Sunday, 30 June 2013

SPORTS: FAINALI CONFEDERATIONS CUP BRAZIL VS SPAIN LEO USIKU

Mtanange wa kombe la mabara(Confederation cup) unaoendelea huko nchini Brazil leo utafikia tamati ambapo ni fainali kati ya Brazil na Spain . Kwa Brazil hii ni furaha kwao kuingia fainali kwani wana historia nzuri ya fainali kwenye mtanange huo na mara tano za mwisho kuingia fainali hawajapoteza mchezo. Kwa Spain hii ni changamoto kubwa hasa baada ya kupita kwa mikwaju ya penati na hali ya Brazil kutumia faida ya kuwa nyumbani . Hata hivyo kocha wa Brazil (Scolari) amesema amejiandaa vyema na mchezo huo, atawatumia wachezaji wake wazuri kupambana na Spain na dakika 90 zitaamua mshindi kati yao. Timu hizo mbili mara ya mwisho kucheza ni miaka 14 iliyopita ambapo walitoa suluhu ya 0 - 0.
Mtanange huo utapigwa usiku wa leo (Saa Sita Kamili Usiku- Saa za Afrika Mashariki)
Wakati vigogo hao wawili wakipambana kwenye fainali hiyo, Uruguay na Italy watakuwa wanashindania mshindi wa tatu.

No comments: