Naibu Waziri wa Ujenzi, Gerson Lwenge alitoa taarifa hiyo bungeni jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Temeke, Abas Mtemvu (CCM).
Dodoma. Wizara ya Ujenzi inatekeleza miradi ya Sh. 876.336
bilioni katika Jiji la Dar es Salaam,yenye lengo la kutafutia ufumbuzi
wa kupunguza msongamano wa magari katika Jiji hilo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Gerson Lwenge alitoa
taarifa hiyo bungeni jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Temeke, Abas
Mtemvu (CCM).
Katika swali lake,mbunge huyo alitaka kujua mpango
wa Serikali wa kulitafutia ufumbuzi tatizo la msongamano wa magari
katika Jiji la Dar es Salaam hasa katika Barabara ya Ali Hassan Mwinyi.
Lwenge aliiitaja miradi hiyo kuwa ni Barabara ya
Kimara- Kivukoni, Fire-Kariakoo na Magomeni hadi Morocco na ujenzi wa
karakana na vituo vya mabasi yaendayo kwa haraka pamoja na kuhamisha
nguzo za umeme.
“Barabara ya Mwenge-Tegeta, Barabara ya Kilwa
Bendera Tatu-Mbagala Rangi Tatu, ujenzi wa daraja la Kigamboni, Flyover
ya TAZARA, Barabara ya Gerezani, Barabara ya Mandela na Barabara ya Wazo
Hill-Bagamoyo hadi Msata,’ alisema Lwenge.
Alisema kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya
mabasi yaendayo haraka (RBT) kutoka Morocco kwenda Magomeni hadi
Kivukoni na Kimara kutapunguza msongamano wa magari kati ya Oysterbay
Polisi na Daraja la Salender.
Kuhusu mipango ya baadaye, alisema Serikali
itaangalia uwezekano wa kujenga barabara ya juu pande zote za daraja la
Salender, kupanua barabara kwenye maingilio ya daraja, kujenga lingine
pembeni mwa daraja au kujenga mbadala kutokea Kenyata Drive kuunganisha
na Ocean Road.

No comments:
Post a Comment