Wednesday, 13 March 2013

Muargentina awa Baba Mtakatifu wa kwanza kutoka Amerika ya Kusini,aitwa Francis I




Ni Baba Mtakatifu wa kwanza kutoka Amerika ya Kusini. Kwenye hotuba yake ya kwanza amwombea Benedict, aomba Kanisa "litembee pamoja katika imani"
Jesuit Cardinal Jorge Bergoglio wa Buenos Aires amechaguliwa kuongoza Wakatoliki billioni moja kama Papa Francis I.

Ni Baba Mtakatifu wa kwanza kutoka Amerika ya Kusini. Kwenye hotuba yake ya kwanza amwombea Benedict, aomba Kanisa "litembee pamoja katika imani".

Ametoa baraka yake ya kwanza ya umma saa nne unusu EAT. Awaomba waumini wamwombee.Wachambuzi wasema Francis ni Papa "mnyenyekevu."

Dk Slaa amkumbuka Sitta


Mvutano uliopo hivi sasa kati ya Chadema na Bunge ulianza Februari 4 katika kikao cha Bunge mjini Dodoma baada ya wabunge wa Chadema kupinga msimamo wa kiti cha Spika wakieleza unapendelea

Boniface Meena na Mussa Juma, Mwananchi
Kutokana na mvutano ambao umekuwapo mara kwa mara kati ya Chadema na Spika wa Bunge, Anne Makinda, chama hicho kimemkumbuka aliyekuwa Spika wa Bunge la 10, Samuel Sitta kikieleza kuwa alikuwa hapindishi sheria na kanuni za Bunge na ndiyo maana lilikuwa limetulia.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kuhusu wabunge wa chama hicho kutakiwa kuhojiwa na Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema Spika Makinda amekuwa akipindisha kanuni na ndiyo maana kumekuwa hakuna utulivu bungeni.


“Spika Sitta aliyekuwepo kabla ya Makinda alikuwa hapindishi sheria na alikuwa anajirekebisha pale anapokosea na tulikuwa tukishauriana kwamba asijihusishe na mambo ya vyama,” alisema Dk Slaa.


Alisema Sitta, ambaye hivi sasa ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki alikuwa hafuati mambo ya vyama kwa kuwa alitakiwa kuwa ni mtu ambaye hapendelei upande wowote. Sitta, ambaye alikuwa Spika kuanzia mwaka 2005-2010, alikuwa anajinadi kwa kuendesha Bunge kwa spidi na viwango.


“Makinda aachane na ushabiki wa CCM kwani anajua kabisa kanuni ya nane inamtaka Spika asifungamane na upande wowote hivyo aache kufanya hivyo,” alisema Dk Slaa.


Alisema ni muhimu Spika akawaeleza kimaandishi amepata wapi mamlaka ya kuruhusu kamati iendelee wakati zote zilivunjika rasmi katika Bunge lililopita.
“Spika kama hajui kanuni aende shule kujifunza kuliko kututia aibu, wanasheria, wabunge wamsaidie ili aweze kuelewa.”


Dk Slaa alisema katika mabunge ya kidemokrasia, kupongeza ni jambo halali na kuzomea pia ni jambo halali hivyo kitendo cha wabunge wao kuzomea ni sawa kwa kuwa ni njia yao ya kufikisha ujumbe. Akizungumzia suala la wabunge wake kuhojiwa na kamati hiyo ya Bunge, alisema hawatakwenda kuhojiwa na kamati hiyo na kama Bunge litaamua kuwafukuza lifanye hivyo ili wananchi waelewe.


“Hawawezi kwenda kuhojiwa na kamati ambayo haipo kisheria, nilipokuwepo bungeni nilishiriki kuandaa kanuni hizi za Bunge, Spika hana mamlaka anayojipa ya kuongeza muda wa kamati, hivyo aache kulidhoofisha Bunge na badala yake alisaidie,” alisema Dk Slaa.


Akizungumzia suala hilo, Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alisema anashangazwa na Naibu Spika, Job Ndugai kusema kuwa kuna kamati ambazo huwa zinaendelea wakati nyingine zinapokuwa zimemaliza muda wake.


Lema aitisha maandamano
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, ametangaza kuandaa maandamano makubwa yatakayoshirikisha wanawake na watoto katika Jiji la Arusha ili kushinikiza Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Arusha (AUWSA) kuwasambazia maji.


Akizungumza jana, Lema alisema ameamua kuandaa maandamano hayo ya kudai maji kwani kwa zaidi ya miezi sita sasa asilimia 70 ya wakazi wa Jiji la Arusha hawapati maji safi.


“Nimewaandikia barua AUWSA wiki mbili sasa nikiwataka wanipe mipango yao ya muda mfupi na mrefu ya kuondoa tatizo la maji Arusha, kwani mimi kama mbunge ninaweza kushirikiana nao kupunguza tatizo hili, lakini hawajajibu sasa tutawashinikiza kwa nguvu wa umma,” alisema Lema.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa AUWSA, Mhandisi Ruth Koya hakupatikana kuelezea kama amepokea barua hiyo baada ya kutopatikana ofisini, pia simu yake ya mkononi ilikuwa haipatikani.

Monday, 11 March 2013

Ushindi wa Kenyatta wachambuliwa


USHINDI wa Uhuru Kenyatta katika kinyang’anyiro cha kihistoria cha Uchaguzi Mkuu wa Kenya, umeonesha kuwa siasa za ukabila nchini humo, bado zina nguvu.

Uhuru juzi alitangazwa kuwa Rais wa nne wa Kenya, baada ya kujipatia asilimia 50.07 ya kura zote zilizopigwa, dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga, aliyepata asilimia 43.28 ya kura hizo.

Kwa mujibu wa Katiba mpya ya Kenya, mgombea wa urais, ni lazima afikishe zaidi ya asilimia 50 ya kura, masharti ambayo Uhuru aliyatimiza japo kwa asilimia 0.07.

Akizungumza jana na gazeti hili, Mhadhiri wa Siasa na Utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana, alisema siasa za ukabila ni saratani ambayo bado inaendeleao kuitafuna Kenya na kuwa jambo hilo si zuri kwa mustakabali wa nchi hiyo.

Alisema ukabila ni vigumu kuumaliza nchini humo, na imejionesha katika uchaguzi uliomalizika, jinsi wapigakura walivyokwenda kupiga kura zao kwa kumfuata mtu na si sera na itikadi za vyama.

Kauli hiyo pia imeungwa mkono na mhadhiri mwingine wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Audax Kweyamba, aliyesema kuwa Kenya bado inasumbuliwa na donda la ukabila.

“Nimefuatilia sana uchaguzi wa Kenya, hata ushindi unaonesha kabisa siasa za ukabila ni tatizo jambo ambalo si zuri kwa mustakabali wa nchi hiyo,” alisema.

Ushauri Bana alisema katika kutekeleza kauli yake ya kuunda Kenya moja, ni vema Uhuru aje Tanzania kujifunza msingi ya kujenga taifa kama alivyofanya Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere.

“Uhuru kama anataka kujenga nchi yenye umoja, aje kujifunza namna ya kujenga taifa, lakini hili hawezi kumaliza peke yake, isipokuwa kwa kusaidiwa na kambi ya Odinga na Wakenya kwa ujumla.

“Kinyume chake Wakikuyu (kabila la Uhuru) na Wakalenjini (kabila la Mgombea Mwenza, William Ruto), wataendelea kuongoza kwa sababu ndio wengi na wanajitokeza kupiga kura,” alisema Dk Bana. Kweyamba yeye alishauri Uhuru ateue viongozi au mawaziri, kulingana na uwezo wao na kuzingatia sura ya utaifa ili kuondoa picha ya ukabila iliyojengeka. Asilimia 0.07?

Akizungumzia ushindi mwembamba wa Uhuru, Dk Bana alisema haijalishi, ilimradi Katiba ya Kenya iliyopitishwa na wananchi wenyewe, inaruhusu mshindi kutangazwa akiwa amefikia zaidi ya asilimia 50 ya kura.

Hata hivyo, alisema ni vema nchi za Afrika ikiwemo Tanzania inayojiandaa kupata Katiba mpya, ziangalie suala hilo katika katiba zao.

Alipendekeza Katiba ziagize uundwaji wa Serikali ya Umoja ya Kitaifa, endapo kunakuwa na kuzidiana kwa kura chache, ili kuondoa manung’uniko kwa walioshindwa.

“Katika hali ya kawaida, ukishindwa kwa tofauti ndogo huamini matokeo, lakini hili linaweza kumalizwa kwa kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, kinyume chake kiongozi aliyeshinda, atatawala kwa nguvu ya dola kutokana na sehemu kubwa kumpinga,” alisema.

Naye Kweyamba alisema jambo la msingi ni hiyo asilimia 0.07 iliyompa Uhuru ushindi, iwe imetokana na Tume kuendesha uchaguzi huru na wa haki na imepatikana kihalali.

Wapigakura Kweyamba alisema Kenya imevunja rekodi ya idadi kubwa ya wapiga kura kujitokeza kutumia haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi, kwa kile kinachoonekana ni kuwa na matumaini mapya baada ya vurugu zilizotokea mwaka 2007.

“Tuombe Mungu, mambo yote yaishe salama na Kenya iwe salama, kwani endapo kutatokea machafuko, kuna hatari ya kushusha morali ya wananchi, ambao wamejitoa kutumia haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi,” alisema Kweyamba.

Alisema, Watanzania wanatakiwa kujifunza namna ya kutumia haki ya kuchagua vongozi, na kuachana na tabia ya kuona kuwa hawana haja ya kushiriki kwenye uchaguzi.

Alisema asilimia 42.8 zilizofikiwa mwaka 2010 haikuwa idadi nzuri. Naye Dk Bana alisema hiyo ni hatua nzuri, ambayo inaonekana imechangiwa na vyama siasa vya Kenya kutoa hamasa kwa wananchi na jinsi Serikali ilivyofanya kazi ya kutoa elimu ya uchaguzi kwa wananchi wake.

Mauaji ya albino yaichafua Tanzania


Mpango wa Afrika wa Kutathmini Utawala Bora (APRM), umebaini kwamba rushwa na ukiukaji wa haki za binadamu ni tatizo kubwa nchini linalohitaji kufanyiwa kazi ili kuimarisha utawala bora.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim alisema jana jijini Dar es Salaam kwamba, licha ya Tanzania kuonyesha mafanikio katika utawala bora, bado maeneo hayo yanahitaji nguvu za ziada.

Mahadhi alisema hayo wakati wa kuadhimisha Siku ya APRM ikiwa ni miaka 10 tangu ilipoanzishwa.

“Ripoti ya APRM iliwasilishwa na Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa wakuu wa nchi za Kiafrika na kusifiwa sana,” alisema.

Alisema kuna mambo machache yalijitokeza na yanayoharibu jina la Tanzania na watu wake.
Alisema kukithiri kwa rushwa ni sehemu ambayo ilitia doa katika ripoti hiyo na kwamba inahitaji kufanyiwa kazi.

“Tunahitaji kuimarisha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Tume ya Maadili ya Viongozi ili kuondokana na kasoro hizo,” alisema Mahadhi.
Aidha alisema eneo la haki za binadamu nalo lilitia doa katika ripoti hiyo hasa mauaji ya walemavu wa ngozi (albino).

Uchaguzi Mkuu Kenya: Ghasia zaanza Kisumu





Nairobi: Polisi wa kutuliza ghasia juzi walilazimika kutumia mabomu ya machozi Mjini Kisumu kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakipinga kutangazwa kwa matokeo ya urais ambayo mgombea wao, Raila Odinga alianguka.

Vurugu hizo ziliibuka, baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais yaliyompa ushindi Uhuru Kenyatta.

Maelfu ya vijana wamekuwa wakirandaranda kwenye maeneo kadhaa ya Kisumu wakichoma majengo na kufunga barabara, huku wakiimba: “Bila Raila, hakuna amani.”

Vurugu hizo zilizoanza juzi jioni zimesababisha maduka kufungwa huku makundi ya vijana wenye hasira wakiendelea kurandaranda mitaani wakipambana na polisi ambao walifanya jitihada za kuwatuliza na kurejesha amani.

Ilielezwa kwamba, muda mfupi tu baada ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kumtangaza Kenyatta kuwa mshindi, zaidi ya vijana 100 waliibuka na kuanza kuwarushia mawe polisi na muda mfupi baadaye idadi ya vijana hao iliongezeka na kusambaa katika maeneo karibu yote ya Kisumu.

Odinga ambaye alikuwa mgombea wa Muungano wa Cord, amewataka wafuasi wake kuwa watulivu kwa kuwa anahitaji kufuata mkondo wa sheria kupinga matokeo hayo.
Matokeo hayo yaliyotangazwa juzi, yalimpa ushindi Kenyatta aliyesimama kwa tiketi ya Muungano wa Jubilee, wa asilimia 50.07 dhidi ya asilimia 43 alizopata Raila.

Raila atinga mahakamani
Muungano wa Cord, leo utawasilisha vielelezo mahakamani kupinga ushindi wa Kenyatta.
Mwanasheria Mkuu wa zamani wa Kenya, Amos Wako ametajwa kuwa miongoni mwa wajumbe wa jopo la wanasheria watakaopinga ushindi wa Kenyatta.

Jopo hilo la wanasheria linaongozwa na mwanasheria mkongwe, George Oraro na baadhi ya mawaziri wakiwamo; Mutula Kilonzo, James Orengo na Ababu Namwamba ambao ni washauri wakuu wa jopo.

Oraro alimtetea aliyekuwa Waziri wa Viwanda, Henry Kosgei wakati alipokabiliwa na kesi kwenye Mahakama ya Kimataifa ya ICC, The Hague.
Wengine wanaounda timu hiyo ni Gitobu Imanyara, Pheroze Nowrojee, Chacha Odera, Ambrose Rachier na Paul Mwangi.

Cord imepanga kufungua kesi ikitaka Mahakama itengue hatua ya kutangazwa kwa Kenyatta kuwa Rais wa Kenya kwa kuwa taratibu za ukusanyaji matokeo zilikiukwa.
Tangu juzi, jopo hilo la wanasheria lilikuwa na vikao mfululizo kuandaa ushahidi wa kesi hiyo ikiwamo kukusanya vielelezo watakavyosimamia katika kesi hiyo kwa mujibu wa Kifungu namba 163 cha Katiba ya Kenya.

Mfuasi wa Uhuru afariki
Shamrashamra za kushangilia ushindi wa Kenyatta ziliingia doa kwenye Mji wa Nyeri baada ya lori lililobeba mashabiki wa mgombea huyo kutumbukia kwenye korongo na kuua mtu mmoja. Katika ajali hiyo watu 30 walijeruhiwa lakini wakiwa katika hali mbaya.

Mwili wa mtu aliyefariki ulipelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Nyeri wakati wengine waliojeruhiwa wamelazwa kwenye hospitali hiyo.
Lori hilo lilikuwa likienda maeneo ya Giakanja kwa ajili ya kukusanya mashabiki wengine na kuanza safari ya kuzunguka mitaa ya mji huo kushangilia ushindi. Kamanda wa Polisi Nyeri, Kirunya Limbitu alithibitisha ajali hiyo na kusema lori hilo lilikuwa kwenye mwendokasi na kupoteza mwelekeo kabla ya kutumbukia kwenye korongo na kupinduka.

Kibaki set to hand over mantle of power to his godson Uhuru


Is it a twist of fate or Shakespeare’s predetermined destiny that President Kibaki will be handing over power to Mr Uhuru Kenyatta?

No one would have imagined it 51 years ago. Not even Uhuru’s mother, Mama Ngina, nor even his father, Mzee Jomo Kenyatta, would have had such inkling.

That time, Mr Kibaki, a staunch Catholic like Mama Ngina, was to be Mr Kenyatta’s godfather following the birth of Uhuru on October 26, 1961.

Executive officer

The outgoing Head of State has had his life tied by fate to the incoming President from the latter’s birth, on the eve of Uhuru (independence), when young Kibaki was the executive officer of Kanu, the party that was to usher in freedom in the country two years later.

Mr Njenga Karume, in his book From Charcoal to Gold, says he and Mr Kibaki went to visit Mama Ngina in the company of Mzee Kenyatta at home in Gatundu following the birth of a baby boy.

Mr Karume says it was Mr Kibaki who suggested to Mzee that the new-born be named Uhuru since independence was only a few months away.

Other accounts from those close to the family indicate that Mr Joseph Murumbi, the man who was to become Kenya’s second vice-president and a close friend of Mzee Kenyatta, also suggested the name.

Still, Mr Kibaki, who is expected to hand over power to Mr Kenyatta on March 26, has had to fight political wars with his godson.

Such was the bitter fight during the 2002 presidential elections pitting Mr Kibaki in Narc against Mr Kenyatta as the Kanu candidate to succeed President Moi.

Mr Kibaki was to trounce his godson, garnering 62 per cent of all the votes cast in the election.

Though political foes, Mr Kibaki still had a soft spot for Uhuru, even as they had gone different ways in politics.

This was the case after the 2005 referendum when Mr Kenyatta teamed up with Mr Raila Odinga in the Orange team that successfully campaigned to defeat the draft Constitution. Mr Kenyatta later aligned himself to his godfather ahead of the 2007 poll.

Mr Kibaki went on to appoint Mr Kenyatta as Deputy Prime Minister after a negotiated coalition government against all expectations. Many thought he would appoint former Gichugu MP Martha Karua, who was instrumental in the negotiations on the Kibaki side after violence broke out following the disputed presidential elections of 2007.

Safari kuelekea uchaguzi wa Papa yaanza kesho Vatican


Afrika na Amerika Kusini, zikilinganishwa na mabara ya Ulaya na Marekani, zinaelezwa kuwa zina idadi kubwa ya waumini wapya , makanisa yake yanajaa, idadi ya mapadri inaongezeka, tofauti na Ulaya na Marekani inakopungua

VATICAN CITY, Vatican
MCHAKATO rasmi wa kumpata kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani atakayemrithi Papa Benedict XVI aliyejiuzulu Februari 28, unaanza kesho. Katika mchakato huo, makardinali 115 wataingia kwenye Kanisa la Sistine kwa kazi hiyo ngumu ya kupiga kura.

Kura hiyo ya siri inatarajiwa kurudiwa mara kadhaa hadi apatikane mtu anayekubalika.
Tayari kanuni za uchaguzi huo zimeshaandaliwa zikiwamo za namna ya kupiga kura kwa usiri na wasimamizi wa kura.

Makardinali hao kutoka mataifa mbalimbali duniani, wamekuwapo Vatican ambako kila walipowasili walikula kiapo cha kutunza siri wakati wote wa kikao hicho muhimu.
Viongozi hao wa kidini, wataongozwa zaidi na sala na maombi kwa roho mtakatifu.

Kama ilivyokuwa katika miaka ya nyuma, kampeni haziruhusiwi katika mchakato huu mzima.

Kukosekana kwa kampeni, hata hivyo, hakuzuii watu kutoa mawazo yao kuhusu nani angefaa kuchaguliwa.

Wengine wanaipa nafasi kubwa Italia, yaliko makao makuu ya kanisa hilo, Vatican, ingawa pia kuna wale wanaofikiri kuwa sasa ni zamu ya Afrika na Amerika Kusini kutoa kiongozi wa juu wa kanisa hilo lenye waumini bilioni 1.2.

Pia, wengine wanadhani kuwa Ulaya, ambayo ina makardinali wengi zaidi, bado inastahili kutoa kiongozi huyo kama ilivyokuwa kwa Poland na Ujerumani katika miaka ya hivi karibuni.

Kwanini Afrika?
Sababu ya msingi inayotajwa kuipendelea Afrika kwa sasa ni, ongezeko la waumini wapya ambako takwimu zinaonyesha kuwa nchi kama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Tanzania, Uganda zimo katika orodha ya 20 bora duniani kwa waumini wengi wa Kikatoliki.

Afrika na Amerika Kusini, zikilinganishwa na mabara ya Ulaya na Marekani, zinaelezwa kuwa zina idadi kubwa ya waumini wapya , makanisa yake yanajaa, idadi ya mapadri inaongezeka, tofauti na Ulaya na Marekani inakopungua .

Makardinali wawili, Francis Arinze mwenye umri wa miaka 80, raia wa Nigeria na mwenzake, Peter Turkson (64) kutoka Ghana, wamekuwa wakitajwa kuwa miongoni mwa wale wanaofaa kwa kazi hiyo.

Wakati wote wa mchakato huo, makardinali hao 115 hawatakuwa na mawasiliano yoyote na ulimwengu wa nje hadi apatikane papa mpya ndani ya wiki mbili.

Kwa pamoja, wataishi katika hosteli ya kisasa iliyomo ndani ya eneo hilo, umbali mdogo kutoka katika Kanisa la Sistine, ambalo milango na madirisha yake yamezibwa kuzuia watu kuchungulia ndani yake.
Hosteli hiyo ya kisasa inayojitegemea, imeandaliwa mahsusi kwa kazi hiyo, ikiwa na huduma zote za msingi. Ina madaktari, mapadri ambao watawahudumia makardinali hao wakihitajika.

Kila kardinali ataishi katika chumba chake kidogo chenye kitanda, meza ndogo na kabati la nguo, akisali zaidi na wakati huo akifanya tafakuri ya kina kati yake na Mungu ni nani hasa kati yao aliyeteuliwa kuliongoza kanisa hilo.
Inaelezwa kuwa wakati wote wa mchakato, makardinali hao hawazungumzi, bali kusali na kufanya tafakuri na kukutana wakati wa chakula.

Ni nchi gani zinawakilishwa?
Zipo nchi kadhaa ambazo zina uwakilishi katika uchaguzi huo.
Hizi ni pamoja na: Italia (28), Marekani (11), Ujerumani (6), Hispania, India, Brazil (5) kila moja, Ufaransa, Poland (4) kila moja Mexico, Canada (3) kila moja
Ureno, Nigeria, Argentina ( 2) kila moja

Australia, Austria, Ubelgiji, Bolivia, Bosnia Herzegovina, Chile, China, DR Congo, Colombia, Croatia, Cuba,Czech , Dominica, Ecuador, Misri, Ghana, Guinea,Honduras, Hungary, Ireland, Kenya,Lebanon, Lithuania, Uholanzi, Peru, Ufilipino, Senegal, Slovenia, Afrika Kusini, Sri Lanka, Sudan, Uswisi, Tanzania, Venezuela, Vietnam (1) kila moja.

Sunday, 10 March 2013

Ni kuonewa Ni stahili Katiba mbovu Siri za Zitto nje


SIRI kubwa kuhusu mwenendo wa Zitto Kabwe (Mb) ndani ya chama chake zimeanikwa mitaani na zinaweza kumzamisha kisiasa,.

Siku nne baada ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Willibrod Slaa kusema wamenasa taarifa za mawasiliano ya Zitto, baadhi ya taarifa zimepatikana jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Zitto ananukuliwa akiapa kusaidia wagombea uongozi katika vyama vingine; na katika moja ya taarifa ananukuliwa akisema atasaidia David Kafulila kupata ubunge “hata kabla ya akina John Mnyika…”

Mnyika ni Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa CHADEMA na Kafulila alikuwa Afisa Habari ambaye baada ya kuondolewa wadhifa huo amekimbilia NCCR-Mageuzi. Mnyika anatarajia kugombea ubunge jimbo la Ubungo.

Naye Zitto amenukuliwa na gazeti la Mwananchi la Jumatatu akilalamika kuwa ameingiliwa katika mawasiliano yake ya baruapepe (e-mail); jambo ambalo Mkurugenzi wa Upelelezi, Robert Manumba, amedakia haraka na kusema Zitto akiwapelekea malalamiko watashughulikia.

Kwa mujibu wa mpangilio wa taarifa husika, lazima aliyezitoa amepata ufunguo wa baruapepe (password) wa ama Zitto au mwandishi wa habari wa Mwananchi, Denis Msacky.

Karibu mawasiliano yote ni kati ya Zitto na Msacky juu ya “ushujaa” wa Zitto na jinsi anavyopendwa nje ya chama huku “akichukiwa” na viongozi wake wakuu.

Katika moja ya mawasiliano, inaonyeshwa kuwa Msacky alimwandikia Zitto akieleza, “Leo hii Mrema (Augustine Lyatonga) anasema anakuheshimu wewe, lakini si Mbowe; hivyo hivyo, Lipumba (Profesa Ibrahim) na James Mbatia wanasema wewe una visheni.”

Katika mawasiliano hayo ya Jumanne, 1 Desemba 2009, saa 6.45 adhuhuri, Msacky anaonyeshwa kumwambia Zitto pia kuwa, “CCM nao…wanakusifu kwamba pamoja na kwamba unawaliza sana, lakini ni kiongozi shupavu.”

“Leo hii siasa za CHADEMA zingekuwa zinatisha kama ungekuwa mwenyekiti wa CHADEMA, vijana nchi nzima wangejiunga na chama, uko nao karibu, unaongea nao, una elimu nzuri, unajua mambo, unasoma sana,” imeeleza sehemu ya mawasiliano kutoka kwa Msacky kwenda kwa Zitto.

Kinacholeta wasiwasi ndani ya CHADEMA kinaweza kuwa lugha inayotumiwa katika mawasiliano hayo. Kwa mfano, katika waraka huohuo, Msacky ananukuliwa akiandika:

“Wanataka kukumaliza, nami sitakubali mtu ammalize rafiki yangu nikiangalia…wanasema Mbowe hata Mbatia akikaa vema anaweza kumpita kama siasa za kufukuza zitaendelea. Muhimu, usisikilize watu, tulia, urudi tupange tufanye nini? Lakini ukweli ni kwamba sasa wanakuogopa…Mwenyekiti Mtarajiwa…”

Mawasiliano yanaonyesha kuwa Zitto hakufurahishwa sana na taarifa za Mwananchi kuwa amemsaidia Kafulila magari matatu kwenda Kigoma kufanya kampeni chini ya NCCR-Mageuzi, lakini Msacky anaonyesha kumfariji.

“Kaka, mimi nimeiona story, haina matatizo zaidi ya kuwafanya akina Mbowe kusitisha mpango mbaya dhidi yako maana wanaanza kuogopa. Hata Mrema Lyatonga amesema kwamba Zitto huwa unamsaidia akiwa na shida. This shows that ur a leader katika opposition, wewe ni mtu wa maridhiano, unakuza upinzani Kigoma,” anaeleza.

Anasema, “Leo nasikia akina Mnyika wanahaha sana, waambie familia yako wasiingie katika mtego wa kuanza kuhojiwa na akina Kubenea (Saed wa MwanaHALISI), watawachanganya. Wewe usiongee kitu chochote, wabaki wanahaha, lakini for sure you are safe, na hizo kampeni za Mnyika kukuchafua huku akitaja majina ya Kafulila, ataziacha.”

Akionyesha juhudi za kushawishi, kuliwaza au kufarakanisha, Msacky anaandika, “Katika hili Zitto, mimi niko na wewe, huna kosa ambalo umefanya, na wala usihofu maana wewe utakuwa nguzo ya upinzani Tanzania…Wanakupa majina ya ajabu, wanakuita Mr Dowans, wanatumia akina Halima Mdee kukuchafua katika magazeti…”

Awali Zitto alikuwa amemwandikia Msacky akisema, “Stori niliyoiona kwenye mwananchi itaniletea matatizo sana.” Hiyo ilikuwa Jumatatu 30 Novemba 2009, saa 5.21 asubuhi. Baruapepe hiyo ilikuwa na kichwa kisemacho: “Muhimu na haraka.”

Aidha, katika mawasiliano mengine, Zitto anaendelea kuonyesha kutofurahishwa na taarifa juu ya magari matatu kwa safari ya Kafulila.

Naye anaandika kwa Msacky, “tatizo la stori ni wingi wa magari, itaonekana mimi nina magari mengi na ni fisadi unajua? Hilo ndio tatizo.”

Saini ya Zitto inatofautiana katika baadhi ya baruapepe. Pengine anaandika “zitto” na kwingine anaandika “Zi.”

Moja ya mawasiliano ambayo yanazua mashaka yanaonyesha Zitto akikiri kuwa na mawasiliano na waasi nchini Kongo akiandika, “take it from me (niamini), nina contacts nyingi sana Congo na hao rebels (waasi) huwa wananiomba sana ushauri na kutaka kuwaunganisha.”

Katika moja ya mawasiliano, Msacky anamwonya Zitto kutotumia baruapepe ya “CHADEMA kwa mawasiliano ya siri” na kutaka amwambie mama yake Shida Salum akatae kuongea na waandishi wa habari. “…nasikia Mbowe anataka mama awe akiongea na waandishi, usikubali,” alieleza.

Zitto alipoulizwa kuhusu taarifa ya Mwananchi kuwa anatembea na barua mfukoni ya kujiuzulu uanachama CHADEMA, alisema “Sina la kusema.”

Alipong’ang’anizwa kwamba imekuwaje hawezi kuzungumzia suala hilo ambalo ni muhimu kwa mustakabali wake wa kisiasa kwa chama chake, Zitto alisema, “Ni kwa sababu sitaki kuingia katika malumbano na katibu mkuu wangu (Dk. Willibrod Slaa) kwani malumbano hayo hayataijenga CHADEMA.”

Alipotakiwa kueleza juu ya baruapepe ambazo zinadaiwa kuwa mawasiliano kati yake na Msacky, haraka alijibu, “Sina la kusema.”

Alipoelezwa umuhimu wa yeye kueleza msimamo wake juu ya baruapepe hizo, Zitto alijibu, “Chochote nitakachosema sasa hivi, kitawachanganya Watanzania.

“Sitaki malumbano. Hakuna sababu ya kuwachanganya Watanzania. Hiyo haina maana yoyote,” alisema Zitto kwa sauti ya ukali. Zitto alikuwa akiongea kutoka Ujerumani kwa simu Na. +4915222493231.

MwanaHALISI ilimtafuta Msacky. Baada ya kuita kwa muda mrefu bila kupokelewa, hatimaye aliandika ujumbe “Kaka, niko katika kikao. Tuma ujumbe.”

Msacky aliulizwa, “Kaka, tumesikia kwamba umetajwa katika sakata la Zitto na chama chake na kwamba wewe ndiye mtibuaji. Je, ni kweli?” Hakujibu ujumbe na alipopigiwa simu ilikuwa inaita hadi kukatika.

Gazeti lilipowasiliana na Mnyika na kumueleza kwamba amekuwa akitajwa katika ujumbe wa Zitto na Msacky, alikiri kupokea ujumbe huo wa baruapepe uliotoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa ni “Mtanzania mwema.”

Alisema alipoona ujumbe mmoja unahusu Zitto kushauri Msacky kutochapisha habari za mkutano wake na waandishi wa habari, ndipo aliamua kupeleka ujumbe huo kwa Zitto.

“Nilimuuliza kuna hiki kitu nimetumiwa. Je, haya ni maandishi yako au kuna mtu ameingilia emaili yako na kujiandikia haya? Hadi leo hii, bado sijapata jibu,” alisema Mnyika kwa sauti ya masikitiko. Alisema yeye hana cha kusema na kuongeza, “labda umuulize Zitto.”

Alipoulizwa anachukuliaje suala hilo, Mnyika alisema, “Ukiniuliza mimi kwa upande wangu, nilitegemea mambo hayo yangemalizwa katika vikao vya chama na si kwa vyombo vya habari. Lakini kwa hatua ya hivi sasa, nadhani Zitto bado anayo fursa ya kulieleza hili.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe alipoulizwa juu ya madai ya kuwapo njama za kuhujumu chama chake zinazofanywa na Msacky kwa kumtumia Zitto, haraka alijibu, “tuna utaratibu wetu wa kushungulikia mambo ndani ya CHADEMA.”

Alisema, “Sina la kusema. CHADEMA ina utaratibu wake wa kushughulikia mambo yake.”

Kwa kadri mawasiliano ya Zitto na Msacky yanavyoonyesha na iwapo yatathibitishwa kuwa kweli, jambo ambalo linaanza kuthibitishwa na Zitto kwa kulalamika kuingiliwa kwenye faragha, basi uhusiano wake katika chama utakuwa umepata nyufa.

Wachunguzi wa siasa za upinzani nchini wanasema kwa hali hii, uwezekano wa Zitto kubaki ndani ya chama chake ni mdogo. “Ama atajiondoa mwenyewe au hatimaye atafukuzwa,” ameeleza mkufunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Hata hivyo, Zitto amenukuliwa na Mwananchi akisema, “Sitaki kugombana na mtu mimi. Wala msiniweke kwenye kifungo cha siasa. Ni bora niishi huru kuliko katika mateso ya siasa za kipumbavu kabisa. Nitafanya maamuzi ambayo hayajawahi kufikiriwa.”

Wiki iliyopita Kafulila aliwaambia waandishi wa habari kwamba Zitto atafanya maamuzi makubwa ambayo hawakutegemea.



Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu ambao ni mkusanyiko wa asasi zaidi ya 70 za kiraia zinazotetea haki za binadamu (THRD-Coalition) , kwa kushirikiana na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC),vimeelezea kulaani vikali shambulio la kinyama alilofanyiwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda.

Uchunguzi tulioufanya bado haujatujapatia habari za undani zaidi na uhakika wa tukio hilo, lakini kwa taarifa za awali kwa asilimia kubwa linahusiana na kazi yake ya utetezi wa haki za binadamu kupitia taaluma yake ya uandishi wa habari.

"Tunasema hivyo kwa sababu vitisho dhidi ya wanahabari na watetezi wengine wa haki za binadamu,vinataka kuzoeleka sasa hapa nchini jambo ambalo halikuwapo katika miaka ya nyuma.

"Takribani ndani ya miezi 10 sasa, zaidi ya watetezi wa haki za binadamu 10 wakiwamo waandishi wa habari wameshajeruhiwa, wamepata vitisho au kuuawa."

Ilisema taarifa hiyo iliyosainiwa na Onesmo Olengurumwa, Mratibu wa Mtandao huo kuwa matukio hayo yanaashiria lengo la kutaka kuzima sauti za watetezi wa wanyonge kwa visingizio mbalimbali na wakati mwingine matukio haya yakipewa sura tofauti ikiwamo uhalifu wa kawaida, visa vya kudhulumiana na visasi vya kimapenzi.

"Hatupendi kuingilia wala kukwamisha utendaji kazi wa jeshi hilo, lakini pia hatupendi wanahabari na watetezi wengine wafanye kazi yao katika mazingira ya woga. Tunaamini kwamba zipo njia muafaka zaidi za kushughulikia masuala yanayohusu taaluma ya habari," ilisema taarifa hiyo.

Mtandao huo umewataka watu wote wanaotumika au wanaoendeleza wimbi la mashambulizi kwa wanahabari na watetezi wote wa haki za binadamu kwa ujumla, waache kufanya hivyo kwani wataliingiza nchi katika machafuko makubwa pamoja na kuisihi Polisi na Serikali kubeba jukumu lao la kuhakikisha usalama wa watetezi wa haki za binadamu, na raia wote.
Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu ambao ni mkusanyiko wa asasi zaidi ya 70 za kiraia zinazotetea haki za binadamu (THRD-Coalition) , kwa kushirikiana na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC),vimeelezea kulaani vikali shambulio la kinyama alilofanyiwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda.

Uchunguzi tulioufanya bado haujatujapatia habari za undani zaidi na uhakika wa tukio hilo, lakini kwa taarifa za awali kwa asilimia kubwa linahusiana na kazi yake ya utetezi wa haki za binadamu kupitia taaluma yake ya uandishi wa habari.

"Tunasema hivyo kwa sababu vitisho dhidi ya wanahabari na watetezi wengine wa haki za binadamu,vinataka kuzoeleka sasa hapa nchini jambo ambalo halikuwapo katika miaka ya nyuma.

"Takribani ndani ya miezi 10 sasa, zaidi ya watetezi wa haki za binadamu 10 wakiwamo waandishi wa habari wameshajeruhiwa, wamepata vitisho au kuuawa."

Ilisema taarifa hiyo iliyosainiwa na Onesmo Olengurumwa, Mratibu wa Mtandao huo kuwa matukio hayo yanaashiria lengo la kutaka kuzima sauti za watetezi wa wanyonge kwa visingizio mbalimbali na wakati mwingine matukio haya yakipewa sura tofauti ikiwamo uhalifu wa kawaida, visa vya kudhulumiana na visasi vya kimapenzi.

"Hatupendi kuingilia wala kukwamisha utendaji kazi wa jeshi hilo, lakini pia hatupendi wanahabari na watetezi wengine wafanye kazi yao katika mazingira ya woga. Tunaamini kwamba zipo njia muafaka zaidi za kushughulikia masuala yanayohusu taaluma ya habari," ilisema taarifa hiyo.

Mtandao huo umewataka watu wote wanaotumika au wanaoendeleza wimbi la mashambulizi kwa wanahabari na watetezi wote wa haki za binadamu kwa ujumla, waache kufanya hivyo kwani wataliingiza nchi katika machafuko makubwa pamoja na kuisihi Polisi na Serikali kubeba jukumu lao la kuhakikisha usalama wa watetezi wa haki za binadamu, na raia wote.

Besigye beats security to attend Kategaya’s burial



Presidential security appeared anxious in Itojo, Ntungamo District, yesterday when Dr Kizza Besigye made a surprise appearance, joining thousands of mourners at the burial of First Deputy Prime Minister Eriya Kategaya.

Amidst a heavy downpour, the arrival of the former leader of the Forum for Democratic Change coincided with the landing of a military helicopter carrying President Museveni.

Dignitaries from government institutions like, judiciary, military and parliament attended the somber occasion that saw Mr Museveni describe his former bosom buddy as a “well-formed gentleman who kept no grudges.

“We disagreed twice but reconciled. In 1973, we disagreed on the setbacks we encountered when we attacked Mbarara. We parted ways; he went to Lusaka (Zambia) and I to Arusha. We later reconciled and worked together,” Mr Museveni said.

Making mention of the 2001-2003 events that split the once bosom-buddies, Mr Museveni said;“If you go left and I go right, that does not stop us from working together in the future,” giving the example of the third deputy premier Moses Ali.

“I salute him for being a fully reformed person in terms of character and ideology. There should be no need for us as men to endlessly be at loggerheads,” he added.

Kategaya fell out with the President and joined the opposition when he opposed the lifting of presidential term limits from the Constitution by the Seventh Parliament at the reported instigation of the country’s leader. He was sacked from Cabinet and Mr Museveni, who had then come to his second and last constitutionally-accepted a five-year term and went on to run for office again in 2006.

Ms Joan Kategaya, first wife to the deceased, asked government to construct a fully-equipped hospital in Kategays’s memory.

“We were only looking for a hydro-therapy machine to save his life. That is why we had to go to Nairobi,” Ms Kategaya said.

Mr Museveni proposed the construction of a technical school in Ntungamo to be named after Kategaya.

Besigye arrives
At approximately 1.30pm, Dr Besigye walked into the main square at the Itojo home just as Mr Museveni’s chopper appeared over the Kategaya homestead.

Catching mourners by surprise, Dr Besigye’s arrival was announced by the master of ceremonies, State Minister for Labour Mwesigwa Rukutana, prompting a rapturous welcome from the crowd.
Current FDC president, Maj. Gen. Mugisha Muntu left his chair to welcome Dr Besigye who sat next to him.

Since Tuesday, Dr Besigye has repeatedly been arrested almost the moment he steps out of his Kasangati residence. Police has accused him of attempting to restart the walk-to-work activities that nearly paralysed operations in Kampala city for close to a year.

FDC western youth leader Francis Mwijukye said it was imperative for Besigye to bury his former comrade-in-arms, who was one of the founders of the FDC.

In Kampala, security around Dr Besigye’s residence appeared unaware that he had slipped past them.
They (security personnel) sleep hungry, on water and biscuits and are expected to guard and follow a person they do not know what his day’s plans are. Their superiors take all the operations money. Besides, we have the capacity to be anywhere at any time,” Mr Mwijukye said.

Security sources have told this newspaper Mr Museveni’s security detail was unsure how the public would react in the presence of the two politicians in the same place, who are former friends, but now arch rivals.