“Baada ya kufa kwa Azimio la Arusha nchi ilipoteza itikadi imara ya kitaifa, kukosekana kwa itikadi hii ndiyo kumesababisha nchi kuongozwa bila kuwa na mfumo unaoeleweka. Mambo hayo ndiyo yanayosababisha migogoro…,” alisema Profesa Mpangala.
lakini walifumbiwa macho na kutochukuliwa hatua yoyote, sasa tabia hiyo imeota mizizi.
Juzi maaskofu hao walitoa tamko hilo katika ibada ya Ijumaa Kuu mjini Dodoma, kusema umefika wakati ambao Wakristo wamechoka na vitendo wanavyofanyiwa na baadhi ya waumini wa dini zingine.
“Tatizo ni kuwa Serikali inashindwa kuchukua hatua mapema, makanisa yanachomwa moto visiwani Zanzibar, migogoro inazidi, lakini hakuna hatua zozote ambazo Serikali inachukua katika kunusuru hali hiyo, tumechoka,” ilisema taarifa ya maaskofu.
Wakati maaskofu hao wakieleza hayo, jana Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum aliliambia Mwananchi Jumapili kwamba Serikali inatakiwa kuwakutanisha masheikh na maaskofu ili kumaliza tofauti zilizopo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Helen-Kijo Bisimba alisema Serikali ilitakiwa kuchukua hatua miaka mingi iliyopita kwa kuwa mgogoro huu haukuanza leo.
“Migogoro ya kidini ilianza siku nyingi lakini Serikali ilikuwa kimya, wapo watu waliokamatwa kwa tuhuma za kukashifu dini za wenzao lakini hawajachukuliwa hatua yoyote,” alisema Bisimba.
Akizungumzia hali hiyo Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Profesa Gaudence Mpangala alisema migogoro hiyo ilianza kuchipua miaka michache baada ya kufa kwa Azimio la Arusha.
“Baada ya kufa kwa Azimio la Arusha nchi ilipoteza itikadi imara ya kitaifa, kukosekana kwa itikadi hii ndiyo kumesababisha nchi kuongozwa bila kuwa na mfumo unaoeleweka. Mambo hayo ndiyo yanayosababisha migogoro…,” alisema Profesa Mpangala.
Alisema jambo jingine ni kufa kwa Siasa za Ujamaa na Kujitegemea, ongezeko la umaskini na watu kukosa ajira, hivyo kuwa wepesi kushawishika kujiingiza katika migogoro ya kidini.
“Nadhani umefikia wakati wa Serikali kufuata sheria ili kumaliza hali hii, ikiwa ni pamoja na kukutana na pande zenye migogoro,” alisema Mpangala.
Mhadhiri mwingine wa Chuo hicho, Dk Kitila Mkumbo alisema Serikali inatakiwa kufanya mambo mawili ili kumaliza tatizo hilo. Jambo la kwanza ni kuzikutanisha pande zote mbili huku yenyewe ikiwa katikati na kutoegemea upande wowote.
Katika maelezo yake, Sheikh Mussa alisema, “Serikali ndiyo mlinzi wa amani hivyo inatakiwa kuhakikisha inawakutanisha watu wa pande zinazosigana kiitikadi, lakini Watanzania pia tunatakiwa kutambua thamani ya amani yetu hivyo tunatakiwa kuisaidia Serikali katika jambo hili.”
Katika tamko la maaskofu hao lililosomwa na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu alisema, “Serikali imeshindwa kuchukua hatua kwa muda mwafaka, pindi inapotokea migogoro au dini moja kutishiwa amani.”
“Matokeo yanayotokea Zanzibar mathalan, Wakristo wanaoishi huko yamewasababishia hofu, hivyo wengi kuanza kuvikimbia visiwa hivyo na kukimbiliaTanzania Bara.”
Kwa mujibu wa Askofu Kinyunyu, suala la uchomaji wa makanisa hadi sasa limeshindwa kupatiwa ufumbuzi na kila kukicha bado makanisa yanaendelea kuchomwa moto akahoji Serikali kukaa kimya maana yake nini?
Saturday, 30 March 2013
Ni simanzi, taharuki zatawala D’Salaam
Zoezi la kutafuta miili iliyokwama katika vifusi inaendelea, zaidi ya maiti 22 zapatikana.
Dar es Salaam. Idadi ya watu waliokufa kutokana na kufukiwa na kifusi cha jengo la ghorofa 16 lililoporomoka juzi asubuhi jijini Dar es Salaam, imefikia 22.
Habari zilizopatikana kutoka eneo la uokoaji na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova zinaeleza kuwa miili iliyopatikana imepelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Jengo hilo lililokuwa likijengwa mkabala na Msikiti wa Shia Ithnasheri ulioko Barabara ya Indira Gandhi na Kampuni ya Lucky Construction Limited liliporomoka saa 2.30 asubuhi wakati mafundi na vibarua wakiendelea na ujenzi huku chini watoto wakicheza mpira na mama lishe wakiendelea na biashara zao kama kawaida.
Rais Kikwete
Rais Jakaya Kikwete ambaye jana pia alifika katika eneo la tukio, kama ilivyokuwa juzi, alipata taarifa fupi ya maendeleo ya uokoaji kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, Said Meck Sadik na Kamanda Kova.
Baada ya kupewa taarifa hiyo, Rais Kikwete alimwagiza Kamanda Kova kuhakikisha wahusika wanakamatwa akiwamo Mkadiriaji Majengo (Quantity surveyor), mchora ramani za majengo (Architecturer), Mhandisi Mshauri (Consultant) na Mhandisi wa Jiji la Dar es Salaam. Juzi baada ya kutembelea eneo la tukio, Rais Kikwete aliagiza wahusika wote wa ujenzi huo wachukuliwe hatua kali.
Habari zilizopatikana jana zilidai kuwa Diwani wa Kata ya Goba, Wilaya Kinondoni, Ibrahim Kisoka ambaye ndiye mmiliki wa kampuni ya ujenzi, na Mhandisi Mshauri kwa pamoja wamejisalimisha Kituo Kikuu cha Polisi na hadi saa 8:00 jana mchana walikuwa wakihojiwa.
Awali Kamanda Kova aliwaambia waandishi wa habari kuwa amemtaka mmiliki wa Kampuni ya Lucky Construction Limited ambaye ni Diwani wa Kata ya Goba, Kisoka na wahusika wengine kujisamilisha kituo cha polisi, kabla hawajaamua kutumia nguvu kumtafuta.
Pinda atembelea eneo la tukio
Waziri Mkuu Mizengo Pinda alifika eneo hilo saa 3:41 asubuhi, kujionea hali ilivyo, lakini hakutoa tamko lolote. “Sina la kusema,” alisema Waziri Mkuu alipoulizwa na waandishi wa habari kutoa kauli ya serikali kuhusiana na tukio hilo.
Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi aliyefuatana na Pinda, alisikika akimwagiza Kamanda Kova kuhakikisha mchora ramani wa jengo hilo naye anatiwa nguvuni kwa kuwa jengo hilo lilikuwa la ghorofa 10, lakini likajengwa hadi 16. Mtu mwingine ambaye anatafutwa na jeshi la polisi kukamatwa ni Mhandisi Mshauri.
Lukuvi alimwagiza Kova kuwa watu waliokuwa karibu na jengo jingine la ghorofa 15 lililojengwa na mkandarasi huyo, kuhama mara moja na ubomoaji ufanyike bila kuleta madhara.
Mwenyekiti wa CUF
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba alitumia fursa hiyo kuitaka Serikali kuwabana makandarasi wasio na sifa kwani wanahatarisha maisha ya watu.
“Huu ni uzembe, wahandisi wa jiji walikuwa wapi? Wasimamizi na washauri walikuwa wapi hadi jengo linafikia ghorofa 16?” Alihoji Profesa Lipumba.
Profesa Lipumba aliitaka Bodi ya Makandarasi (CRB) kufuta leseni ya kampuni hiyo, kwani imeonyesha kuwa haiwezi kusimamia ujenzi na hivyo kusababisha vifo.
Huzuni, vilio na simanzi
Vilio na huzuni viliendelea kutanda jana katika eneo hilo ambapo waokoaji walikuwa wakijitahidi kufukua vifusi na kuzingirwa na watu waliokuwa wakisubiri ndugu zao waliofukiwa na kifusi kutolewa.
Watu wengi tangu asubuhi walikuwa wamesimama karibu na eneo hilo huku wengi nyuso zao zikiwa zimegubikwa na simanzi na wengine wakilia. Mama mmoja aliyekuwa akilia mapema asubuhi katika Mtaa wa Mshihiri, alisema mwanawe ni fundi na jana hakurudi, lakini pamoja na kilio, alisema bado haamini kama mwanawe amepoteza maisha.
Mwingine aliyekuwa ameshikiliwa na wenzake, alisikika akisema miongoni mwa waliopotea ni mume wake aliyemuaga asubuhi kuwa anakwenda kibaruani lakini hadi usiku wa manane hakurudi hivyo ilibidi afike eneo hilo.
Mama mwingine wa jamii ya Kihindu aliyekuwa akilia, alizirai kabla ya kuzinduka baada ya kupatiwa huduma ya kwanza. Mama huyo alisema mtoto wake ni miongoni mwa waliokwama kwenye kifusi hicho.
Barabara zafungwa
Mbali ya watu hao barabara zote zinazoingia katika eneo hilo zimefungwa.
Barabara hizo ni Mshihiri na Morogoro, Hazrat Abbas, Mali -Asia, Mali-Zanaki, Mtaa wa Zanaki, India na Indira Ghandhi.
Wachina walishangaa ‘zege’
Wachina wa Kampuni za ujenzi za China zilizopo nchini, Beijing Construction Engineering Group, BCEG iliyojenga Uwanja wa Taifa, na ile ya China Civil Engineering Construction Company (CCECC) inayojipanga kwa ujenzi wa Daraja la Kigamboni, ni miongoni mwa waliofika kusaidia uokoaji.
0
inShare
Mmoja wa Wachina hao alichukua kipande cha zege kilichotoka kwenye jengo hilo, na kukisaga kwa kutumia mkono, kikapukutika.
“Hii mchanga mingi..., hakuna zege kama hii,” alisema Mchina huyo kutoka Kampuni ya CCECC ambaye hata hivyo alikataa kutaja jina lake.
Wachina hao walitoa kijiko ambacho ndicho kilichosaidia kwa kiasi kikubwa katika uokoaji huo.
Huduma za kijamii
Mashirika mbalimbali ya hisani, yalikuwa na kazi ya kuleta vyakula, maji na vitu vingine kwa waokoaji ili kazi iendelee bila kusimama.
Malori ya Kampuni ya Strabag yanayotumika kwa ujenzi wa Barabara ya Morogoro kwa mabasi yaendayo kasi, yalishiriki kikamilifu saa 24 kuzoa kifusi hicho kilichokuwa kimejaa nondo za kila saizi.
Vikosi vya uokoaji pamoja na manesi wa Hospitali ya Mwananyamala, Hospitali ya Ibrahim Hajj na Chama cha Msalaba mwekundu, wameweka kambi wakiwa na dawa, dripu, na vitu mbalimbali vya huduma ya kwanza.
Matukio mengine
Hii ni mara ya pili kwa mwaka huu jengo kuanguka, kwani Februari jengo la ghorofa nne lilianguka maeneo ya Kijitonyama Mpakani jijini Dar es Salaam na kusababisha kifo cha mtoto wa miaka 9.
Licha ya ujenzi wa jengo hilo kusimamishwa miaka 10 iliyopita, familia ya marehemu iliendelea kuishi katika jengo hilo.
Juni 21, 2008 jengo la ghorofa 10 lilikuwa likiendelea kujengwa na Kampuni ya NK Decorators katika Mtaa wa Mtendeni Kisutu jijini Dar es Salaam liliporomoka na kuua mtu mmoja.
Mwaka 2006 jengo la ghorofa lilianguka eneo la Chang’ombe Village Inn na kuua mtu mmoja, baada ya tukio hilo aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, Edward Lowassa aliunda tume kuchunguza tukio hilo ambayo ilibaini kuwa zaidi ya maghorofa 100 jijini Dar es Salaam yalikuwa yamejengwa kinyume na taratibu za ujenzi.
Dar es Salaam. Idadi ya watu waliokufa kutokana na kufukiwa na kifusi cha jengo la ghorofa 16 lililoporomoka juzi asubuhi jijini Dar es Salaam, imefikia 22.
Habari zilizopatikana kutoka eneo la uokoaji na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova zinaeleza kuwa miili iliyopatikana imepelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Jengo hilo lililokuwa likijengwa mkabala na Msikiti wa Shia Ithnasheri ulioko Barabara ya Indira Gandhi na Kampuni ya Lucky Construction Limited liliporomoka saa 2.30 asubuhi wakati mafundi na vibarua wakiendelea na ujenzi huku chini watoto wakicheza mpira na mama lishe wakiendelea na biashara zao kama kawaida.
Rais Kikwete
Rais Jakaya Kikwete ambaye jana pia alifika katika eneo la tukio, kama ilivyokuwa juzi, alipata taarifa fupi ya maendeleo ya uokoaji kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, Said Meck Sadik na Kamanda Kova.
Baada ya kupewa taarifa hiyo, Rais Kikwete alimwagiza Kamanda Kova kuhakikisha wahusika wanakamatwa akiwamo Mkadiriaji Majengo (Quantity surveyor), mchora ramani za majengo (Architecturer), Mhandisi Mshauri (Consultant) na Mhandisi wa Jiji la Dar es Salaam. Juzi baada ya kutembelea eneo la tukio, Rais Kikwete aliagiza wahusika wote wa ujenzi huo wachukuliwe hatua kali.
Habari zilizopatikana jana zilidai kuwa Diwani wa Kata ya Goba, Wilaya Kinondoni, Ibrahim Kisoka ambaye ndiye mmiliki wa kampuni ya ujenzi, na Mhandisi Mshauri kwa pamoja wamejisalimisha Kituo Kikuu cha Polisi na hadi saa 8:00 jana mchana walikuwa wakihojiwa.
Awali Kamanda Kova aliwaambia waandishi wa habari kuwa amemtaka mmiliki wa Kampuni ya Lucky Construction Limited ambaye ni Diwani wa Kata ya Goba, Kisoka na wahusika wengine kujisamilisha kituo cha polisi, kabla hawajaamua kutumia nguvu kumtafuta.
Pinda atembelea eneo la tukio
Waziri Mkuu Mizengo Pinda alifika eneo hilo saa 3:41 asubuhi, kujionea hali ilivyo, lakini hakutoa tamko lolote. “Sina la kusema,” alisema Waziri Mkuu alipoulizwa na waandishi wa habari kutoa kauli ya serikali kuhusiana na tukio hilo.
Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi aliyefuatana na Pinda, alisikika akimwagiza Kamanda Kova kuhakikisha mchora ramani wa jengo hilo naye anatiwa nguvuni kwa kuwa jengo hilo lilikuwa la ghorofa 10, lakini likajengwa hadi 16. Mtu mwingine ambaye anatafutwa na jeshi la polisi kukamatwa ni Mhandisi Mshauri.
Lukuvi alimwagiza Kova kuwa watu waliokuwa karibu na jengo jingine la ghorofa 15 lililojengwa na mkandarasi huyo, kuhama mara moja na ubomoaji ufanyike bila kuleta madhara.
Mwenyekiti wa CUF
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba alitumia fursa hiyo kuitaka Serikali kuwabana makandarasi wasio na sifa kwani wanahatarisha maisha ya watu.
“Huu ni uzembe, wahandisi wa jiji walikuwa wapi? Wasimamizi na washauri walikuwa wapi hadi jengo linafikia ghorofa 16?” Alihoji Profesa Lipumba.
Profesa Lipumba aliitaka Bodi ya Makandarasi (CRB) kufuta leseni ya kampuni hiyo, kwani imeonyesha kuwa haiwezi kusimamia ujenzi na hivyo kusababisha vifo.
Huzuni, vilio na simanzi
Vilio na huzuni viliendelea kutanda jana katika eneo hilo ambapo waokoaji walikuwa wakijitahidi kufukua vifusi na kuzingirwa na watu waliokuwa wakisubiri ndugu zao waliofukiwa na kifusi kutolewa.
Watu wengi tangu asubuhi walikuwa wamesimama karibu na eneo hilo huku wengi nyuso zao zikiwa zimegubikwa na simanzi na wengine wakilia. Mama mmoja aliyekuwa akilia mapema asubuhi katika Mtaa wa Mshihiri, alisema mwanawe ni fundi na jana hakurudi, lakini pamoja na kilio, alisema bado haamini kama mwanawe amepoteza maisha.
Mwingine aliyekuwa ameshikiliwa na wenzake, alisikika akisema miongoni mwa waliopotea ni mume wake aliyemuaga asubuhi kuwa anakwenda kibaruani lakini hadi usiku wa manane hakurudi hivyo ilibidi afike eneo hilo.
Mama mwingine wa jamii ya Kihindu aliyekuwa akilia, alizirai kabla ya kuzinduka baada ya kupatiwa huduma ya kwanza. Mama huyo alisema mtoto wake ni miongoni mwa waliokwama kwenye kifusi hicho.
Barabara zafungwa
Mbali ya watu hao barabara zote zinazoingia katika eneo hilo zimefungwa.
Barabara hizo ni Mshihiri na Morogoro, Hazrat Abbas, Mali -Asia, Mali-Zanaki, Mtaa wa Zanaki, India na Indira Ghandhi.
Wachina walishangaa ‘zege’
Wachina wa Kampuni za ujenzi za China zilizopo nchini, Beijing Construction Engineering Group, BCEG iliyojenga Uwanja wa Taifa, na ile ya China Civil Engineering Construction Company (CCECC) inayojipanga kwa ujenzi wa Daraja la Kigamboni, ni miongoni mwa waliofika kusaidia uokoaji.
0
inShare
Mmoja wa Wachina hao alichukua kipande cha zege kilichotoka kwenye jengo hilo, na kukisaga kwa kutumia mkono, kikapukutika.
“Hii mchanga mingi..., hakuna zege kama hii,” alisema Mchina huyo kutoka Kampuni ya CCECC ambaye hata hivyo alikataa kutaja jina lake.
Wachina hao walitoa kijiko ambacho ndicho kilichosaidia kwa kiasi kikubwa katika uokoaji huo.
Huduma za kijamii
Mashirika mbalimbali ya hisani, yalikuwa na kazi ya kuleta vyakula, maji na vitu vingine kwa waokoaji ili kazi iendelee bila kusimama.
Malori ya Kampuni ya Strabag yanayotumika kwa ujenzi wa Barabara ya Morogoro kwa mabasi yaendayo kasi, yalishiriki kikamilifu saa 24 kuzoa kifusi hicho kilichokuwa kimejaa nondo za kila saizi.
Vikosi vya uokoaji pamoja na manesi wa Hospitali ya Mwananyamala, Hospitali ya Ibrahim Hajj na Chama cha Msalaba mwekundu, wameweka kambi wakiwa na dawa, dripu, na vitu mbalimbali vya huduma ya kwanza.
Matukio mengine
Hii ni mara ya pili kwa mwaka huu jengo kuanguka, kwani Februari jengo la ghorofa nne lilianguka maeneo ya Kijitonyama Mpakani jijini Dar es Salaam na kusababisha kifo cha mtoto wa miaka 9.
Licha ya ujenzi wa jengo hilo kusimamishwa miaka 10 iliyopita, familia ya marehemu iliendelea kuishi katika jengo hilo.
Juni 21, 2008 jengo la ghorofa 10 lilikuwa likiendelea kujengwa na Kampuni ya NK Decorators katika Mtaa wa Mtendeni Kisutu jijini Dar es Salaam liliporomoka na kuua mtu mmoja.
Mwaka 2006 jengo la ghorofa lilianguka eneo la Chang’ombe Village Inn na kuua mtu mmoja, baada ya tukio hilo aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, Edward Lowassa aliunda tume kuchunguza tukio hilo ambayo ilibaini kuwa zaidi ya maghorofa 100 jijini Dar es Salaam yalikuwa yamejengwa kinyume na taratibu za ujenzi.
Saturday, 23 March 2013
Wanyamapori 15,000 wauawa nchini

Moshi. Zaidi ya wanyamapori 15,220 wameuawa na majangili katika hifadhi mbalimbali zilizopo chini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) katika kipindi cha miaka minne iliyopita wakiwamo tembo 419.
Kutokana na ukubwa wa tatizo hilo, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka alipendekeza kuundwa kwa kamati teule ya Bunge kuchunguza kuimarika kwa mtandao wa ujangili nchini.
“Ni mtandao wa kimafia ambao hata baadhi ya watendaji serikalini wanaujua, lakini wanauogopa sasa. Katika mazingira haya ni vyema Bunge likachunguza ni kina nani hawa ambao wanaogopwa,” alisema.
Kwa mujibu wa Mhifadhi Mkuu wa Tanapa, Mtango Mtahico, baadhi ya wanyama waliouawa kwa ajili ya kitoweo walikaushwa na kusafirishwa nje ya nchi zikiwamo nchi za Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Sudan.
Mtahico alisema katika wanyamapori hao 15,220 waliouawa na majangili kati ya mwaka 2009 na 2012, kwa ajili ya kitoweo wamo nyumbu, mbogo, nyamera, pofu, pundamilia, swala na wanyama wengine.
Mhifadhi huyo alitoa taarifa hiyo juzi katika kikao cha wadau wa uhifadhi Kanda ya Kaskazini kilichohudhuriwa na wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wabunge na wakurugenzi wa halmashauri.
“Ujangili huu wa wanyama ambao unaongezeka nchini unachochewa na mahitaji ya kitoweo na pia mahitaji ya kibiashara kama ya pembe za ndovu na faru duniani”alisema Mhifadhi Mkuu huyo.
Mtahico alisema katika miaka ya hivi karibuni, mitandao ya ujangili imekuwa ikijiimarisha na kutumia silaha za kivita, sumu na nyaya ambazo mpaka sasa hazijulikani zinatoka maeneo gani ya nchi.“Utafiti unaendelea kujua hizi nyaya zinatoka wapi maana zinakamatwa nyingi, lakini hazipungui na hizi hazichagui zikishategeshwa zinaweza kuua hata nyumbu 100 kwa mara moja,” alisema Mtahico.
Akizungumza katika mkutano huo wa siku mbili, mbunge wa Karatu, Israel Natse alilalamikia unyama unaofanywa na askari wa Tanapa wanaodhibidi ujangili akitaka wabadili mtazamo wa utendaji kazi.
“Rangers (askari) ni wanyama mno, vitendo wanavyofanya utadhani ni vitendo vile vilivyokuwa vikifanywa na Makaburu,” alisema Natse akilalamikia pia fidia ndogo kwa watu wanauawa na wanyama.
Kauli hiyo iliungwa mkono pia na mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari ambaye alisema kuna udhalilishaji mkubwa wanaofanyiwa wananchi wanaokutwa wakiwa ndani ya hifadhi hizo.
Xi Jinping kusaini mkataba ujenzi wa Bandari Bagamoyo

Dar es Salaam. Rais wa China, Xi Jinping anatarajiwa kuwasili nchini kesho kwa ziara ya siku moja, ambapo pamoja na mambo mengine atasaini mikataba 17, kati ya nchi hiyo na Tanzania, ukiwamo wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Ujenzi huo utakaofanywa na Kampuni ya Merchants Holding ya China, utakwenda sambamba na ujenzi wa barabara inayounganisha bandari hiyo na Reli ya Kati na Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara).
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisema ujio wa rais huyo aliyechaguliwa wiki mbili zilizopita, utakuwa wa manufaa makubwa kwa Tanzania.
“Mbali na mkataba huo pia tutasaini mikataba wa kidiplomasia. Vilevile, China imefungua soko la Watanzania kuuza tumbaku nchini humo na mkataba wa kuliendeleza Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC),” alisema Membe.
Waziri huyo alisema kiongozi huyo wa China pia atafungua jengo la kisasa la mikutano la Mwalimu Nyerere.
“Kwa kuwa anakuja Afrika kwa mara ya kwanza huku Tanzania ikiwa nchi ya kwanza, Jinping pia atatoa hotuba yake juu ya msimamo wa China kwa Tanzania na Afrika kwa jumla,” alisena Membe.
Waziri Sitta awaanika wabunge wa Afrika Mashariki kuhusu posho

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amewajibu wabunge wa Afrika Mashariki akisema wengi hawahudhurii vikao vya kupewa mwongozo kuhusu bunge hilo kwa kuwa “wanataka kulipwa posho”.
Kauli hiyo ya Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, imekuja siku moja tangu wabunge hao waichongee wizara hiyo kwa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, kwamba imeshindwa kuwapa mwongozo pale wanapokwenda kwenye vikao vya Bunge la Afrika Mashariki.
Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo jana, Sitta alisema wabunge hao wamekuwa vinara wa kuomba posho kila wanapotakiwa kuhudhuria kwenye mikutano ya wizara yake.
Katika maelezo yake Sitta alimeshutumu Katibu wa Wabunge hao, Shyrose Bhanji kuwa ndiye anayeongoza kwa kutoa udhuru mara kadhaa, hivyo kutoudhuria vikao vinavyoitishwa na wizara hiyo.
“ Wizara imejiwekea utaratibu mzuri wa kukutana na wabunge hao, lakini nafikiri katibu wao ndiye anayeongoza kwa kutohudhuria,” alisema Sitta na kuongeza:
“Nadhani amekuwa na shughuli nyingi sana, tuna utaratibu wa kukutana kila baada ya miezi mitatu, lakini ndiye aliyeongoza pia kutoa malalamiko hayo yasiyo na ukweli.”
Waziri Sitta katika majibu yake alifafanua kwamba wizara hiyo bado haijapewa majukumu rasmi ya kutoa mwongozo kwa wabunge hao.
Mbali na Sitta, naibu wake, Abdullah Juma Saddallah naye alieleza tabia za wabunge hao huku akisisitiza kuwa posho kwao ndiyo jambo la umuhimu zaidi.
Saddallah alisema malalamiko hayo ni ya ajabu na yamewashtua kwa sababu hayana ukweli, lakini wamekuwa wakijikuta kwenye mtihani kwani kuna baadhi ya wabunge hao wakiitwa kuudhuria vikao utambulia kuuliza posho.
“Wizara haina fungu la kuwahudumia wabunge hao, hili limekiwishajadiliwa katika vikao vya kamati vilivyopita na ilikubalika kuwa ofisi ya bunge itaangalia uwezekano wa kuwapatia ofisi na vitendea kazi vingine,” alisema Saddallah.
Alisema pia kabla ya kuteuliwa wabunge hao wizara hiyo kwa kushirikiana na ofisi ya Bunge ilifanya uchambuzi na kuandaa mwongozo utakaowezesha ushirikiano na uwajibikaji baina ya Bunge la Tanzania na wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA).
“Mwongozo huu umewezesha kuundwa kwa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambayo awali ilitarajiwa kuwa Kamati ya Bunge ya Afrika Mashariki inayotoa nafasi ya kutoa taarifa za utekelezaji na kupata mwongozo,” alisema Naibu Waziri huyo.
Naibu Waziri huyo alisema katika semina waliyopewa wabunge hao mbala na kutolewa kwa mada mbalimbali kuhusu mfumo wa utendaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki pia wabunge
walipewa vitabu ambavyo vinaonyesha ni taratibu, misingi na hatua za Mtangamano.
Naibu Waziri huyo alibainisha zaidi kuwa wabunge hao wa EALA wamekuwa wakishirikishwa katika shughuli mbalimbali za wizara, akitoa mfano kuwa mwenyekiti wao hualikwa katika uwasilishaji wa hotuba ya Bajeti na uzinduzi wa shuhghuli mbalimbali za wizara hiyo.
Katika madai yake juzi Bhanji alidai kuwa wanashindwa kujadili maslahi ya wananchi katika Bunge la Afrika Mashariki kutokana na kutengwa na wizara, huku mwenzake Abdalah Mwinyi akisema kuwa, mpaka sasa serikali haina sera ya mtangamano ambao utawaweka pamoja wabunge wa Tanzania.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mussa Zungu alisema kamati imeridhika na maelezo yaliyotolewa na wizara hiyo, ikiwa ni pamoja na hatua ambazo imezichukua katika kuhakikisha sera inakuwepo.
Thursday, 14 March 2013
Tume ya Mizengo Pinda yaanza kuhoji wanafunzi, walimu

Mwenyekiti wa tume hiyo Profesa Sifuni Mchome, alisema jana kwamba shughuli hiyo imeanza katika Kanda ya Dar es Salaam ambapo wajumbe watatembelea shule 12.
“Tumeamua kuzungumza na wanafunzi waliopo shuleni na wale waliofanya mtihani huo watakaopatikana ili kujua ni nini kilichofanya wakapata alama hizo, pia itakuwa njia rahisi ya kupata watu wengi ikiwa ni pamoja na bodi za shule,” alisema Profesa Mchome:
“Kazi kwa Dar es Salaam ilianza Jumatatu na itaisha Ijumaa, kuna shule ambazo zimeainishwa. Tukifika kwenye hizo shule na kama zipo shule zingine jirani tutawaita waje kutoa maoni yao.” alisema.
Profesa Mchome alisema kuwa, ili kufanikisha shughuli hiyo wameteua kanda tano ikiwamo ya Dar es Salaam, Kusini, Mashariki, Kati na Kanda ya Magharibi ambayo itahusisha Mikoa ya Geita na Simiyu.
Profesa Mchome alieleza kuwa, ili kupata maoni ya wananchi wengi wamefungua tovuti inayoitwa www.tumek4.go.tz ili wengine watoe maoni huko.
Alisema kuwa, kanda hizo zimetengwa kwa kuzingatia hadidu za rejea zilizotolewa na Waziri Mkuu, ambapo wamechangua shule zilizofanya vibaya, zilizokuwa na ufaulu wa kati na zilizofanya vizuri ambazo ni zile za Serikali na zisizo za Serikali.
Alisema kuwa, tayari wameshazungumza na maofisa elimu pamoja na Muungano wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (Tahosa).
Alisema kuwa, baada ya kutembelea shule hizo Dar es Salaam, juma lijalo timu hiyo itaenda katika kanda nyingine ambapo zitatembelewa shule 13.
Alisema kuwa, leo ratiba ya shughuli ya tume hiyo itawekwa katika tovuti yao.Profesa mchimo aliwataka wananchi watoe zaidi maoni yao kupitia tovuti hiyo, pamoja na vyombo vya habari ili waweze kukamilisha shughuli hiyo kwa kupata maoni ya watu wengi.
Papa mpya apatikana, achagua jina la Francis

Baada ya kuchaguliwa na makardinali wenzake 115, Kardinali Jorge Bergoglio (76) alichagua kufahamika kwa jina la Francis I.
Maelfu ya mahujaji, watalii na waumini wa Kanisa Katoliki waliokuwa wamejazana katika Viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Petro, Vatican kushuhudia moshi mweupe uliofuka saa 4:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki kuashiria kuchaguliwa kwake, waliripuka kwa shangwe, nderemo na vifijo.
Muda mfupi baada ya moshi huo kutoka, kardinali mmoja alisimama katika ‘varanda’ ya Kanisa la Mtakatifu Petro na kutangaza “Habemus Papum” (tumepata papa mpya).
Papa Francis I alikuwa miongoni mwa waliokuwa wanawania nafasi hiyo na papa anayeondoka, Benedict XVI mwaka 2005, ambapo aliripotiwa kuibuka wa pili.
Kabla ya kuchaguliwa kwake, Papa Francis I ambaye kwa wadhifa wake pia anakwenda kuwa Askofu wa Roma, alikuwa Askofu Mkuu wa Jimbo la Buenos Aires, Argentine na kwa muda wote wa utumishi wa utumishi alikuwa huko huko nyumbani.
Anakuwa Papa wa 266 kuwahi kuongoza kanisa hilo lenye waumini zaidi ya bilioni 1.2 duniani.
Baada ya kutangazwa kwake, Papa Francis I alijitokeza kuzungumza kwa mara ya kwanza kama Askofu wa Roma.
Akiwa amechaguliwa katika awamu ya tano ya upigaji kura, inaelezwa kuwa alikuwa miongoni mwa mapapa waliochaguliwa kwa haraka baada ya muda mrefu, akiwa sawa na Benedict XVI (2005) na Pius XII aliyechaguliwa mwaka 1939.
Mshindi alitakiwa kupata kuta 77 au robo tatu ya makardinali 115 walioshiriki uchaguzi huo.
Papa Francis I anachukua nafasi iliyoachwa na Papa Benedict XVI aliyejiuzulu Februari 28, mwaka huu, ikiwa ni miaka 600 tangu Papa wa mwisho kujiuzulu.
Yeye ni nani
Papa Francis I, ni Papa wa kwanza kutoka Shirika la Jesuit ambaye ametumia muda wake mwingi wa utumishi nyumbani Argentina.
Anafahamika kwa utumishi uliotukuka kwa uangalizi wa kanisa na mapadri, mambo ambayo yanatajwa kuwa sifa kubwa ya kuchaguliwa kuwa Papa.
Papa huyo amedumu katika maisha ya kufundisha na kuongoza mapadri. Amefanya kazi Amerika ya Kusini ambako kuna Wakatoliki wengi. Kardinali Bergoglio anatambulika kwa kutamadunisha Kanisa la Argentina, lililokuwa miongoni mwa makanisa ya kihafidhina huko Amerika Kusini.
Amechagua jina la Papa Francis I, chini ya uangalizi wa Mtakatifu Francis wa Assisi.
Alizaliwa Buenos Aires katika familia ya mfanyakazi wa reli. Alipata upadrisho mwaka 1969.
Aprili 15, 2005, mwanasheria wa haki za binadamu alimfungulia mashtaka ya jinai kwa kushirikiana na maofisa wa jeshi kuwateka mapadri wawili wa Jesuit mwaka 1976, akiwa kiongozi wao aliwafukuza katika utumishi kutokana na migogoro katika jumuiya hiyo.
Msemaji wake alikanusha vikali tuhuma hizo na hakuna uthibitisho uliotolewa kumhusisha na madai hayo.
Kauli yake ya kwanza
Baada ya kutangazwa kuwa Papa wa 266, Kardinali Jorge Bergoglio (76) aliwataka waumini wa Kanisa Katoliki duniani kumwombea.
Papa huyo aliyechagua jina la Francis I, alisema: “Kama mnavyofahamu, kazi ya mkutano wa uchaguzi ilikuwa ni kuchagua Askofu wa Roma,” Francis I aliueleza umati uliokuwa unashangilia katika Viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Petro, huku akiwapungia mikono.
“Ni mimi hapa. Ninadhani makardinali wenzangu wamenichagua mimi kutoka mbali...Niko hapa. Ninapenda kuwashukuru kwa kunipokea.”
Akiwa kardinali alipambana na Serikali ya Argentina chini ya Rais Cristina Fernandez de Kirchner kuhusu msimamo wake dhidi ya ndoa za mashoga na utoaji bure wa huduma za uzazi wa mpango, ambazo zimekuwa zikipingwa na Kanisa Katoliki duniani kote.
Wednesday, 13 March 2013
Waislamu waonya kauli za uchochezi

Dar es Salaam. Wakati Kiongozi wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila akitiwa mbaroni kwa tuhuma za uchochezi wa kidini, viongozi wa Jumuiya ya Kiislamu Tanzania wametoa tamko na kusema kuwa baadhi ya kauli za viongozi wa Serikali na viongozi wa dini zina mwelekeo wa kukuza mfarakano wa kidini kuliko kuleta maelewano.
Wiki iliyopita Mchungaji Mtikila alikamatwa mkoani Rukwa akituhumiwa kuwahamasisha Wakristo wawavamie Waislamu.
Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema Mchungaji Mtikila alichochea uhasama kwa kuwaeleza viongozi wa Kikristo kuwa, wamekuwa wakionewa na Waislamu kutokana na matukio yanayoendelea kutokea hapa nchi.
Katika tamko lao, viongozi wa Kiislamu walisema kuwa mara nyingi kauli za viongozi wa dini na Serikali hazina nia njema bali zimekuwa za kibaguzi au za kiupendeleo.
“ Imekuwa ni kawaida kila anaposhambuliwa au kuuawa Padri baadhi ya viongozi wa Serikali, na wale wa Kikristo, vyombo vya habari, baadhi ya asasi na taasisi za kiraia wamekuwa wakiwanyooshea vidole na kuelekeza lawama zao kwa jamii ya Waislamu,” lilisema tamko hilo.
Katika tamko hilo Jumuiya ya Waislamu ilieleza kuwa Waislamu wamekuwa wakinyooshewa vidole kutokana na matukio hayo pasipo kuwa na ushahidi.
Iliongeza kuwa wamekuwa wakishutumiwa kuhusika katika matukio kabla hata ya uchunguzi wa vyombo vya usalama na polisi kufanyika.
Tamko hilo lilisema kuwa serikali kupitia waziri wa mambo ya ndani ilitoa kauli kuwa mauaji ya padri huyo ni matokeo ya kazi za ugaidi.
Tamko hilo lilisisitiza kuwa linaungana na wapenda amani wote kulaani mauaji, manyanyaso na udhalilishaji wa aina yoyote unaowalenga viongozi wa dini.
Jumuiya hiyo imewataka viongozi wa dini na Serikali kuhakikisha wanahimiza amani na mshikamano badala ya kuwa vyanzo vya kuchochea vurugu.
Wamesema hawatafumbia macho tabia ya kuendelea kunyoshewa vidole Waislamu kila linapotokea tukio la uvunjifu wa amani nchini na wamewataka Watazania wote kwa umoja wao kusimamia ushirikiano na kuiimba amani ili kulinusuru taifa na aina yoyote ya vurugu.
Benki Kuu yaingilia kati wizi wa ATM

Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika sekta ya benki nchini.
Kutokana na wizi huo kukithiri katika baadhi ya benki, wafanyabiashara na wananchi wameanza kujipanga kuondoa fedha zao katika akaunti.
Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndullu alizungumza kwa njia ya simu mwishoni mwa wiki kwamba wameziagiza benki kuweka kifaa cha umeme (electronic chip) kwenye kadi zao za ATM ambazo si rahisi kughushi.
“Wizi kama huo unatokea wakati mtu anaweka namba za siri kwenye ATM kwani kuna watu huweka kamera ambazo husoma na namba hizo kufanikiwa kuzipata kisha kufanya wizi ,” alisema Profesa Ndullu.
Alisema kuwa kutokana na wizi kukithiri wamezitaka benki zote kuweka mifuniko katika eneo la namba za siri ili wezi wanaoweka kamera ili kuzinasa wakati mtu anatoa fedha washindwe kufanya hivyo.
Profesa Ndullu alisema wanafuatilia mfumo wa utendaji wa benki ili kuondokana na tatizo hilo ambalo hivi sasa limeibua mijadala na hofu kubwa miongoni mwa wananchi.
Benki kubwa nchini zimekumbwa na mtikisiko wa wizi wa fedha kwa kadi za ATM, ambao umeongezeka kwa kasi kiasi cha kufanya wananchi wengi kuhifadhi fedha zao kwenye mitandao ya makampuni mbalimbali ya simu za mikononi ambayo hata hivyo ripoti zimekuwa zikieleza kuwa nako usalama wake si wa kiwango cha juu.
Baadhi ya benki ambazo zimekumbwa na matukio hayo zimekuwa zikisita kutoa taarifa kueleza sababu za kushindwa kuzuia wizi huo na badala yake zimekaa kimya kuhofia kupoteza wateja.
Kukua kwa teknolojia za kifedha ambako kumerahisisha ufanisi wa matumizi na utunzaji wa fedha, sasa kunaonekana kugeuka na kuwa balaa kutokana na kuibuka kwa wizi mkubwa mahala zinakohifadhiwa kwenye akaunti za wateja kwa kutumia njia ya mtandao.
Taarifa za wizi huo zilianza kurindima mwezi Machi, 2010, ambako kiasi cha mabilioni ziliibwa kupitia katika mashine za ATM huku kati ya kiasi hicho jumla ya Sh360 milioni zikihusisha benki moja nchini.
Hata hivyo, mwaka huo watu wanne walikamatwa baada ya kuripotiwa wizi huo mkubwa. Sambamba na kukamatwa kwa watu hao, pia alikamatwa mfanyabiashara mmoja aliyekuwa akifanya jaribio la kuiba kimafia Sh221 milioni kutoka benki ya NBC.
Wimbi la wizi huo limeibuka tena katika kipindi cha Oktoba 2012 hadi Februari 2013 na inakadiriwa kuwa jumla ya kiasi cha Sh700 milioni kimeibwa katika benki mbalimbali kwa nyakati tofauti.
Hivi karibuni, Polisi mkoani Mwanza kwa kusaidiana na maofisa wa Benki ya NMB, iliwatia mbaroni watu watatu ambao walidaiwa kuiba kiasi cha Sh700 milioni kwa nyakati tofauti.
Watuhumiwa hao walinaswa baada ya kuwekewa mtego na maofisa wa benki pamoja na polisi usiku wa Februari 10, mwaka huu. Mtuhumiwa mmoja alinaswa akichukua fedha katika mashine ya ATM ya NMB kwenye Tawi la PPF Plaza.
Baada ya kunaswa kwa mtuhumiwa huyo, alisaidia kuwaelekeza polisi walipo wenzake, ambao walikutwa katika hoteli moja jijini Mwanza wakiwa wamejipumzisha.
Subscribe to:
Comments (Atom)

