni sababu zipi zilizoifanya Serikali kurekebisha ngazi ya mshahara kutoka TGS na sasa kutumia ngazi mpya ya LSS, Waziri Kombani alisema. “Hayo ni masuala ya kitaalamu zaidi.”

Kombani alikiri kima cha chini cha mshahara ni kidogo na kueleza kuwa, Serikali ipo katika majadiliano.

“Kima cha chini kilipanda kutoka Sh 130, 000 hadi Sh 170, 000. Tunajua kima hiki hakitoshi lakini tupo katika majadiliano,” alisema.

Chadema waonyesha picha za video alivyouawa Mwangosi



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeonyesha picha za mnato na video zinazoonyesha jinsi Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Television cha Channel Ten, Daudi Mwangosi, alivyouawa.

Picha hizo zilionyeshwa jana jijini Dar es Salaam, wakati wa kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho kilichohudhuriwa pia na waandishi wa habari. Kikao hicho cha Kamati Kuu kilikuwa ni cha dharura na kilifunguliwa na kuongozwa na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe.


Wakati picha hizo zikionyeshwa wazi wazi, viongozi wa CHADEMA na waandishi wa habari, walishindwa kujizuia kwani baadhi yao walijikuta wakiangua vilio wakionyesha kusikitishwa na jinsi Mwangosi alivyouawa.

Katika tukio hilo, Mbowe ni kati ya waliolia na ilifika wakati akanyanyuka kutoka meza kuu na kwenda nje ya ukumbi, ili asiendelee kushuhudia Mwangosi alivyouawa.

Wakati picha hizo zikionyeshwa kwa zaidi ya masaa mawili, askari polisi walioshiriki kumuua Mwangosi walionekana wazi wazi na pia Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, alionekana pia eneo la tukio akishuhudia Mwangosi akiuawa.

Kwa mujibu wa picha hizo, mwandishi wa habari aliyeanza kukamatwa na askari polisi na kupata kipigo ni Godfrey Mushi wa Gazeti la Nipashe.

Picha hizo za video zilionyesha kuwa, baada ya Mushi kukamatwa, Mwangosi alikwenda kumuokoa mwenzake huyo na alipofika eneo la tukio, askari hao walianza kumpiga na hatimaye kumuua mbele ya Kamanda Kamuhanda.

Picha hizo zinaonyesha kuwa, kabla Mwangosi hajauawa, polisi mmoja alipitisha bunduki yake miguuni kwa polisi mwenzake kisha Mwangosi akauawa.

Baada ya tukio hilo, picha hizo zinaonyesha kuwa, baadhi ya askari polisi waliokuwa wakimpa kipigo Marehemu Mwangosi, walikimbia na kuacha mwili wa marehemu ukiwa vipande vipande.

Kwa mujibu wa picha hizo, polisi hao walipokuwa pembeni, wenyewe kwa wenyewe walianza kulaumiana huku baadhi yao wakimlaumu muuaji na kusema umefanya nini hicho?.

Baada ya hapo, mmoja wa polisi hao alisikika akisema twende tukamchukue mwenzetu na walipofika mahali alipokuwa mwenzao ambaye alikuwa amejeruhiwa kwa bomu lililomuua Mwangosi, gari ya Kamanda Kamuhanda ilisogea karibu na kumpakia askari polisi aliyejeruhiwa.

Picha hizo za video ambazo zinaonekana zilirekodiwa kwa umakini wa hali ya juu, zinaonyesha baada ya mauaji hayo, askari walishikwa na butwaa huku baadhi yao wakionekana kushika pua.

Wakati hayo yakiendelea baadhi ya askari ambao ni wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), walionekana katika mkanda huo wa video, wakifungua kofia zao zilizokuwa zimefunika uso na macho yao, ili waone vizuri maiti ya Mwangosi iliyokuwa vipande vipande.

Wakati wakivua kofia hizo, baadhi yao walikuwa wakinawa nyuso zao kutokana na moshi uliokuwa umesambaa eneo la tukio wakati walipokuwa wakiwatawanya wafuasi wa CHADEMA.

Pia picha hizo, zilionyesha askari polisi mmoja akiwa amevaa kiraia, huku shingoni akiwa na skafu ya CHADEMA lakini baada ya vurugu kuanza, askari huyo alionekana akiivua skafu hiyo na kuiweka mfukoni.

Alipoivua na kuiweka katika mfuko wa nyuma wa kaptula aliyokuwa amevaa, mwenzake mmoja akampa kofia ya kujikinga na moshi kisha askari huyo akachomoa bastola kwa ajili ya mapambano.

Pamoja na picha hizo kuwaonyesha askari polisi walivyotekeleza tukio hilo, Kamanda wa Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) wa CHADEMA, Benson Kigaila, alionekana pia akijibizana na ofisa mmoja wa Jeshi la Polisi, Mkoa wa Iringa kuhusu wafuasi wa CHADEMA kuwepo katika Kijiji cha Nyololo kilichopo Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa.

Vile vile, picha hizo za video, awali zilionyesha marehemu Mwangosi alivyokuwa akimuuliza Kamanda Kamuhanda kuhusu sheria ya kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na maswali hayo yalionyesha jinsi kamanda huyo wa polisi alivyokuwa amechukizwa nayo.

Kutokana na picha hizo, Mbowe alisema huo ni ushahidi wa kutosha kuonyesha jinsi Jeshi la Polisi lilivyokuwa limedhamiria kuua.

Kwa mujibu wa Mbowe, CHADEMA itatoa tamko zito leo kuonyesha ni hatua gani zitachukuliwa baada ya kifo cha Mwangosi.

Serikali yamwaga ajira kwa walimu

SERIKALI imetangaza kumwaga ajira mpya za walimu 28,746 katika shule za msingi na sekondari, kuanzia mwezi huu. Hatua hiyo, itapunguza nusu ya ukosefu wa walimu katika shule za Serikali.

Mpaka sasa, Tanzania ina upungufu wa walimu 57,177 katika shule za Serikali, tatizo ambalo Serikali inasema italimaliza katika miaka michache ijayo, kutokana na idadi kubwa ya walimu wanaofundishwa katika vyuo mbalimbali kuhitimu masomo.

Rais Jakaya Kikwete, alitoa kauli hiyo mjini Igunga juzi, ambapo alisema kati ya walimu watakaoajiriwa na kusambazwa, 14,600 watakuwa wa shule za msingi, walimu 14,060 watakuwa wa shule za sekondari na 80 watakuwa walimu wa vyuo vya ualimu.

Akihutubia maelfu ya wananchi wa mjini Igunga kwenye Uwanja wa Barafu, Rais Kikwete alisema mikoa yenye uhaba mkubwa zaidi wa walimu, ndiyo itapewa kipaumbele katika mgawo huo wa walimu.

Mkoa wa Tabora ni moja ya mikoa yenye uhaba mkubwa wa walimu, ikiwa na ukosefu wa walimu 2, 055 na Wilaya ya Igunga pekee inahitaji walimu 285.

Hii itakuwa mara ya pili, Serikali kuajiri na kusambaza idadi kubwa ya walimu wa shule za msingi na sekondari katika jitihada za kumaliza tatizo hilo.

Mwaka juzi, Serikali iliajiri na kusambaza walimu 24,621 ambao kati yao 11,379, walikuwa wa shule za msingi, walimu 13,246, walikuwa wa shule za sekondari na walimu 42 walikuwa ni wa vyuo vya elimu.

Wakati shule za Serikali, zinaendelea kukabiliwa na upungufu wa walimu, shule binafsi zina ziada ya walimu, shule za msingi zikiwa na ziada ya walimu 2, 857 na zile za sekondari zikiwa na ziada ya walimu 459, hali inajionyesha katika matokeo mazuri ya mitihani kwa wanafunzi wa shule hizo.

Rais Kikwete aliwaambia wananchi kuwa Serikali, inakabiliana ipasavyo na matatizo mengine yanayoikabili sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maabara, ukosefu wa nyumba za kutosha za walimu na ukosefu wa vitabu vya wanafunzi.

Pia alizungumzia suala la huduma ya maji, akisema Serikali imeonyesha jitihada za kukabiliana na ukosefu wa maji katika maeneo mbalimbali ya Tanzania.

Kwa upande wa Igunga, Rais Kikwete alisema kufuatia kuzinduliwa kwa mradi wa Maji wa Bulenya, mji wa Igunga na vijiji vitatu vinavyozunguka mji huo sasa vinapata maji kwa asilimia 70.
CWT YAJIBU
Akizungumzia ajira mpya za walimu, Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania, Ezekiel Oluochi, alisema Serikali imefanya jambo la maana, lakini imechelewa kuchukua hatua haraka.

“Naipongeza Serikali, lakini kimsingi natofautina na Serikali katika hili, imechelewa sana kutoa ajira kwani takwimu zinaonyesha kuna upungufu wa walimu 150,000 kwa shule za msingi na 50,000 shule za sekondari.

“Mpaka sasa walimu waliopo ni 234,054, tunahitaji walimu 200,000, kwa maana hiyo walimu waliopo hivi sasa ni asilimia 90,” alisema Oluochi.

Aliitaja mikoa ambayo, inakabiliwa na uhaba wa walimu, kuwa ni Shinyanga, Singida na Arusha katika wilaya za Ngorongoro, Longido na Monduli.

Aliitaja mikoa mingine na wilaya zake kwenye mabano kuwa ni Dodoma (Kondoa), Kagera (Muleba), Mwanza (Ukerewe, Misungwi), Tabora (Uyui, Sikonge na Urambo), Lindi (Kilwa, Nachingwe, Liwale, Ruangwa, Lindi Mjini na Lindi Vijijini).

Alisema mikoa ya Mtwara na Lindi, ina hali mbaya zaidi kuliko mingine Tanzania.

“Sababu kubwa ya mikoa hii kuwa na hali mbaya, inatokana na mazingira magumu wanayokutanayo walimu wapya wanaopangiwa huko.

“Asilimia 12 ya walimu wapya wanaoajiriwa, wanaacha kazi hasa wa shule za msingi na walimu wenye shahada ambao wengi wao wanapelekwa vijijini na kujikuta hawatimizi ndoto zao,” alisema Oluochi.

Alisema kama kweli Serikali imedhamiria kumaliza tatizo hilo, basi kuanzia sasa ihakikishe walimu wapya wote wanalipwa stahiki zao, ikiwa ni pamoja na nauli, posho ya siku saba na fedha za kusafirishia mizigo ya tani moja na nusu, kama sheria inavyotaka.

Monday, 25 February 2013

MAUAJI YA PADRI Z'BAR Pengo atoa tamko zito

SIKU moja baada ya Padri Evaristus Mushi wa Kanisa Katoliki la Minara miwili Zanzibar, kuuawa kwa kupigwa risasi tatu kichwani na watu wasiofahamika, Askofu Mkuu wa kanisa hilo Jimbo Kuu
la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo,
ametoa tamko zito kwa Serikali.


Padri Mushi aliuawa juzi asubuhi wakati akishuka katika gari lake
ili kwenda kuongoza ibaada katika Kanisa la Betras ambapo tayari Jeshi la Polisi nchini, limeanza uchunguzi wa kina ili kuhakikisha wahusika wa tukio hilo, wanakamatwa kwa gharama yoyote.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana,
Kardinali Pengo alivitupia lawama vyombo vya ulinzi na usalama
kwa kushindwa kuzuia mifarakano kati ya dini moja na nyingene.

Alisema vyombo hivyo vimeshindwa kusoma alma za nyakati kwani baada ya tukio la kupigwa risasi Padri Ambrose Mkenda wa kanisa hilo Parokia ya Mpendaye, Desemba 24,2012, wafuasi wa Jumuiya ya Uamsho Zanzibar walisambaza vipeperushi vilivyokuwa na ujumbe uliokusudia kufanya jambo kubwa la uhalifu.

“Vipeperushi hivi vilikuwa na ujumbe unaosema, mapambano yataendelea hivyo vyombo vya ulinzi na usalama vilipaswa
kufanya uchunguzi wa kina ili kuzuia ualifu uliopangwa
kufanywa na wafuasi hao.

Aliongeza kuwa, tukio la kuuawa Padri Mushi halikutokea kwa dharura bali vyombo hivyo vilikuwa vinafahamu mkakati wa
jumuiya hiyo lakini bado vilishindwa kuchukua hatua.

“Padri Mushi hakuuawa akiwa baa wala sehemu nyingine tofauti na eneo lake la kazi bali mauaji yamemkuta akiwa kanisani ambako alikwenda kutekeleza jukumu lake la kikzai,” alisema.

Alisema mauaji hayo ni pigo kubwa kwa Taifa ambapo usaalama
wa imani moja ukikosekana kutokana na imani ya dini nyingine
ni tatizo na haijulikani nini kitatokea siku za mbeleni.

Alivitaka vyombo hivyo kuwa makini, kusoma alama za nyakati
ili kuzuia machafuko yanayoendelea yasitokee tena na kuwakata
waumini wa kanisa hilo, kutolipiza kisasi badala yake watulie, kuomba amani na kumuombea Padri Mushi.

Aliwataka Mapadri wengine wa kanisa hilo kuchukua tahadhari
ili kujiepusha na vitendo vya uhalifu dhidi yao na kusisitiza kuwa, umefika wakati wa viongozi wa nchi kulinusuru Taifa lisigawanyike kwa misingi ya imani za dini.

Kardinali Pengo, alisema Februari 24 mwaka huu, kanisa hilo litafanya ibada kubwa Zanzibar na Dar es Salaam kwa ajili ya kumuombea Padri Mushi.

Aliongeza kuwa, vipeperushi vilivyomfikia ambavyo alidai vimesambazwa na wafuasi wa jumuiya hiyo vina ujumbe
unaosema; “Kwa nguvu hizo, tumeweza kuyachoma makanisa
yao na kumtuliza kibaraka wa Kiislamu Soroga, alhamdulillah
hata nje hatoki (laanatullah).

“Lakini nguvu za ushindi mkubwa tulioupata ni huu wa kuwatuliza Makatoriki katika mkesha wao wanaoujua wenyewe (laanatullah), kumkosa Ambrose wa Kanisa la Mpendae, haijawa mwisho wa mapambano, tutahakikisha kila kiongozi wa Makanisa hapa
Zanzibar, hapati nafasi tena ya kuendeleza ujumbe wao”

“Wapenzi Waislamu, viongozi wetu (waliopo mahabusu), wanaendelea vizuri, ipo siku watatoka ishallah kwa nguvu za
allah, jambo kubwa la faraja viongozi wetu waliomo ndani ya Serikali na nje ya nchi, wametuhakikishia huu ndio mwisho wa kusherehekea sherehe za Mapinduzi (laanatullah)”

“Vijana wetu waliokuwa masomoni Somari, wametuhakikishia
kabla ya kusherehekea siku ya kuzaliwa Mtume Mohamed (s.a.w), kutatokeza sherehe nyingine yoyote,” ulisema ujumbe huo.

Katika ujumbe huo, Soroga ambaye ametajwa na wafuasi hao ni Katibu wa Mufti wa Zanzibar na jina lake kamili ni Shekhe Fadhil Soroga ambaye alimwagiwa tindikali na kukimbizwa Dar es Salaam ili kupata matibabu zaidi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kardinali Pengo alisema, kutokana na vyombo hivyo kukosa umakini, ndiyo maana vipeperushi vyenye ujumbe mzito kama
huo, vilisambazwa hadi kumfikia yeye ambaye ni kiongozi wa
ngazi ya juu katika kanisa hilo jambo ambalo kama hatua za
haraka hazitachukuliwa, kutatokea madhara makubwa.

Dkt. Shein ashtushwa

Kutokana na mauaji hayo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein, amepokea msiba
huo kwa mshtuko mkubwa, kutoa pole kwa waumini, ndugu,
jamaa, marafiki na wananchi wote wa Zanzibar.

Akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Dkt. Shein, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Bw. Mohamed Aboud Mohamed, alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga upya kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama na vyengine kutoka nchi za nje ili kuongeza nguvu ya kuwasaka wauaji.

“Zipo kasoro katika Jeshi la Polisi lakini limekuwa likifanya kazi nzuri, nawaomba wananchi mtoe ushirikiano ambao utafanikisha kukamatwa wahalifu wanaofanya matukio mbalimbali.

Alisema kutokana na jiografia ya Zanzibar, kuna maeneo
ambayo watu wanaweza kupitisha silaha lakini Jeshi la Polisi
kwa kushirikiana na Vikosi vya SMZ, litaziba mianya yote.

Bw. Mohamed, alikanusha taarifa zilizopo mitaani kuwa silaha nyingi zipo mikononi mwa wasiostahili kuwa nazo na kuwataka kuondoa hofu waliyonayo kwani hizo ni njama za watu wachache wanaotaka kuiingiza nchi katika machafuko ya kidini.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete na Dkt. Shein hawapendi kusikia vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani vikitokea nchini, kutokana na sababu hizo wameomba
msaada kwa nchi nyengine kuja kufanya uchunguzi wa
kuwabaini wahusika wanaofanya vitendo hivi,” alisema.

Maalim Seif alaani

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amelaani mauaji ya Padri Mushi na kusema kitendo hicho kimevuruga sifa njema ya Zanzibar kuwa kisiwa cha amani.

Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), aliyasema hayo Kisiwani Pemba wakati akifungua semina
ya madiwani wa chama hicho.

Alisema mauaji hayo hayakubaliki kwani Wazanzibari wamekuwa wakiishi kwa kuvumiliana hivyo ni wajibu wao kuendeleza sifa hiyo kwa kuendeleza upendo dhidi yao na kuwapa matumaini wageni wanaokuja kuitembelea Zanzibar kwa shughuli mbalimbali.

Marekani walaani mauaji

Katika hatua nyingine, Serikali ya Marekani imelaani vikali tukio
la mauaji ya Padri Mushi na kutoa salamu za pole kwa ndugu,
jamaa na marafiki wa familia ya marehemu.

Balozi wa Marekani nchini, Bw. Alfonso Lenhardt, aliyasema hayo katika taarifa yake aliyoituma kwa vyombo vya habari na kusisitiza kuwa, nchi yake ipo tayari kushirikiana na Watanzania ili kukomesha matukio ya aina hiyo.

Alisema vurugu za kidini hazipaswi kupewa nafasi Tanzania nchi ambayo inasifika kwa amani na utulivu, umoja na mshikamano
wa Watanzania wote.

“Watanzania mnapaswa kupuuzia vurugu hizi ambazo zinachochewa na watu wachache wenye dhamira ya kusambaratisha amani, utulivu, usalama na taswira ya muonekano bora wa ardhi yenu,” alisema.

Jumuiya ya Maimamu

Nayo Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) imedai kupokea taarifa za mauaji hayo kwa masikitiko makubwa na kulaani kitendo hicho ambacho wamekihusisha na uharamia ili kuitia doa Zanzibar.

Taarifa waliyoitoa kwa vyombo vya habari jana na Katibu wa jumuiya hiyo, Shekhe Juma Muhiddin, imesema Zanzibar ni
kisiwa cha amani na ukarimu tokea enzi na enzi.

Alisema kutokana na mauaji hayo, jumuiya hiyo inawataka Wanzanzibari wote pamoja na dini zote, kuwa watulivu katika
kipindi hiki kigumu, kutunza amani iliyopo na mshikamano
chini ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Kanisa lapigwa moto tena Z'bar *Walianza kulipiga mawe, wahusika wasakwa *Utaratibu wa kuyalinda na polisi waandaliwa



Rushwa yatajwa kutawala ndani ya JWTZ nchini




Kwa ufupi

“Hakuna kitu kibaya kama la rushwa kwenye jeshi, maana kuna fedha nyingi inatembea kutokana na ughali wa vifaa vya kijeshi. Bado Serikali nyingi zinafanya mambo haya kuwa siri na kutoa mwanya kwa rushwa kutembea.

TANZANIA imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi zinazokabiliwa na tatizo la rushwa ndani ya jeshi.
Taasisi ya Transparency International (TI), ambayo hutafiti masuala ya rushwa duniani imeitaja Tanzania kwamba jeshi lake lina rushwa kubwa na ndogondogo.

Kwa mujibu wa gazeti dada la The Citizen la jana Jumapili, uongozi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) umekanusha vikali taarifa ya taasisi hiyo.

TI inadai katika taarifa yake kuwa sekta ya ulinzi ya Tanzania inakabiliwa na tatizo hilo na hiyo ni kutokana na mambo yake kuendeshwa kwa usiri mkubwa.

“Hakuna kitu kibaya kama la rushwa kwenye jeshi, maana kuna fedha nyingi inatembea kutokana na ughali wa vifaa vya kijeshi. Bado Serikali nyingi zinafanya mambo haya kuwa siri na kutoa mwanya kwa rushwa kutembea.
“Fedha inayotumika vibaya kwa masuala ya kijeshi, ingeweza kutumia vizuri zaidi katika masuala ya maendeleo,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo iliyoandikwa na Mark Pyman, ambaye ni Mkurugenzi wa Kitengo cha masuala ya Ulinzi cha Transperancy International.

Transparency International inaeleza kuwa fedha ya rushwa inayotembea kwenye sekta ya ulinzi inakadiriwa kufikia kiasi cha Dola 20 bilioni (Sh32 trilioni).

“Ripoti ya Transparency International itufungue macho Watanzania maana kwa kawaida huwa kila watu wakihoji mapato na matumizi ya jeshi tunaambiwa hatuwezi kujibiwa kwa madai ya woga wa kuhatarisha usalama wa taifa,” alikaririwa mbunge mmoja na gazeti la The Citizen.

Tanzania, hata hivyo, iko juu ya nchi nyingi za Afrika kwa tatizo la rushwa ingawa inatakiwa kurekebisha mianya mingi kwenye sekta hiyo.

“Tunaona Tanzania ina changamoto ya kuimarisha vyombo vya kutupa jicho kwenye jeshi. Mathalani, kuna Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Mambo ya Nje, lakini haina meno ya kuingia kwa undani masuala ya kijeshi,” iliongeza Transparency International.
Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe, hata hivyo, alikaririwa na gazeti la The Citizen akidai kuwa taasisi yake imekuwa ikifanya kazi kitaalamu na kimaadili akitolea mfano jinsi wanavyoajiri wanajeshi kwa kufuata vigezo.

Transparency International inasema kuwa kuna Kitengo cha Utawala Bora cha Serikali ambacho hufanya ukaguzi kwenye jeshi ingawa halijatoa ripoti ya aina yoyote kuhusiana na ukaguzi wa bajeti ya jeshi. “Mfano kuna taarifa kuwa Kitengo cha Kilimo cha Jeshi la Kujenga Taifa (Suma-JKT) kuna kinajishughulisha na uchimbaji madini na biashara nyingine lakini kuna udhibiti mdogo,” iliongeza taarifa yao.

Julai mwaka jana, maofisa saba waandamizi wa Bodi ya Zabuni ya Suma-JKT walifunguliwa mashitaka ya matumizi mabaya ya ofisi na uhamishaji usio wa halali wa zaidi ya Sh 3.8 bilioni.
Waliotuhumiwa ni pamoja na Kanali Ayoub Mwakang’ata, Luteni Kanali Mkohi Kichogo, Luteni Kanali Paul Mayavi, Meja Peter Lushika, Sajini John Laizer, Meja Yohana Nyuchi na Luteni Kanali Felix Samillan wanaodaiwa kufanya makosa hayo mwaka 2009.

Tanzania imewekwa katika Kundi D kwenye orodha hiyo ya Transperancy International ya nchi zinazokabiliwa na kiwango cha juu cha rushwa na vigezo vinavyoangaliwa ni sekta za siasa, fedha, utumishi wa Kundi la D ni nchi ambazo zinakabiliwa na kiwango cha juu cha rushwa na katika orodha hiyo zimo pia nchi za Russia na China.

Hata hivyo, nchi zenye kiwango cha juu cha rushwa ziko katika Kundi F wakati zile zenye kiwango cha chini cha rushwa ziko Kundi A.

“Inasikitisha kuona kuwa Tanzania bado hakuna uwazi katika matumizi ya fedha za jeshi. Hata Kamati ya Bunge ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya nje haina meno,” alikaririwa Semkae Kilonzo wa Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali ya Policy Forum.

Haya yanatokea wakati hivi karibuni Kamati ya Bunge ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje iligawanywa. Sasa kutakuwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama na nyingine itakuwa inashughulikia Mambo ya Nje.

Naibu Waziri aiomba Serikali kupunguza kodi


Kwa ufupi

“Serikali ifanye jitihada ya kuwawekea mazingira mazuri ya kazi wananchi ili waweze kulipa kodi kwa wakati ambayo itapelekwa kwenye maendeleo ya jamii,”

Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Janet Mbene ameiomba Serikali kuwatengenezea mazingira mazuri ya kazi wananchi ili waweze kulipa kodi kwa wakati ambayo itasaidia kuleta maendeleo ya taifa.

Waziri Mbene aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati akifanya ziara ya kukagua nyumba 491 zilizopo eneo la Buyuni Kata ya Majohe Wilaya ya Ilala ambazo zimejengwa na Mradi wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF). Alisema lengo la kujengwa kwa nyumba hizo ni kuwanufaisha wanachama na wananchi na kwamba Serikali itakapoweka mazingira mazuri ya kazi kwa wananchi wake wataweza kulipa kodi ambayo itasaidia kuleta maendeleo katika jamii.

Aliongeza kuwa kila mwananchi ana wajibu wa kuchangia kodi ambayo itafanya kazi ya kuibua miradi mbalimbali ya kuleta maendeleo ya jamii ikiwamo ujenzi wa miundombinu ya barabara
“Serikali ifanye jitihada ya kuwawekea mazingira mazuri ya kazi wananchi ili waweze kulipa kodi kwa wakati ambayo itapelekwa kwenye maendeleo ya jamii,” alisema Mbene.

Pia, aliwataka wanachama wa PSPF kuchangamkia nyumba hizo waweze kununua au kukopa ili kujikwamua na adha ya kupanga ikiwamo kupata nyumba bora na za kisasa.

“Nyumba ni nzuri na zitawasaidia wananchi wa kawaida katika suala la ulipaji wa kodi, wamehakikisha haumizwi katika ulipaji, ndiyo maana wameamua mtu awe analipa kuanzia miaka 15 hadi miaka 20,” alisema na kuongeza:

“Nawaomba PSPF kuhakikisha mahitaji muhimu yote yanayohitajika yanapatikana kama maji, umeme, usafiri na barabara iwekwe kiwango cha lami itamrahisishia mwananchi atakayehamia kuwa na uhakika wa usalama wake,” alisema Mbene. Kaimu Mkurugenzi wa PSPF, Adamu Mayunga alisema wamejipanga kuhakikisha miundombinu ya maji, umeme na barabara ambavyo ni kilio cha muda mrefu kwa wakazi wa eneo hilo vinapatikana.

“Tumeshapata mkandarasi wa Manispaa ya Ilala ambaye amekubali kupeleka greda kwa ajili ya kuchonga barabara na kwa upande wa maji, Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasco) ilitujibu itachukua muda mrefu kufikisha mabomba kwenye eneo hili hivyo tumejipanga kuchimba visima vya maji,” alisema Mayunga.

Alisema nyumba hizo zimejengwa kwa awamu ya kwanza ambazo zipo kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro Shinyanga, Tabora na Mtwara hivyo wanachama hao wanatakiwa kununua popote wanakotaka.

Kwa mujibu wa Mayunga, nyumba hizo zitaanza kuuzwa kwa Sh64 milioni hadi Sh94 milioni kulingana na mahali nyumba ilipojengwa hiyo gharama ikiwa ni pamoja na kodi ya ongezeko la VAT.

Mtoto anayeungua nguo bila kujiona atua Dar



Kwa ufupi

Mwandishi wa habari hizi alifika katika Kanisa la House of Prayer, lililopo eneo la Boko Magengeni alipo Christina, ambapo alionekana akiwa mwenye furaha pamoja na mama yake, Calister Massawe.



CHRISTINA Mjema (12) kutoka mji mdogo wa Kabuku, wilayani Handeni, mkoani Tanga, ambaye nguo zake zimekuwa zikiungua kwa moto bila ya yeye kuungua amefikishwa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya maombi.

Mwandishi wa habari hizi alifika katika Kanisa la House of Prayer, lililopo eneo la Boko Magengeni alipo Christina, ambapo alionekana akiwa mwenye furaha pamoja na mama yake, Calister Massawe.

Akizungumza, Mwanjilisti wa kanisa hilo, Vera Nzowa alisema baada ya kusoma gazeti la Mwananchi Jumamosi toleo la Februari 16 kuhusu mateso aliyokuwa akiyapata binti huyo, uongozi wa kanisa hilo uliamua kuwatuma watumishi wake kwenda kumchukua mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Kabuku mjini Handeni.

“Jumatano iliyopita niliongoza wenzangu kwenda katika eneo la Kabuku ili kumtafuta mtoto huyo, ambaye alikuwa katika mateso makubwa,” alisema.

Nzowa alisema kuwa alipofika katika nyumba hiyo alikutana na mama wa mtoto huyo na kumweleza nia ya kanisa hilo, ambapo kutokana na shida alizokuwa akizipata alikubali.

“Tulikwenda polisi kwa ajili ya kutoa taarifa za kuondoka na mama na mtoto huyo nao walikubali kutokana na matatizo, ambayo wamekuwa wakishuhudia yakimpata mtoto huyo,” alisema.

Alisema baada ya kukabidhiwa na polisi na viongozi wa kijiji hicho kwa ajili ya kuondoka naye, walifanya maombi na kumpaka mafuta ya baraka ili kuzuia moto huo usitokee wakati wakisafiri.

Alisema kuwa walisafiri salama hadi katika kanisa hilo na kufanya maombi, ikiwamo mkesha maalumu, ambao ulifanyika usiku wa Alhamisi iliyopita.

“Tangu amefika kanisani hapa tatizo la nguo za mtoto huyo kuwaka moto halijatokea tena, tuna imani hali ile haitajitokeza tena,” alisema Mwinjilisti Nzowa.

Alisema wamebaini kwamba mtoto huyo amekuwa akiteswa kwa nguvu za giza na ushirikina.

“Hapa wamefika mahali pake, tatizo hili haliwezi kujirudia,” alisema.

Ingawa hakusema lini ataruhusiwa kurudi nyumbani Kabuku, lakini alisema kuna mikesha kadhaa imeandaliwa kwa ajili ya kuendelea kumwombea mtoto huyo.


Katika matokeo ya utafiti huo uliofanywa Desemba mwaka jana, Dk Slaa anafuatiwa kwa mbali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amefungana na Naibu Katibu Mkuu wa


WAKATI baadhi ya wanasiasa wakiwa wameanza kujiwinda kwa ajili ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Shirika la Utafiti la Synovate limetoa matokeo ya utafiti wake ambao unaonyesha vigogo tisa kuwamo katika mchuano huo.

Utafiti huo umeonyesha kuwa endapo uchaguzi huo ungefanyika sasa, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa angeibuka mshindi baada ya kuongoza orodha hiyo akipata asilimia 17.


Katika matokeo ya utafiti huo uliofanywa Desemba mwaka jana, Dk Slaa anafuatiwa kwa mbali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amefungana na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kila mmoja akipata asilimia tisa.


Hata hivyo, licha ya kuongoza, Dk Slaa ameporomoka kwa asilimia 25 ikilinganishwa na matokeo ya utafiti kama huo uliofanywa na taasisi hiyo mwaka 2011 ambapo alipata asilimia 42.


Kadhalika, umaarufu wa Pinda ambaye anaongoza miongoni mwa wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeshuka kwa asilimia tatu kutoka 12 za mwaka juzi, wakati Zitto ameendelea na kiwango kilekile cha asilimia tisa alizopata katika utafiti uliotangulia.
Wengine wanaofuata na asilimia walizopata kwenye mabano ni Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli (8), Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (7) na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (5).


Pia wamo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (4) ambaye amefungana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (4) na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (2).

Ikilinganishwa na utafiti wa 2011, Lipumba ameporomoka kwa asilimia tisa.
Lowassa amepanda kwa asilimia sita, Dk Magufuli asilimia nne, Mbowe na Membe wamepanda kwa asilimia mbili kila mmoja, wakati Sitta amebaki katika kiwango kilekile cha asilimia mbili.


Hata hivyo, utafiti huo umeonyesha kuwa wananchi ambao hawana uamuzi wa kuchagua mtu yeyote kati ya hao kwa sasa ni asilimia 18, likiwa ni ongezeko la asilimia 12 ikilinganishwa na utafiti uliotangulia.

CCM yatamba
Katika utafiti huo, CCM kimeonyesha kuwa ni chama ambacho asilimia 52 ya wananchi wangependa kujiunga nacho, kikiwa kimepanda chati kwa asilimia moja kutoka asilimia 51 mwaka jana.


Kwa upande wa Chadema, wananchi ambao wanapenda kujiunga nacho imeshuka kutoka asilimia 35 mwaka 2011 hadi 31 mwaka jana.


Uwezekano mkubwa wa CCM kupanda chati ni kutokana na ukweli kuwa mwaka jana kilikuwa na uchaguzi ulioanzia ngazi ya mashina hadi taifa na kuibua vuguvugu kubwa masikioni mwa wananchi.


Chadema hakikuwa na harakati kubwa za kisiasa ukiacha kampeni ya Movement For Change (M4C), ambayo kwa kiasi haikuwa na pilika kama uchaguzi wa CCM.
Chama kingine ni CUF ambacho kimeporomoka kwa kupata asilimia 10 mwaka 2011 hadi nne mwaka 2012.


Hata hivyo, asilimia ya wananchi kutokutaka kujihusisha na chama chochote imepanda kutoka asilimia mbili mwaka 2011 hadi 12 mwaka 2012.

Rushwa
Katika suala la rushwa nchini, utafiti huo umeonyesha kuwa kati ya watu 10 waliohojiwa, wanne walikuwa na maoni kuwa rushwa imeongezeka kufikia asilimia 41, asilimia 30 walisema iko palepale, asilimia 23 walisema imepungua na asilimia tano hawajui.tafiti huo unaonyesha kuwa mapambano dhidi ya rushwa hayajabadilika tangu 2011katika taasisi za Serikali ukisema haionekani kama kuna utashi wa kisiasa kupambana na tatizo hilo katika taasisi hizo kama Jeshi la Polisi na Mahakama ambazo zimeonekana kuwa nyuma katika mapambano hayo.


Katika utafiti huo, polisi ndiyo inayoongoza kwa rushwa baada ya asilimia 33 ya watu waliohojiwa kulitaja jeshi hilo, ikifuatiwa na Mahakama asilimia 16 na sekta ya afya ikiwa na asilimia 16.


Utafiti huo umeonyesha matatizo makubwa yanayoikabili nchi kwa sasa ni njaa, gharama za maisha, umaskini, migogoro ya kidini na ukosefu wa ajira.


“Asilimia 50 wametoa maoni kuwa njaa ni tatizo kubwa ikifuatiwa na gharama za maisha asilimia 44, migogoro ya ya kidini asilimia 43 na ukosefu wa ajira asilimia 34.”


“Inamaanisha kuwa rushwa na mfumuko wa bei havichukuliwi kama ni tatizo kwa Watanzania wengi kama ilivyojionyesha mwaka 2011,” inaeleza taarifa ya utafiti huo.
Wananchi wameeleza kuwa mambo muhimu ambayo yanatakiwa kupewa kipaumbele ni pamoja na sekta ya afya kwa asilimia 24, elimu asilimia 21, ajira asilimia 18, chakula asilimia 17 na miundombinu asilimia 16.

Thursday, 7 February 2013

Matokeo ya kidato cha Nne: Wakuu wa shule wadai ilitungwa kwa mfumo tofauti


Kwa ufupi

MATOKEO mabaya ya mtihani wa kidato cha nne yamezidi kuibua mapya, baada ya wamiliki wa shule na vyuo binafsi nchini kusema mitihani ilitungwa kwa mfumo tofauti na uliozoeleka miaka yote, huku tume iliyounndwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ikipondwa na baadhi ya watu.

MATOKEO mabaya ya mtihani wa kidato cha nne yamezidi kuibua mapya, baada ya wamiliki wa shule na vyuo binafsi nchini kusema mitihani ilitungwa kwa mfumo tofauti na uliozoeleka miaka yote, huku tume iliyounndwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ikipondwa na baadhi ya watu.

Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi nchini (TAMONGSCO), Mahmoud Mringo alisema kwamba maswali waliyoulizwa watahiniwa yalikuwa ya kujieleza tofauti na miaka ya nyuma, ambapo mfumo uliotumika uliwataka watahiniwa kutaja vitu tu bila ya kulazimika kuvielezea kwa undani.

Kauli yake iliungwa mkono na Mkuu wa Taaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Marian, Florence Mapunda ambaye alisema kuwa mtihani wa mwaka jana ulitaka zaidi watoto kujieleza tofauti na miaka ya nyuma wakati wanafunzi walipokuwa wanakariri.

Hata hivyo, Msemaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), John Nchimbi alisema mfumo wa mtihani haukubadilika kwa namna yoyote na kuwa upo kama ule wa miaka yote.

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo, kwa upande wake alisema madai yanayotolewa hayana msingi, huku akihoji kwa nini yasitoke tangu mitihani ilipokuwa ikifanyika na badala yake yanatoka baada ya kutangazwa kwa matokeo.

Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana yanaonyesha kuwa watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 wamepata sifuri, huku wanafunzi 23,520 tu ambao ni sawa na asilimia 5.16 ndiyo waliofaulu na wengine 103,327 sawa na asilimia 26.02 wamepata daraja la nne.

Kutokana na matokeo hayo, Waziri Mkuu Pinda, juzi alitangaza kuunda tume ya kuchunguza chanzo cha matokeo hayo kuwa mabaya, hatua ambayo hata hivyo imekosolewa na wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Tume hiyo inayoundwa na wajumbe kutoka Taasisi za Elimu, Chama cha Waalimu, Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii na Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (Tahossa) inatarajiwa kuanza kazi wiki hii.

Profesa Gaudence Mpangala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alisema kuunda tume ni kupoteza muda kwa sababu matatizo na changamoto zote ndani ya sekta hiyo yanajulikana, huku mwenzake, Profesa Chriss Maina pia wa UDSM akisema kuunda tume hakutaisaidia kwa kuwa Serikali inaidharau sekta ya elimu.

“Tatizo ni kutowekeza kikamilifu katika sekta ya elimu, imekuwa na matumizi makubwa katika mambo yasiyokuwa ya lazima,”alisema Profesa Mpangala.

Alisema matatizo mengine ni mazingira magumu ya kufundisha na uhaba wa walimu. “Kinachotakiwa wajipange kufanyia kazi changamoto hizi zilizopo badala ya kuunda tume, wakati fedha nyingi tunasikia inapotea kwenye ubadhirifu,”alisema Profesa Mpangala.

Naye Profesa Maina alisema: “Hiyo tume ya kazi gani kwa sababu matatizo yanafahamika wazi, umewahi kusikia taifa gani ambalo halina mtalaa wa elimu. Hiyo ndiyo hali halisi kwa nchi yetu. ”
Kauli ya TAMONGSCO

Mwenyekiti wa TAMONGSCO, Mringo alisema: “Kwenye mitihani ya miaka ya nyuma, mtu alikuwa anaulizwa kwa mfano, taja sehemu tatu za mti. Akitaja mizizi, shina na matawi anakuwa amepata.”

Aliongeza: “Mwaka jana mtihani ulivyokuwa ni kwamba walikuwa wanatakiwa kutaja sehemu tatu za mti, halafu wanaambiwa waseme ni nini kinazunguka mti huo. Hapo ndiyo ilifanya mambo kuwa magumu.”

Mringo alisema mfumo huo umetokana na mtalaa mpya ambao unataka zaidi kuangalia uwezo tofauti na ule wa nyuma ambao uliwafanya wanafunzi wawe wanakariri zaidi, lakini akakosoa utaratibu wa kuanza kutumika kwake bila watahiniwa kufundishwa.

Kwa mujibu wa Mringo, ili watoto waweze kujibu aina hiyo ya maswali, inatakiwa waandaliwe kuanzia kwenye shule za msingi.

Alisema pia kuwa, mwaka huu alama za maendeleo ya mwanafunzi katika mitihani ya shule (continuous assessment) hazikutumika kama miaka mingine ambayo alama hizo zilikuwa zikichangia kwa asilimia 40 katika mtihani wa mwisho.

Mringo alizitaja sababu nyingine kuwa ni pamoja na wizi na udanganyifu wa mtihani ulidhibitiwa kwa kiasi kikubwa.

Naye Mapunda alisema:“ Mtihani wa mwaka jana ulikuwa unapima zaidi uwezo wa watoto kuelewa siyo kukariri. Miaka ya nyuma watoto walikuwa wanaogopa zaidi mitihani ya ndani ya shule kuliko ile ya nje, ukiwaambia wasome kwa ajili ya mtihani wa taifa wanasema haina shida siyo migumu na kuwa ile ya ndani ndiyo ilikuwa migumu zaidi.”

Necta na Mulugo

Msemaji wa Necta, Nchimbi alisema mfumo wa mitihani ulibadilika 2008 baada ya mtalaa kubadilika kwa kuondoa baadhi ya mada za masomo na kuweka mpya.

“Tangu 2008, mitalaa ya fizikia na kemia tu ndiyo haikubadilika, yenyewe ilikuja kubadilika 2011 na katika kipindi chote mitihani imekuwa ikitungwa kwa mfumo huo huo na hakuna watu waliolalamika,” aliongeza Nchimbi.

Naye Mulugo alisema kwa sasa watu wanatoa sababu nyingi na kuhadharisha kuwa ni vizuri wakaiachia tume iliyoundwa na Waziri Mkuu ifanye kazi yake.
Mulugo alisema Necta ni chombo cha kusimamia mitihani, lakini mitihani inatungwa na walimu pamoja na maofisa elimu na kusahihishwa na walimu wenyewe.

“Kwa nini haya madai wayatoe sasa hivi, sababu za msingi ninazoziona mimi ni kuwa watoto sasa hivi hawasomi, hebu tuache tume iliyoundwa ifanye kazi yake kwa sababu itaangalia ngazi zote za mitihani,”alieleza Mulugo.