Sunday, 23 August 2015

Aliyeshindwa kurejesha fomu abomolewa nyumba

Nyumba ya mgombea ubunge jimbo jipya la

Nyumba ya mgombea ubunge jimbo jipya la Nanyamba,Twahil Saidi (CUF) iliyobomolewa na watu wasiojulikana kwa kile kilichodaiwa ni baada ya kushindwa kurudisha fomu hadi muda ulipoisha. Picha na Haika Kimaro  
Haika Kimaro
Mtwara. Kundi la watu wasiofahamika wamevamia na kubomoa nyumba ya mgombea ubunge wa jimbo jipya la Nanyamba kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF) lililogawanywa kutoka Jimbo la Mtwara Vijijini, Twahil Saidi kwa kile kilichodaiwa kuwa amekihujumu chama hicho baada ya kushindwa kurejesha fomu.
Hali hiyo imempa fursa mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) jimboni humo kuwa mgombea pekee.
Tukio hilo lilitokea juzi usiku. Inadaiwa kuwa mgombea huyo alipotafutwa na viongozi wa chama hicho juzi baada ya kushindwa kutokea katika ofisi za halmashauri alikopaswa kufika kurejesha fomu, hakupatikana na simu zake za kiganjani inadaiwa pia kuwa zilikuwa zimezimwa.
Wakizungumza na gazeti hili jana, baadhi ya wafuasi wa CUF, walidai kuwa hatua hiyo imewapunguzia thamani ya chama chao, lakini wataendelea kumtafuta ili kujua sababu iliyomfanya ashindwe kurejesha fomu.
Mkazi wa Nanyamba, Ally Jumbe alisema tukio la kubomolewa kwa nyumba hiyo huenda likahusishwa na kushindwa kurejesha fomu. “Tunahisi labda waliofanya hivi ni wanachama wenzake na wale wa vyama shirika vya Ukawa. Lakini mpaka tunapozungumza sasa, hakuna mtu aliyefahamika.”
Kwa upande wake msimamizi wa uchaguzi wa Jimbo la Nanyamba, Osca N’gitu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mji wa Nanyamba, alisema kati ya wagombea watatu waliochukua fomu za kuomba kugombea nafasi ya ubunge, ni mmoja kupitia CCM ndiye aliyerejesha fomu.
“Tulikuwa na wagombea watatu kutoka CUF, Chadema na CCM na kazi ya urudishaji fomu ilikuwa jana (juzi), ilianza saa mbili asubuhi hadi saa 10 jioni na mpaka inamalizika ni mgombea mmoja tu wa CCM, Abdallah Chikota ndiye aliyefanikiwa kurejesha fomu zake,” alisema na kuongeza:
“Baada ya hapo tuliendelea na utaratibu mwingine kama sheria zinavyoelekeza lakini leo (jana) asubuhi nikapata taarifa kuwa nyumba ya mgombea aliyechukua fomu kupitia CUF imebomolewa na watu wasiojulikana. Nilienda eneo hilo na kufanya kikao na viongozi wa serikali ngazi ya kijiji, kata na viongozi wa CUF, kimsingi nimewaomba kufanya utafiti wa kina ili kubaini waliohusika na tukio hilo na pili, kubaini ni kipi kilichomsibu mgombea huyo kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Henry Mwaibambe alipotafutwa alisema yuko nje ya ofisi ila ana taarifa ya kuwapo kwa tukio hilo.

Thursday, 13 August 2015

Mgeja, Guninita wajiengua CCM, wajiunga Chadema

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja na aliyekuwa mwenyekiti mkoa wa Dar es Salaam John Guninita wametangaza leo kuachana na CCM na kujiunga Chadema.
Makada hao wa CCM wametangaza kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Dar es Salaam leo.
Wakizungumza katika mkutano huo, makada hao wamesema wamechukua uamuzi huo baada ya kubaini CCM imepoteza mwelekeo na kwamba kinaendeshwa kibabe tofauti na misingi ya kuasisiwa kwake.
Wametolea mfano wa kukiukwa kwa demokrasia kulikofanywa wakati wa mchakato wa kutafuta mgombea urais wa chama hicho ambapo Dr John Magufuli aliteuliwa kupeperusha bendera ya CCM.
Hatua ya makada hao imekuja ikiwa ni siku moja tu tangu aliyekuwa mbunge wa chama hicho jimbo la Sikonge, Said Nkumba atangaze kuachana na chama hicho na kujiunga na Chadema.
Huo ni mwendelezo wa matukio ya makada na wabunge chama hicho kuhamia upinzani hasa Chadema kwani awali aliyekuwa waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa aliachana na CCM baada ya jina lake kukatwa na kamati ya maadili ya chama hicho.
Wengine waliohama CCM ni aliyekuwa mbunge wa Arumeru Magharibi, Goodluck Ole Medeye, aliyekuwa mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga ambaye pia ni naibu waziri Kazi na Ajira, aliyekuwa mbunge wa Kahama, James Lembeli, aliyekuwa mwenyekiti wa wenyeviti wa CCM, Mgana Msindai na mbunge wa viti maalumu anayemaliza muda wake Esther Bulaya.

Wednesday, 12 August 2015

Said Nkumba ahama CCM, ajiunga Chadema. Nini hatima ya CCM 25 Oct?

Mbunge wa Sikonge, CCM, Said Nkumba ametangaza kukihama hicho na kujiunga na Chadema, kwa madai CCM ‘haina mapenzi na watu’.
Nkumba anakuwa mbunge wa sita kutoka CCM kutimkia upinzani katika kipindi kisichopungua mwezi mmoja.
Wabunge waliokihama chama hicho ni Edward Lowassa (Monduli), Goodluck Ole Medeye (Arumeru Magharibi), Makongoro Mahanga (Segerea), James Lembeli (Kahama) na mbunge wa viti maalum, Esther Bulaya.
Lowassa ametimkia Chadema na ndiye aliyepewa jukumu la kupeperusha bendera ya chama hicho kwa mwavuli wa Ukawa, kugombea urais katika uchaguzi wa Oktoba 25, mwaka huu.
Akizungumza na Mwananchi kwa simu jana kutoka Tabora, Nkumba alisema: “Sikushawishiwa, nimejiondoa CCM kwa uamuzi wangu na nimefanya hivi kwa kuwa sikuwa nasikilizwa kwa kile nilichokisema.
“Niliipenda CCM kwa dhati kabisa, lakini sikuona sababu ya kuendelea kubakia CCM, sisikilizwi, chama hakina mapenzi na watu, ndiyo maana tunaondoka.”
Nkumba aliyekuwa kinara wa kuipinga Ukawa ambao baada ya kutoka bungeni kwenye Bunge la Katiba, alisimama kidete na kuanzisha “Tanzania Kwanza, Mbili yatosha” alisema amejiunga na upinzani ili kujenga chama cha Chadema.
“Mimi najiamini, ninakubalika ndani ya chama, sasa nimekuja huku, nataka kuendelea mazuri ya Chadema, ninaona huku kunanifaa,” alisema Nkumba.
Akizungumzia kuwa wanaokwenda upinzani ni makapi, Nkumba alisema kuwa hata makapi bado yanakuwa na faida.
“Unajua kuwa wakati mwingine makapi ya asali labda ukamua sawasawa, lakini kwa hapa, sisi bado tuna asali, si makapi yasiyokuwa na kitu.”
Kuhusu hatma ya CCM na kuondokewa watu mbalimbali na kujiunga upinzani, Mbunge huyo alisema kuwa wakuu wa chama hicho, lazima washtuke na wasipokuwa makini, huu utakuwa mwisho wa CCM.
“Hivi wewe hushtuki, wanaona kabisa chama kikubwa lakini watu wanaondoka, wanaona kabisa mwelekeo haupo, halafu wanaendelea na yao, ni wazi kuwa wataanguka,” alisema.

Saturday, 1 August 2015

Nape afafanua sakata lake na Takukuru Lindi

Lindi. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amefafanua sakata lake la kuchukuliwa na askari wa Takukuru kwa mahojiano muda mfupi baada ya kuchukua fedha benki, akisema alikuwa akielekea kulipa mawakala.
Nape, anayewania ubunge wa Jimbo la Mtama, jana mchana aliamriwa na maofisa wa Takukuru kufika ofisi zao baada ya kutoka kuchukua fedha benki ya NMB eneo la Misonobarini mkoa Lindi.
“Ninadhani hawa jamaa walipotoshwa. Mimi nimekwenda zangu benki kuchukua fedha, lengo langu ni kuwalipa mawakala,” alisema Nape jana jioni alipopigiwa simu na Mwananchi kutoa ufafanuzi wa sakata hilo.
“Wakaja hawa jamaa, wakajitambulisha kuwa wanatoka Takukuru, wakaniuliza ‘mbona ninachukua fedha nyingi kipindi hiki?’ Nikawaambia ‘nakwenda kulipa mawakala, na fedha zenyewe ni hizi Sh3.6 milioni’.
“Basi, tukatoka taratibu tukaenda ofisini kwao, ni karibu tu na benki. Wakanihoji hata haikumalizika nusu saa, niliwaambia nataka kulipa mawakala wangu, tena fedha zenyewe hazitoshi, wako zaidi ya 100.”
Nape aliongeza kusema kuwa walimkamata na akawaambia kuwa yeye ni mwadilifu.
“Halafu ninyi, mnaacha marushwa makubwa makubwa huko, watu wanahonga halafu mnamvizia Nape masikini kwa Sh3mil?,” alisema.
Nape alielezea kufadhaishwa na tukio hilo akidai kuwa limetengenezwa kwa ajili ya kumchafua hasa kwa kuwa leo kuna kura za maoni, lakini akasema anaamini yeye ni msafi.
Kamanda wa Takukuru wa Mkoa wa Lindi, Stephen Chami alikiri kumhoji Nape, lakini akasema walijiridhisha kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kulipa mawakala.
“Unajua tuna watu wetu, kwenye maeneo mbalimbali hasa kipindi hiki cha uchaguzi, tumeweka watu wetu maeneo mengi, tunataka kukomesha rushwa,” alisema.
Kilango ageuka ‘mbogo’
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango Malecela juzi aligeuka mbogo baada ya kuzushiwa katika mitandao ya kijamii kuwa anashikiliwa na polisi.
Taarifa hizo zilizosambazwa jana, zilidai kuwa Kilango alikamatwa juzi saa 5:00 usiku katika eneo la Dimbi, kijiji cha Bagamoyo kwa tuhuma za kutoa rushwa, madai ambayo ameyakanusha.
Hata hivyo, Kilango alipoulizwa jana alisema tuhuma hizo ni uzushi uliotengenezwa na baadhi ya washindani wake wakiamini kwa kufanya hivyo watamvurugia katika kura ya maoni inayofanyika leo.
“Sijakamatwa na wala sijaona hata polisi mmoja nyumbani kwangu. Nimelala nyumbani kwangu jana (juzi) na leo (jana) nimeamka nyumbani kwangu na niko kwenye mikutano ya kuomba kura,” alisema.
Kilango aliongeza,”Sasa hivi nimetoka kuomba kura Mtii nilikuwa peke yangu wagombea wanzangu wameingia mitini. Niko Bombo sasa hivi (saa 9;00 alasiri) ndio wanakuja nishapiga bao.”
Kwa mujibu wa Kilango, baadhi ya wagombea wamekuwa wakifanya kampeni zisizo za kistaarabu kwa kuandaa vijana aliodai wamepewa pombe ili wamzomee katika baadhi ya maeneo aliyopita.

Sifa 10 za mgombea urais bora wa upinzani 2015


Ni jana tu nimemaliza uchambuzi wa watu wanaotajwa au waliojitokeza kugombea urais au wale ambao hawajajitangaza na hawana nia lakini jamii ndani na nje ya vyama vyao inawataja kama watu wenye sifa, uwezo na hata vigezo vya kuiongoza nchi yetu, kutoka vyama vya upinzani.
Lengo la uchambuzi huu ni kuwafanya Watanzania waanze kuwafahamu viongozi wao wajao na hata aina ya sifa wanazoweza kuwa nazo. Inawezekana kabisa kuwa wagombea waliochambuliwa asitokee mmoja wao kugombea au la, lakini hapa ninachoangalia ni kwamba tayari wananchi watakuwa “wamesogezwa karibu na ajenda ya uchaguzi” na hata akiletwa mgombea kutoka wapi, walau wananchi watakuwa wanajua wafanye uamuzi wa namna gani.
Leo nahitimisha hoja ya wagombea wa upinzani kwa kutoa sifa 10 za mgombea urais bora kutoka upinzani ambaye anaweza kupigiwa kura nyingi na Watanzania na hatimaye kuwa rais mpya wa Tanzania:
1. Mwenye umaarufu/umashuhuri na anayekubalika
Sifa hii ni muhimu, unapokuwa nje ya dola na nje ya chama tawala siyo rahisi kukishinda chama kinachoongoza Serikali. Umaarufu, umashuhuri na kukubalika ni mambo ya lazima. Ukitizama historia ya dunia na hata Afrika, vyama vikongwe vilipoondolewa madarakani waliofanya hivyo walikuwa wapinzani mashuhuri. Umuhimu wa sifa hii ni kuwa walau mtu maarufu na mashuhuri au anayekubalika, tayari amewekeza “mbegu” kwenye mioyo ya wananchi, wanaweza kumwamini ili waondoe hatima ya nchi mikononi mwa chama kilichowaongoza kwa miaka 50 na kuiweka mikononi mwa watu wapya. Wananchi wasipomwamini kiongozi wa upinzani anayekuja kwa sababu wanamkubali, ndipo huzuka ile kasumba ya “tupige kura kwenye zimwi likujualo”.
Hatari ya sifa hii
Umaarufu, umashuhuri na kukubalika vitaweza kufanya kazi kwa upinzani ikiwa mgombea husika hatatumia mwanya wa kukubalika kwake kujenga kiburi na hatimaye kuwasaliti wananchi. Ndiyo kusema kuwa vyama vya upinzani vitapaswa kuchagua mtu bora ambaye atatimiza matakwa ya wananchi “hata kama ni maarufu kuliko jua”.
2. Atakayebeba ajenda bora na kuifafanua vizuri
Kubeba ajenda bora na kuwa na uwezo wa kuifafanua kwa lugha rahisi ni jambo la muhimu kwa mtarajiwa kutoka upinzani. Moja kati ya makosa makubwa ya vyama vya upinzani katika bara la Afrika ni kutaka kubeba ajenda nyingi na kumrundikia mgombea urais, nakubali kuwa Afrika ina matatizo katika kila sekta ya maisha ya mwanadamu, lakini lazima iwe na vipaumbele vinavyowaumiza wananchi. Mgombea bora wa urais kutoka upinzani atapaswa kuwa na ajenda bora kuliko ile ya CCM na atapaswa kuwa na uwezo wa kuifafanua akaeleweka na mipango ya utekelezaji wake ikawa siyo ya “kusadikika”.
Hatari ya sifa hii
Ni pale inapotokea kuwa mgombea bora wa urais kutoka upinzani anazunguka nchi na ajenda iliyo bora kabisa lakini utekelezaji wake ukifanana au kushabihiana moja kwa moja na ule wa mgombea wa CCM. Wananchi wakiona upinzani unahubiri mipango na mbinu zilezile za CCM wataamua pia kuchagua “shetani wanayemjua” ili kujiweka kwenye mazingira ya usalama zaidi. Hivyo, ajenda ya mgombea bora wa upinzani na utekelezaji wake vinapaswa kuwa “vya kipekee”.
3. Mwenye uzoefu na rekodi ya uchapakazi
Uzoefu wa uongozi na uchapakazi unaofahamika ni jambo la msingi kwa mgombea bora wa urais kutoka upinzani. Vyama vya upinzani haviwezi kushinda uchaguzi na mgombea bora vitakayekuwa naye ikiwa mtu huyo si mzoefu na mchapakazi anayefahamika, mtu mwenye kujali wengine katika kazi lakini ambaye wananchi wataamini kuwa huyu atasimama pamoja na sisi usiku na mchana kuleta mabadiliko ya nchi.
Katika siasa, wananchi hupaswa kwanza kuamini na kisha hufanya uamuzi. Ikiwa mgombea bora wa urais wa upinzani hatakuwa na rekodi za uzoefu wa utumishi (katika taasisi za dini, serikali, vyama vya siasa na nyinginezo) si rahisi kumuuza kwa wananchi. Pia, ni lazima awe ni mtu ambaye rekodi zake zinatajwa kuwahi kuleta mabadiliko makubwa mahali alipofanya kazi.
Hatari ya sifa hii
Sifa hii hupaswa kuelezewa na kufahamika kwa wananchi kutoka kwa timu za kampeni za wagombea, wakati mwingine wapambe wa wagombea huchukua muda mwingi kutaja elimu ya mgombea wakidhani wananchi wanachagua elimu, kumbe elimu ni jambo moja tu kati ya sifa 100 za kiongozi. Ikiwa sifa hii muhimu haielezwi kwa uwazi kwa wananchi na hasa kwa kutaja rekodi bora za mgombea wa upinzani, wananchi wanaweza kumpa kisogo.
4. Mwenye uadilifu usio na shaka
Mgombea bora wa upinzani katika uchaguzi, anapaswa kuwa na uadilifu uliotukuka, usio na madoa wala shaka. Hapa nina maana kuwa, awe ni mtu ambaye uadilifu wake unatambulika kwa wananchi na kwa Taifa zima. Awe na rekodi za uadilifu kumshinda mgombea wa CCM, nina maana kuwa, wananchi wakimpima huyu wa upinzani na yule wa CCM – haraka haraka wasimame na kusema, “…naam! Huyu wa upinzani ni mwadilifu zaidi”. Marais wengi walioingia madarakani hasa hapa Afrika na hata Ulaya na Marekani kwa kuviondoa vyama vilivyokuwa madarakani, walipimwa kwa sifa hii.
Hatari ya sifa hii
Kigezo hiki hupata shida kubwa katika nchi ambazo uelewa wa wananchi vijijini na hata mjini si mkubwa. Wagombea waadilifu nao huweza kuchafuliwa ndani ya siku moja tu. Katika nchi ambayo si ajabu mgombea akawa hata na uwezo wa “kuhonga” chombo cha habari ili kimchafue mwenzake, sifa za mgombea bora zinaweza kuingizwa katika tope. Vyama vya upinzani vitapaswa kuwa na mfumo sahihi wa kuhakikisha uadilifu wa mgombea wake unazungumzwa kama ulivyo na haubadilishwi na propaganda za CCM.
5. Mwenye uwezo wa kusimamia, kuinua uchumi
Moja ya matatizo ambayo hayana dawa hapa Tanzania ni usimamizi wa uchumi. Nchi yetu inayumba kila mara na tunashindwa kutekeleza mipango yetu kwa sababu ya uchumi dhaifu, unaobadilika kila dakika na ambao hauna dira. Mgombea bora wa urais kutoka upinzani atapaswa kuwa na uwezo wa kusimamia na kuinua uchumi wa nchi. Awe ni mtu ambaye akisimama na kuweka ajenda ya uchumi mezani, Watanzania wote wanamwelewa, kwamba “naam, huyu ana uwezo wa kusimamia uchumi na kuondoa umaskini wa nchi”.
Hatari ya sifa hii
Ni pale mgombea wa upinzani atazunguka na mipango kabambe ya uchumi lakini yenye shaka kubwa kwenye utekelezaji au kuondoa umaskini, lakini pia ni pale mipango hiyo haitakuwa ya muda mfupi. Katika nchi maskini, wananchi wanahitaji matokeo haraka, vyama vya upinzani vitakuwa na jukumu la kuwa na mipango ya mfano ya muda mfupi ili kuwahakikishia wananchi kuwa ile ya muda mrefu pia itaweza kutekelezeka kwa wakati
6. Kuongoza mapambano dhidi ya rushwa
Rushwa ni adui wa haki na ni tatizo kubwa katika ukuaji wa uchumi wa Afrika. Mgombea bora wa urais kutoka upinzani atapaswa kuwa mtu wa kipekee ambaye moja ya sifa zake kuu ni mapambano dhidi ya rushwa, ndogo na kubwa. Awe ni Mtanzania ambaye si tu kwamba anapiga vita rushwa, bali anawachukia wala rushwa kama “kifo” na ni mtu ambaye yuko mbali kabisa na wala “rushwa”. Ndani ya CCM kwenyewe nadhani watatafuta mgombea wa namna hii ili kulinda hadhi yao, vyama vya upinzani vitakuwa na jukumu la kutafuta mpinga rushwa mahiri kuliko yule wa CCM, kwamba ukiwaweka pamoja hawa wawili – wananchi wenyewe waseme “…naam huyu wa upinzani anaweza mapambano haya zaidi kuliko huyu wa CCM”
Hatari ya sifa hii
Ikiwa upinzani utakuwa na mtu mashuhuri katika mapambano ya rushwa lakini ukawa hauna mipango ya kuhuisha haraka mifumo inayoleta mianya ya rushwa ndani ya nchi. Ndiyo kusema kuwa moja ya mipango ya upinzani inapaswa kuwa ni pamoja na kuweka wazi mifumo mipya ya usimamizi wa mapambano dhidi ya rushwa na hata kueleza watu watakaokuwa na sifa za kufanya kazi na mifumo hiyo.
7. Asiyependa kulipiza visasi na atakayefuata sheria
Jambo hili si dogo katika siasa. Rais ajaye kutoka upinzani anapaswa kuwa na sifa hii. Kwamba afahamike na kujulikana kwa kutokuwa na tabia ya kulipiza visasi lakini ambaye atazingatia matakwa ya sheria katika utendaji na awe na rekodi hizo. Unajua, kuna mambo ya kisheria ambayo ni lazima rais yeyote yule akiingia lazima ayafuate, mfano, wizi wa pesa za umma, hata kama umefanywa mwaka 1960 na ushahidi upo, lazima watuhumiwa wachukuliwe hatua leo, “jinai haifi wala kupotea”. Lakini kuna masuala mengine mengi tu ya kawaida ambayo yalikuwa yanatendwa na uongozi uliopita kwa sababu “za kipuuzi” na zisizo na maana, hayana haja ya kuwa kichwani kwa rais anayekuja.
Hatari ya sifa hii
Wananchi wengi huhofia masuala ya usalama iwapo vyama vipya vitaingia madarakani, hasa Afrika na moja ya masuala ambayo hupoteza usalama ni “kulipiza visasi”. Ndiyo maana vyama vya upinzani vinawajibika kuwa na mgombea ambaye hatalipiza visasi kwa makosa ya nyuma ya kiutendaji, ila atafanya hivyo kwa yale yaliyokosewa kwa makusudi na kwa kutofuata sheria.
8. Uwezo wa kubadilisha mfumo wa nchi
Tangu tumepata uhuru, nchi yetu imekuwa inasifika kwa kuwa na mifumo mibovu na isiyo na tija katika kila sekta. Hili ni janga kubwa. Rais bora ajaye kutoka upinzani ana kazi kubwa ya kubadilisha mfumo wa sasa wa nchi katika kila eneo ili mifumo ifanye kazi kwa mbio na kwa tija kubwa zaidi. Leo kuna watu walishtakiwa miaka ya 1990 na bado wako gerezani bila kuhukumiwa, kuna Kiwanda cha Sukari Kilombero na huko bei ya sukari ni kubwa kuliko Dar es Salaam. Haya ni matatizo makubwa ya kimfumo. Wananchi watahitaji kuwa na kiongozi ambaye atakuja kubadilisha kabisa mifumo ya utendaji kazi katika nchi. Kwa bahati nzuri, upinzani unaweza kuwa na hoja kama hii kwani vyama hivyo havikuwahi kuongoza Serikali na vimekuwa “waathirika” wa mfumo uliopo.
Hatari ya sifa hii
Ubadilishaji wa mifumo ukifanywa haraka na kwa pupa, utaingilia na kuvunja hata mifumo ambayo ilikuwa imeanza kukua na kukomaa kwa upande chanya. Ni jukumu la mgombea bora wa upinzani na timu zake kutambua mifumo yote ya utendaji katika sekta za jamii na kubainisha tangu wakati wa kampeni, ipi itavunjwa na ipi itarekebishwa ili kutoleta hofu yoyote kwa wapiga kura.
9. Msimamo unaoeleweka juu ya Katiba
Suala la katiba mpya ni ajenda muhimu katika uchaguzi wa mwaka huu. Mgombea bora wa upinzani atapaswa, yeye mwenyewe kuwa na busara za kutosha na msimamo thabiti juu ya masuala ya kikatiba na hasa mchakato wa Katiba Mpya. Naona kuna Watanzania wengi watapiga kura katika uchaguzi wa mwaka huu kwa chama au mgombea ambaye atakuwa na misimamo ya wananchi katika suala la katiba. Hadi sasa hatuelewi kama katiba itapitishwa au la na hatuelewi kama wananchi wanaikubali au wanaikataa. Nani atatuvusha na kwa utaratibu gani? Majibu atakuwa nayo mgombea bora wa urais kutoka upinzani.
Hatari za sifa hii
Msimamo wowote ule wa mgombea urais wa upinzani katika jambo hili unaweza kuwa na athari chanya au hasi kulingana na namna wananchi wanavyolitazama suala la katiba. Kama mgombea huyu atakuwa na msimamo katika kuikataa Katiba Inayopendekezwa na kwamba ataanzisha mchakato mpya na ikiwa hayo ndiyo matakwa ya wananchi walio wengi, jambo hili peke yake litamuongezea kura za kutosha. La ikiwa kinyume chake, litakuwa na athari ya kiwango hichohicho bila kujali kama athari yenyewe ni chanya au hasi.
10. Uzoefu wa masuala ya kimataifa
Moja ya kazi kubwa za mkuu wa nchi ni kuliwakilisha Taifa katika masuala ya kimataifa. Rais bora kutoka upinzani hakwepi kuwa na rekodi imara ya masuala ya kimataifa, si kuishi Ulaya na Marekani, lakini kuwe na ushahidi wa kutosha kuwa amewahi kushiriki katika baadhi ya shughuli muhimu za kimataifa na kwamba huenda hata kimataifa yeye ni mtu bora. Nadhani CCM inaweza kuwa na mgombea mwenye sifa hii pia, ni jukumu la upinzani pia kuwa na mtu ambaye amejipanga vyema kimataifa na mambo aliyoyasimamia kimataifa pia yanajulikana, si lazima yawe ya kiserikali, yanaweza kuwa ya kijamii, ya kitaasisi au ya kitaaluma.
Hatari ya sifa hii
Sifa hii inaweza kufanywa moja ya propaganda za kuisaidia CCM, kwamba ndicho chama pekee chenye watu waliofanya kazi za kimataifa na wataifanya Tanzania ikubalike kimataifa. Vyama vya upinzani vitakuwa na jukumu la kupambana na propaganda hii kwa kuwa na mgombea ambaye tayari wananchi wanatambua kuwa ana uzoefu wa kimataifa usio na shaka ili kusiwe na tabu ya kuanza kumwelezea muda mrefu kwa wapigakura juu ya eneo hili.
HITIMISHO
Andiko hili peke yake haliwezi kujadili sifa zote muhimu za kiongozi bora kutoka vyama vya upinzani anayeweza kulivusha Taifa. Nimechokoza mjadala wa masuala muhimu tu. Tukumbuke kuwa, kazi ya kuongoza Serikali si nyepesi, inataka kujipanga kila idara na kuwathibitishia wapigakura kuwa mnaweza bila shaka. Tabia ya wapigakura huwa ni kutafuta namna gani watawaamini watu wanaowapa madaraka. Bahati nzuri vyama vya upinzani katika Taifa letu vimekwishafanya kazi ya kupigiwa mfano inayothibitisha, uzalendo, uadilifu, uzoefu uwajibikaji

Monday, 27 July 2015

Ukawa watangaza kumkaribisha Lowassa

Hai. Mwenyekiti wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Freeman Mbowe amesema kampeni za mwaka huu zitakazofanywa na umoja huo, hazijawahi kuonekana tangu nchi ipate uhuru 1961.
Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, alisema Ukawa itafanya kampeni kwa kutumia usafiri wa anga na ardhini na kuongeza kuwa safari hii hakutakuwa na mgombea wa CCM atakayesimama bila kupingwa na upinzani.
Ukawa unaundwa na vyama vinne ambavyo ni Chadema, NCCR-Mageuzi, NLD na Chama cha Wananchi (CUF) na vyote vimekubaliana kuweka mgombea mmoja wa urais, ubunge na udiwani.
Hata hivyo, hadi sasa umoja huo haujamtangaza atakayewania urais na pia haujaweka wazi majimbo ambayo wamekubaliana kuachiana ili kusimamisha mgombea mmoja.
“Tutafanya kampeni, ambazo hazijawahi kuonekana nchini. Naomba mtembee kifua mbele kwa sababu nina hakika tunakwenda kuchukua dola kutokana na kampeni za kisayansi tutakazokwenda kufanya,” alisisitiza Mbowe.
Mbowe alitoa kauli hiyo juzi wilayani Hai, wakati akiwashukuru wanachama wa Chadema waliomchagua baada ya kupata kura 269 kati ya kura 274 zilizopigwa katika Jimbo la  Hai.
Mbowe aliionya CCM kutotarajia mteremko na hata zile jitihada zao za kutaka kushinda uchaguzi kwa goli la mkono hazitakubalika.
“Tunaiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufanya kazi kwa weledi ili uchaguzi uwe wa huru na haki,” alisema na kuongeza:
Mwenyekiti huyo aliwataka wanachama wanaounda Ukawa na wafuasi wake kujiandaa kwa ushindi katika Uchaguzi Mkuu baadaye mwaka huu.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini wa Chadema, Mchungaji Israel Natse alisema hawakichukii chama tawala, bali matendo mabaya kama ufisadi na rushwa yanayofanywa na viongozi wake.

Siri nzito Ukawa, vikao vyaendelea mfululizo

Dar/Arusha. Licha ya Baraza Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi (CUF) kupokea taarifa ya Ukawa na kuamua chama hicho kiendelee kushiriki katika umoja huo, bado suala la mgombea urais wa vyama vinavyounda umoja huo limeendelea kuwa siri nzito.
Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya CUF jana, zilisema kuwa katika kikao chake kilichoketi juzi na jana mjini Zanzibar, baraza hilo lilipokea taarifa ya Ukawa, kuithibitisha na kuamua chama hicho kiendelee na ushirikiano huo.
Mkutano wa waandishi wafutwa
Pamoja na hayo, jana kutwa nzima viongozi wa Ukawa walikuwa kwenye vikao mfululizo na hakukuwa na taarifa rasmi zilizopatikana na hata mkutano na waandishi wa habari ulioitishwa jana jioni uliahirishwa bila kueleza utaitishwa tena lini.
Ingawa taarifa ya mkutano wa Ukawa na wanahabari haikutaja ajenda, habari zilizoenea katika mitandao ya kijamii zilibainisha kuwa walikuwa wanakusudia ama kutangaza chama kilichopitishwa na Ukawa kusimamisha mgombea urais au kutangaza jina la mgombea mwenyewe pamoja na mgombea mwenza.
Vyanzo mbalimbali ndani ya Ukawa, vilieleza kuwa ufunguo wa hatua hiyo ulikuwa unashikiliwa na CUF, ambayo hivi karibuni ilijitenga na umoja huo ili masuala yake yajadiliwe kwanza na vikao vyake vya maamuzi kabla ya kurejea kwenye meza ya majadiliano.
Taarifa za uhakika kutoka katika kikao hicho kilichoketi Zanzibar kwa siku mbili, zilibainisha kuwa wajumbe waliafikiana kinyume na ilivyotarajiwa kuwa wangevurugana.
Miongoni mwa mambo ambayo inadaiwa wameafikiana ni kuwa mgombea urais atoke Chadema na chama hicho kitoe mgombea mwenza.
Jussa: Watanzania mtafurahi
Hata hivyo, mmoja wa wajumbe wa baraza hilo, Jussa Ismail Ladhu alipoulizwa alisema ikiwa itaamuliwa mgombea mwenza wa Ukawa atoke CUF, hakutakuwa na shida kwa kuwa chama hicho kina wanasiasa wazuri, safi na makini na kwamba kitatoa mtu ambaye Watanzania wote watafurahi.
“Ikiamuliwa kuwa mgombea mwenza atoke CUF, wananchi msiwe na wasiwasi, CUF ina hazina nyingi, itatoa mtu bora, itawapa chaguo ambalo Watanzania wote wataridhika nalo,” alisema Jussa.
Pamoja na kuthibitisha kuwa Baraza hilo limeamua CUF iendelee kushiriki katika umoja huo, Jussa alisema kwenye mjadala matatizo kidogo yalikuwapo katika mgawanyo wa majimbo.
Hata hivyo alisema baada ya kuweka vigezo vya kuwa na mgombea wa Ukawa, sasa hakuna shida kwa kuwa majimbo machache yaliyosalia utaratibu wake utatangazwa hivi karibuni.
Kuhusu mgombea mwenza, Jussa alisema CUF ina nafasi kubwa ya kutoa mgombea huyo kwa sababu ndicho chama chenye nguvu Zanzibar na kina wanasiasa mahiri na makini.
Wagombea wetu tunataka wawe ni wale watakaohakikisha kuwa Katiba Mpya inapatikana mara baada ya uchaguzi ili kuyaweka sawa mambo yanayohitaji kuwekwa sawa.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Katiba, mgombea urais na mgombea mwenza wanapaswa kutoka chama kimoja, hivyo kama Chadema itamtoa mgombea urais inabidi pia mgombea mwenza atoke chama hicho.
Habari ambazo bado si rasmi zinasema kuwa mmoja wa viongozi wa CUF anaweza kuhamia Chadema ili kukidhi matakwa hayo ya Katiba.
Mkurugenzi wa Haki za Binadamu, Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salim Bimani alisema kuwa mambo katika Ukawa ni mazuri, wapo waliofikiri kuwa watavurugana, lakini wamekubaliana na sasa Watanzania wasubiri kupata wagombea safi katika ngazi zote.
Bimani alisema CUF kitaendelea kushirikiana na vyama vingine vya upinzani nchini ili kuhakikisha demokrasia inazidi kukua.
Vikao mfululizo Chadema
Habari zaidi zilizolifikia gazeti hili zilisema mshirika mwingine wa Ukawa, Chadema jana viongozi wake walikuwa katika kikao cha dharura cha Kamati Kuu kilichoshirikisha wajumbe wachache, hasa wale wanaopatikana kwa kupigiwa kura ili kuweka mambo sawa.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema, Tumaini Makene alikiri kuwapo kwa kikao hicho.
“Kamati Kuu ya Chadema inaendelea kukutana jijini Dar es Salaam kwa kikao maalumu cha dharura kujadili mambo mbalimbali,” alisema Makene katika taarifa yake fupi aliyotuma jana usiku.
“Mambo hayo ni pamoja na maandalizi ya chama kuelekea uchaguzi mkuu, kupokea taarifa za mwenendo wa kura za maoni na uteuzi wa awali wa nafasi za ubunge wa majimbo na viti maalumu zinazoendelea nchini nzima,” alisema Makene.
Habari za ndani ya kikao hicho kilichofanyika katika Hoteli ya Bahari Beach jijini Dar es Salaam, zilisema kuwa kilikuwa na jukumu la kupokea taarifa ya utafiti iliyofanywa nchini kote kuhusu mgombea anayekubalika zaidi.
Ingawa hakukuwa na taarifa rasmi kuhusu utafiti huo, lakini taarifa zinazoendelea kusambaa zinalitaja jina la waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuwa yuko mbioni kuhama chama chake cha CCM na kwenda Chadema, huku mgombea mwenza akitajwa kuwa atatoka upande wa Zanzibar CUF.
Mgombea mwenza kuhamia Chadema
Habari za ndani ya Ukawa zinasema chini ya makubaliano ya Ukawa ikiwa mgombea urais atatoka Chadema, mgombea mwenza akitoka chama kingine itabidi ahame chama chake ili aingie chama alicho mgombea urais ili kukidhi matakwa ya kikatiba.
“Tutakaposhinda uchaguzi, kama makamu wa rais atatoka CUF itabidi kila akitoka katika ofisi ya makamu wa rais, kituo cha kwanza atasimama Makao Makuu ya CUF kwa ajili ya kupeleka taarifa na kupata baraka za chama katika masuala muhimu.”
Chanzo chetu cha habari kinasema:  “Ikiwa Ukawa tutashinda Uchaguzi Mkuu Oktoba 25 na kupata nafasi ya urais, jambo la kwanza litakuwa ni kufanya Mabadiliko ya Katiba na kuruhusu demokrasia pana ya watu kuungana.”
Alisema hakuna ajabu yoyote kwa rais kutoka chama kimoja na makamu wa rais kutoka chama kingine.
“Hilo hata sasa linatendeka Zanzibar ambako Rais na Makamu wa Kwanza wa Rais wanatoka vyama tofauti na hakuna matatizo yoyote katika utendaji wa Serikali, kila mmoja anasimamia kwanza maslahi ya Taifa pili kuhakikisha sera za chama chake zinatekelezwa,” kilieleza chanzo cha habari.
Lowassa atajwa
Hii ndiyo ajenda ambayo imetawala mijadala kuhusu fununu za Lowassa kuhama CCM kwenda Chadema ili kukamilisha safari yake ya matumaini.
Gazeti hili linafahamu kuwa mazungumzo na Lowassa yamekwishafikia hatua nzuri ingawa kulikuwa na viongozi wachache ndani ya Chadema waliokuwa wameshikilia msimamo wa kumkataa lakini kutokana na presha iliyopo ndani na nje ya chama wasingefua dafu.
Mtei amkaribisha
Huku mjadala kuhusu Lowassa ukizidi kukolea, mwasisi wa Chadema, Edwin Mtei amemkaribisha mwanasiasa huyo na makada wengine wa CCM kujiunga na chama hicho kikuu cha upinzani.
Akizungumza na Mwananchi jana, Mtei alisema kwa sasa Chadema na Ukawa wanahitaji kura za kutosha kuing’oa CCM, hivyo hata kura ya mtu mmoja ni muhimu.
“Nimesikia Lowassa anatajwa kutaka kujiunga na Chadema, mimi namkaribisha aje, si yeye tu, aje na makada wengine wa CCM kwa kuwa tunapaswa kuimarisha nguvu za kuiondoa CCM madarakani,” alisema.
Alisema Chadema ni chama cha Watanzania wote hivyo hakiwezi kumfungia milango Mtanzania mwenye sifa za kujiunga na chama hicho asijiunge.
Hata hivyo, Mtei alisema makada hao wa CCM ambao wanataka kujiunga na Chadema endapo watakuwa na nia ya kupata uongozi, wajue kuna vikao vya kuwapitisha.
“Tunawakaribisha Chadema makada wote wa CCM bila masharti na kama wana nia ya uongozi Chadema ina vikao vya kupitia kulingana na sifa zao na vikao vitakuwa na maamuzi ya mwisho,” alisema.
Akizungumzia uchaguzi mkuu ujao, alisema ana uhakika muungano wa upinzani ndio silaha kubwa ya kuing’oa CCM madarakani.
“Uchaguzi uliopita Chadema tulishinda lakini tulichakachukuliwa lakini safari hii kupitia Ukawa tumejipanga kuhakikisha upinzani tunashinda kwa kiasi kikubwa,” alisema.
Alisema hadi sasa Chadema na ukawa kwa ujumla wake kuna viongozi wenye sifa ya kushinda urais na wanakubalika nchi nzima.

Thursday, 16 July 2015

S1522 SCOLASTICA SECONDARY SCHOOL


NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

CSEE 2014 EXAMINATION RESULTS

DISTINCTION = 44 MERIT = 41 CREDIT = 8 PASS = 0 FAIL = 0



CNO
SEX
GPA
CLASS
DETAILED SUBJECTS
S1522/0001
F
3.9
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+' COMM - 'B+' B/KEEPING - 'B+'
S1522/0002
F
4.0
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'A'
S1522/0003
F
4.0
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B+' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0004
F
3.9
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0005
F
4.1
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B+' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0006
F
2.1
CREDIT
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'C' BIO - 'C' B/MATH - 'C' COMM - 'C' B/KEEPING - 'C'
S1522/0007
F
3.3
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'C' COMM - 'B+' B/KEEPING - 'C'
S1522/0008
F
4.4
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B+' GEO - 'B' KISW - 'B+' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'A' CHEM - 'B+' BIO - 'A' B/MATH - 'B+'
S1522/0009
F
3.9
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0010
F
4.0
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0011
F
3.3
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' BIO - 'B' B/MATH - 'B' COMM - 'B' B/KEEPING - 'B'
S1522/0012
F
3.0
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B' COMM - 'C' B/KEEPING - 'B'
S1522/0013
F
2.9
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B'
S1522/0014
F
3.6
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0015
F
4.0
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'A' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0016
F
3.3
MERIT
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B+'
S1522/0017
F
2.7
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'D' COMM - 'C' B/KEEPING - 'D'
S1522/0018
F
3.7
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+' COMM - 'B' B/KEEPING - 'B+'
S1522/0019
F
4.0
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'A' COMM - 'B' B/KEEPING - 'B+'
S1522/0020
F
4.0
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'A' B/MATH - 'B'
S1522/0021
F
3.6
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B+' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B' COMM - 'B' B/KEEPING - 'B'
S1522/0022
F
3.1
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0023
F
4.0
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B+' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B' COMM - 'B+' B/KEEPING - 'B+'
S1522/0024
F
2.9
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'E' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'C'
S1522/0025
F
4.1
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B+' GEO - 'B+' KISW - 'B+' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0026
F
3.4
MERIT
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'C' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0027
F
3.6
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' BIO - 'B' B/MATH - 'B+' COMM - 'B' B/KEEPING - 'B+'
S1522/0028
F
2.1
CREDIT
CIV - 'C' HIST - 'E' GEO - 'C' KISW - 'E' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'D' COMM - 'D' B/KEEPING - 'D'
S1522/0029
F
3.3
MERIT
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'C' COMM - 'B' B/KEEPING - 'D'
S1522/0030
F
4.1
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B+' KISW - 'B+' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0031
F
3.3
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'B' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0032
F
3.6
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'E' GEO - 'B' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0033
F
3.9
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B+' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0034
F
2.9
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0035
F
2.4
CREDIT
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'D' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'D' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'E'
S1522/0036
F
3.9
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0037
F
3.3
MERIT
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0038
F
2.4
CREDIT
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'D' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'E'
S1522/0039
F
3.6
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0040
F
4.3
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B+' KISW - 'B+' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'A' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0041
F
2.7
MERIT
CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' BIO - 'C' B/MATH - 'B' COMM - 'B' B/KEEPING - 'C'
S1522/0042
F
3.6
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'E' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0043
M
3.4
MERIT
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0044
M
2.6
MERIT
CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'C'
S1522/0045
M
3.0
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B' COMM - 'C' B/KEEPING - 'B'
S1522/0046
M
2.9
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'E' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'D' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'B'
S1522/0047
M
3.7
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B+' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'B+' BIO - 'B' B/MATH - 'B+'
S1522/0048
M
4.4
DISTINCTION
CIV - 'B+' HIST - 'B' GEO - 'B+' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'A' CHEM - 'B+' BIO - 'A' B/MATH - 'B+'
S1522/0049
M
3.7
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' BIO - 'B' B/MATH - 'B' COMM - 'B+' B/KEEPING - 'B+'
S1522/0050
M
1.9
CREDIT
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'B' LIT ENG - 'C' BIO - 'C' B/MATH - 'C' COMM - 'C' B/KEEPING - 'D'
S1522/0051
M
2.7
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B' COMM - 'C' B/KEEPING - 'C'
S1522/0052
M
3.3
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B'
S1522/0053
M
4.1
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'A'
S1522/0054
M
3.9
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0055
M
3.1
MERIT
CIV - 'E' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0056
M
3.6
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0057
M
3.4
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'B' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B+' COMM - 'B' B/KEEPING - 'B'
S1522/0058
M
2.7
MERIT
CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'D' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'C'
S1522/0059
M
3.4
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0060
M
3.4
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0061
M
1.6
CREDIT
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'C' ENGL - 'C' LIT ENG - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'E' COMM - 'E' B/KEEPING - 'D'
S1522/0062
M
3.3
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0063
M
2.9
MERIT
CIV - 'D' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0064
M
3.0
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0065
M
3.1
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0066
M
4.1
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B+' GEO - 'B+' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0067
M
3.4
MERIT
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B'
S1522/0068
M
3.4
MERIT
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0069
M
2.6
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'C' B/MATH - 'E'
S1522/0070
M
2.3
CREDIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'C' BIO - 'C' B/MATH - 'E' COMM - 'C' B/KEEPING - 'C'
S1522/0071
M
3.3
MERIT
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0072
M
3.3
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'B+'
S1522/0073
M
2.4
CREDIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'D' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'C' COMM - 'C' B/KEEPING - 'C'
S1522/0074
M
3.1
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0075
M
3.6
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B+'
S1522/0076
M
3.0
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'B'
S1522/0077
M
3.1
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B' COMM - 'C' B/KEEPING - 'B+'
S1522/0078
M
3.7
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0079
M
3.0
MERIT
CIV - 'E' HIST - 'C' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B'
S1522/0080
M
2.7
MERIT
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0081
M
4.1
DISTINCTION
CIV - 'B+' HIST - 'B+' GEO - 'B+' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0082
M
3.6
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0083
M
4.1
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'A'
S1522/0084
M
2.6
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'D' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'C' B/MATH - 'B'
S1522/0085
M
3.9
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'D' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0086
M
3.9
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'B+' LIT ENG - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+' COMM - 'B+' B/KEEPING - 'B+'
S1522/0087
M
3.7
DISTINCTION
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0088
M
4.0
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0089
M
4.0
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'B' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+' COMM - 'B+' B/KEEPING - 'B+'
S1522/0090
M
2.9
MERIT
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' BIO - 'C' B/MATH - 'B' COMM - 'C' B/KEEPING - 'C'
S1522/0091
M
4.0
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'
S1522/0092
M
3.6
DISTINCTION
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B' PHY - 'B+' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S1522/0093
M
4.1
DISTINCTION
CIV - 'B+' HIST - 'B' GEO - 'B+' KISW - 'B' ENGL - 'A' LIT ENG - 'B+' PHY - 'B+' CHEM - 'B+' BIO - 'B+' B/MATH - 'B+'