Mtanange wa kombe la mabara(Confederation cup) unaoendelea huko nchini
Brazil leo utafikia tamati ambapo ni fainali kati ya Brazil na Spain .
Kwa Brazil hii ni furaha kwao kuingia fainali kwani wana historia nzuri
ya fainali kwenye mtanange huo na mara tano za mwisho kuingia fainali
hawajapoteza mchezo. Kwa Spain hii ni changamoto kubwa hasa baada ya
kupita kwa mikwaju ya penati na hali ya Brazil kutumia faida ya kuwa
nyumbani . Hata hivyo kocha wa Brazil (Scolari) amesema amejiandaa vyema
na mchezo huo, atawatumia wachezaji wake wazuri kupambana na Spain na
dakika 90 zitaamua mshindi kati yao. Timu hizo mbili mara ya mwisho
kucheza ni miaka 14 iliyopita ambapo walitoa suluhu ya 0 - 0.
Mtanange huo utapigwa usiku wa leo (Saa Sita Kamili Usiku- Saa za Afrika Mashariki)
Wakati vigogo hao wawili wakipambana kwenye fainali hiyo, Uruguay na Italy watakuwa wanashindania mshindi wa tatu.
Mtanange huo utapigwa usiku wa leo (Saa Sita Kamili Usiku- Saa za Afrika Mashariki)
Wakati vigogo hao wawili wakipambana kwenye fainali hiyo, Uruguay na Italy watakuwa wanashindania mshindi wa tatu.

No comments:
Post a Comment