Hata baada ya kuhamia Uswis bado maisha yanaendelea kuwa magumu.Alijikuta akiandamwa na majanga zaidi.
Mbembele anaendelea na simulizi yake, anasema
mwishoni mwa mwaka 1999 alifanikiwa kuhamia nchini Uswizi,
alijiandikisha kama mkimbizi kutoka Msumbiji.
Hali ilivyokuwa nchini Uswizi
“Nilivyofika Uswizi, nilipelekwa moja kwa moja kwenye kambi ya wakimbizi iliyokuwapo jimbo la Debendorf katika Jiji la Zurich, nilijitambulisha kama John ‘Chuma’ Fernando kutoka Msumbiji.
Alipokelewa vizuri na maofisa wa uhamiaji na kupewa chumba kilichokuwa na mahitaji muhimu ya maisha ya mtu wa kawaida.
“Nilivyofika Uswizi, nilipelekwa moja kwa moja kwenye kambi ya wakimbizi iliyokuwapo jimbo la Debendorf katika Jiji la Zurich, nilijitambulisha kama John ‘Chuma’ Fernando kutoka Msumbiji.
Alipokelewa vizuri na maofisa wa uhamiaji na kupewa chumba kilichokuwa na mahitaji muhimu ya maisha ya mtu wa kawaida.
“Nilianza maisha mapya katika kambi hiyo,
nilikutana na wazamiaji wengi kutoka nchi za Afrika mashariki na kati
kama Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Demokrasia ya Kongo,”
anasema na kuongeza.
“Maisha yalikuwa mazuri kwa sababu tulikuwa
tunapewa kiasi cha dola 600 kila mwezi pamoja na mahitaji na huduma
nyingine kama za michezo na cha kufurahisha zaidi tulikuwa huru kufanya
mambo yetu”.
“Baada ya maisha ya miaka mitatu kambini pale
ilitokea kampeni ya kuwarudisha watu waliokuwa na mazingira mazuri
nchini mwao kutokana na kuporomoka kwa uchumi katika nchi za Ulaya”
“Kiongozi wa kambi yetu ‘Shefa’ alisikia taarifa
halisi za uraia wangu kuwa ni Mtanzania na akaamua kufikisha taarifa
hizo kwa maofisa wa uhamiaji ambao walinipeleka kwa Balozi wa Msumbiji
kwa mahojiano,” anabainisha na kuongeza;“Nilifikishwa kwa Balozi wa
Msumbiji, nilifanya naye mahojiano kuhusu uraia wangu, baadaye
alinishtukia kutokana na kutokuongea vizuri kireno”
Anasema baada kushtukiwa na balozi alimueleza kuwa
yeye ni Mmakonde wa Msumbiji ambaye hakubahatika kwenda shule ndiyo
maana hakuweza kuongea Kireno kwa Ufasaha.
“Nilimwambia natokea Mweda mji wa Msumbiji unaopakana na Tanzania ambapo watu wake walikuwa wanaongea Kimakonde mchanganyiko na Kireno kama mimi”
“Nilimwambia natokea Mweda mji wa Msumbiji unaopakana na Tanzania ambapo watu wake walikuwa wanaongea Kimakonde mchanganyiko na Kireno kama mimi”
Mbembele anaongea kwa kuonyesha ushujaa wa
kumshinda balozi katika maongezi kwa kumdanganya “Balozi alinibembeleza
nirudi msumbiji lakini nilikataa kwa kudai kuwa sababu nilizoondokea
kule bado hazikutatuliwa”.
“Baada ya maongezi, balozi alishindwa kutafuta
sababu ya kuniruidisha Msumbiji hivyo nikaendelea na maisha ya ukimbizi
pale Dubendorf,”anasimulia kuwa wakati akishangilia ushindi wa
kumdanganya balozi kumbe alikuwa ameshawekwa katika kitabu cha watu
watukutu na wenye makosa.
Matukio ya ushirikina na jaribio la kutolewa sadaka
Baada ya kushinda jaribio la kurudishwa nyumbani Mbembele anasema chuki ilizidi baina yake na baadhi ya raia wa Kenya waliokuwapo kambini hapo na kumtengenezea mazingira magumu ya kuishi.
Baada ya kushinda jaribio la kurudishwa nyumbani Mbembele anasema chuki ilizidi baina yake na baadhi ya raia wa Kenya waliokuwapo kambini hapo na kumtengenezea mazingira magumu ya kuishi.
“Nilikosa rafiki, nilihisi kila mtu ni adui yangu.
Sikuwa na chakufanya zaidi ya kumuomba Mungu na kuendelea na maisha kwa
kuwa raia wengi walikuwa wanarudishwa makwao kwa wingi”.
Anasema siku moja akiwa matembezini alikutana na wazungu watatu
ambao walikuwa wanaelekea katika sherehe kubwa ya utamaduni wa Waswizi
ambayo hujumuisha toleo la sadaka ya damu ya binadamu.
“Kule Uswizi tarehe 1 Agosti kila mwaka
huazimishwa sherehe ya nchi nzima, baadhi ya wenyeji husherekea na kutoa
sadaka ya damu kwa miungu na mizimu yao,” anabainisha Mbembele na
kuongeza;
“Wale watu watatu walinibembeleza tukashirikiane
nao katika sherehe hizo mpaka nikakubali kuandamana nao huku tukitembea
taratibu kuelekea katika msitu mkali uliopo ndani ya milima iliyopo
pembezoni mwa mji”
Huku akionyesha dalili za kusisitiza uwepo wa
uchawi uliopitiliza huko Uswizi, Mbembele anasema “Wanasema Tanzania
kuna uchawi, aaah uchawi Ulaya bwana”
“Tulipoingia katikati ya poli tukielekea katika
viwanja maalumu vya sherehe hizo, mtu mmoja kati ya wale watatu
alibadilika ghafla akawa kama sokwe mkubwa mwenye meno ya kutisha kiasi
cha kunitisha na kufanya niishiwe nguvu” anasema na kuongeza kuwa jambo
hilo lilimtisha mno na kumkosesha raha.

No comments:
Post a Comment