Friday, 11 October 2013

Tanzania, Burundi zashikilia msimamo EAC



 Kenya, Uganda na Rwanda wachafua hali ya hewa

HALI ya mambo imezidi kuwa tete katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya Tanzania na Burundi kutaka maelezo ya kina kutoka kwa nchi nyingine tatu wanachama za Kenya, Uganda na Rwanda zilizoanzisha ushirikiano mpya kinyemela kati yao, kwa kuzitenga nchi hizo mbili.Katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita kumekuwa na mfululizo wa matukio yanayoashiria kuwa Tanzania na Burundi zimetengwa na nchi hizo tatu ambazo zimeanzisha ushirikiano mpya kati yao kinyemela, kinyume cha mkataba ulioanzisha Jumuiya hiyo mwaka  1999.Jumuiya ya sasa ilizaliwa tena upya Novemba 30, mwaka 1999 ikishirikisha nchi za Tanzania, Uganda na Kenya, wakati Rwanda na Burundi zilikaribishwa baadaye mwaka 2008.Jumuiya hiyo mpya ilizaliwa baada ya ile ya awali iliyoanzishwa mwaka 1968 kuvunjika mwaka 1977 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kushindwa kuelewana kwa wakuu wa nchi wanachama kwa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere (Tanzania), Jommo Kenyatta (Kenya) na Idd Amin (Uganda).Habari za hivi karibuni zilizopatikana kutoka ndani ya EAC zinabainisha kwamba Tanzania na Burundi zimekerwa na hatua ya nchi wanachama wenzao za Kenya, Uganda na Rwanda kuanza mchakato wa kuanzisha shirikisho la kisiasa bila ya kuzishirikisha nchi hizo.Tanzania na Burundi zinaelezwa kuwa kupitia kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Agosti 31, mwaka huu, mjini Arusha zilimtaka Mwenyekiti wa Baraza hilo, Shem Bageine, kutoka Uganda kutoa maelezo ya kina kuhusu hatua za nchi hizo tatu kufanya mambo ambayo yanakwenda kinyume cha mkataba wa Jumuiya hiyo.Taarifa zinaeleza kuwa hata hivyo Bageine hakuwa na majibu muafaka kuhusu hatua hiyo na ndipo nchi hizo mbili zilipoazimia kuhitaji majibu ya kina zaidi kuhusu suala hilo katika kikao kijacho kitakachofanyika Novemba, mwaka huu.Pamoja na suala la kuanzisha mchakato wa shirikisho la kisiasa, nchi hizo tatu pia zinaelezwa kukubaliana kuanzisha ushirikiano katika eneo la kukusanya kodi  (single costumes territory).Masuala mengine ambayo yanaelezwa kutozifurahisha nchi za Tanzania na Burundi ni hatua yao ya kukubaliana kuwa na visa moja kwa watalii watakaotembelea nchi hizo, kuimarisha miundombinu hasa ujenzi wa reli kutoka Bandari ya Mombasa-Kenya hadi Kigali Rwanda kupitia Kampala-Uganda.Moja wa maofisa wa EAC ambaye ni Mtanzania (jina linahifadhiwa) alilimbia gazeti hili la Raia Mwema kuwa hali ndani ya sekretarieti ya jumuiya hiyo ni mbaya na hata watumishi kutoka nchi za Tanzania na Burundi wameanza kutengwa na wenzao.“Kumekuwa na kutokuaminiana miongoni mwa maofisa wa juu katika jumuiya yetu, watumishi wa Tanzania ni kama tunatengwa na wenzetu,” alidai mtumishi huyo bila ya kufafanua zaidi.Katika mkutano wake na waandishi wa habari mwezi uliopita Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya EAC, Dk. Richard Sezibera, alikanusha madai kuwa hali si shwari ndani ya Jumuiya anayoiongoza.Dk. Sezibera alikaririwa akisema: “Hali ni shwari katika jumuiya na kila kitu kinakwenda vizuri kulingana na mkataba wa jumuiya tofauti zinazojitokeza ni za kawaida katika jumuiya yoyote ile ya watu kutofautiana mawazo.”!Taarifa zinaeleza kuwa katika utetezi wake, Bagaine ambaye pia ni Waziri wa Afrika Mashariki nchini Uganda, aliwaeleza washiriki wa kikao hicho kuwa mikutano iliyowakutanisha viongozi wakuu wa nchi hizo tatu iliratibiwa na wizara za mambo nje katika nchi husika.Waziri huyo alieleza kuwa kwa kawaida mikutano inayohusiana na masuala ya Afrika Mashariki huratibiwa na wizara husika katika kila nchi, lakini kwa suala hilo ilikuwa kinyume hivyo asingekuwa na majibu muafaka.“Kutokana na mgongano uliojitokeza ujumbe wa Tanzania ulitaka upewe maelezo yanayotosheleza katika kikao kijacho cha Baraza la Mawaziri kinachotarajiwa kufanyika mapema Novemba, mwaka huu, kabla ya kikao cha wakuu wa nchi ambao watakutana Novemba 30,” kinaeleza chanzo chetu cha habari.Akizungumzia mzozo huo aliyekuwa Waziri wa kivuli wa Afrika Mashariki kutoka Kambi Upinzani Bungeni- CHADEMA, Mustafa Akonaay, alisema ilikuwa mapema kwa nchi wanachama waanzilishi wa jumuiya kuziruhusu Rwanda na Burundi kujiunga na jumuiya hiyo.“Hizi nchi mbili zilikuwa na matatizo ya ndani ya kiutawala baada ya kupigana vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa muda mrefu, hivyo ilikuwa ni mapema sana kuziruhusu kujiunga na jumuiya wakati bado zina matatizo ya ndani,” alieleza Akonaay.Naye mwanzuoni maarufu katika diplomasia, Profesa Abdallah Safari, anasema katika msuguano huo kuna taarifa za muda mrefu kuwa baadhi ya wakuu wa nchi za Afrika Mashariki wanataka kuharakisha shirikisho la kisiasa kwa maslahi yao wenyewe.“Tetesi kuhusu suala hilo ni za muda mrefu na kulikuwa na mipango ya kupanua kitu kinachoitwa dola ya Wahima (Hima Empire) katika eneo la Maziwa Makuu hadi Tanzania, kuna uwezekano mipango hiyo bado iko vichwani mwa viongozi hao,” anasema Profesa Safari.Anaongeza kusema; “Wakati mwingine sisi Watanzania ni chanzo cha kuanza kutengwa na wenzetu kutokana na kushamiri kwa tabia ya urasimu, uzembe na wizi katika sekta mbalimbali za umma na hata kushindwa kwenda sambamba na wenzetu ambao wanadhamira ya kufanya mambo kwa weledi zaidi.”!Akitoa mfano Profesa huyo anasema katika sekta ya biashara Tanzania imeshindwa kuondoa urasimu katika Bandari ya Dar es Salaam kiasi cha wafanyabiashara kutoka nchi jirani wanaoitumia kusafirisha bidhaa zao kupata hasara.
“Mlolongo  huo wa mambo yasiyo na msingi unasababisha usumbufu kwa wafanyabiashara wengi wanaopitisha bidhaa zao katika ardhi ya Tanzania na bidhaa hizo hupanda bei marudufu katika masoko zinakopelekwa na hivyo kuongeza gharama kwa watumiaji,”!Katika hatua nyingine, alidai hatua ya Tanzania kuanza kutengwa inatokana na uongozi dhaifu wa serikali.“Hili la Rais kusafiri sana nalo ni tatizo na wenzetu wameona sisi kama Taifa hatuko makini  na wametumia mwanya huo kutaka kujitenga, kama kuna uongozi imara wasingethubutu kuanza kufanya mambo kama hayo kwa mlango wa nyuma,” anasema Profesa Safari.Hata hivyo, kwa mujibu wa Profesa Safari, ni vigumu kwa shirikisho hilo la kisiasa kufanikiwa haraka kutokana na changamoto kadhaa ikiwamo nchi husika kuwa na matatizo ya ndani, hasa ya kidemokrasia ambayo yalitakiwa kupatiwa ufumbuzi kwanza.
  • Kenya, Uganda na Rwanda wachafua hali ya hewa
HALI ya mambo imezidi kuwa tete katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya Tanzania na Burundi kutaka maelezo ya kina kutoka kwa nchi nyingine tatu wanachama za Kenya, Uganda na Rwanda zilizoanzisha ushirikiano mpya kinyemela kati yao, kwa kuzitenga nchi hizo mbili.
Katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita kumekuwa na mfululizo wa matukio yanayoashiria kuwa Tanzania na Burundi zimetengwa na nchi hizo tatu ambazo zimeanzisha ushirikiano mpya kati yao kinyemela, kinyume cha mkataba ulioanzisha Jumuiya hiyo mwaka  1999.
Jumuiya ya sasa ilizaliwa tena upya Novemba 30, mwaka 1999 ikishirikisha nchi za Tanzania, Uganda na Kenya, wakati Rwanda na Burundi zilikaribishwa baadaye mwaka 2008.
Jumuiya hiyo mpya ilizaliwa baada ya ile ya awali iliyoanzishwa mwaka 1968 kuvunjika mwaka 1977 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kushindwa kuelewana kwa wakuu wa nchi wanachama kwa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere (Tanzania), Jommo Kenyatta (Kenya) na Idd Amin (Uganda).
Habari za hivi karibuni zilizopatikana kutoka ndani ya EAC zinabainisha kwamba Tanzania na Burundi zimekerwa na hatua ya nchi wanachama wenzao za Kenya, Uganda na Rwanda kuanza mchakato wa kuanzisha shirikisho la kisiasa bila ya kuzishirikisha nchi hizo.
Tanzania na Burundi zinaelezwa kuwa kupitia kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Agosti 31, mwaka huu, mjini Arusha zilimtaka Mwenyekiti wa Baraza hilo, Shem Bageine, kutoka Uganda kutoa maelezo ya kina kuhusu hatua za nchi hizo tatu kufanya mambo ambayo yanakwenda kinyume cha mkataba wa Jumuiya hiyo.
Taarifa zinaeleza kuwa hata hivyo Bageine hakuwa na majibu muafaka kuhusu hatua hiyo na ndipo nchi hizo mbili zilipoazimia kuhitaji majibu ya kina zaidi kuhusu suala hilo katika kikao kijacho kitakachofanyika Novemba, mwaka huu.
Pamoja na suala la kuanzisha mchakato wa shirikisho la kisiasa, nchi hizo tatu pia zinaelezwa kukubaliana kuanzisha ushirikiano katika eneo la kukusanya kodi  (single costumes territory).
Masuala mengine ambayo yanaelezwa kutozifurahisha nchi za Tanzania na Burundi ni hatua yao ya kukubaliana kuwa na visa moja kwa watalii watakaotembelea nchi hizo, kuimarisha miundombinu hasa ujenzi wa reli kutoka Bandari ya Mombasa-Kenya hadi Kigali Rwanda kupitia Kampala-Uganda.
Moja wa maofisa wa EAC ambaye ni Mtanzania (jina linahifadhiwa) alilimbia gazeti hili la Raia Mwema kuwa hali ndani ya sekretarieti ya jumuiya hiyo ni mbaya na hata watumishi kutoka nchi za Tanzania na Burundi wameanza kutengwa na wenzao.
“Kumekuwa na kutokuaminiana miongoni mwa maofisa wa juu katika jumuiya yetu, watumishi wa Tanzania ni kama tunatengwa na wenzetu,” alidai mtumishi huyo bila ya kufafanua zaidi.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari mwezi uliopita Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya EAC, Dk. Richard Sezibera, alikanusha madai kuwa hali si shwari ndani ya Jumuiya anayoiongoza.
 Dk. Sezibera alikaririwa akisema: “Hali ni shwari katika jumuiya na kila kitu kinakwenda vizuri kulingana na mkataba wa jumuiya tofauti zinazojitokeza ni za kawaida katika jumuiya yoyote ile ya watu kutofautiana mawazo.”!
Taarifa zinaeleza kuwa katika utetezi wake, Bagaine ambaye pia ni Waziri wa Afrika Mashariki nchini Uganda, aliwaeleza washiriki wa kikao hicho kuwa mikutano iliyowakutanisha viongozi wakuu wa nchi hizo tatu iliratibiwa na wizara za mambo nje katika nchi husika.
Waziri huyo alieleza kuwa kwa kawaida mikutano inayohusiana na masuala ya Afrika Mashariki huratibiwa na wizara husika katika kila nchi, lakini kwa suala hilo ilikuwa kinyume hivyo asingekuwa na majibu muafaka.
“Kutokana na mgongano uliojitokeza ujumbe wa Tanzania ulitaka upewe maelezo yanayotosheleza katika kikao kijacho cha Baraza la Mawaziri kinachotarajiwa kufanyika mapema Novemba, mwaka huu, kabla ya kikao cha wakuu wa nchi ambao watakutana Novemba 30,” kinaeleza chanzo chetu cha habari.
Akizungumzia mzozo huo aliyekuwa Waziri wa kivuli wa Afrika Mashariki kutoka Kambi Upinzani Bungeni- CHADEMA, Mustafa Akonaay, alisema ilikuwa mapema kwa nchi wanachama waanzilishi wa jumuiya kuziruhusu Rwanda na Burundi kujiunga na jumuiya hiyo.
“Hizi nchi mbili zilikuwa na matatizo ya ndani ya kiutawala baada ya kupigana vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa muda mrefu, hivyo ilikuwa ni mapema sana kuziruhusu kujiunga na jumuiya wakati bado zina matatizo ya ndani,” alieleza Akonaay.
Naye mwanzuoni maarufu katika diplomasia, Profesa Abdallah Safari, anasema katika msuguano huo kuna taarifa za muda mrefu kuwa baadhi ya wakuu wa nchi za Afrika Mashariki wanataka kuharakisha shirikisho la kisiasa kwa maslahi yao wenyewe.
“Tetesi kuhusu suala hilo ni za muda mrefu na kulikuwa na mipango ya kupanua kitu kinachoitwa dola ya Wahima (Hima Empire) katika eneo la Maziwa Makuu hadi Tanzania, kuna uwezekano mipango hiyo bado iko vichwani mwa viongozi hao,” anasema Profesa Safari.
Anaongeza kusema; “Wakati mwingine sisi Watanzania ni chanzo cha kuanza kutengwa na wenzetu kutokana na kushamiri kwa tabia ya urasimu, uzembe na wizi katika sekta mbalimbali za umma na hata kushindwa kwenda sambamba na wenzetu ambao wanadhamira ya kufanya mambo kwa weledi zaidi.”!
Akitoa mfano Profesa huyo anasema katika sekta ya biashara Tanzania imeshindwa kuondoa urasimu katika Bandari ya Dar es Salaam kiasi cha wafanyabiashara kutoka nchi jirani wanaoitumia kusafirisha bidhaa zao kupata hasara.
“Mlolongo  huo wa mambo yasiyo na msingi unasababisha usumbufu kwa wafanyabiashara wengi wanaopitisha bidhaa zao katika ardhi ya Tanzania na bidhaa hizo hupanda bei marudufu katika masoko zinakopelekwa na hivyo kuongeza gharama kwa watumiaji,”!
Katika hatua nyingine, alidai hatua ya Tanzania kuanza kutengwa inatokana na uongozi dhaifu wa serikali.
“Hili la Rais kusafiri sana nalo ni tatizo na wenzetu wameona sisi kama Taifa hatuko makini  na wametumia mwanya huo kutaka kujitenga, kama kuna uongozi imara wasingethubutu kuanza kufanya mambo kama hayo kwa mlango wa nyuma,” anasema Profesa Safari.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Profesa Safari, ni vigumu kwa shirikisho hilo la kisiasa kufanikiwa haraka kutokana na changamoto kadhaa ikiwamo nchi husika kuwa na matatizo ya ndani, hasa ya kidemokrasia ambayo yalitakiwa kupatiwa ufumbuzi kwanza.

Soma zaidi kuhusu:

Tufuatilie mtandaoni:

Maoni ya Wasomaji

Historia hujirudia. Chonde yasitupate yale ya 1977 jumuia ya awali ya Afrika Mashariki iliposambaratika. Sababu zilikuwa tofauti za kiuchumi na kisiasa. Baada ya miaka miwili Tz na Uganda zikaingia vitani! Kumbe chokochoko za kisiasa kati ya hizi nchi mbili zilikuwa zikikua tangu Idd Amin alipompindua Obote mwaka 1971.Tofauti za kiuchumi kati ya Kenya na Tz kutokana na siasa za ujamaa(tz) na siasa ya upebari(Kenya)zilisababisha kutoelewana, Kenya ikidhani inacheleweshwa na Tz. Leo mambo yanaelekea kujirudia. Kuna chokochoko za kisiasa kati ya Rwanda na Tz. Hatutarajii kunyukana lakini upepo haujakaa sawa. Bandari ya Dar ni tishio kwa uchumi wa kenya. Kama bidhaa za Uganda na Rwanda zinaweza kupitia Mombasa Kenya itapumua zaidi. Kwa hali hiyo sishangai Kenya kuungana na Uganda na Rwanda katika harakati za kuikwepa bandari ya Dar! Katibu wa sasa wa jumuia hii Sezibera nadhani ni Myarwanda kama sio mtu wa Uganda. kwa vyovyote vile hawezi kukwepa mbinu hizi ili kuikomoa Tz. Mbona haya hayakuwepo wakati Mwapachu ni katibu wa jumuia hii? Rwanda kaingia juzi juzi katika jumuia hii. Sasa anaanza kuwa mwenyewe! Dunia hii!! Tuwashauri viongozi wetu waache ubinafsi na wajikite katika kushauriana na kushirikiana ili wawe na nguvu zaidi.

Toa maoni yako

- See more at: http://www.raiamwema.co.tz/tanzania-burundi-zashikilia-msimamo-eac#sthash.XWXpKgzg.dpuf
  • .Kenya, Uganda na Rwanda wachafua hali ya hewa
HALI ya mambo imezidi kuwa tete katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya Tanzania na Burundi kutaka maelezo ya kina kutoka kwa nchi nyingine tatu wanachama za Kenya, Uganda na Rwanda zilizoanzisha ushirikiano mpya kinyemela kati yao, kwa kuzitenga nchi hizo mbili.
Katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita kumekuwa na mfululizo wa matukio yanayoashiria kuwa Tanzania na Burundi zimetengwa na nchi hizo tatu ambazo zimeanzisha ushirikiano mpya kati yao kinyemela, kinyume cha mkataba ulioanzisha Jumuiya hiyo mwaka  1999.
Jumuiya ya sasa ilizaliwa tena upya Novemba 30, mwaka 1999 ikishirikisha nchi za Tanzania, Uganda na Kenya, wakati Rwanda na Burundi zilikaribishwa baadaye mwaka 2008.
Jumuiya hiyo mpya ilizaliwa baada ya ile ya awali iliyoanzishwa mwaka 1968 kuvunjika mwaka 1977 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kushindwa kuelewana kwa wakuu wa nchi wanachama kwa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere (Tanzania), Jommo Kenyatta (Kenya) na Idd Amin (Uganda).
Habari za hivi karibuni zilizopatikana kutoka ndani ya EAC zinabainisha kwamba Tanzania na Burundi zimekerwa na hatua ya nchi wanachama wenzao za Kenya, Uganda na Rwanda kuanza mchakato wa kuanzisha shirikisho la kisiasa bila ya kuzishirikisha nchi hizo.
Tanzania na Burundi zinaelezwa kuwa kupitia kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Agosti 31, mwaka huu, mjini Arusha zilimtaka Mwenyekiti wa Baraza hilo, Shem Bageine, kutoka Uganda kutoa maelezo ya kina kuhusu hatua za nchi hizo tatu kufanya mambo ambayo yanakwenda kinyume cha mkataba wa Jumuiya hiyo.
Taarifa zinaeleza kuwa hata hivyo Bageine hakuwa na majibu muafaka kuhusu hatua hiyo na ndipo nchi hizo mbili zilipoazimia kuhitaji majibu ya kina zaidi kuhusu suala hilo katika kikao kijacho kitakachofanyika Novemba, mwaka huu.
Pamoja na suala la kuanzisha mchakato wa shirikisho la kisiasa, nchi hizo tatu pia zinaelezwa kukubaliana kuanzisha ushirikiano katika eneo la kukusanya kodi  (single costumes territory).
Masuala mengine ambayo yanaelezwa kutozifurahisha nchi za Tanzania na Burundi ni hatua yao ya kukubaliana kuwa na visa moja kwa watalii watakaotembelea nchi hizo, kuimarisha miundombinu hasa ujenzi wa reli kutoka Bandari ya Mombasa-Kenya hadi Kigali Rwanda kupitia Kampala-Uganda.
Moja wa maofisa wa EAC ambaye ni Mtanzania (jina linahifadhiwa) alilimbia gazeti hili la Raia Mwema kuwa hali ndani ya sekretarieti ya jumuiya hiyo ni mbaya na hata watumishi kutoka nchi za Tanzania na Burundi wameanza kutengwa na wenzao.
“Kumekuwa na kutokuaminiana miongoni mwa maofisa wa juu katika jumuiya yetu, watumishi wa Tanzania ni kama tunatengwa na wenzetu,” alidai mtumishi huyo bila ya kufafanua zaidi.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari mwezi uliopita Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya EAC, Dk. Richard Sezibera, alikanusha madai kuwa hali si shwari ndani ya Jumuiya anayoiongoza.
 Dk. Sezibera alikaririwa akisema: “Hali ni shwari katika jumuiya na kila kitu kinakwenda vizuri kulingana na mkataba wa jumuiya tofauti zinazojitokeza ni za kawaida katika jumuiya yoyote ile ya watu kutofautiana mawazo.”!
Taarifa zinaeleza kuwa katika utetezi wake, Bagaine ambaye pia ni Waziri wa Afrika Mashariki nchini Uganda, aliwaeleza washiriki wa kikao hicho kuwa mikutano iliyowakutanisha viongozi wakuu wa nchi hizo tatu iliratibiwa na wizara za mambo nje katika nchi husika.
Waziri huyo alieleza kuwa kwa kawaida mikutano inayohusiana na masuala ya Afrika Mashariki huratibiwa na wizara husika katika kila nchi, lakini kwa suala hilo ilikuwa kinyume hivyo asingekuwa na majibu muafaka.
“Kutokana na mgongano uliojitokeza ujumbe wa Tanzania ulitaka upewe maelezo yanayotosheleza katika kikao kijacho cha Baraza la Mawaziri kinachotarajiwa kufanyika mapema Novemba, mwaka huu, kabla ya kikao cha wakuu wa nchi ambao watakutana Novemba 30,” kinaeleza chanzo chetu cha habari.
Akizungumzia mzozo huo aliyekuwa Waziri wa kivuli wa Afrika Mashariki kutoka Kambi Upinzani Bungeni- CHADEMA, Mustafa Akonaay, alisema ilikuwa mapema kwa nchi wanachama waanzilishi wa jumuiya kuziruhusu Rwanda na Burundi kujiunga na jumuiya hiyo.
“Hizi nchi mbili zilikuwa na matatizo ya ndani ya kiutawala baada ya kupigana vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa muda mrefu, hivyo ilikuwa ni mapema sana kuziruhusu kujiunga na jumuiya wakati bado zina matatizo ya ndani,” alieleza Akonaay.
Naye mwanzuoni maarufu katika diplomasia, Profesa Abdallah Safari, anasema katika msuguano huo kuna taarifa za muda mrefu kuwa baadhi ya wakuu wa nchi za Afrika Mashariki wanataka kuharakisha shirikisho la kisiasa kwa maslahi yao wenyewe.
“Tetesi kuhusu suala hilo ni za muda mrefu na kulikuwa na mipango ya kupanua kitu kinachoitwa dola ya Wahima (Hima Empire) katika eneo la Maziwa Makuu hadi Tanzania, kuna uwezekano mipango hiyo bado iko vichwani mwa viongozi hao,” anasema Profesa Safari.
Anaongeza kusema; “Wakati mwingine sisi Watanzania ni chanzo cha kuanza kutengwa na wenzetu kutokana na kushamiri kwa tabia ya urasimu, uzembe na wizi katika sekta mbalimbali za umma na hata kushindwa kwenda sambamba na wenzetu ambao wanadhamira ya kufanya mambo kwa weledi zaidi.”!
Akitoa mfano Profesa huyo anasema katika sekta ya biashara Tanzania imeshindwa kuondoa urasimu katika Bandari ya Dar es Salaam kiasi cha wafanyabiashara kutoka nchi jirani wanaoitumia kusafirisha bidhaa zao kupata hasara.
“Mlolongo  huo wa mambo yasiyo na msingi unasababisha usumbufu kwa wafanyabiashara wengi wanaopitisha bidhaa zao katika ardhi ya Tanzania na bidhaa hizo hupanda bei marudufu katika masoko zinakopelekwa na hivyo kuongeza gharama kwa watumiaji,”!
Katika hatua nyingine, alidai hatua ya Tanzania kuanza kutengwa inatokana na uongozi dhaifu wa serikali.
“Hili la Rais kusafiri sana nalo ni tatizo na wenzetu wameona sisi kama Taifa hatuko makini  na wametumia mwanya huo kutaka kujitenga, kama kuna uongozi imara wasingethubutu kuanza kufanya mambo kama hayo kwa mlango wa nyuma,” anasema Profesa Safari.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Profesa Safari, ni vigumu kwa shirikisho hilo la kisiasa kufanikiwa haraka kutokana na changamoto kadhaa ikiwamo nchi husika kuwa na matatizo ya ndani, hasa ya kidemokrasia ambayo yalitakiwa kupatiwa ufumbuzi kwanza.
- See more at: http://www.raiamwema.co.tz/tanzania-burundi-zashikilia-msimamo-eac#sthash.XWXpKgzg.dpuf

Serikali yatangaza nafasi za kazi 1,100

Serikali kupitia Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imetangaza nafasi za kazi 1,134 katika sekta mbalimbali za ofisi za umma.
Kwa mujibu wa Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Xavier Daudi nafasi hizo za kazi ambazo zinapatikana katika tovuti ya Sekretarieti ya Ajira ya www.ajira.go.tz ni kwa ajili ya waajiri mbalimbali wa ofisi za umma.
Katibu alifafanua kuwa nafasi 949 ni kwa ajili ya waajiri walioainishwa katika ofisi za wizara, halmashauri na nyingine 185 ni za taasisi na wakala mbalimbali za Serikali.
Aidha, amewataka waombaji wote wa fursa za ajira kufungua matangazo yote mawili ya kazi na kuzingatia masharti ya Matangazo yote kama yalivyo katika lugha ya Kiingereza na Kiswahili kabla ya kutuma maombi yao Aprili 9, 2013.
Daudi alifafanua kuwa waajiri ambao watatoa ajira hizo ni makatibu wakuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha, Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi na Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Maendeleo Jinsia na Watoto, Wizara ya Kazi na Ajira na Ofisa Mtendaji Mkuu Wakala wa Vipimo.
Wengine ni Makatibu wakuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Ardhi Nyumba na Makazi, Wizara ya Maji na Katibu Ofisi ya Rais Maadili.
Wengine ni Makatibu Tawala wa Mikoa ya Kagera, Iringa, Ruvuma, Mbeya, Mwanza, Shinyanga, Manyara, Dar es Salaam, Morogoro, Geita, Pwani, Mara, Kilimanjaro, Lindi, Singida, Tabora, Tanga, Katavi na Arusha; pamoja na wakurugenzi wa halmashauri za majiji na manispaa Mwanza, Iringa, Songea, Shinyanga, Morogoro, Singida, Kigoma/ Ujiji na Temeke.
Nafasi nyingine ni kwa ajili ya wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya Mufindi, Kyela, Rungwe, Mbeya, Chunya, Biharamulo, Bukoba, Muleba, Namtumbo, Songea, Morogoro, Makete, Mkuranga, Mbinga, Tunduru, Ukerewe, Sengerema, Ilemela, Busega, Maswa na Meatu.
Nyingine ni Wilaya za Shinyanga, Kishapu, Kilosa, Msalala, Rufiji, Rorya, Ruangwa, Lushoto, Mkinga, Mpanda, Monduli, Ngorongoro, Kigoma, Nachingwea, Rombo, Same, Singida, Urambo, Tabora, Babati, Mbulu, Simanjiro na Kiteto.
Pia zimo Wilaya za Handeni, Pangani, Kibondo, Chamwino Mtwara, Nanyumbu, Mpwapwa, Kongwa na Tandahimba pamoja na halmashauri za miji ya Njombe na Kibaha. Nafasi nyingine ni za Baraza la Kiswahili la Taifa (Bakita) na Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa).
Nafasi hizo zilizotangazwa zimegawanyika katika kada zifuatazo; Mchambuzi Mifumo ya Kompyuta daraja la II – (nafasi 10), Ofisa Vipimo II – nafasi 6, Mpima Ardhi, daraja la II (nafasi 26), Mhandisi daraja la II – Ufundi Umeme – Nafasi 9, Ofisa Mipango Miji daraja la II– nafasi 13 na Mhandisi daraja la II - Ujenzi (Nafasi 16).
Pia wanahitajika wahandisi daraja la II - Maji (Nafasi 13), Ofisa Misitu daraja la II (nafasi 7), Ofisa wa Sheria daraja la II – nafasi 3, Mtakwimu daraja la II – nafasi 8 na nyingine mbalimbali.

Pinda atengua amri ya Magufuli

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana amefuta agizo lililotolewa na Waziri wa Ujenzi, John Magufuli la kuwataka wamiliki wa magari makubwa ya mizigo, kutozwa asilimia tano kwa kila gari litakalozidisha uzito na kuagiza kurudiwa kwa utaratibu wa zamani wa msamaha wa asilimia tano ya tozo hiyo.
Pinda pia ametoa muda wa mwezi mmoja kwa Wizara ya Ujenzi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Uchukuzi na Ofisi ya Waziri Mkuu kukutana na Chama cha Wamiliki wa Mabasi (Taboa),Chama cha Wamiliki wa
Malori (Tatoa) ili kukubaliana kwa pamoja kuhusu tozo hiyo. Agizo hilo la Magufuli alilolitoa takribani siku nne zilizopita, liliathiri kasi ya upakuaji wa mizigo katika bandari ya Dar es Salaam kutokana na mgomo huo wa malori.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Pinda alisema, katika mazingira yaliyopo sasa, ushirikiano kati ya Serikali na wadau unahitajika. “Ni lazima wadau washirikishwe ili kusiwe na malalamiko na mambo yaende vizuri,” alishauri Pinda.
Alisema, awali utaratibu uliokuwa unatumika ulipewa baraka na aliyekuwa Waziri wa Miundombinu (sasa Ujenzi), Basil Mramba ambaye baada ya wadau wa usafirishaji kulalamika kuhusu ubovu wa barabara na mizani, alitoa unafuu wa kupunguza asilimia tano ya uzito utakaosomwa katika mizani (utakaozidi).
“Lengo lake ilikuwa ni kufidia matatizo ya upungufu wa mizani kutoweza kupima kwa usahihi uzito wa magari yanayopimwa katika vituo mbalimbali vya mizani nchini, lakini hivi sasa mizani yetu ni mizuri na ya kisasa,” alisema na kuongeza:
“Lakini ikumbukwe kuwa agizo hilo lilikuwa kinyume na Sheria ya Usalama Barabarani sura ya 168 toleo la 2002 na kanuni zake za mwaka 2001, ambayo inazuia malori kuzidisha uzito. Mramba aliamua vile ili kumaliza hali iliyokuwa imejitokeza wakati akiwa Wizara ya Miundombinu,” aliongeza Pinda. Alisema kati ya kanuni hizo, kanuni ya 7(3) inatoa sharti la kama lori likibainika kuzidisha mzigo,sharti ni ama kupanga upya mzigo ili kupunguza uzito,kuushusha mzigo uliozidi au kupigwa faini mara nne ya faini ya kawaida. Pinda alisema baada ya kuibuka kwa mgomo huo alikutana na wadau wa usafirishaji na mawaziri wa wizara zenye dhamana na ujenzi na usafirishaji, kubaini kuwa kulikuwa na ulazima wa wizara hizo kukutana na wadau ili wakubaliane.
Bandari walia na mgomo
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA),imeeleza kuwa wananchi ndiyo wataumia kwa kulazimika kulipa hasara iliyotokana na mgomo huo.
Kaimu Meneja Mawasiliano wa Bandari hiyo, Janeth Ruzangi alisema hali hiyo itatokana na wafanyabiashara kulazimika kupandisha bei ya bidhaa mbalimbali zilizokwama kwa siku kadhaa bandarini hapo ili kufidia gharama walizotozwa na wamiliki wa meli.

Tumetoka kifungoni na hamasa kubwa

Gazeti la Mwananchi leo limerudi tena mitaani baada ya Serikali kulifungia kwa wiki mbili. Kama wasomaji wetu na wananchi kwa jumla wanavyokumbuka, Serikali kupitia Idara ya Habari (Maelezo) ililifungia gazeti hili Septemba 27, 2013 kwa madai kwamba lilichapisha habari mbili tofauti ambazo ilidai zilikuwa za uchochezi na kwamba zilikuwa na lengo la kuwafanya wananchi waichukie pamoja na vyombo vyake vya ulinzi na usalama.
Sio nia yetu hapa kueleza kwa undani maudhui ya habari tulizozichapisha na Serikali kuzitumia kama nondo ya kulifungia kwa muda huo mrefu. Hata hivyo, yafaa angalau kwa muhtasari tu kuweka sawa kumbukumbu za hatua hiyo ya Serikali ambayo tunasema bila kutafuna maneno kwamba ilikuwa ya uonevu na ya kiwango cha juu cha matumizi mabaya ya madaraka.
Hata hivyo, huu hakika sio wakati wa kumtafuta mchawi, kwa maana ya kutaka kujua nani hasa serikalini alitoa amri ya kulifungia gazeti hili kwa sababu ambazo sisi tunaona hazikuwa na chembe ya mashiko. Tulishangazwa kuona amri hiyo ya Serikali ikitolewa wakati mkuu wa nchi, Rais Jakaya Kikwete akiwa nje ya nchi, tena akiwa katika majukumu mazito ambayo dunia nzima ilikuwa ikiyafuatilia kwa shauku na umakini mkubwa.
Kulifungia gazeti wakati huo hatuoni kama ilikuwa kwa masilahi ya taifa kwa sababu hatua hiyo iliichafua taswira ya nchi yetu na bila shaka Rais Kikwete alijikuta katika wakati mgumu kila alipoulizwa kuhusu hatua hiyo iliyochukuliwa na Serikali yake.
Ni habari zipi zilizolipeleka gazeti hili kifungoni? Habari ya kwanza ilikuwa juu ya waraka kuhusu mishahara mipya ya watumishi wa Serikali ambayo tuliithibitisha pasipo kuacha shaka yoyote kutoka katika vyanzo vyetu vya habari vya kuaminika katika mamlaka za juu serikalini.
Tuliuchukulia kama taarifa muhimu sana kwa watumishi wa Serikali na wananchi kwa jumla na hatukuona sababu ya Serikali kutaka wananchi wafichwe kuhusu kuwapo kwa mishahara mipya kwa watumishi wake.
Itakumbukwa kuwa, wiki chache kabla ya gazeti hili halijachapisha habari hiyo, lilikuwa pia limechapisha habari kuhusu mishahara mipya katika sekta binafsi kwa mujibu wa waraka wa Serikali uliotolewa na Wizara ya Kazi na Ajira. Swali linalojitokeza hapa ni hili: Inakuwaje mishahara mipya ya watumishi wa Serikali iwe siri na mishahara mipya kwa sekta binafsi iwe kinyume chake?
Tunaamini kwamba utamaduni wa Serikali kuficha habari na taarifa zenye manufaa kwa umma siyo utawala bora hata kidogo. Ni hivi majuzi tu Rais Kikwete alipomwagiwa sifa na Rais Barrack Obama kwa kutia saini mkataba wa uendeshaji wa shughuli za Serikali kwa uwazi.
Habari ya pili iliyochapishwa Agosti 17 mwaka huu na kusababisha gazeti hili kufungiwa ilihusu Serikali kuimarisha ulinzi katika maeneo ya karibu na misikiti jijini Dar es Salaam jana yake kufuatia kuwapo tetesi kwamba waumini wa Kiislamu siku hiyo wangeandamana kupinga kitendo cha Jeshi la Polisi kumuweka mahabusu Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda. Baadhi ya waumini walikuwa wameonyesha kukasirishwa na kitendo cha polisi kumwondoa Sheikh Ponda katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi) na kumpeleka katika Gereza la Segerea, jijini Dar es Salaam.
Habari hiyo yenye kichwa cha habari; ‘Waislamu wasali chini ya ulinzi mkali wa polisi’ ilichapishwa ikiwa na mmoja wa mbwa waliokuwa na polisi katika doria kutokana na hofu ya kuzuka vurugu baada ya Swala ya Ijumaa, Agosti 16. Habari hiyo ilisema Waislamu hawakuandamana na waliswali kwa amani na utulivu na kwamba polisi hao waliokuwa na mbwa, huku wengine wakitumia pikipiki kufanya doria walitanda katika mitaa mbalimbali kwa lengo la kuimarisha ulinzi. Lakini kwa mshangao wetu, Serikali katika kujaribu kuhalalisha kulifungia gazeti hili ilitoa tafsiri ya uongo kwamba habari tuliyochapisha ilisema kwamba mbwa walipelekwa katika maeneo ya ibada, wakati habari hiyo haikuwa na kitu kama hicho. Serikali ilidai katika taarifa hiyo, kwamba lengo la habari hiyo lilikuwa kuichonganisha na waumini wa Kiislamu ili waichukie pamoja na vyombo vyake vya ulinzi na usalama, kwani kwa Waislamu mbwa ni haramu na picha hiyo iliudhalilisha Uislamu. Taarifa hiyo potofu ya Serikali imetuthibitishia pasipo kuacha shaka kwamba haikuwa na nia njema na gazeti hili.
Hatua ya kulifungia gazeti hili kwa sababu za kufikirika imesababisha maumivu kwa watu wengi. Vijana (vendors) waliokuwa wakiuza na kusambaza gazeti hili pamoja na familia zinazowategemea wameumia. Waandishi wa kujitegemea wanaolipwa kutokana na habari wanazotuma gazetini wameumia pamoja na familia zao. Hivyo hivyo, watoa matangazo na wasomaji waliokuwa wakilitegemea gazeti hili kwa habari za uhakika nao pia wameumia. Hasara ambayo MCL imepata kutokana na hatua hiyo ya Serikali haitamkiki.
Pengine huu ni wakati mwafaka wa kuikumbusha Serikali kwamba, gazeti hili pamoja na mengine yanayochapishwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), ni magazeti makini sana yenye waandishi wa habari wanaoheshimu maadili ya taaluma yao. Hatusemi kwamba hatuwezi kufanya makosa, kwani sisi ni binadamu.
Hata hivyo, inapotokea tukafanya makosa tunafanya masahihisho stahiki haraka kwa lengo la kupunguza maumivu kwa yeyote tuliyemkosea. Makosa ya makusudi kama kuandika habari za uongo hayavumiliki na kila mwandishi wa kampuni yetu anatambua fika kwamba kufanya hivyo ni kujitakia kiama.
MCL imeweka miongozo ya sera na malengo ya uhariri kwa waandishi. Lengo ni kuhakikisha habari zinazochapishwa ni sahihi, zinatenda haki na haziegemei upande wowote. Kwa maana hiyo, vyombo vyake vya habari vinasimamia ukweli na haki na waandishi wake wana jukumu la kuhakikisha wanakuwa na kiwango cha juu cha weledi na maadili ili kuwawezesha kutoa habari kwa umma.
Tumetoka kifungoni tukiwa na somo muhimu. Kwamba sheria kandamizi kama Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 haisimamii masilahi ya taifa, bali kundi la watu wachache. Ni sheria kandamizi ambayo kwa umoja wetu tunaweza kuifuta. Tungependa kuwashukuru wasomaji wetu na wananchi kwa jumla kwa kuwa nasi katika kipindi kigumu tulichokuwa kifungoni. Vilevile, tunavishukuru kwa namna ya pekee vyombo vyote vya habari vya ndani na nje ambavyo vilisimama imara kupinga hatua ya Serikali kufungia magazeti.
Tutakuwa watu wasio na shukurani kama hatutatambua mshikamano mkubwa ulioonyeshwa na asasi za kiraia, mabalozi na watu mbalimbali kupinga matumizi ya sheria hii kandamizi. Hatujakata tamaa, bali tumetoka kifungoni tukiwa na hamasa kubwa kuendelea kuwapa habari wananchi pasipo woga wala upendeleo.
Hatupambani na Serikali, lakini tutaendelea kuikosoa pale inapofanya makosa na tutaipongeza pale inapotimiza wajibu wake. Tunawaomba wasomaji wetu mwendelee kutuunga mkono.

Friday, 4 October 2013

HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA WANANCHI, TAREHE 4 OKTOBA-2013.

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWA WANANCHI, TAREHE 4 OKTOBA, 2013
Ndugu Wananchi;
Namshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehma, kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kumaliza mwezi Septemba salama na kuwasiliana kwa kutumia utaratibu wetu huu mzuri. Naomba radhi kuzungumza nanyi siku ya leo kwa sababu nilikuwa safari na nilirejea jioni ya tarehe 30 Septemba, 2013. Awali nilifikiria nisiseme, nisubiri mwisho wa mwezi wa Oktoba. Lakini, baada ya kupata taarifa ya yaliyojiri, nimeshauriwa na nimekubali angalau niyasemee baadhi ya mambo huenda itasaidia. Niwieni radhi nisipoyasemea baadhi ya mambo siyo kwa kuyapuuza, bali kwa kuepuka hotuba kuwa ndefu mno. Nitayatafutia mahali pengine pa kuyasemea.
Uhusiano na Rwanda
Ndugu Wananchi;
Katika hotuba yangu ya mwisho wa mwezi wa Julai, nilizungumzia hali ya uhusiano wetu na Rwanda kutokuwa mzuri na tatizo la ujambazi na wahamiaji haramu katika Mikoa ya Kigoma, Geita na Kagera. Nafurahi kusema kuwa kwa yote mawili kuna maendeleo ya kutia moyo.(P.T)

Tarehe 5 Septemba, 2013, nilikutana na kuzungumza na Mheshimiwa Rais Paul Kagame wa Rwanda mjini Kampala. Tuliitumia fursa ya ushiriki wetu katika Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu kuzungumzia uhusiano baina yetu na nchi zetu. 
Mazungumzo yalikuwa mazuri na sote tulikubaliana kuwa yaliyopita si ndwele tugange yajayo. Kwa sababu hiyo tulielewana kuwa tutengeneze mazingira yatakayosaidia kutuliza hali na kurudisha nchi zetu katika uhusiano mwema kama ilivyokuwa siku zote. Nawaomba ndugu zangu hususan wanasiasa, watumishi wa umma, wanahabari na wenye mitandao ya kijamii na blog na wananchi kwa ujumla tusaidie kuimarisha uhusiano mwema baina ya Rwanda na Tanzania na watu wake.
Majambazi na Wahamiaji Haramu
Ndugu Wananchi;
Katika hotuba hiyo pia nilisema kuwa tutachukua hatua thabiti dhidi ya majambazi na wageni wanaoishi nchini bila ya kuzingatia taratibu zinazohusika. Niliwataka majambazi wajisalimishe wao na silaha zao kwa hiari. Wale wanaoishi nchini bila ya kuwa na kibali halali wahalalishe ukaazi wao au warejee makwao. Nilitoa siku 14 kuanzia tarehe 29 Agosti, 2013 wafanye hivyo kwani baada ya hapo tungeanzisha operesheni maalum ya kushughulika na watu wa makundi yote mawili.
Ndugu Wananchi;
Kumekuwepo na mafanikio ya kutia moyo. Kwa upande wa wahamiaji wanaoishi nchini kinyume cha sheria watu wapatao 21,254 waliondoka kwa hiari. Hali kadhalika zaidi ya ng'ombe 8,000 waliondolewa na silaha 102 zilisalimishwa. Baada ya operesheni kuanza tarehe 6 Septemba, 2013 na kumalizika tarehe 20 Septemba, 2013, wahamiaji haramu 12,828 walirejeshwa makwao na watuhumiwa 279 wa unyang'anyi wa kutumia silaha walikamatwa. Aidha, mabomu 10 ya kutupa kwa mkono (offensive hand grenades), silaha 80, risasi 780 na mitambo 2 ya kutengeneza magobole vilikamatwa. Pia, ng'ombe 8,226 walikamatwa wakichungwa katika mapori ya hifadhi. Kwa upande wa mazao ya misitu, mbao 2,105 zilikamatwa pamoja na nyara mbalimbali za Serikali.
Ndugu Wananchi;
Agizo la kuwataka watu wanaoishi nchini isivyo halali wahalalishe ukaazi wao au waondoke kwa hiari au wataondolewa lilipotoshwa hasa na vyombo vya habari vya nje ya Tanzania. Walikuwa wanadai eti Tanzania ilikuwa inafukuza wakimbizi. Madai hayo si ya kweli hata kidogo. Hadi kufikia tarehe 30 Septemba, 2013 wakimbizi 68,711 walikuwepo kwenye Kambi ya Nyarugusu, Mkoani Kigoma. Hakuna mkimbizi ye yote aliyetakiwa kuondoka. Ukweli ni kwamba hakuna mtu ye yote kati ya wale watu walioondoka kwa hiari au kusaidiwa kuondoka wakati wa operesheni ambaye ni mkimbizi. Kama ingekuwa hivyo, wa kwanza kulalamika wangekuwa wenzetu wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa. Bahati nzuri jambo hilo halikutokea.
Ndugu Wananchi;
Yalikuwepo pia madai kwamba tunawaonea na kuwatesa watu walioishi nchini miaka mingi. Ati iweje sasa ndiyo waambiwe kuwa siyo raia. Siku zote Serikali ilikuwa wapi? Uraia haupatikani kwa kuishi nchi ya kigeni kwa miaka mingi. Unapatikana kwa kutimiza masharti ya kuomba na kupewa uraia. Kama mtu hakufanya hivyo anabaki kuwa raia wa nchi aliyotoka au walikotoka wazazi wake. Ipo mifano ya watu mashuhuri ambao walilazimika kuachia nyadhifa zao baada ya kugundulika kuwa siyo raia. Hawakuwa wanaonewa, ndiyo matakwa ya Katiba na Sheria za nchi yetu.
Ndugu Wananchi;
Katika kutekeleza operesheni hii niliagiza kuwa wale watu ambao wameishi hapa nchini miaka mingi ambao wana nyumba, mashamba au mali mbalimbali au wameoa au kuolewa na wana watoto au hata wajukuu waelekezwe kuhalalisha ukaazi wao. Iwapo watakataa kufanya hivyo basi wasaidiwe kurejea kwao. Pia niliagiza watu wasiporwe mali zao wala kudhulumiwa. Sijapata taarifa ya kufanyika kinyume na maelekezo yangu. Lakini kama wapo watu waliotendewa tofauti, taarifa itolewe kwa Wakuu wa Wilaya na Mikoa au hata Ofisi ya Rais ili hatua zipasazo zichukuliwe. Hatutaki watu wadhulumiwe au kuonewa.
Napenda kutumia nafasi hii kumpongeza Waziri wa Ulinzi na JKT, Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Emmanuel Nchimbi kwa uongozi wao mzuri katika zoezi hili. Pia, nawapongeza Makamanda na askari wa JWTZ na Polisi pamoja na maafisa wa Idara ya Uhamiaji, Idara ya Mifugo, Idara ya Wanyamapori, Idara ya Misitu na Idara nyinginezo za Serikali kwa kazi kubwa na nzuri waliyofanya. Najua awamu ya kwanza imeisha tarehe 20 Septemba, 2013 na kama nilivyosema kuwa safari hii operesheni itakuwa endelevu, muda si mrefu awamu ya pili itafuata. Nawaomba waendelee kuchapa kazi kwa bidii, maarifa na nidhamu ya hali ya juu.
Ziara ya Canada na Marekani
Ndugu Wananchi;
Kati ya tarehe 17 na 28 Septemba, 2013 nilifanya ziara ya kikazi katika nchi za Canada na Marekani. Nchini Canada nilitembelea Chuo Kikuu cha Guelph ambapo nilitunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu kwa kutambua jitihada zetu tuzifanyazo kujiletea maendeleo na mafanikio ya kutia moyo tunayoendelea kupata licha ya changamoto zinazotukabili. Katika mazungumzo yangu na uongozi wa chuo hicho wamekubali kuwa na ushirikiano wa karibu na Wizara zinazohusika na Elimu, Kilimo na Mifugo pamoja na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Morogoro na Chuo Kikuu cha Dodoma. Nimewataka Mawaziri wa Wizara hizo na viongozi wa vyuo hivyo kuchangamkia fursa hiyo bila kuchelewa.
Ndugu Wananchi;
Nchini Marekani nilikutana na kuzungumza na maafisa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya nchi hiyo wakiwemo Rais Barack Obama na baadhi ya Wabunge wa Bunge la Marekani. Mazungumzo yetu yalilenga kuimarisha ushirikiano baina ya nchi zetu na mambo yalienda vizuri. Wote walituhakikishia kuwa mambo tuliyoyazungumza na kukubaliana na Rais Barack Obama wakati wa ziara yake nchini yanaendelea kufanyiwa kazi. Miongoni mwa hayo maombi yetu ya kupatiwa vitabu milioni 2.4 vya sayansi na hisabati yamekubaliwa na utekelezaji umeanza. Upatikanaji wa vitabu hivyo utamwezesha kila mwanafunzi wa sekondari kuwa na kitabu chake.
Ndugu Wananchi;
Jambo lingine kubwa na la faraja kwetu ni kuwa mapendekezo yetu ya miradi ya umeme na barabara za vijijini za kugharamiwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika lao la Changamoto za Milenia yamepokelewa vizuri. Kinachosubiriwa ni miradi ipi itakubaliwa na Bodi ya MCC na kiasi gani cha fedha kitatengwa na Bunge la Marekani kwa ajili hiyo.
Tuzo ya Uhifadhi
Jambo lingine muhimu katika safari yangu ya Marekani ni kutunukiwa tuzo na "International Congressional Conservation Foundation" kwa kutambua juhudi zetu katika kuhifadhi wanyama pori na mafanikio tuliyoyapata. Licha ya changamoto mbalimbali tunazokabiliana nazo, tuzo hii imetupa moyo wa kuongeza nguvu katika jitihada tunazozifanya sasa kupambana na ujangili na matatizo mengine ya uhifadhi wa wanyama na misitu.
Ndugu Wananchi;
Kilichotupa moyo zaidi ni kauli za utayari wa kutusaidia katika mapambano hayo zilizotolewa wakati wa kupewa tuzo na katika mkutano wa mfuko wa Maendeleo wa Clinton na katika mkutano maalum wa kupambana na ujangili na biashara ya meno ya tembo duniani.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
Ndugu Wananchi;
Shabaha kuu ya safari yangu ya Marekani ilikuwa kuhudhuria Mkutano wa 68 wa Umoja wa Mataifa unaoendelea jijini New York mpaka Desemba, 2013. Mada kuu ya mkutano wa mwaka huu ni kuandaa agenda ya maendeleo baada ya mwaka 2015 yaani: Post 2015 Development Agenda: Setting the Stage. Kama mtakavyokumbuka Malengo ya Milenia yaliyoamuliwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2000, yanafikia ukomo wa utekelezaji wake mwaka 2015.
Katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka huu mjadala umehusu nini kifanyike baada ya mwaka 2015. Hata hivyo, mjadala huo unaanza kwa kufanya tathmini ya utekelezaji wa yale Malengo Manane ya Milenia ya mwaka 2000 umefikia wapi mpaka sasa na utafikia wapi mwaka 2015 kwa kila nchi na kwa dunia kwa ujumla. Tathmini ya jumla inaonesha kuwa kumekuwepo na jitihada kubwa ya kutekeleza malengo haya katika kila nchi. Yapo malengo ambayo utekelezaji wake umefikia shabaha hivi sasa na yapo ambayo upo uwezekano wa shabaha kufikiwa ifikapo mwaka 2015. Vile vile yapo ambayo shabaha haitafikiwa.
Ndugu Wananchi;
Kwa upande wetu, Tanzania, tumefikia shabaha katika mambo yafuatayo:
(1) Lengo la Milenia namba 2 kuhusu uandikishaji wa watoto wenye umri wa kwenda shule ya msingi;
(2) Lengo la Milenia namba 3 hasa kuhusu usawa wa kijinsia katika Shule za Msingi na Sekondari. Ukweli ni kwamba, wasichana wanaanza kuwa wengi kuliko wavulana. Hatujafikia shabaha kwa upande wa usawa wa kijinsia katika elimu ya juu na ni vigumu kulifikia ifikapo 2015. Pia hatujafikia lengo kwa upande wa usawa wa Wabunge wanawake na wanaume. Hata hivyo, kwa kutumia mchakato wa Katiba unaoendelea sasa tunaweza kufikia lengo katika uchaguzi wa 2015 iwapo tutaamua iwe hivyo;
(3) Lengo la Milenia namba 4 kuhusu kupunguza idadi ya vifo vya watoto wachanga na wale wenye umri chini ya miaka mitano;
(4) Tumefikia shabaha kwa Lengo la Milenia Namba 6 kuhusu kupunguza maambukizi ya UKIMWI; na
(5) Kwa upande wa lengo namba 7 kuhusu mazingira, tumefikia shabaha kwa upande wa upatikanaji wa maji mijini. Bado tuko nyuma kwa maji vijijini ingawaje tunaweza kufikia lengo ifikapo mwaka 2015 kama tutaendeleza uwekezaji tulioamua kufanya katika bajeti ya mwaka huu. Lakini, hatutaweza kufikia shabaha kwa upande wa usafi wa mazingira mijini na vijijini ifikapo mwaka 2015. Safari bado ndefu sana.
Ndugu Wananchi;
Malengo ya Milenia namba 1 na namba 5 ambayo bado tuko nyuma sana ya shabaha hatutafikia lengo ifikapo 2015. Tumeendelea kutekeleza lengo la Milenia namba 1 kuhusu kupunguza umaskini na njaa kwa zaidi ya nusu kutoka kiwango cha mwaka 2000. Hatua tunazochukua kuleta mageuzi katika kilimo zina lengo la kuhakikisha usalama wa chakula na kuongeza mapato ya wakulima. Mafanikio yanaanza kuonekana lakini si ya kiwango cha kutufikisha kwenye lengo ifikapo mwaka 2015. Tunao, pia, mpango wa kupanua programu ya TASAF ya Conditional Cash Transfer ili tuwafikie watu wengi maskini. Hata kama tutafanikiwa kuutekeleza mapema mpango huu utatusogeza sana mbele lakini bado tutakuwa chini ya lengo kwa upande wa kupunguza umaskini ifikapo 2015.
Ndugu Wananchi;
Kwa upande wa Lengo la Milenia namba 5, kuhusu afya ya kina mama wajawazito bado tuko nyuma katika kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na kuongeza idadi ya wajawazito wanaojifungua chini ya uangalizi wa wataalamu wa afya. Hatutaweza kufikia shabaha ifikapo mwaka 2015. Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (2007 – 2017) una nia ya kukabiliana na matatizo haya. Tumeongeza ujenzi wa zahanati, vituo vya afya na hospitali, tumeboresha upatikanaji wa dawa na tumepanua sana mafunzo ya madaktari, wauguzi na wakunga mambo ambayo yamesaidia kutufikisha hatua tuliyopiga mpaka sasa. Naamini juhudi zetu tukiziendeleza zitatusogeza mbele zaidi ingawaje bado tutakuwa chini ya lengo. Miaka michache ijayo, tatizo hili nalo litakuwa historia.
Ndugu Wananchi;
Lengo la Milenia namba 8 linazihusu nchi tajiri kuongeza michango yao kusaidia nchi zinazoendelea kutekeleza Malengo ya Milenia. Bahati mbaya sana mataifa tajiri hayajafikia viwango wanavyotarajiwa kutoa na hata vile wanavyoahidi wenyewe kutoa katika majukwaa mbalimbali. Kama wangetimiza ahadi zao, sura ya utekelezaji wa Malengo ya Milenia ingekuwa tofauti kabisa.
Ndugu Wananchi;
Hiyo ndiyo hali ya utekelezaji wa Malengo ya Milenia hapa nchini. Hakuna nchi ye yote duniani iliyofanikiwa kutekeleza shabaha za malengo yote kwa ukamilifu. Ushauri wa viongozi wote waliozungumza ulitaka mataifa yaliyoendelea yatimize ahadi zao za kuchangia utekelezaji wa Malengo ya Milenia. Ilionekana suala la upatikanaji wa fedha halina budi kuangaliwa kwa makini sasa na baada ya mwaka 2015. Bila ya hivyo ufanisi utakuwa mdogo katika kuongeza kasi ya utekelezaji kwa pale paliposalia kufikia malengo ya 2015 na hata kwa Malengo ya baada ya mwaka 2015.
Mashambulizi ya Kigaidi ya Westgate, Nairobi
Ndugu Wananchi;
Wakati nikiwa safarini, tarehe 21 Septemba, 2013 kulitokea shambulilizi la kigaidi katika Jengo la Biashara la Westgate, huko Nairobi, Kenya. Watu 67 walipoteza maisha na zaidi ya 200 walijeruhiwa. Nilituma salamu za pole na rambirambi kwa Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta na wananchi wa Kenya na kuwahakikishia kuwa tupo pamoja nao katika wakati huu wa majonzi.
Nafahamu kuwa baada ya tukio hilo watu wengi hapa nchini wameingiwa na hofu kuhusu usalama wetu. Ni hofu ya msingi kwani tarehe 8 Agosti, 1998 Ubalozi wa Marekani hapa nchini ulishambuliwa na magaidi na ndugu zetu 11 wasio na hatia walipoteza maisha.
Ndugu Wananchi;
Napenda kuwafahamisha kuwa tangu shambulio la mwaka 1998, Serikali imekuwa inajenga uwezo wa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kupambana na ugaidi katika nyanja mbalimbali. Tunaendelea kujiimarisha bila kusita siku hadi siku. JWTZ, Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa wamekuwa na ushirikiano wa karibu kwa ajili hiyo. Juhudi zetu hizo ndizo zinazotufanya tuwe salama hadi sasa.
Baada ya tukio la Kenya, vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vimeimarisha mikakati yao maradufu. Pamoja na kujizatiti kwetu huko hatuwezi kusema kuwa tukio la kigaidi halitaweza kutokea nchini. Uhakika huo hatuna kwani hata mataifa makubwa na tajiri yameshambuliwa. Kilicho muhimu ni kuendelea kuchukua tahadhari na wananchi kusaidia ili vyombo vyetu vifanikiwe zaidi.
Hali kadhalika, tumewataka watu wote wenye shughuli zinazokusanya watu wengi kama vile maduka, maofisi, mahoteli, migahawa n.k. waweke kamera za ulinzi nje na ndani ya maeneo yao. Pia waangalie uwezekano wa kuweka vifaa vya upekuzi (metal detectors and x-rays). Najua watu wanaweza kulalamikia usumbufu au gharama, lakini gharama na hasara ya kushambuliwa ni kubwa zaidi kuliko ya usumbufu huo.
Ndugu Wananchi;
Nawaomba muendelee kufanya shughuli zenu bila ya hofu ingawaje msiache kuwa makini na kuchukua tahadhari. Watu watoe taarifa kwa vyombo vya usalama wanapoona mtu au watu au kitu cha kutilia shaka. Ni muhimu kwa usalama wake, wa kila mtu, jamii na taifa. Maafisa husika wa vyombo vya ulinzi na usalama wataendelea kuelimisha umma kuhusu hatua mbalimbali za tahadhari za kuchukua. Sisi Serikalini tumejipanga kuchukua hatua zaidi kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi yetu na watu wake.
Mchakato wa Katiba Mpya
Ndugu Wananchi;
Kama mtakavyokumbuka, Bunge lilitunga Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Novemba, 2011. Sheria hii imeweka mchakato mzima wa kupata Katiba hiyo na kuunda taasisi zake. Mwezi Mei, 2012, Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliundwa na imekamilisha hatua tatu muhimu katika mchakato huo. Hatua hizo ni kupokea maoni ya wananchi, kutayarisha rasimu ya kwanza ya Katiba Mpya na kupokea maoni ya Mabaraza ya Katiba ya Wilaya na ya taasisi. Hivi sasa Tume inaandaa mapendekezo ya Rasimu ya Pili ya Katiba itakayopelekwa kwenye Bunge Maalum. Baada ya tafakuri zake, Bunge Maalum litatoa rasimu ya mwisho ya Katiba ambayo itapelekwa kwa wananchi kwa ajili ya uamuzi wa mwisho kupitia kura ya maoni. Baada ya hatua hiyo, ndipo tutakapokuwa tumepata Katiba Mpya.
Ndugu Wananchi;
Baada ya Bunge la Novemba, 2011 kupitisha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, kulikuwepo na madai ya kutaka sheria hiyo iboreshwe kutoka vyama vyote vya siasa vikiwemo vyama vya upinzani na Chama tawala. Majadiliano yalifanyika baina ya Serikali na vyama hivyo pamoja na shirikisho la asasi za kiraia. Makubaliano yalifikiwa kuwa marekebisho yafanyike kwa awamu. Awamu ya kwanza ihusishe Tume ya Mabadiliko ya Katiba kisha hapo yafanyike marekebisho yanayohusu Bunge Maalum na mwisho Kura ya Maoni.
Kama ilivyokuwa kwa mabadiliko yaliyohusu Tume ya Mabadiliko ya Katiba, safari hii nayo vyama vya siasa vilitoa mapendekezo yao. Yalifanyika mazungumzo kati yao na Serikali na maelewano kufikiwa kuhusu maeneo ya kufanyiwa marekebisho. Serikali ilitayarisha rasimu ya Muswada na kuuwasilisha kwa wenzetu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Ndugu Wananchi;
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilitoa mapendekezo yake na ushauri kwenye maeneo mawili. Kwanza kwamba uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalum ufanywe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushauriana na kuafikiana na Rais wa Zanzibar. Pili walishauri kwamba kama Bunge Maalum litashindwa kufikia maamuzi ndani ya siku 70 zilizopendekezwa, liweze kuongezwa muda hadi kufikia siku 90. Maeneo mengine ya Muswada waliafikiana nayo.
Ndugu Wananchi;
Kwa kuzingatia utaratibu wa kutunga Sheria, Serikali ilifikisha Muswada kwa Spika wa Bunge ambaye nae aliuwasilisha kwenye Kamati ya Kudumu ya Katiba, Sheria na Utawala. Kama ilivyo ada, Kamati hiyo ilifanya vikao na wadau na kupokea maoni yao kuhusu Muswada. Nimeambiwa kulikuwa na mjadala wa kina na mapendekezo mazuri yalitolewa na wadau. Kisha hapo Wajumbe wa Kamati walikaa wenyewe kujadili Muswada walikuwepo pia Wabunge ambao si Wajumbe wa Kamati walioshiriki kwa vile Kanuni zinaruhusu. Nimeambiwa pia kwamba mjadala ulikuwa mpana na wa kina zaidi. Mapendekezo kadhaa yalitolewa na Wajumbe kuhusu vifungu mbalimbali vya Muswada.
Ndugu Wananchi;
Nimefahamishwa kuwa Wabunge wa vyama vyote walichangia na kwamba baadhi ya nyakati mambo yalipokuwa ugumu mawazo mazuri ya baadhi ya Wabunge wa upinzani yalisaidia kupata ufumbuzi. Nimeambiwa pia kwamba Wajumbe wa Kamati na upande wa Serikali walikubaliana kwa maeneo mengi isipokuwa machache ambayo walikubaliana kwa pamoja wayapeleke Bungeni ili Wabunge nao wayajadili na kuyapatia ufumbuzi.
Ndugu Wananchi;
Baada ya Kamati kumaliza kazi yake, Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Mathias Chikawe aliwasilisha Muswada Bungeni. Akafuatiwa na Mheshimiwa Gosbert Blandes kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, kutoa maoni ya Kamati. Baadaye Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Mheshimiwa Tundu Lissu alitoa maoni yake.
Ndugu Zangu;
Baada ya watu hao watatu kutoa maoni yao ilitarajiwa kuwa Wabunge wangeanza kujadili Muswada. Naambiwa mambo hayakuwa hivyo. Badala yake kukazuka malumbano baina ya Spika na baadhi ya Wabunge wa Upinzani wakitaka Muswada usijadiliwe. Ilifikia wakati hoja hiyo ikabidi iamuliwe kwa kura ambapo ilishindwa. Katika hali isiyotarajiwa, Wabunge wote wa upinzani wakatoka nje ya Bunge isipokuwa wawili. Kitendo hicho kimewanyima Wabunge wengi wa upinzani fursa ya kutetea hoja zao walizozitoa kupitia hotuba ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani. Pia wamejinyima nafasi ya kusema mambo mengine wakati wa mjadala na Kamati ya Bunge zima.
Wabunge waliokuwepo waliendelea kuujadili Muswada na kutoa hoja na mapendekezo ya kuuboresha. Walifanya hivyo wakati wa mjadala na wakati wa kupitia kifungu kwa kifungu. Baadhi ya hoja na mapendekezo yalikubaliwa na mengine yalikataliwa. Miongoni mwa yaliyokubaliwa na Wabunge, kwa mfano, ni kuhusu elimu ya mtu atakayekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum na lile la ukomo wa uhai wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Ndugu Wananchi;
Kwa maoni yangu madai ya Kambi ya Upinzani yanazungumzika na hata baadhi yangeweza kukubalika kama Wabunge wake wangekuwepo Bungeni na kushiriki mchakato wote wa kujadili na kupitisha Miswada Bungeni. Bahati mbaya hawakuwepo, hivyo hapakuwepo na mtu wa kusema mawazo yao. Baada ya kupoteza fursa yao halali, kutaka kupata ufumbuzi nje ya Bunge ni jambo lisilowezekana. Haya ni masuala yanayohusu Bunge ambayo hujadiliwa na kuamuliwa Bungeni na si vinginevyo. Kuandamana nchi nzima au kuchukua hatua za kutotii sheria kama Mwenyekiti wa CHADEMA, Mheshimiwa Freeman Mbowe anavyotaka, hakutaleta mabadiliko wanayoyataka katika sheria hii. Naamini na wao wanautambua ukweli huo.
Ndugu Wananchi;
Kuna msemo wa wahenga kuwa "historia hujirudia". Naomba hekima ziwaongoze viongozi wa CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi na zituongoze sote kutumia utaratibu tulioutumia mwaka 2012. Kulipotokea mazingira kama haya pande zote zilikaa pamoja na kuzungumzia hoja moja baada ya nyingine na kukubaliana nini kifanyike na kifanyike vipi. Baada ya kuridhiana hatua zipasazo za kisheria na kanuni zilichukuliwa na kumaliza mzozo.
Ndugu Wananchi;
Kufanya kinyume cha hayo hakutaleta ufumbuzi wa mzozo huu. Tutaliingiza taifa kwenye matatizo yasiyokuwa ya lazima. Tukikataa kufanya hayo Watanzania wanayo kila sababu ya kuhoji dhamira zetu na kutilia shaka nia zetu. Watakuwa na haki ya kuuliza nia ni hii yetu sote ya kupata Katiba Mpya kwa kutumia njia za kikatiba na kisheria au tuna dhamira nyingine iliyojifisha?
Kama dhamira yetu ni kutaka kupata Katiba mpya kwa mujibu wa Katiba na Sheria, ushauri wangu na rai kwa ndugu zetu wa CHADEMA, CUF na NCCR-Maguezi ni kuwa waachane na mipango ya maandamano na kufanya ghasia. Badala yake watumie njia halali zinazotambulika kikatiba na kisheria kujenga hoja za kufanya marekebisho wanayoyaona wao yanafaa kuboresha Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Tukifanya hivyo tutakuwa tunajenga badala ya kubomoa. Tutaliponya taifa. Sisi katika Serikali tuko tayari.
Ndugu Wananchi;
Napenda pia kuzisemea baadhi ya hoja zilizotolewa na Kambi ya Upinzani. Kwanza kabisa nasema kuwa nimesikitishwa sana na madai na tuhuma za uongo eti katika uteuzi wa Tume ya Katiba sikuheshimu mapendekezo ya TEC, CCT na walemavu.
Ndugu Zangu, Watanzania Wenzangu;
Siyo tu kauli hiyo ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu. Nasema hivyo kwa sababu, sipendi kuamini kuwa Mheshimiwa Mbunge amesema yale kwa kutokufahamu ukweli au kwa bahati mbaya. Amesema yale kwa makusudi mazima ya kupotosha ukweli ili pengine isaidie kujenga hoja yake ya kutaka Rais asiteue wale Wajumbe 166 wa Bunge Maalum.
Napenda ieleweke kuwa siishabikii kazi hiyo, lakini kwa kutimiza wajibu na maslahi ya taifa nikiagizwa na Sheria za nchi nitafanya. Nasema hivyo kwa sababu nafahamu ni kazi ngumu. Kama kazi ya uteuzi wa Wajumbe 30 wa Tume haikuwa rahisi hata kidogo, hii ya uteuzi wa watu 166 itakuwa ngumu zaidi. Ile ya Tume ilikuwa ngumu kwa namna mbili. Kwanza, kwamba taasisi zilizoomba na waombaji walikuwa wengi mno kuliko nafasi za kujaza yaani 15 Zanzibar na 15 Bara. Zanzibar ziliomba taasisi zaidi ya 60 na waombaji walikuwa zaidi ya 200 wakati Bara kulikuwa na taasisi zaidi ya 170 zikiwa na waombaji zaidi ya 500. Kupata watu 30 kutoka orodha kubwa kiasi hicho si mtihani mdogo. Pili kwamba tulitakiwa kuunda Tume inayoasili sura ya taifa, yaani watu wa nchi yetu kwa maeneo, vyama vya siasa, dini, wanawake, vijana, walemavu, wafanyakazi, wasomi, Wabunge, Wawakilishi, wanasheria, wafanyabiashara, wakulima, asasi za kiraia n.k.
Ndugu Wananchi;
Pamoja na changamoto hizo, lakini tulifanikiwa kuunda Tume iliyopokelewa vizuri na jamii na kufanya watu wengi hata wale ambao hawakuteuliwa wahisi kuwakilishwa. Tulifanyaje? Kwanza kabisa tulihakikisha kuwa tunapata wawakilishi wa vyama vya siasa vyenye wawakilishi Bungeni na kwenye Baraza la Wawakilishi na tunapata wawakilishi wa mashirika ya dini zetu kubwa yaani, TEC, CCT na BAKWATA. Ndiyo maana nikasema kuwa kwa Mheshimiwa Tundu Lisu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu.
Baada ya hapo ndipo tukaangalia waombaji wa makundi na taasisi nyingine. Tulijitahidi sana kupata watu ambao wanawakilisha kundi zaidi ya moja. Tulifikiria hivyo kwa sababu ni ukweli ulio wazi kuwa si kila taasisi iliyoomba itapata mwakilishi kwani hata tungependa iwe hivyo nafasi hazikuwepo. Kwa kutumia utaratibu huu makundi mengi yamepata uwakilishi kutokana na watu waliopendekezwa na makundi mengi. Tumefanya kazi kubwa sana ya kuwianisha mambo na makundi ya maslahi mbalimbali nchini.
Ndiyo maana naiona mantiki ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akishirikiana na Rais wa Zanzibar wa kuwateua Wajumbe wa Bunge Maalum. Dhana kuwa kila kikundi kiteue chenyewe watu ingefaa sana kama kungekuwepo na nafasi za kutosha kila kundi nchini. Hilo haliwezekani, labda tuwe na Bunge Maalum lisilokuwa na ukomo wa wajumbe.
Ndugu Wananchi;
Mimi na Rais wa Zanzibar tumekuwa tunajiuliza baada ya kazi ngumu na nzuri tuliyoifanya na iliyopongezwa na wengi ya kuteua Tume ya Mabadiliko ya Katiba nini kilichoharibika sasa hata tuonekane hatuaminiki kuteua hawa 166? Kama ni kwa sababu za Mheshimiwa Tundu Lissu, nimeshasema hazina ukweli wowote. Ninapojiuliza kwa nini aseme uongo nashindwa kupata jibu linaloingia akilini. Wakati mwingine nafikiria kuwa ni hiana. Lakini nadhani ni hila za kisiasa zenye nia ya kutaka kupata watu wa kutetea maslahi ya chama chake. Kama hiyo ndiyo shabaha basi amekosea sana.
Ndugu Zangu, Watanzania Wenzangu;
Hatutengenezi Katiba ya Chama fulani bali Katiba ya nchi, Katiba ya watu wa vyama vyote na wasiokuwa na vyama ambao ndiyo wengi kuliko wote. Lazima tuongozwe na ukweli huo na tuwe na msimamo huo wakati wote. Lazima tukumbuke kuwa si watu wote wanaostahili au kuwa na sifa ambao wataomba na kupata nafasi ya kuwa Wajumbe, hivyo wale wachache watakao bahatika lazima wawasemee wote. Wanatakiwa kusikiliza na kuwakilisha mawazo ya wote hata wale wasiokuwa wa Chama chao au kundi lao.
Ndugu Wananchi;
Bahati nzuri hii ndiyo sifa kubwa iliyooneshwa na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Wamewasimamia na kuwasemea watu wote bila ya kubagua. Natambua kuwepo kwa baadhi ya watu ambao hawafurahii msimamo huo na matokeo ya kazi yao. Watu hao kuwalaumu Wajumbe wa Tume kwa ajili hiyo ni kuwaonea na kutowatendea haki. Tunataka watakaokuwa Wajumbe wa Bunge Maalum nao waige mfano huu mzuri. Wajali maslahi mapana ya taifa letu na watu wake badala ya kujali yale ya taasisi zao au makundi yao.
Zanzibar Kutokushirikishwa
Ndugu Wanachi;
Nimeambiwa pia kuliwepo madai ya Zanzibar kutokushirikishwa ipasavyo. Nimeeleza kwa kiasi gani Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeshirikishwa na kutoa maoni yake yaliyojumuishwa katika Muswada. Hivyo basi napata tabu kuyaelewa madai kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haikushirikishwa msingi wake nini! Labda kuna kitu sikuambiwa!
Nimeulizia kuhusu hoja ya Kamati kutokufanya vikao Zanzibar kusikiliza maoni ya wadau wa Zanzibar. Nimeambiwa kuwa Kanuni za Bunge hazina sharti hilo hivyo Kamati haistahili kulaumiwa. Kama hivyo, nashauri kuwa suala hili lirudishwe Bungeni ili Wabunge walizungumze na kulifanyia uamuzi muafaka. Vinginevyo watu wataendelea kulauminiana isivyostahili. Hivyo basi, kuligeuza jambo hili kuwa ni suala la kukataa Muswada au kususia vikao vya Bunge au kufanya maandamano sidhani kama ni sawa.
Ndugu Wananchi;
Nimeambiwa pia kuwa kulikuwa na hoja ya kutaka idadi ya Wajumbe wa kutoka Tanzania Bara na Zanzibar iwe sawa kama ilivyo kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Sababu ya idadi ya Wajumbe wa Tume kuwa sawa inatokana na utaratibu wao wa kufikia uamuzi. Ni kwa maelewano ya wote (consensus) na siyo kwa kupiga kura. Ndiyo maana idadi imewekwa sawa ili sauti za pande zote zisikike sawia. Bunge Maalum lina sharti la kufanya uamuzi kwa theluthi mbili ya kura za kila upande kukubali. Bila ya hivyo hakuna uamuzi.
Hivyo basi, katika Bunge Maalum nguvu si uwingi wa kura ambazo upande fulani unaweza kupata bali ni ulinganifu sawa wa kura za kila upande peke yake. Huu ndiyo msingi unaotumika katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivi sasa kwa lengo la kulinda maslahi ya Zanzibar. Zanzibar ina Majimbo 50 ya uchaguzi na Tanzania Bara ina Majimbo 189, hivyo ukiamua kwa wingi kila wakati Wazanzibari watashindwa. Lakini, hapajakuwepo madai ya Zanzibar nao kutaka kuwa na idadi sawa ya majimbo kama Bara au kupunguza majimbo ya Bara yawe sawa na ya Zanzibar kwa sababu wingi si hoja. Msingi unaotumika ni kutoa nguvu sawa za uamuzi kwa kila upande wa Muungano wakati wa kuamua masuala ya Katiba. Hakuna mdogo wala mkubwa, wote wako sawa. Hakuna mdogo kumezwa na mkubwa. Ndiyo msingi unaopendekezwa kutumika kwenye Bunge Maalum hivyo hakuna kitakachoharibika kwa idadi ya Wajumbe kutokukulingana. Nadhani inafaa ibaki ilivyo. Lakini kama Wabunge wataamua waongeze idadi itakuwa kwa sababu nyingine siyo hii ya mfano wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Ndugu Wananchi;
Katika orodha ya madai ya ndugu zetu wa upinzani lipo suala la uhai wa Tume ya Katiba. Wanataka usiishe wanapokabidhi rasimu ya pili kwa Bunge Maalum bali waendelee kuwepo mpaka mwisho wa mchakato. Nimeulizia ilikuwaje? Nimeelezwa kuwa jambo hili halitokani na mapendekezo ya Serikali wala ya Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala. Limetokana na pendekezo la Mbunge katika Bunge wakati wa kupitia vifungu na kuungwa mkono na Wabunge wengi. Kwa hiyo kuilaumu Serikali si haki. Serikali inaweza kuwa mshirika katika hoja hii.
Nami naiona hoja ya Wajumbe wa Tume kuwa na wajibu wakati wa Bunge Maalum hasa wa kusaidia kufafanua mapendekezo ya Tume. Je ushiriki huo uwe vipi? Je ni Wajumbe wote au baadhi yao ni jambo linaloweza kujadiliwa.
Ndugu Wananchi;
Naomba nimalizie kwa kuwasihi viongozi wa CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi kuongozwa na hekima iliyotumika wakati tulipokuwa na tatizo linalofana na hili kuhusu Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Mimi naamini kama iliwezekana kufanikisha mambo wakati ule inaweza kufanya hivyo hata safari hii. Itatufikisha pale tunapopataka salama salimini bila maandamano, kushupaliana au uvunjifu wa amani. Kupanga ni kuchagua, naomba sote, mmoja mmoja na kwa umoja wetu tuchague njia ya mazungumzo na maelewano kwani itaihakikishia nchi yetu amani, usalama na utulivu. Tukifanya hivyo historia itatuhukumu kwa wema.
Mungu Ibariki Tanzania. Nawashukuru sana kwa kunisikiliza.

Friday, 20 September 2013

Bagamoyo na maeneo ya kihistoria yasiyojulikana

Siku chache zilizopita nilitembelea Kitongoji cha Magomeni, mjini Bagamoyo, katika kitongoji hicho nilipiga picha vipande vya nguzo ambayo ni mabaki ya lango la mji huo.
Dereva wa bodaboda aliyenipeleka hapo nilimuuliza kama anaelewa chochote kuhusu kuta hizo mbili, lakini cha ajabu alisema hajui licha ya kuishi  Bagamoyo miaka mingi.
Baada ya hapo nilikutana na dada ambaye anasema amezaliwa na kuishi eneo la Magomeni, lakini hajui maana ya kuta hizo. Nilimwambia kijana kwamba enzi hizo, Bagamoyo ilipokuwa chini ya Wakoloni wa Kiarabu, eneo hilo palikuwa na lango likionyesha mtu anaingia mjini na kwa wenye nchi.
Misafara ya watumwa, wamisionari na wavumbuzi, wafanyabiashara, walipita katika lango hilo. Kuta  nyingine zilizokuwa upande mwingine wa barabara, zimepotea. Kuta nilizopiga picha ziko kwenye uwanja wa mtu. Zinaweza kupotea kwa kuharibiwa wakati wowote.
Pia kulikuwa na nguzo nyingine pale ‘top life bar’ lakini sasa imebaki moja, nyingine imepotea. Nilielezwa na wahifadhi kwamba eneo linalozunguka Caravan Serai, katika soko, na kule kituo cha mabasi kipya lilitumika kujenga kambi za watumwa. Lakini hakuna anayefahamu hilo.
Katika Idara ya Mambo ya Kale, inayoshughulikia masuala ya historia, hakuna maelezo yanayoonyesha eneo hilo kulikuwa na lango hilo. Hakuna kumbukumbu yoyote.
Nimekwenda Bagamoyo mara kadhaa, kila unapotembelea moja ya kivutio cha historia utapata habari tofauti, aidha itatofautiana na ya zamani, au itapotoshwa kidogo. Inafika mahali unashindwa kuelewa ukweli ni upi.
Baada ya kusoma kitabu cha Henry Morton Stanley anaeleza walipoanza safari walipumzika kwenye shamba la mama mmoja, Gonera wa Kihindi, nje ya Bagamoyo. Lakini safari hii niliambiwa Gonera alikuwa ni askari mlinzi aliyejengewa nguzo pale eneo la Mji Mkongwe na von Wisman mwaka 1898.
 Inaonekana Bagamoyo ina maeneo mengi ya kihistoria ambayo hayajawekwa katika historia kuu. Na hili ni kosa la idara husika.