CHRISTIANS and Muslims in Tanzania can be partners in building a society shaped by the values taught by God: tolerance, justice, peace and concern for the poorest and the weakest.” Hiyo ni kauli ya kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani wakati huo, Baba Mtakatifu Yohane Paulo II aliyoitoa kwa Watanzania alipozuru nchini Septemba mwaka 1990.
Kwa tafsiri isiyo rasmi, ujumbe huu ulitaka kumaanisha kwamba, “Wakristu na Waislamu wa Tanzania wanaweza kuwa wadau katika kujenga jamii yenye maadili ya Kimungu; uvumilivu, haki, amani na kuwajali maskini na wanyonge.”
Nimelazimika kuanza na nukuu hii ili kuwaonyesha tu wafuasi wa kweli wa dini hizi jinsi walivyo na jukumu kubwa katika kuunda jamii yenye uvumilivu na mshikamano wa dhati ambao ndio msingi wa namna Mungu anavyotaka tuishi.
Kwa ufahamu mdogo nilionao kuhusu Uislamu (ninaweza kusahihishwa katika hili), ni kwamba jina tu lenyewe linamaanisha unyenyekevu na zaidi sana Uislamu ni dini ya amani na ukiwasikiliza baadhi ya wanazuoni wa Kiislamu wanasema Waislamu pia wamefundishwa namna ya kuishi na watu wasio wa dini yao kwa amani.
Na kwa kweli ziko baadhi ya hadithi zinashuhudia kuwa hata Mtume Mohamad (S.A.W) alipata msaada kwa namna moja ama nyingine kutoka kwa Wakristo na watu wengine wasio Waislamu, wakati anahamia Madina toka Makka.
Lakini pia katika Ukristu, upo msingi mmoja mkubwa wa imani yao, wanatakiwa wawapende jirani zao kama nafsi zao na zaidi sana wanatakiwa wawapende hata adui zao kwa sababu upendo ndiyo amri yao kuu.
Yako masimulizi katika Injili kwamba Bwana Yesu aliwaambia wale wote wanaomfuata na kuamini katika yeye kuwa wanaweza kuwa na uwezo hata wa kuhamisha milima, lakini kama wanatindikiwa na upendo ni kazi bure, utaona ni jinsi gani upendo ulivyo sehemu muhimu ya imani hii.
Bahati mbaya tuliyonayo katika jamii yetu kwa sasa, tumeanza kutumia dini hizi badala ya kuwa daraja la kutuunganisha, kutumia tofauti zetu kama njia ya kutuweka pamoja zaidi, sasa tunatumia tofauti za dini zetu kama sababu ya kuwa maadui na kujenga matabaka hasimu katika jamii yetu.
Kipo kitu kimoja ambacho viongozi na wafuasi wa imani hizi wanatakiwa watambue kuwa ni mpango wa Mungu wanayesema wanamwabudu, kutuumba tukiwa tunatofautiana.
Jinsi ambavyo tunatofautiana sura zetu na mawazo yetu ndivyo ambavyo tunatakiwa tutarajie tutatofautiana katika mitazamo ya mambo mbalimbali ikiwemo ya imani. Hili Mungu wanayemwabudu analijua na ndiyo maana kuna mbingu na jehanamu.
Sasa kama Mungu mwenye kuwaumba Binadamu hawa pamoja na uwezo wake wote usio na mipaka, lakini amewaacha binadamu hawa hawa waamue kuishi maisha watakayo kwa utashi wao binadamu mwingine ni nani mpaka atake watu wote waamini kama anavyoamini yeye?
Wataalamu wa elimu ya genetic wanatuambia kuwa ili kuwe na mtu ambaye anafanana na wewe kwa kila kitu, yaani sura, mawazo unayowaza wewe na yeye awaze hivyo na muwe na mtazamo unaofanana kwa kila kitu, ni lazima mzaliwe watoto laki tatu katika familia ya baba mmoja na mama mmoja, mtoto wa laki tatu na moja ndiye atakuwa anafanana kwa kila kitu na yule mzaliwa wa kwanza wa familia hiyo.
Hapa tunaweza kuona ni jinsi gani haiwezekani kutaka kufananisha mitazamo, kwa kuwa ni Mungu pekee na mwenye uwezo wa kila jambo chini na juu ya jua aliyeamua kutuwekea tofauti hizi na sisi hatuna namna wala uwezo wa kufanya vinginevyo, tunachoweza kufanya ni kutaka kuziishi tofauti hizo kwa manufaa yetu na kuifanya Tanzania iwe sehemu nzuri ya kuishi kila mmoja wetu apendavyo bila kuingilia uhuru wa mtu.
Kwa hakika ni uendawazimu na ujinga wa kiimani kutaka au hata kuthubutu tu kuwaza mikakati na mbinu za kuwafanya watu wote wawe Wakristu au Waislamu, hilo halitawezekana kwa sababu ni Mungu aliyedhamiria kutufaya tutofautiane namna hii, hizi tofauti zetu hatukuchagua wenyewe, tumejikuta kwa njia mbalimbali tuna mitazamo hiyo inayokinzana ambayo siyo lazima itufanye tupigane.
Dini hizi ni kama zinataka kuharibu taifa hili kama tu ambavyo dini zimeharibu mataifa mengine mengi yaliyotukuka kwa kuwa na amani na mshikamano na nguvu za kiuchumi.
Madai yanayoendelea sasa ya nani ana haki ya kuchinja kuliko mwingine, yanaweza kuwa ya msingi kulingana na imani za watu na hapa sitaki kuingia katika mtego wa kupuuza imani ya mtu, lakini hivi waumini hawa wamejiuliza ni kwa kiasi gani maisha ya mtu yana thamani kuliko hiyo nyama wanayogombania kuchinja?
Haiwezekani kwamba, Waislamu na Wakristu ambao hawazidi asilimia 50 ya Watanzania wote wanataka ndiyo wawe madereva wa nchi hii, wapo pia Watanzania wenye haki zao ambao wana haki ya kuishi kwa amani na hapa ndiyo wajibu wa Serikali unapoingia.
Katika hiki, Serikali haiwezi kukwepa wajibu wake katika damu za Watanzania zilizomwagika. Kwa sababu ni kweli kwamba, Serikali imetajwa legelege mno katika kusimamia mambo ya msingi ya taifa, hatimaye tumejikuta tunaliingiza taifa katika hali ambayo kama tukipuuzia kuchukua hatua za makusudi kulimaliza hili, tutaingia katika zama ambazo tunaweza tusitoke huko.
Tumeshindwa kuvumiliana kwa sababu ya vibaraka na uzembe wa Serikali kutotambua wajibu wake, ama imeamua kuupuuza kwa makusudi na sijui ni kwa maslahi ya nani.
Ole wetu tusipochukua hatua mujarabu kwa wakati na wananchi na wafuasi wa dini hizi wanaoshabikia mambo kama vile Yanga na Simba, wasifikiri hii ni ngoma ya kitoto.
Nchi hii ikilipuka wote tutakuwemo bila kujali nani anamwabudu nani kwa imani gani.
Yale tuliyozoea kuyaona kwenye mchakato wa Katiba, watu wanagombania kila mtu awe na mamlaka juu ya Katiba dhidi ya wenzao, hili nao lilikuwa Salamu ya jinsi gani tumefika hapa, kila jambo siku hizi tunahitaji kuliangalia kwa jicho la dini kwa manufaa ya dini zetu, hili halitatufikisha siyo tu tuendako kama taifa, bali hata wanaomwamini hawatafika kwa Mungu wao kwa mtindo huu.
Hili hata kwenye haki za kikatiba pia, hatuwezi kuwa waumini safi wa dini zetu kama tunapoandika Katiba kila mtu anataka imtambue yeye zaidi kuliko wengine, wako watoto wa mitaani, hawa wanatakiwa Waislamu na Wakristu wanaokwenda kutoa maoni kwenye Tume ya kuratibu maoni ya Katiba wawatetee.
Wako watoto wadogo wanaodhulumiwa haki, hawa hawawezi kusema kwenye Katiba, wakuwasemea ni sisi Waislamu na Wakristu tunaomjua Mungu kwa sababu Mungu kawaweka hawa katikati yetu ili aone sisi aliotujalia zaidi kuliko wao, tunatumia vipi neema hizo kwa manufaa ya wenzetu wasiojiweza.
Tuzifanye dini zetu ziwe sehemu ya kutupatanisha kwa msingi wa uvumilivu kwa sababu Mungu mwenyewe mwenye dini hizi tunazotumia kumwabudu ni mvumilivu kuliko tunavyoweza kufikiri.
Jaribu kujiuliza wewe unayetaka dini yako tu ndiyo iwe bora kuliko ya wengine, unadai huwezi kuvumilia wenye imani tofauti na wewe, hebu fikiria Mungu angekuwa siyo mvumilivu hata kwa nukta moja.
Wewe kiongozi wa dini unayehamasisha watu wa imani yako wawachukie na wasifungamane na wengine, jiulize kwa siku moja unawaza na kufanya mangapi ambayo Mungu angeamua kukushughulikia hapo hapo ungeweza kudumu kwa muda gani?
Mungu anavyotupenda tumezungukwa na mifano mingi sana ya jinsi dini na tofauti zozote za kijamii zimesababisha machafuko katika nchi za wenzetu, lakini sijui kwanini hatutaki kujifunza.
Migogoro inayozaa vita za kidini au za kikabila huwa inaanza namna hii kwa kukosa uvumilivu miongoni mwa wanajamii, tujue kwamba hata mbuyu ulipoanza kuchipua ardhini ulikuwa mdogo na dhaifu kama mchicha, lakini baada ya muda ukawa ulivyo.
Chokochoko za kidini tunaweza kuziona ndogo na zinafanywa na wapuuzi, hivyo haziwezi kutuletea madhara na mitafaruku katika jamii.
Tutakuwa tunajidanganya, tusipokuwa macho na kuchukua hatua sasa mambo yakishashika kasi sina hakika tutakimbilia wapi, lakini walau nina hakika na jambo moja kwamba, machafuko yakianza hakuna atakayebaki salama, si Muislamu au Mkristo.
Ole wao wanaoziona dini ni bora kuliko Mungu.
Kwa tafsiri isiyo rasmi, ujumbe huu ulitaka kumaanisha kwamba, “Wakristu na Waislamu wa Tanzania wanaweza kuwa wadau katika kujenga jamii yenye maadili ya Kimungu; uvumilivu, haki, amani na kuwajali maskini na wanyonge.”
Nimelazimika kuanza na nukuu hii ili kuwaonyesha tu wafuasi wa kweli wa dini hizi jinsi walivyo na jukumu kubwa katika kuunda jamii yenye uvumilivu na mshikamano wa dhati ambao ndio msingi wa namna Mungu anavyotaka tuishi.
Kwa ufahamu mdogo nilionao kuhusu Uislamu (ninaweza kusahihishwa katika hili), ni kwamba jina tu lenyewe linamaanisha unyenyekevu na zaidi sana Uislamu ni dini ya amani na ukiwasikiliza baadhi ya wanazuoni wa Kiislamu wanasema Waislamu pia wamefundishwa namna ya kuishi na watu wasio wa dini yao kwa amani.
Na kwa kweli ziko baadhi ya hadithi zinashuhudia kuwa hata Mtume Mohamad (S.A.W) alipata msaada kwa namna moja ama nyingine kutoka kwa Wakristo na watu wengine wasio Waislamu, wakati anahamia Madina toka Makka.
Lakini pia katika Ukristu, upo msingi mmoja mkubwa wa imani yao, wanatakiwa wawapende jirani zao kama nafsi zao na zaidi sana wanatakiwa wawapende hata adui zao kwa sababu upendo ndiyo amri yao kuu.
Yako masimulizi katika Injili kwamba Bwana Yesu aliwaambia wale wote wanaomfuata na kuamini katika yeye kuwa wanaweza kuwa na uwezo hata wa kuhamisha milima, lakini kama wanatindikiwa na upendo ni kazi bure, utaona ni jinsi gani upendo ulivyo sehemu muhimu ya imani hii.
Bahati mbaya tuliyonayo katika jamii yetu kwa sasa, tumeanza kutumia dini hizi badala ya kuwa daraja la kutuunganisha, kutumia tofauti zetu kama njia ya kutuweka pamoja zaidi, sasa tunatumia tofauti za dini zetu kama sababu ya kuwa maadui na kujenga matabaka hasimu katika jamii yetu.
Kipo kitu kimoja ambacho viongozi na wafuasi wa imani hizi wanatakiwa watambue kuwa ni mpango wa Mungu wanayesema wanamwabudu, kutuumba tukiwa tunatofautiana.
Jinsi ambavyo tunatofautiana sura zetu na mawazo yetu ndivyo ambavyo tunatakiwa tutarajie tutatofautiana katika mitazamo ya mambo mbalimbali ikiwemo ya imani. Hili Mungu wanayemwabudu analijua na ndiyo maana kuna mbingu na jehanamu.
Sasa kama Mungu mwenye kuwaumba Binadamu hawa pamoja na uwezo wake wote usio na mipaka, lakini amewaacha binadamu hawa hawa waamue kuishi maisha watakayo kwa utashi wao binadamu mwingine ni nani mpaka atake watu wote waamini kama anavyoamini yeye?
Wataalamu wa elimu ya genetic wanatuambia kuwa ili kuwe na mtu ambaye anafanana na wewe kwa kila kitu, yaani sura, mawazo unayowaza wewe na yeye awaze hivyo na muwe na mtazamo unaofanana kwa kila kitu, ni lazima mzaliwe watoto laki tatu katika familia ya baba mmoja na mama mmoja, mtoto wa laki tatu na moja ndiye atakuwa anafanana kwa kila kitu na yule mzaliwa wa kwanza wa familia hiyo.
Hapa tunaweza kuona ni jinsi gani haiwezekani kutaka kufananisha mitazamo, kwa kuwa ni Mungu pekee na mwenye uwezo wa kila jambo chini na juu ya jua aliyeamua kutuwekea tofauti hizi na sisi hatuna namna wala uwezo wa kufanya vinginevyo, tunachoweza kufanya ni kutaka kuziishi tofauti hizo kwa manufaa yetu na kuifanya Tanzania iwe sehemu nzuri ya kuishi kila mmoja wetu apendavyo bila kuingilia uhuru wa mtu.
Kwa hakika ni uendawazimu na ujinga wa kiimani kutaka au hata kuthubutu tu kuwaza mikakati na mbinu za kuwafanya watu wote wawe Wakristu au Waislamu, hilo halitawezekana kwa sababu ni Mungu aliyedhamiria kutufaya tutofautiane namna hii, hizi tofauti zetu hatukuchagua wenyewe, tumejikuta kwa njia mbalimbali tuna mitazamo hiyo inayokinzana ambayo siyo lazima itufanye tupigane.
Dini hizi ni kama zinataka kuharibu taifa hili kama tu ambavyo dini zimeharibu mataifa mengine mengi yaliyotukuka kwa kuwa na amani na mshikamano na nguvu za kiuchumi.
Madai yanayoendelea sasa ya nani ana haki ya kuchinja kuliko mwingine, yanaweza kuwa ya msingi kulingana na imani za watu na hapa sitaki kuingia katika mtego wa kupuuza imani ya mtu, lakini hivi waumini hawa wamejiuliza ni kwa kiasi gani maisha ya mtu yana thamani kuliko hiyo nyama wanayogombania kuchinja?
Haiwezekani kwamba, Waislamu na Wakristu ambao hawazidi asilimia 50 ya Watanzania wote wanataka ndiyo wawe madereva wa nchi hii, wapo pia Watanzania wenye haki zao ambao wana haki ya kuishi kwa amani na hapa ndiyo wajibu wa Serikali unapoingia.
Katika hiki, Serikali haiwezi kukwepa wajibu wake katika damu za Watanzania zilizomwagika. Kwa sababu ni kweli kwamba, Serikali imetajwa legelege mno katika kusimamia mambo ya msingi ya taifa, hatimaye tumejikuta tunaliingiza taifa katika hali ambayo kama tukipuuzia kuchukua hatua za makusudi kulimaliza hili, tutaingia katika zama ambazo tunaweza tusitoke huko.
Tumeshindwa kuvumiliana kwa sababu ya vibaraka na uzembe wa Serikali kutotambua wajibu wake, ama imeamua kuupuuza kwa makusudi na sijui ni kwa maslahi ya nani.
Ole wetu tusipochukua hatua mujarabu kwa wakati na wananchi na wafuasi wa dini hizi wanaoshabikia mambo kama vile Yanga na Simba, wasifikiri hii ni ngoma ya kitoto.
Nchi hii ikilipuka wote tutakuwemo bila kujali nani anamwabudu nani kwa imani gani.
Yale tuliyozoea kuyaona kwenye mchakato wa Katiba, watu wanagombania kila mtu awe na mamlaka juu ya Katiba dhidi ya wenzao, hili nao lilikuwa Salamu ya jinsi gani tumefika hapa, kila jambo siku hizi tunahitaji kuliangalia kwa jicho la dini kwa manufaa ya dini zetu, hili halitatufikisha siyo tu tuendako kama taifa, bali hata wanaomwamini hawatafika kwa Mungu wao kwa mtindo huu.
Hili hata kwenye haki za kikatiba pia, hatuwezi kuwa waumini safi wa dini zetu kama tunapoandika Katiba kila mtu anataka imtambue yeye zaidi kuliko wengine, wako watoto wa mitaani, hawa wanatakiwa Waislamu na Wakristu wanaokwenda kutoa maoni kwenye Tume ya kuratibu maoni ya Katiba wawatetee.
Wako watoto wadogo wanaodhulumiwa haki, hawa hawawezi kusema kwenye Katiba, wakuwasemea ni sisi Waislamu na Wakristu tunaomjua Mungu kwa sababu Mungu kawaweka hawa katikati yetu ili aone sisi aliotujalia zaidi kuliko wao, tunatumia vipi neema hizo kwa manufaa ya wenzetu wasiojiweza.
Tuzifanye dini zetu ziwe sehemu ya kutupatanisha kwa msingi wa uvumilivu kwa sababu Mungu mwenyewe mwenye dini hizi tunazotumia kumwabudu ni mvumilivu kuliko tunavyoweza kufikiri.
Jaribu kujiuliza wewe unayetaka dini yako tu ndiyo iwe bora kuliko ya wengine, unadai huwezi kuvumilia wenye imani tofauti na wewe, hebu fikiria Mungu angekuwa siyo mvumilivu hata kwa nukta moja.
Wewe kiongozi wa dini unayehamasisha watu wa imani yako wawachukie na wasifungamane na wengine, jiulize kwa siku moja unawaza na kufanya mangapi ambayo Mungu angeamua kukushughulikia hapo hapo ungeweza kudumu kwa muda gani?
Mungu anavyotupenda tumezungukwa na mifano mingi sana ya jinsi dini na tofauti zozote za kijamii zimesababisha machafuko katika nchi za wenzetu, lakini sijui kwanini hatutaki kujifunza.
Migogoro inayozaa vita za kidini au za kikabila huwa inaanza namna hii kwa kukosa uvumilivu miongoni mwa wanajamii, tujue kwamba hata mbuyu ulipoanza kuchipua ardhini ulikuwa mdogo na dhaifu kama mchicha, lakini baada ya muda ukawa ulivyo.
Chokochoko za kidini tunaweza kuziona ndogo na zinafanywa na wapuuzi, hivyo haziwezi kutuletea madhara na mitafaruku katika jamii.
Tutakuwa tunajidanganya, tusipokuwa macho na kuchukua hatua sasa mambo yakishashika kasi sina hakika tutakimbilia wapi, lakini walau nina hakika na jambo moja kwamba, machafuko yakianza hakuna atakayebaki salama, si Muislamu au Mkristo.
Ole wao wanaoziona dini ni bora kuliko Mungu.
No comments:
Post a Comment