Sunday, 10 March 2013

Balozi India ahoji uadilifu viongozi nchini


“Sielewi vizuri sababu za Tanzania kutowashtaki mahakamani viongozi wanaokataa kutaja mali, labda ndivyo mnavyotaka, lakini nchini kwetu mali za viongozi ziko wazi, tena iko tovuti maalumu ambayo viongozi huandikwa mali zao, sisemi sheria zenu mbaya, bali ni maamuzi yenu Watanzania kuangalia,” alisema Shaw katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hii jana ofisini kwake.


Wakati Watanzania wakiilalamikia Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuwa ni mzigo kwa taifa kwa vile haina meno ya kuwashughulikia wanaokataa kutaja mali, Balozi wa India nchini, Debnath Shaw anasema kwao usipotaja mali unashtakiwa.

“Sielewi vizuri sababu za Tanzania kutowashtaki mahakamani viongozi wanaokataa kutaja mali, labda ndivyo mnavyotaka, lakini nchini kwetu mali za viongozi ziko wazi, tena iko tovuti maalumu ambayo viongozi huandikwa mali zao, sisemi sheria zenu mbaya, bali ni maamuzi yenu Watanzania kuangalia,” alisema Shaw katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hii jana ofisini kwake.

Hapa nchini iko sheria inayowataka viongozi kutangaza mali zao, hata hivyo, hakuna rekodi yoyoye inayoonyesha kama kuna kiongozi yeyote nchini aliyewahi kufikishwa mahakamani kwa kukataa kwake kutaja mali alizonazo.

Hali kadhalika mali zinazotangazwa haziko wazi kwa wananchi, hata mtu anapokwenda ofisi za tume ya maadili ili kujua kiongozi gani anamiliki nini, hatakiwi kudurufu alichokiona wala kutangaza, hivyo kuondoa maana au umuhimu wa chombo hicho.

India yakataa kuikopesha tena Tanzania

Balozi huyo pia alizungumzia taarifa za India kukataa kuikopesha tena matrekta Tanzania akisema “Hatujakaa kutoa mkopo kwa sababu nyingine zozote, bali mkopo una taratibu zake”.

Hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete alilitaka Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (Suma JKT), kulipa deni.Serikali za India na Tanzania ziliingia mkataba wa mkopo wa Sh40 bilioni kwa ajili ya ununuzi wa matrekta ambayo yalikabidhiwa kwa Suma JKT, hata hivyo kumekuwa na kashfa za baadhi ya vigogo kunufaika isivyo halali na matrekta hayo, tofauti na ilivyolengwa kwamba yangekopeshwa zaidi wananchi wa kawaida wanaojihusisha na kilimo.

Mkopo huo uliosainiwa mwaka 2010 utadumu kwa miaka mitano huku Tanzania kupitia Suma JKT, ikitakiwa kulipa Sh42 bilioni ikiwemo riba.

Hadi sasa Suma JKT imekusanya Sh16 bilioni ambazo ni kiasi kidogo ikilinganishwa na ukubwa wa deni, jambo ambalo Kikwete alikiri lingeweza kuifanya isikidhi vigezo vya kukopeshwa tena.

Hivi karibuni Tanzania iliomba tena mkopo, lakini India ilikataa. Balozi alipoulizwa kama kutolipwa madeni kwa ufasaha ni sababu ya kutokopeshwa tena alijibu kwa kifupi “Nafikiri madeni yanapolipwa, tutapata nguvu za kukopesha zaidi”.

Alipoulizwa kuhusu Serikali kuwa na deni kubwa, hivyo kuwekewa vikwazo vya kupewa mikopo, Waziri wa Fedha, William Mgimwa alisema kuwa jambo hilo analifahamu na kutaka atafutwe leo mchana ili aweze kulitolea ufafanuzi.

Mgimwa ambaye ni mbunge wa Kalenga alisema, “Kwa sasa niko jimboni, ila kuhusu hili suala la Suma JKT naomba unitafute kesho (leo) mchana tutazungumza na kukupa ufafanuzi zaidi.”

Uhuru Kinyatta atafuata nyayo za baba yake?




Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta amewashukuru wananchi pamoja na Mwenyezi Mungu kwa kumwezesha kushinda nafasi hiyo huku akiahidi kuijenga upya Kenya.

Uhuru amesema ataweka kipaumbele kwenye kutunza rasilimali za nchi na kuhakikisha zinawanufaisha wananchi wote, pia kuwawezesha wanawake na vijana.
Katika hotuba yake aliyotoa muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi jana, Kenyatta alisema anawashukuru wagombea alioshirikiana nao katika mchakato wote wa uchaguzi na kuwakaribisha kuungana.


“Nawashukuru wagombea wenzangu wote kwa kujitolea kwa moyo kushiriki katika kinyang’anyiro hiki kwa kuwa jambo hilo limezidi kuonyesha demokrasia iliyopo nchini,” alisema.


Aliongeza kuwa anaahidi kushirikiana vyema na wagombea hao akiwamo Raila Odinga kwa ajili ya kuijenga upya nchi yao, akiwakaribisha na kuwataka waondoe kinyongo kutokana na ushindi alioupata.


“Tulianza zoezi zima kama timu na nitashirikiana nanyi kama timu, ikiwamo kuhakikisha tunafuata yale yote yaliyopo kwenye katiba hususan kuhakikisha kila mwananchi anapata haki yake anayostahili.”


Kiongozi huyo pia aliwashukuru watu mbalimbali waliofanikisha uchaguzi huo kwenda vyema ikiwamo vyombo vya habari katika nchi hiyo ambavyo vilikwenda sambamba katika kuripoti matukio yote ya uchaguzi, pamoja na vyombo vya usalama vilivyosimamia chaguzi hizo.


“Usalama bado ni tatizo katika nchi yetu, lakini ningependa kuvishukuru vyombo husika kwa kufanikisha tunavyozidi kuendelea suala hilo litakuwa vizuri,” alisema.

Uhuru alieleza hayo baada ya Tume Huru ya Mipaka na Uchaguzi (IEBC) kumtangaza kuwa mshindi katika uchaguzi uliofanyika Machi 4 akiwa amegombea kwa tiketi ya muungano wa Jubilee.

Uhuru aliibuka mshindi katika uchaguzi huo kwa kupata zaidi ya asilimia 50 ya kura zilizohitajika ili kupata ushindi kulingana na mahitaji ya Katiba Mpya ya nchi.

Matokeo yaliyotolewa na IEBC yanaonyesha kuwa Uhuru alipata kura 6,173,433 ambazo ni asilimia 50.07 huku mpinzani wake Raila Odinga akipata 5,340,546 ambazo ni asilimia 43.28.

Kwa ushindi huo, Uhuru amepata idadi kubwa ya kura inayohitajika na Katiba Mpya ambayo ni zaidi ya asilimia 50+1 na kuzuia uwezekano wa kurudiwa kwa uchaguzi.

Uhuru pamoja na mgombea mwenza wake, William Ruto wamepata ushindi huo huku wakiwa wanakabiliwa na mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.

Ushindi huo umepingwa na mpinzani mkuu wa Uhuru, mgombea urais kupitia muungano wa Cord, Raila Odinga ambaye amesema ‘kamwe hawatayatambua’ na kuahidi kuyapinga mahakamani.

Akizungumza muda mfupi baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Odinga alisema anajiandaa kwenda mahakamani kupinga matokeo ya urais yaliyompa ushindi Uhuru.

Odinga, aliwaambia waandishi wa habari kuwa matokeo yaliyotolewa na tume hiyo yalikuwa yamehujumiwa hasa baada ya kutokea hitilafu katika mitambo ya elektroniki iliyokuwa inatumiwa katika shughuli hiyo.

“IEBC imerudia makosa yaleyale ya uchaguzi mkuu wa 2007, kwa kuwa tuna mahakama tunayoiamini tunaomba watu wetu watulie hadi mahakama itakapotoa uamuzi. Wenzetu pia wajiepushe na aina yoyote ya ghasia,” alisema.

Alisema kwamba hana tatizo la kushindwa iwapo ameshindwa kihalali, lakini kwa matokeo haya ana jukumu kubwa la kupinga mahakamani ili kulinda mahitaji na heshima ya wapiga kura.

Aidha, alisema kugoma kwa mitambo hiyo kulichanganya mambo katika shughuli ya kuhesabu kura.

Alisema kuwa baada ya kutokea hitilafu, kura alizokuwa amepata katika maeneo bunge ambayo ni ngome zake, ziliongezwa kwenye hesabu ya kura za muungano pinzani wa Jubilee.

Siku moja kabla ya kutangaza matokeo hayo, IEBC ilikiri kuwa matatizo yaliyosababishwa na mtambo wake wa kupeperusha matangazo ni pamoja na kuongeza mara nane kura zilizoharibika.

Baadhi ya wananchi walieleza kuwa na wasiwasi kuhusu idadi kubwa ya kura zilizoonekana kuharibika, kwani zilikuwa kura zaidi ya 300,000 ambapo kwa sasa zimepungua mpaka kufika idadi ya kura 80,000, baada ya kuhakiki kura hizo kwa mara ya pili.

Pingamizi lao lilikataliwa

Mapema wiki hii, wakati shughuli ya kuhesabu kura za urais ilikuwa inafanyika, wanaharakati walifungua kesi mahakamani kutaka uchaguzi usimamishwe kutokana na hitilafu mbalimbali zilizotokea , lakini mahakama kuu ilitupilia mbali kesi yao ikisema kuwa haina uwezo wa kufanya uamuzi katika kesi hiyo, na kuwa ni mahakama ya juu zaidi pekee inayoweza kusikiliza kesi hiyo.

Matokeo hayo na mivutano yote iliyopo kwa sasa vinatokea baada ya siku tano tangu Wakenya kupiga kura kuchagua rais, magavana, maseneta, wabunge, wawakilishi wanawake na wawakilishi wodi.

Tume ya uchaguzi ilichukua zaidi ya saa tano kukagua hesabu ya kura hizo kabla ya kutangaza matokeo hayo jana mchana.

Kwa mujibu wa maagizo yaliyopo katika Katiba Mpya ya nchi hiyo, mshindi wa uchaguzi anatakiwa kutangazwa iwapo tu ametimiza masharti ya kikatiba ya kutangazwa kuwa rais wa nne wa Kenya.

Pamoja na ushindi wa kura kwa zaidi ya asilimia 50 lazima awe ameshinda asilimia 25 katika nusu ya kaunti zote 47 nchini Kenya.


Thursday, 28 February 2013

Photo show ends on Monday, the day Kenyans go for the General Election




Head of Public Service Francis Kimemia (left) and Presidential Press Service boss Isaiya Kabira tour the photo exhibition, The Kibaki Years, which Mr Kimemia officially opened at KICC on February 4. It ends on March 4. Photo/FILE NATION MEDIA GROUP
The story of President Kibaki and his political journey has been told for the whole month on the walls of an expansive room.

The room at the Kenyatta International Conference Centre in Nairobi, has a collection of his memorable pictures on display.

Kenyans who’ve been at the photo collection have left glowing messages for their President, and many more were streaming in to view the photo collection, with just four days left to the election date.

The photo exhibition too will close on March 4 — next Monday — when Kenyans go to the ballot to pick Mr Kibaki’s successor.

There are those like Charles Kinyua who viewed the exhibition as “a great idea”, and others like Philip Masese who viewed it as a “remarkable exhibition” according to comments left in the visitors’ book at the KICC.

There’s a video with his clips at different functions, like the one where he’s telling all parents to take their children to primary school, and another clip where he’s warning all those businessmen who dodge taxes that tax evasion will not be tolerated.

There are sections at the exhibition showing Kibaki as a family man, his life in Parliament, his contribution to the economy, his days with Kenyatta, and then there’s the First Lady Lucy Kibaki.

There is one where the President is all smiles between Olympic athletics champions David Rudisha and Ezekiel Kemboi. Interestingly, the one that he took with Jamaica’s athlete Usain Bolt is not there.

There’s also a picture of President Kibaki with former US president Bill Clinton and two pictures showing Mr Kibaki with the current US President Barack Obama, when he visited Kenya as a senator, and one taken at the White House with Michelle Obama, after Mr Obama was elected for his first term. There is also a photo of the President with great African icon Nelson Mandela.

A section shows how Mr Kibaki was instrumental in ensuring regional stability, and he is right there with Dr John Garang, the then leader of the Sudan People’s Liberation Army, which was fighting for secession. Dr Garang died in 2005, but the Comprehensive Peace Agreement brokered by Kenya ensured that in the end, the South became independent in 2011.

And just for the record, Mr Kibaki met former Libyan leader Muammar Gaddafi, and was also given a replica shirt of the Brazilian football team, with number 10 at the back.

If the exhibition was meant to show President Kibaki as the man who rebuilt Kenya — the roads, the schools, the hospitals and the sports — it achieved exactly that.

“A great journey enviable by anyone. Great job!” Daniel Ng’etich noted in his comments on the visitors’ book.

Ms Michelle Muthoni wrote in past tense: “He was a great and inspirational leader. Fantastic job!”

Others like Edward Wafula saw all the pictures and simply wrote: “Enjoy your retirement”. Lyne Kayugira added: “History made to be remembered”.

“This is a wonderful journey. Great achievements. I am very proud of you,” noted Njeri Kiragu.

There’s also another picture of President Kibaki pushing a wheelbarrow full of wet concrete when he launched a road construction in Lilongwe, Malawi.

The only thing that might make one sad is that some of the pictures have no captions, and still others with captions, do not have dates or places where they were taken.
Then there’s the promise that more pictures can be viewed and downloaded on the website (http://www.kibakipresidency.go.ke) but when the Nation visited the website, using multiple browsers, there was no photo gallery or even information. It is still a skeleton.

Trained curators, who spoke to the Nation, off-the-record complained that the photos are not chronologically arranged, but they hope that if President Kibaki sets up a gallery in future the pictures will have to be arranged in a way that tell a story to people who do not know the history of Kenya.

The hope is that the photo gallery and the video might all be uploaded on the website for those Kenyans who would want to know their President a bit more, but did not get the chance to visit the KICC for the exhibition.

“This is a great step. It keeps us in touch with the outgoing President. God bless him and (Jomo) Kenyatta,” noted Linah Kimani.

Ann Ayodi added: “Old man, may the almighty God bless you for the rest of your life”.

Harambee Cash from the poor must have hurt Kibaki

There are two pictures at the exhibition that might inform why President Kibaki banned harambees (public fundraisings involving government officers) when he got into office.

Of course the official version was that the President wanted to keep public servants away from temptation of extorting people or stealing public resources, to get money for harambees..

But those two pictures show President Kibaki receiving donations from poor people, back in the days when he was Finance minister.

“A one-shilling donation may not be very much, but when it is all you’ve got, it means a great deal,” reads a caption of a photo showing Mr Kibaki in a suit getting the one shilling from a shy boy in small short, and an ill-fitting shirt in Isiolo. The money was for Merti Primary School and Sh21,000 was raised in 1972.

Another undated photo shows a mother lifting her four-year-old daughter so that the daughter hands over a Sh20-donation for building Kwale Primary School. Mr Kibaki then Vice President .

No wonder he quickly agreed with Mr Muriuki Karue, a former ol Kalou MP, when he proposed the Constituency Development Fund.

When a cheaper diploma pays more than a costly degree

Results. The A-Level results show that 76, 151 obtained at least two principal passes, which ideally qualifies them to enlist for post-secondary education.
Kampala.

Three years ago, Samuel Imbadi eyed an under-graduate course in Electrical Engineering. Kyambogo University was his choice institution.

An Advanced-Level subject combination of Physics, Economic and Mathematics (PEM) theoretically placed him in good stead to achieve his dream.
When results of the 2010 Uganda Advanced Certificate of Education (UACE) were released in early 2011, Mr Imbadi garnered 8 points, significantly lower than what is required for admission for a Bachelor of Electrical Engineering degree course. He was dejected.
His colleague and alumni of Old Kampala SS opted to repeat, enlist as private students on other university course(s) or drop out altogether – and many of last year’s A-Level students, whose resulted were released yesterday, face similar choices.

Uganda’s largely theoretical education focused on literacy, numeracy and the learning has encouraged recitation and memorisation, but not practical skills crucial for innovations, production and wealth creation. Yet the country has chosen sciences over humanities, which President Museveni preaches as the right medicine to transform Uganda.
But what does his government do to realise this vision?
The A-Level results show some 76, 151 obtained at least two principal passes, which ideally qualifies them to enlist for post-secondary education.

Government sponsors only some 4, 000 students at the five public universities; Makerere, Kyambogo, Mbarara, Gulu and Busitema. Others with handsome financing will enroll and pay for – perhaps buy – degree courses at these public and the other 27 private universities.
However, several thousand will miss out either because they lack money for tuition or have significantly lower scores than the threshold admission requirement.
So what are the alternatives, or should they even be second-rate options?

“Successful candidates”, Education Minister Jessica Alupo said while releasing the results on Tuesday; will get university slots.
She added: “I must (however) encourage A-Level leavers to seriously consider enrolling for technical, vocational and other courses at diploma level that lead to employment opportunities at the middle-level in the economy in both formal and non-formal sectors.”
Experts criticise such casual – almost derogatory - manner in which bureaucrats rate technical and vocational training as an anathema.

According to Fagil Mandy, an education consultant who chairs the country’s examinations body, “people managing education don’t understand and articulate the critical role vocational and technical skills play in a nation’s transformation”.
This skewed view is premised on the “deceptive” notion that tertiary institutions are for ‘failed students’, who in turn pity instead of asserting themselves, the former commissioner in the Ministry of Education said.

Self-pity is what Imbadi felt before he found himself offering a diploma in Automobile Maintenance and Repair at Nakawa Vocational Training Institute, a few kilometres from Kyambogo University where he originally intended to enroll.
“At first I didn’t like [the idea of joining a technical institute],” he said a matter-of-factly, before an exposure to vehicle handling at a garage during his vacation changed things.

Now he relishes the sight of vehicles he has helped fix wheeze out of the Nakawa workshop – a fulfillment that only a hand-on involvement can bring. “You get the real feel of doing something, not just the theory,” he said. Besides, there is money to make for upkeep and Imbadi, 22, just started his 2nd year at the institute.
More, university students doing the related courses come for practicals at Nakawa Vocational Training centre where Imbadi says he has on occasions shown them “how to do mechanical and electrical things”.

“People should stop looking at Business, Technical, Vocational education and training as a last resort,” said Paul Amoru, spokesman of the statutory entity that examines these courses. “We are looking for the best brains, not failures.”

A person who learns automobile servicing like Imbadi will become a mechanic, another one smart in wood work can own or be employed at a workshop making fine furniture and diploma-level masonry training produces a fine builder – all job creators of sorts.

And there are at least 10 public institutions offering diplomas in diverse fields such as cooperatives and business administration, boat building and marine mechanics, fisheries management and technologies, cartography, physical planning, land management and valuation, surveying, meteorology as well as wild life and allied natural resources management.

So, why are these courses that give practical skills often shunned by students and parents?
The problem, Mr Mandy says, is negative perception. To surmount it, he proposes that institutions (see list in table) should be well managed, financed and the theme of apprenticeship and vocational training articulated and popularised by all education stakeholders.
That tosses the ball back to government’s court. Primary and secondary schools offering practical subjects such as metal or wood works and technical drawing are an exception, rather than the rule, and persuading uninitiated students after A-Level becomes an albatross.

Mr Amoru says Parliament’s enactment of the Business, Technical and Vocational Education and Training (BTVET) Act, establishing Uganda Business and Technical Examinations Board (UBTEB), means the country is on course to streamline and exercise control in technical education. That would entail deeper reforms in the education sector.

Home Business Business Barclays Bank Tanzania worst performer in EA





Barclays Bank’s Adan Mohamed. Analysts cite the bank’s ‘Hello Money’ service as one way of reducing costs instead of laying off workers. le="text-align: left;" trbidi="on">

Barclays Bank’s subsidiary in Tanzania is the lender’s worst performer among its East African units, a new Citi Group research report shows, citing spiralling costs and falling net earnings.

Data from the research released last week shows earnings from the Tanzanian unit have declined at an annual compounded rate of 43 per cent over the past six years.

During that period, the Kenyan unit has recorded a growth of 11.6 per cent while Uganda’s earnings have surged by 5.5 per cent.

The Tanzania unit’s cost to income ratio — a financial measure that shows a company’s costs in relation to its income — stood at 94 per cent, higher than that of the subsidiaries in Kenya and Uganda, a factor that Citi says has eroded the lender’s value.

Kenya’s cost to income ratio is at 52.5 per cent (above the industry average of 50 per cent) while Uganda’s is at 72 per cent. Ordinarily, this ratio gives investors a clear view of how efficiently a firm is being run — the lower it is, the more profitable the bank will be.

“What makes the high cost to income ratio even more unacceptable, in our view, is that Barclays Tanzania earns 44 per cent of its revenue in the form of non-interest revenues (NIR), which is markedly higher than for most of Barclays’ operations in Africa. We believe Barclays Tanzania needs to cut costs and/or increase lending margins otherwise it has no value,” said the analysts.

NIR is basically income earned from sources other than what banks charge customers for loans — such as deposit and transaction fees and monthly account service charges.

Barclays Bank’s operations in the region have struggled to contain expenses, with the Kenyan subsidiary announcing on February 13 it will cut 200 jobs this year as it tries to bring down costs.

For the Kenyan operation, costs jumped by their largest margin in five years for the 12 months ending December 2012. Operating costs jumped five per cent from Ksh13.8 billion ($157 million) to Ksh14.2 billion ($165 million).

Barclays Bank of Kenya posted a 7.7 per cent increase in profits after tax, riding on higher returns from government securities, which pushed net profits to Ksh8.74 billion ($97.6 million) for the full year 2012 compared with Ksh8.11 billion ($94.3 million) a year earlier.

Laying off workers

Last year, Barclays Tanzania closed down 10 branches, and laid off 100 employees in an attempt to bring down costs.

Analysts at Old Mutual see the “laying off workers approach” as unsustainable in the long run. “They can lay off this year, but what about say next year?” asked Erick Munyowki, a research analyst at Old Mutual, adding that investing in technology would be a more suitable way of bringing down costs.

“For example, on average, a bank incurs Ksh7 ($0.08) for every mobile-based transaction compared with Ksh100 ($1.16) for over the counter transactions. Agency transactions cost less than Ksh30 ($0.34),” said Mr Munyowki.

Uganda to spend $377,000 on MPs’ iPads



/-56xvqRDGh6Q/US8ncYSDwDI/AAAAAAAAATw/nxl_IbRhJco/s1600/ipads.jpg" imageanchor="1" >
The Ugandan Parliament is to spend about $377,000 on iPad tablet computers for MPs.

Parliamentary officials say apart from bringing MPs up to speed with evolution in technology, they hope to save money in the long run by cutting on printing and other stationery expenses.

“They (iPads) would be Parliament property but when someone uses one for five years you don’t expect it to be in shape for use by another legislator for another five years,” commissioner Elijah Okupa told the Daily Monitor.

“They will indirectly become their personal property because of depreciation,” he added.

Figures from Parliament show that the government spent at least $12.1 million over the last two financial years on computer supplies, printing, stationery, photocopying, binding, postage, courier and other communication costs.

They hope to save money by moving to paper-less operations in the House. For instance, any document from the Finance ministry has to be photocopied into almost 400 copies for each MP and other Parliament officials. These will now be e-mailed to the MPs instead. “It is a necessary tool of work, and we need them as MPs so that we avoid the amount of paper work which is always put in our pigeon holes,” Busiro East MP Medard Segona (DP) told the Daily Monitor.

Many MPs are not familiar with the gadgets, sources said, and the firm that will be contracted to supply them is expected to receive a training contract as well. “We can mitigate these costs and the only way is to use iPads now which are cheaper by the way if only members are trained on how to use them.

PSI: Tumezuia mimba milioni 1.2 zisizotarajiwa



Mtung’e alisema kifurushi hicho kitakuwa na vifaa vyote vitakavyohitajika kwa mjamzito kujifungua salama ambavyo alivitaja baadhi kuwa ni jozi mbili za glovu, nyuzi mbili, pamba, shuka kwa ajili ya matumizi ya mara moja, kitambaa cha joto cha mtoto, dawa ya kusafishia mikono, vidonge vitatu vya kuzuia mama kutokwa na damu nyingi.


SHIRIKA lisilo la kiserikali la PSI limesema kwamba limefanikiwa kuzuia mimba zisizotarajiwa 1.2 milioni mwaka uliopita.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam juzi, Mkurugenzi wa Afya ya Uzazi wa shirika hilo, Dk Nguke Mwakatundu alisema hiyo ilitokana na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa kwa mkakati wake wa kutoa huduma za uzazi wa mpango nchini.

“Tumefanikiwa kutokana na kutoa huduma za uzazi zaidi ya matumizi ya kondomu. Ukiangalia tangu shirika lilipoanzishwa miaka 20 iliyopita, matumizi ya kondomu yalikuwa yakitumika zaidi. Lakini sasa njia hiyo imepita na nyingine kama lupu, vipandikizi, vidonge na sindano ambazo matumizi yake yameongezeka maradufu,” alisema.

Alisema katika mwaka wa jana, njia za muda mrefu za uzazi wa mpango zilitolewa kwa watu 102,772 ikilinganishwa na watu 48,518 mwaka uliotangulia ikiwa ni ongezeko la asilimia 92.
Alisema mafanikio hayo yametokana na mkakati wa shirika hilo kupanua wigo wake wa kusambaza huduma za afya katika maeneo ya mbali...

“Tumeongeza utoaji wa huduma katika sekta ya umma kwa asilimia 145. Kitu kikubwa tulichofanya ni kuongeza timu ya watoa huduma katika maeneo hayo kutoka tano hadi 10 na kila timu ina wauguzi wawili.”

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa PSI Tanzania, Romanus Mtung’e alisema katika kuhakikisha kwamba utoaji huo wa huduma unakuwa salama, shirika lake linaandaa Kifurushi Salama kwa ajili ya Kujifungua (Clean Delivery Pack), kitakachoanza kusambazwa Aprili mwaka huu.

Mtung’e alisema kifurushi hicho kitakuwa na vifaa vyote vitakavyohitajika kwa mjamzito kujifungua salama ambavyo alivitaja baadhi kuwa ni jozi mbili za glovu, nyuzi mbili, pamba, shuka kwa ajili ya matumizi ya mara moja, kitambaa cha joto cha mtoto, dawa ya kusafishia mikono, vidonge vitatu vya kuzuia mama kutokwa na damu nyingi.

Alisema lengo la shirika lake siyo kupunguza idadi ya watu kama ambavyo imekuwa ikitafsiriwa na wengi, bali kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ili watu wapate watoto kwa mpangilio utakaowawezesha kuwatunza na kuwahudumia vyema na wao kupata fursa ya kushiriki katika masuala ya kiuchumi.

Ole Sendeka ahojiwa na timu ya Mangula





MBUNGE wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na vigogo kadhaa wa CCM Wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Manyara, wamehojiwa na maofisa wa CCM, kuhusiana na malalamiko ya ukiukwaji wa taratibu katika uchaguzi wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa ya chama hicho (Nec) wa wilaya hiyo.


Hatua hiyo ni utekelezaji wa mikakati ya Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), Phillip Mangula, ambaye aliahidi kushughulikia malalamiko yote ya chaguzi zilizopita na kuyatolea uamuzi. Mangula ndiye Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Maadili ya CCM.


Kuhojiwa kwa Sendeka na viongozi wengine wa Simanjiro, kumekuja siku chache baada ya kuhojiwa kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk Mary Nagu ambaye pia ushindi wake wa Nec Wilaya ya Hanang, ulilalamikiwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye akisema kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu na kanuni za uchaguzi wakati wa kinyang’anyiro hicho.


Katika uchaguzi wa Simanjiro, Sendeka alishinda kwa kupata kura 471 dhidi ya Diwani wa CCM Kata ya Mirerani, Justin Nyari ambaye alipata kura 126.


Maofisa hao kutoka Makao Makuu ya CCM, wakiongozwa na Mwanasheria wa CCM, Glorius Luoga waliwahoji Sendeka na Katibu wa CCM Wilaya ya Simanjiro, Jamillah Mujungu, Nyari na viongozi wengine wa chama hicho.


Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho kilichofanyika wikiendi iliyopita, zimebainisha kuwa Nyari na makada kadhaa wa CCM, wanalalamikia ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi huo, ikiwamo kufanyika kwa kampeni kinyume cha taratibu kama kutawaliwa na ukabila, pia baadhi ya wapigakura kutokuwa halali.


Hata hivyo, Luoga ambaye pia ni Mjumbe wa Nec anayetoka Songea Vijijini, alipotakiwa kuelezea hatma ya malalamiko hayo, hakutaka kufafanua kwa maelezo kuwa yupo Zanzibar.
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Manyara, Ndekubali Ndeng’aso alikiri kufika kwa maofisa wa makao makuu ya chama hicho mkoani hapo na kuhojiana na walalamikaji na walilalamikiwa.


“Nadhani hizi ni taratibu za kawaida tu ndani ya chama, kuna ambao wamelalamika sasa chama kimeona ni busara kuwafuata na kujua malalamiko yao,” alisema Ndeng’aso.
Sendeka na Nyari hawakupatikana jana kuelezea kilichojiri katika mahojiano hayo kwani simu zao za mkononi ziliita bila ya kupokewa.


Hata hivyo, Mujungu licha ya kukiri kuhojiwa alisema wenye mamlaka ya kuzungumza ni maofisa hao wa makao makuu... “Hili jambo lipo ngazi za juu nadhani wao ndiyo wana majibu ya maswali yenu.”

Papa wawili katika mgongano wa kimadaraka




YAMETIMIA. Safari ya miaka saba ya Baba Mtakatifu Benedict XVI inakamilika leo pale atakapong’atuka rasmi katika uongozi wa Kanisa Katoliki, ifikapo saa 2:00 usiku kwa saa za Italia (saa 4:00 usiku kwa saa za Tanzania).


Kwa siku mbili, Papa amekuwa na shughuli nyingi katika makao yake, Gandolfo Castel, Vatican akijiandaa kimwili kuondoka, akiweka sawa nyaraka zake binafsi na zile za kanisa ambazo zitawekwa katika kumbukumbu.


Kwa upande mwingine Vatican, nchi ambayo ipo ndani ya Jiji la Rome iliyozungukwa na ukuta, ikiwa na ukubwa wa hekta 44 na wakazi 832 pekee, imekuwa katika hekaheka nyingi.
Jana, waumini zaidi ya 50,000 na wengine wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani wakiwamo makardinali, maaskofu, mapadri na walei walialikwa kwa shughuli rasmi ya kumuaga kiongozi huyo.


Tofauti na kanuni yake, leo Benedict hatavaa viatu vyekundu kama ilivyozoeleka na badala yake amechagua viatu rahisi vya ngozi vilivyobuniwa Mexico. Alipewa viatu hivyo ikiwa ni zawadi wakati wa ziara nchini humo 2012.


Tangu alipotangaza uamuzi wake wa kung’atuka Februari 11, mwaka huu, utata umegubika nafasi yake katika maisha mapya ndani ya Vatican, akiitwa Papa Mstaafu.


Waumini, wataalamu na hata viongozi mbalimbali wa Kikatoliki wameanza kuhoji ni jinsi gani viongozi wawili (Papa) wataishi, huku wote wakivaa mavazi meupe wakiitwa Papa, wakiishi umbali mdogo kati yao, wakiwa na wasaidizi wengi wanaowahudumia.

Vatican
Nje ya Gandolfo Castel, ulinzi umeimarishwa na vibali vya kuingia Vatican vimesitishwa.
Juzi, Vatican ilitangaza kwamba Papa Benedict XVI atajulikana kama ‘Emeritus Pope’, yaani Papa Mstaafu mwenye cheo cha heshima, akiendelea kuitwa, ‘mtakatifu’ na ambaye ataendelea kuvaa nguo nyeupe.


Mavazi na hata jina lake jipya ni masuala ambayo yamezua uvumi mwingi, huku suala la mrithi wake mpya pia likiwa gumzo, kwani tukio kama hilo lilitokea miaka 600 iliyopita.
Ni uamuzi uliolishtua kanisa hilo lenye waumini 1.2 bilioni duniani na wengi wanasema awali, haikushauriwa Papa kustaafu kwani kwa kufanya hivyo kunaacha mizozo na minong’ono ya kuwania madaraka.


Hata hivyo, uongozi wa Vatican umesisitiza kuwa uamuzi huo wa Papa Benedict XVI ni wa kipekee na hakuna mzozo ambao utatokea baina yake na mrithi wake ambaye mchakato wa kumpata unatarajiwa kuanza ndani ya wiki mbili zijazo.


“Kulingana na mabadiliko katika kanisa letu, kuna Papa mmoja. Ni dhahiri kwamba katika hali ya sasa hakutakuwa na tatizo,” anasema Mhariri wa Gazeti la L’Oservatore Romano linalomilikiwa na Vatican, Giovanni Maria Vian.

Hofu iliyopo
Hata hivyo, wakosoaji wa mambo hawakubaliani na hoja hiyo na baadhi ya makardinali walioko Vatican kwa usiri mwingi, wanazungumzia suala hilo wakieleza kwamba litazua tatizo kubwa kwa Papa ajaye, hasa ikiwa mtangulizi wake, Benedict akiwa bado hai.


Mtaalamu wa tauhidi (theolojia), raia wa Uswisi, Hans Kueng ambaye amekuwa mtu wa karibu wa Papa Benedict XVI, ingawa kwa sasa ni mkosoaji wake amesema:
“Kwa sasa, Benedict XVI akiwa bado hai, kuna hatari ya kuwa na Papa kivuli, mwenye mamlaka kamili ambaye kwa chinichini anaweza kumshinikiza mrithi wake kufikia uamuzi.”
Hans Kueng alisema hayo alipozungumza na Gazeti la Der Spiegel la Ujerumani.


Msemaji wa Vatican, Padri Federico Lombardi alisema Papa Benedict XVI kwa upande wake aliamua aitwe Papa Mstaafu au ‘kiongozi mstaafu wa Roma.’ Anasema haelewi ni kwa nini ameamua kuacha jina lake la sasa la Askofu wa Rome.


Kwa wiki mbili zilizopita, maofisa mbalimbali wa Vatican wamekuwa wakifikiri kwamba Papa angeanza kuvaa mavazi meusi na kutumia jina la Askofu Mstaafu wa Rome ili kuepuka mkanganyiko na mrithi wake.
Mwingine ambaye amekuwa akizusha mkanganyiko ni Katibu wa Papa, Askofu Mkuu, George Gaenswein ambaye ataendelea kuwatumikia Papa wote wawili, yaani Benedict XVI kwenye Monasteri ndani ya Vatican na kazi yake ya kawaida ya kuwa kiranja katika nyumba ya Papa mpya.


Kwa upande wake, Papa Benedict XVI anasema anastaafu na sasa ataishi maisha ya sala na tafakuri ya kina, mbali na majukumu mengine ya kidunia.
Hata hivyo, bado atakuwapo kwenye nchi ndogo ya Vatican, mahali ambako makazi yake yatakuwa jirani na mnara wa kurushia matangazo wa Kituo cha Redio cha Vatican, akiliangalia vizuri Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.


Kwa upande wake, Kueng anasema ni kosa kwa Askofu Gaenswein kuwatumikia Papa wawili kwa wakati mmoja na pia Benedict XVI kubakia jirani na mahali hapo.
“Hakuna padri ambaye anapenda mtangulizi wake kuishi karibu naye na kufuatilia anayoyafanya.


Hata kama Askofu wa Rome, haipendezi kutenda kazi huku mtangulizi wako akiona na kufuatilia.”
Mbali na mitazamo hiyo, wengine wamedhani kuwa uamuzi wa Papa Benedict XVI unalenga kudumisha utamaduni wa watangulizi wake.


“Ninashangazwa kuona Papa Benedict XVI akiendelea kuitwa mbarikiwa na kuvaa nguo nyeupe,” anasema Padri James Martin, Mtawa wa Jesuit pia mwandishi na mhariri, lakini baadaye anajirudi na kusema:
“Lakini sioni ajabu, mbona marais wastaafu wa Marekani, bado wanaitwa Rais? ni alama ya heshima kwake.”


Katika mkanganyiko huo, wapo wanaoamini kwamba yanayotokea yanatokana na nguvu ya roho mtakatifu, huku wengine wakipiga upatu kwamba ni zamu ya Afrika kutoa Papa na wanatajwa Makardinali Peter Turkson wa Ghana na Francis Arinze wa Nigeria.

Mtanzania apewa uwaziri Rwanda

Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na

RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.


Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.


Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na Menejimenti ya Maafa) na Oda Gasinzigwa (Ofisi ya Waziri Mkuu- Familia na Jinsia).


Akizungumza kwa simu na mwandishi wetu jana, mdogo wa Profesa Rwakabamba, Timothy Rwamushaija anayeishi Dar es Salaam, alisema ndugu yake alizaliwa katika Kijiji cha Bushagara, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.


Alisema Profesa Rwakabamba alikuwa Mtanzania aliyeamua kuchukua uraia wa Rwanda na wote baba yao ni Mzee Titus Rwamushaija... “Huyu ni kaka yangu wa tumbo moja na kwa kweli tumefurahi sana kwa mafanikio yake sisi kama wanafamilia.”


Naibu Makamu Mkuu - Taaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Profesa Makenya Maboko alisema Profesa Rwakabamba alifanya kazi katika chuo hicho na aliondoka akiwa Mkuu wa Kitivo cha Uhandisi.


“Aliondoka wakati Kagame alipoingia madarakani na alikwenda kuongoza Taasisi ya Teknolojia ya Kigali (KIST) kabla ya kwenda katika Chuo Kikuu cha Kigali,” alisema Profesa Maboko.


Msomi huyo alikwenda Rwanda mwaka 1997, baada ya kuombwa na Rais Kagame ambaye alikwenda UDSM kuwaomba baadhi ya wahadhiri kwenda Kigali kufungua chuo kikuu katika taifa lake baada ya kumalizika vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1994.


Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa kwanza wa KIST na kukifanya kuwa miongoni mwa vyuo bora barani Afrika kwa masuala ya teknolojia jambo lililomfurahisha Rais Kagame.


Baada ya mafanikio hayo, Rais Kagame alimteua kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda, Butare ambako pia alijizolea sifa baada ya kusimamia vyema ujenzi wa mabweni kwa wingi na kiongozi huyo alimtunukia uraia wa nchi hiyo kama zawadi.


Hata hivyo, Profesa Rwakabamba atakuwa amelazimika kuukana uraia wa Tanzania kwa kuwa katiba ya nchi hairuhusu uraia wa nchi mbili.
Profesa Rwakabamba alipata elimu ya msingi huko Muleba na akajiunga na Shule ya Sekondari ya Ihungo.


Baada ya hapo, alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds, Uingereza na kupata Shahada ya Uhandisi mwaka 1971 na 1975 alipata Shahada ya Uzamivu katika fani hiyohiyo.