Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa Mkoa huo, Kanali Mstaafu Fabian Massawe, katika taarifa yake kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk.
SERIKALI mkoani Kagera, kupitia vyama vya kuweka na kukopa, imevikopesha vikundi vya vijana, zaidi ya Sh83 milioni ili kuwawezesha vijana kujiajiri na kujikwamua kiuchumi .
Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa Mkoa huo, Kanali Mstaafu Fabian Massawe, katika taarifa yake kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk.
Fenella Mukangara aliyetembelea mkoa huo, kuangalia namna fedha za mkopo kutoka mfuko wa vijana zilivyoweza kusaidia vijana kujikwamua kimaisha.
Kanali Mstaafu Massawe alisema mikopo hiyo ilitolewa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita na kwamba hatua hiyo inalenga katika kusimamia utekelezaji wa sera ya maendeleo ya vijana. Alisema chini ya sera hiyo, Serikali imekuwa ikiratibu shughuli za mifuko ya vijana na kufuatilia utoaji na urejeshaji wa mikopo.
No comments:
Post a Comment